Tupunguze kujenga Misikiti, hakuna Uislamu kama hakuna maendeleo ya waumini

Tupunguze kujenga Misikiti, hakuna Uislamu kama hakuna maendeleo ya waumini

BAKIIF Islamic hata huku kwenye ukristo hasa PENTECOSTALS kazi yetu kubwa kilasiku tunawaza kufungua makanisa na kufungulia mziki Kwa fujo ....ufike muda walokole nao wajenge hospital,shule na huduma zingine za jamii kama ilivyo Kwa katoliki na kkkt
Ajabu zaidi sasa tukianza kushambuliana mpaka tunatukanana wakati huenda tuko nje ya lengo la Mungu mwenyewe

Maana utakuta waumini kila kitu wana pata katika taasisi nyingine lakini kutoa wanalazimishwa makanisani na misikitini

Tunapaswa sana kubadilika kila mtu kwenye Dini yake kwa kweli!!!

Sent from my Infinix X657 using JamiiForums mobile app
 
Hao ktk bold wanatoa sana sadaka na michango mbalimbali but ninyi huwa mnawacheka kwamba ni wajinga wanapelekea hela mapadre na wachungaji.

Mkiiga kwao mkubali kuwa watoaji.
Ndugu yangu huku Pentecostal tunatoa Sana sadaka isipokuwa shida hizo pesa zinaenda Kwa MTU mmoja Tu tofauti na taasisi kama Catholic na kkkt hawa jamaa wanaona mbali Sana,hii mada ya Leo inatusema hata huku Kwa walokole Kwa mfano mtaa ambao naishi kuna zaidi ya makanisa ya kilokole zaidi ya 7 yaani kila MTU anafungua Tu kanisa,
Tena afadhali Kwa waislamu wanajenga misikiti Kwaajili ya waumini wote lkn Sisi tunaanzisha kanisa Kwaajili yangu na maisha yangu
 
Pale Kinondoni Muslim pangekua hospitali/shule/chuo Kikuu pangeokoa watu wangapi?
Sekondari IPO pale Ila haifanyi vizuri ingawa Wana eneo kubwa Sana pale Hadi uwanja wa Mpira upo tena mkubwa kwelikweli
 
Ametumwa na nani?

Yeye maelezo yake yamewekwa kwa mtindo wa hoja. Unapojibu, jibu kwa hoja ili kuendeleza mjadala chanya.

Unaposema Uislam umejitosheleza, sidhani kama yeye kuna mahali amesema haujajitosheleza, points zake hazijajikita kwenye Uislam, bali kwa waislam, kwa namna wanayo handle mambo.

Ni kweli waislam wenye elimu wako wengi sana, hata nchi hii peke yake, ukitaja matajiri, orodha itajaa waislam, ila impact yao ni ipi?
Exactly [emoji817]
 
Maendeleo ni muhimu katika jamii za Kiislamu.
Uislamu na mendeleo ndiko kutakidhi mahitaji ya kimsingi ya watu.

Kiwango cha maendeleo duni katika maeneo ya Wailslamu hapa nchini kinaonyeshwa kwa kutumia mifano iliyo hai. Maeneo mengi ya Waislamu kuna tatizo kubwa la kukidhi mahitaji ya kimsingi ya watu. Hili linawafanya wasio waislamu kuulaumu Uislamu kuwa ni miongoni mwa sababu za kukosekana kwa maendeleo katika maeneo husika.

Inajadiliwa, sio kwamba uislamu hauna mbinu wala elimu za kiuchumi laa, ispokuwa waislamu wenyewe wameacha kufuata misingi iliyoasisiwa na Mtume wetu Muhammada (s.a.w). Kwamba uislamu daima umekuza shughuli za kiuchumi, na biashara na kipindi cha nyuma uislamu ulikuwa unachukuliwa kuwa njia bora ya kupata riziki ya mtu. Zaidi ya hayo, dhana ya maendeleo katika Uislamu ni mchakato muhimu, ambao unaboresha ustawi wa binadamu katika nyanja zote ikiwa ni pamoja na akhera. Vielelezo vya MAKKA na MADINA vinawasilishwa kama mojawapo ya njia za maendeleo katika Uislamu wetu.

Waislamu kutoka mtaa mmoja wanakutana mara 5 kwa siku (sala tano), waislamu wa kitongoji kimoja wanakutana mara 1 kwa wiki (Sala ya Ijumaa), waislamu wa mkoa mmoja wanakutana mara mbili kwa mwaka (Sala za Eid), waislamu kote duniani tena walio matajiri wanakutana mara moja kwa mwaka (Hija).

