Ujinga uliowagharimu wengi kwenye maisha

Ujinga uliowagharimu wengi kwenye maisha

Namba moja inahitaji mjadala mpana, sina uhakika kama unaweza kujadili. Otherwise tufunike kombe na tucall it a day!
 
mimi napinga hyo ishue sijui mzazi kama hajasoma basi na watoto hawatasoma au kuwa maskini...

wazazi wangu hawakusoma kbsa na tumezaliwa watoto wa 5 ..nataka nkuambie mpka sasa wote tuna degree kasoro mmoja ana diploma.

siioni point kweny hicho kipengele lbda ungesema kuwa inategemea na akili ya mtu.

***********

KUOA SINGLE MOTHER

aisee nina jamaa yangu ameoa binti ambaye ana mtoto .

hivi navyozungumza wana miaka 7 kweny ndoa na hata siku moja sijawahi kuoa wametofautiana kiasi ch kujuta kuwa pamoja.

siamini kwny baadhi ya vipengele ulivyoainisha.

UMESEMA KILA MTU ANA KAUJINGA KAKE NO MATTER HOW PERFECT MTU ANA JI-POTRAY KWA JAMII...

NAAMINI WW KAUJINGA KAKO NI HAKA KUANDIKA VITU UKIWA VERY SURE AS IF U HAVE STUDIED THE HUMAN PHYCHOLOGY TO THE EXTENT OF EXPERTISE.



this is bull shit!!!
Ahsante babaangu yaan huyu anajifanyaga kana kwamba neno lake ni sheria ,kanikwaza kutuponda single mom akat tuna bahat zetu,maisha hayana formula muache abwabwaje
 
Taikon nipumzike sasa!
Kwa wale wasiopenda kusoma nyuzi refu najaribu kufupisha.

Mtoa mada anazungumzia mitazamo mbalimbali ambayo watu wakiwa nayo inaweza kuwagharimu maishani mwao.

Mitazamo hiyo huwakilishwa k2a njia ya maneno,na hayo maneno ni kama yafuatayo.

1. Kusoma sio kufanikiwa maisha(wanabeza elimu)

2. Uliona wapi pipi ikaliwa na maganda yake(wanahamaisha ngono zembe)

3. Siwezi kujenga na kuishi kijijini Mimi(wanabeza kununua maeneo maeneo ya mbali na mji)

4. Ngoja nikupe/niolewe naye nitambadilisha au atabadilika(wwnabeti kwenye ndoa)

5. Acha Nile ujanita nitaolewa tuu(wanakataa ndoa kwa kudhani wakiolewa hawatokula ujana)

6. Pesa hainunui furaha(wanajifariji kwa sababu hawana pesa au hawajazipata)

7.Dini sio tatizo(wanadhani dini haimati kwenye ndoa kumbe si kweli)
kila mtu atakuwa na dini yake, ilimradi tunapendana

8. Kuoa single mother sio tatizo, Inategemea na Mwanamke(wanajaribu kutia mkono gizani kuoa single mother)

9.. Ninatetea na kusaidia Masikini na wanaoonewa, Mungu atanilipa(sio kazi yako kutetea masikini ni kazi ya MMungu.
 
UJINGA ULIOWAGHARIMU WENGI KWENYE MAISHA!

Anaandika, Robert Heriel.

Kila binadamu anakiwango chake cha ujinga, hata Yule unayemuona anaakili Sana ujue anakaujinga kake.
Sasa unaweza ukawa mjinga lakini kamwe Epuka kuwa MPUUZI, mpuuziaji ambaye baadaye itakufanywa uitwe mjuaji wakati hukuwa unajua. Mjinga ajifanyaye anajua huingia katika kundi la wapumbavu, hivyo ndivyo ilivyo ni Sawa na mwerevu mwenye upuuziaji nayr huingia kwenye kundi la wapumbavu.

Na hii sasa ndio orodha ya ujinga ambao ulisababishwa na upuuziaji uliowagharimu watu wengi Duniani;

1. "Kusoma sio kufanikiwa maisha" wakati Vijana wengi walipoambiwa wasome baadhi Yao walikuwa wakisema maneno hayo au Kuambiwa maneno hayo na watu walioshindwa shule. Wapo waliokuwa wakisema kimoyo moyo.