Mlolongo huo alituachia Mwenyezi Mungu s.w kupitia Mtume wetu Muhammada (s.a.w), Lakini kukutana kwetu huko hakutakua na manufaa yoyote ikiwa bado kutakuwa na ukosefu wa maendeleo kwa watu wetu.

Lengo la watu kukutana sio kuswali na kuondoka tu, watu wanatakiwa kujadili, kufahamiana, na kupanga mikakati ya kusonga mbele zaidi kielimu, kiuchumi, kiafya na kimaendeleo kwa ujumla. Nasio kuishia kuswali na kuondoka hata bila kupeana mikono.

Wenzetu wamechukua mfumo huo wa kukutana, leo utaona kuna jumuiya nyingi za Kikristo zinakutana kila wiki asubuhi mapema, leo utaona kuna umoja wa kimataifa (mataifa yote yanakutana) asili yake hii ni Uislamu. Lengo la kukutana misikitini ni kufanya vikao vya kheri kwa umoja wenu msonge mbele kimaendeleo.

Ifake wakati sasa misikiti iyanze kuhudumia watu na kuwafanyia watu mambo yaliyo mema, nasio watu siku zote kuihudumia misikiti. Moyo wa mtu umeumbwa kukipenda na kukithamini kile kitu kinachomjali, na moyo umeumbwa kukichukia na kukidharau kile kitu kisichomjali.

Misikiti mingi haina hata orodha (Record Keeping Books) ya kuwatambua waumini wake, idadi yao na shughuli zao. Misikiti mingi haina vipaombele katika swala la maendeleo, misikiti mingi haina orodha ya wajane, haina orodha ya mayatima, haina orodha ya wanafunzi walio kwama Masomo kwa ukata wa pesa, haina orodha ya wagonjwa, imekuwa ni sehemu ya kuswalia tu na kuondoka.
Msikiti ni kituo cha Kiislamu kinachotakiwa kuzalisha usasa wa kijamii na kiuchumi na maendeleo kwa ujumla.

Dini ni mfumo wa maisha ya mwanaadamu unaofuata sheria za MUNGU. Panapokuwa na dhiki inaashiria kwamba malengo ya Uislamu hayawezi kutimizwa, kwasababu watu hawajiwezi kwa kutofautiana kijamii na kiuchumi, rushwa na ukosefu wa haki. Haina faida kujenga msikiti ilihali wake za Masheikh wanazalishwa na Madaktari wa kiume, haina faida ya kujenga msikiti ilihali kuna kundi kubwa la vijana wa kiislamu wanakwama masomo kwa ukata wa pesa, haina faida ya kujenga msikiti ilihali wanawake wa kiislamu wanadhalilishwa kwenye mikopo ya Riba. Na mambo mengine ya kuudhi yanayoofanyika dhidi ya watu wetu.

Tusisahau kwamba ni kanuni na maadili ya Kiislamu ambayo yalisaidia jamii za Kiislamu kujenga ustaarabu wenye mafanikio makubwa na mafanikio yaliyoonyeshwa katika kukusanya rasilimali na kuunda fursa, na ambayo ilizisaidia jamii kufikia maendeleo makubwa ya kiuchumi hadi karne ya kumi na tisa.

Turudi katika misingi na kanuni zetu. Muislamu kupewa msaada na Kanisa inatia aibu ilihali misikiti ipo.

frauenindermoschee.jpg



BAKIIF ISLAMIC
Kimara, Dar es salaam
Takbirr
Hsya ndiyo maneno ya kuambiana
 
Una uhakika gani, hao ni Waislamu, huku kukiwa na muendelezo wa watu maalumu, wanaotafuta kuidhoovisha Tanzania kupitia imani.

Kila siku kuda mada ya dini ukristo kuuhoji uislamu.
Na mimi baadae nitauliza swali, waliomtesa yesu, kwanini walimvua nguo na kumvisha kile kinguo.
Wewe umewahi kumuona Yesu wapi?
 
Umenisemea Allah anisamehe mwanangu baba ake amempeleka seminary ya masista maana hakuna shule nzuri ya kiislamu ya wasichana,ni mtihani mtupuu
Kuna dhambi gani Kwa mtoto wako kwenda kusoma kwenye shule bora?

Sidhani kama unajuwa hata huo uislamu na Quran, Mwislamu unatakiwa na Quran uitafute elimu hata China siyo shule za masister tu.

Halafu sidhani kama unafahamu kwenye Quran Maria/Mariam ana sura nzima inaitwa Surat Mariam, je unalifahamu hilo?
 
Back
Top Bottom