Usiposoma lazima utumie nguvu kuyamudu maisha hasa ukiwa umetoka familia Masikini. Tena utatumia nguvu na bado utalipwa Kama kibarua. Hii ni Kwa sababu huna tofauti na mnyama Kama punda au ng'ombe ambao nao hutumia nguvu tuu.
Lakini ukitumia akili maslahi yake huwa ya juu.

Vijana Kama huna elimu ni Bora ujiajiri Kwa kweli. Maana wewe ni kibarua na wala haupo kundi la Wafanyakazi. Mshahara wako utakuwa kidunchu wa kula tuu.
Ni Bora ukatembeze karanga, ukauze henge, mkaa, ukawa bodaboda au konda na kazi zingine zisizohitaji elimu kuliko uajiriwe maana utalipwa posho tuu.


2. "Uliona wapi pipi ikaliwa na maganda yake?"
Wengi Kwa ujinga walitumia Kauli hiyo wakaishia kupata UKIMWI, kupata mimba wasizokuwa wamezitarajia. Tena walioolewa au kuoa wakauleta UKIMWI nyumbani na kuiangamiza familia.

3. " Siwezi kujenga na kuishi kijijini Mimi" "Hivyo viwanja vipo mbali na mji"
Wengi wamejikuta wakizeeka pasipo kuwa na Nyumba za kuwastiri wao na watoto wao Kwa akili za kijinga jinga.
Hawakujua kuwa hata hapo wanapopaita Mjini palikuwa kijijini zamani, tena hapakuwa na Nyumba hata moja.
Hujikuta wakiishi maisha Yao Kwa taabu hasa umri ukiwa umeenda, mwishowe huwatesa watoto.

4. " Ngoja nikupe/niolewe naye nitambadilisha au atabadilika"
Wengi wamejikuta wakiyaharibu maisha Yao Kwa ujinga na upuuzi. Unakuta limwanamke ni kahaba, halina sehemu za siri, karibu wanaume wote WA mtaani wanamjua sehemu zake nyeti. Ati unamuoa alafu unahama mtaa, wewe si CHIZI tuu! Malaya hata umpeleke mbinguni ataleta umalaya wake Kwa Malaika. Hujiulizi Kwa nini Huko mbinguni hawataki Malaya, hujiulizi! Sehemu haimbadilishi mtu.
Mtu Kama anatabia mbaya achana naye, tafuta wenye tabia nzuri mbona wapo.

Au unakuta limwanaume haliheshimu wanawake, linazalisha hovyo, linapiga wanawake, linatukana tukana hovyo matusi ya aibu, alafu Kwa ujinga wako unaolewa nalo Kwa matarajio ya kumbadilisha, unaumwa wewe! Mtu kujibadilisha mwenyewe ni shughuli pevu sembuse wewe umbadilishe.
Ndio yake baadaye linatukana wazazi wako, ndugu zako, wengine wanafikia hatua ya kutoka na Dada yako au Mama yako.
Alafu unamlaumu, unalaumu nini wakati wewe ndio ulikuwa mjinga!

Acha Shetani waoane na mashetani.
Malaika waoane na Malaika!
Majini Kwa Majini
Walevi Kwa walevi
Malaya Kwa Malaya n.k.

5. " Acha Nile ujana, nitaolewa tuu"
Asilimia 90 ya wanawake ambao wanaumri wa miaka 30+ waliringa kuolewa na wanaume Fulani Kwa sababu kadha wa kadha!
Wengine walijiona bado wadogo, wakati mwanamke mwenye miaka 20 tuu tayari ni mtu mzima anaukaribia uzee. Akishafikisha 30 tayari keshaondoka kwenye soko.

Ujinga wa baadhi ya wanawake kufikiri Kama wanaume ndio inawagharimu leo hii. Huwezi kuhangaika kutafuta mchumba ukiwa umezeeka, labda utafuta mshirika wa kusogeza siku ziende.

Raha ya Mke umfaidi akiwa mbichi, mtoto bado ngozi inateleza bila hata Mafuta.
Sasa sijui Nani aliwadanganya dada zetu kutafuta kuolewa wakati Sura zao zikiwa zinadondoka chini, na ngozi zikiwa tepetepe!
Anyway!

6. "Pesa hainunui furaha"
Wanaume wenye mtazamo huu huishia kuumia na kugharamika maradufu. Huchukulia mambo rahisi. Hivyo hawawekezi nguvu zao kwenye utafutaji. Mwishowe huishia maisha ya kulalamika.
Mwanaume asipokuwa na pesa hawezi kuwa na nguvu ndani ya Nyumba, na hapa sisemi uwe na pesa nyingi Sana hapana, nazungumzia pesa inayokutosha wewe, Mkeo, na watoto.
Ukikosa hiyo basi Mkeo atakusumbua, asipokusumbua yeye basi Vijana wa mtaani watamsumbua, wasipomsumbua yeye basi watasumbua vibinti vyako vikiwa hata havijafika sekondari wataanza Kula embe na chumvi.
Uchunguzi wangu unaonyesha umasikini WA wasichana wengi husababisha kujiingiza katika mapenzi wakiwa wadogo Sana. Kwani hudanganywa na vijana wa mtaani Kama bodaboda, wauza magenge ya chipsi n.k.

Watoto wengu huiga maisha ya wazazi wao. Hupenda kuona kile unachowashauri wewe mwenyewe ulikifuata. Lakini ni watoto wachache Sana wanaofuata maneno ya wazazi pasipo kuangalia uhalisia wa wazazi.

Mtoto anakuwa inspired na Mzazi Kwa uhalisia sio maneno. Na ndio maana ukiwa hujasoma na Masikini ni rahisi Sana mtoto kuwa Masikini na asiwe na Elimu.
Halikadhalika ukiwa umesoma ni rahisi Sana mtoto kuwa kama Mzazi wake hata usipomwambia mtoto anataka kuwa kama Mzazi wake.

Ndio maana inashauriwa mtoto umwonyeshee matendo zaidi kuliko maneno.
Kama hujasoma na ni Masikini Taikon atakushauri ufanye utakavyoweza uoe msomi na mtu mwenye kipato cha kueleweka Kwa faida ya watoto. Vinginevyo utakuwa unapoteza muda. Ingawaje wapo Exceptional ambao ni wachache Mno, tena wachache Sana.

7. " Dini sio tatizo, kila mtu atakuwa na dini yake, ilimradi tunapendana"
Ukiona uliwahi fikiiria kitu Kama hiki ujue wewe ni mjinga wa kiwango cha juu kabisa. Wengi imewagharimu walipoamua kufuata mtazamo huu. Dini humfanya mtu kuwa na Imani Fulani, Imani huleta falsafa, falsafa huleta Mtazamo wa mtu juu ya Maisha. Kama watu mnatofautiana mtazamo mtawezaje kuishi pamoja, Kama sio kujidanganya.

8. " Kuoa single mother sio tatizo, Inategemea na Mwanamke mwenyewe"
Wengi imewagharimu, tena Sana. Wengi Hufanya hivyo Kwa hisia tuu, tena hisia za kitoto ambazo mtu mwenye akili iliyotulia hawezi kufanya hivyo.

Kuoa tuu mwanamke kama Mwanamke ambaye Hana mtoto na hata hajawahi kumjua mwanaume inatakiwa mwanaume ujishike, uwe umekomaa sembuse mwanamke ambaye ni single mother.

Huwa nawashauri Vijana wadogo ambao ndio Kwanza wanaingia kwenye ndoa, wasiingie ndoani na single mother bali Watafute wanawake WA level zao ambao nao hawajawahi kuolewa.
Single mother wawaachie single father, au Wazee waliofiwa na wake zao, au wastaafu au wanaume wanaotaka kuongeza mke WA pili au watatu kuendelea.

Kanuni ni Ileile!
Mchanga Kwa mchanga
Komavu Kwa komavu
Zee Kwa zee au kuukuu Kwa kuukuu!
Sio mwanaume mchanga achukue mwanamke mkuukuu hiyo ni kutafuta matatizo tuu!

9. " Ninatetea na kusaidia Masikini na wanaoonewa, Mungu atamlipa"
Wengi imewagharimu, hakuna malipo ya hivyo ndugu zangu. Maisha ya mwanadamu ni Kama maisha ya wanyama Porini. Wapo swala wanaoonewa na kila mnyama na kila mahali watakapoenda wataonewa tuu. Ndivyo ilivyo Kwa maisha yetu. Kuna watu wapo Kwa ajili ya kuonea wengine, na wapo waliopo Kwa ajili ya kuonea.
Ukijifanya mtetezi unakuwa kundi la watakaoumizwa.
Aliyeumba hii dunia aliweka hivyo, na ndiye mwenye uwezo wa kuondoa na sio wewe.

Niliwahi kusema; Kama tunataka tusioneana Kama Watanzania basi itatupasa tuvamia mataifa mengine ili tuyapekekea uonevu wetu huko. Yaani tupunguze uonevu ndani ya nchi yetu.
Lakini huwezi kuuondoa uonevu pasipo kujua mahali pa kuupeleka.
Huwezi kuondoa Giza hapa ukadhani limeondoka hapana ulichofanya ni kulihamisha Giza kutoka kwako na kukupeleka sehemu nyingine.

Hata Mungu aliuondoa Uovu na Shetani mbinguni na kuutupa/ kumtupa Duniani.
Huwezi kuondoa takataka alafu usijue pakuzitupa utaishia kuchafua zaidi.

Kama hujanielewa basi.

Taikon nipumzike sasa!

Robert Heriel
Taikon wa Fasihi
Kwa sasa Dar es salaam
nakazia namba 9
 
4. " Ngoja nikupe/niolewe naye nitambadilisha au atabadilika"
Wengi wamejikuta wakiyaharibu maisha Yao Kwa ujinga na upuuzi. Unakuta limwanamke ni kahaba, halina sehemu za siri, karibu wanaume wote WA mtaani wanamjua sehemu zake nyeti. Ati unamuoa alafu unahama mtaa, wewe si CHIZI tuu! Malaya hata umpeleke mbinguni ataleta umalaya wake Kwa Malaika. Hujiulizi Kwa nini Huko mbinguni hawataki Malaya, hujiulizi! Sehemu haimbadilishi mtu.
Mtu Kama anatabia mbaya achana naye, tafuta wenye tabia nzuri mbona wapo.

Au unakuta limwanaume haliheshimu wanawake, linazalisha hovyo, linapiga wanawake, linatukana tukana hovyo matusi ya aibu, alafu Kwa ujinga wako unaolewa nalo Kwa matarajio ya kumbadilisha, unaumwa wewe! Mtu kujibadilisha mwenyewe ni shughuli pevu sembuse wewe umbadilishe.
Ndio yake baadaye linatukana wazazi wako, ndugu zako, wengine wanafikia hatua ya kutoka na Dada yako au Mama yako.
Alafu unamlaumu, unalaumu nini wakati wewe ndio ulikuwa mjinga!

Acha Shetani waoane na mashetani.
Malaika waoane na Malaika!
Majini Kwa Majini
Walevi Kwa walevi
Malaya Kwa Malaya n.k.
Swadakta!
Umenena vyema mkuu 😊
 
Kwa wale wasiopenda kusoma nyuzi refu najaribu kufupisha.

Mtoa mada anazungumzia mitazamo mbalimbali ambayo watu wakiwa nayo inaweza kuwagharimu maishani mwao.

Mitazamo hiyo huwakilishwa k2a njia ya maneno,na hayo maneno ni kama yafuatayo.

1. Kusoma sio kufanikiwa maisha(wanabeza elimu)

2. Uliona wapi pipi ikaliwa na maganda yake(wanahamaisha ngono zembe)

3. Siwezi kujenga na kuishi kijijini Mimi(wanabeza kununua maeneo maeneo ya mbali na mji)

4. Ngoja nikupe/niolewe naye nitambadilisha au atabadilika(wwnabeti kwenye ndoa)

5. Acha Nile ujanita nitaolewa tuu(wanakataa ndoa kwa kudhani wakiolewa hawatokula ujana)

6. Pesa hainunui furaha(wanajifariji kwa sababu hawana pesa au hawajazipata)

7.Dini sio tatizo(wanadhani dini haimati kwenye ndoa kumbe si kweli)
kila mtu atakuwa na dini yake, ilimradi tunapendana

8. Kuoa single mother sio tatizo, Inategemea na Mwanamke(wanajaribu kutia mkono gizani kuoa single mother)

9.. Ninatetea na kusaidia Masikini na wanaoonewa, Mungu atanilipa(sio kazi yako kutetea masikini ni kazi ya MMungu.


🙏🏾🙏🏾🙏🏾

MKUU nashukuru Kwa kutoa Muhtasari
 
Ahsante babaangu yaan huyu anajifanyaga kana kwamba neno lake ni sheria ,kanikwaza kutuponda single mom akat tuna bahat zetu,maisha hayana formula muache abwabwaje

Mimi nazungumzia 99/100 ndio maana nakuwa ninauhakika na nikisemacho.

Wewe unazungumzia 1/100 alafu unakuwa na uhakika nalo.

Nimeongea vile jamii yeti ilivyo, wewe Kama ni single mother hongera Kwa nafasi yako. Sijakusudia kukusema mabaya Ila nilikuwa nawatahadharisha Vijana wadogo wajiepushe na watu wa mfano wako. Hilo ndio kosa?

Kimsingi Mimi ninaamini katika falsafa ya;
Mpya Kwa mpya
Chakavu Kwa Chakavu
Jinga Kwa jinga
Single mother Kwa single Father au MGANE

Kanuni inasema kila mtu atapata wa kufanana maybe iweje kijana mpya achukue mwanamke aliyekwisha kuzaa,
Na iweje mwanamke mpya aolewe na jianaume zee?

Wewe Kama itakuuma utajua mwenyewe, wala sipo Kwa ajili ya kumfurahisha yeyote hapa, nipo Kwa ajili ya kufundisha wale wenye akili na Uelewa kama wangu.

Na Wale wanaotaka kuwa Kama Mimi.
 
mimi napinga hyo ishue sijui mzazi kama hajasoma basi na watoto hawatasoma au kuwa maskini...

wazazi wangu hawakusoma kbsa na tumezaliwa watoto wa 5 ..nataka nkuambie mpka sasa wote tuna degree kasoro mmoja ana diploma.

siioni point kweny hicho kipengele lbda ungesema kuwa inategemea na akili ya mtu.

***********

KUOA SINGLE MOTHER

aisee nina jamaa yangu ameoa binti ambaye ana mtoto .

hivi navyozungumza wana miaka 7 kweny ndoa na hata siku moja sijawahi kuoa wametofautiana kiasi ch kujuta kuwa pamoja.

siamini kwny baadhi ya vipengele ulivyoainisha.

UMESEMA KILA MTU ANA KAUJINGA KAKE NO MATTER HOW PERFECT MTU ANA JI-POTRAY KWA JAMII...

NAAMINI WW KAUJINGA KAKO NI HAKA KUANDIKA VITU UKIWA VERY SURE AS IF U HAVE STUDIED THE HUMAN PHYCHOLOGY TO THE EXTENT OF EXPERTISE.



this is bull shit!!!

Wewe Una degree lakini uwezo wako WA kuchambua mambo ni mdogo Sana.

Mimi nazungumzia 99/100 ndio maana ninaandika Kwa uhakika.

Wewe unazungumzia 1/100 alafu Kwa Uelewa wako mdogo utasema unauhakika.

Nafikiri hujui kitu inaitwa Exceptional Theory.

Unapoambiwa Jamii Fulani IPO hivi ujue watu wanangalia wengi wao, hao wachache hawawezi badili matokeo ya ukweli uliosemwa.
Au ukiambiwa Tanzania ni nchi iliyopo katika ukanda wa tabia ya nchi ya kitropiki ya Savannah ujue Maeneo mengi yanatabia hizo, sasa sio ufike Bukoba uone tabia za kiikweta useme Tanzania inatabia ya nchi ya kiikweta, utakuwa hamnazo na degree zako. Au ufike Dodoma ukute tabia ya nchi ya unusu jangwa alafu useme TANZANIA ni nchi ya unusu jangwa utakuwa hauelewi ukisemacho.

Mungu anaposema wanadamu wote wametenda dhambi na kupungukiwa na utukufu wake, na hakuna mkamilifu haimaanishi hakuna wanadamu wakamilifu ndio maana akamtaja Ayubu alikuwa mkamilifu na hajawahi kutenda dhambi, lakini hawezi kumtumia mtu mmoja kufanya hitimisho lake, Kwa kusema wanadamu wote hawanadhambi kisa mtu mmoja. Ila wengi ndio huingia katika hitimisho.

Au ukiambiwa watu wa sodoma na Gomora walikuwa waovu lakini mbona alikuwepo Lutu nduguye Ibrahimu. Lakini uwepo wa lutu hauna athari katika kubadilisha matokeo ya hitimisho tunalolijua mpaka hivi leo.

Mama na Baba wakiwa Masikini kaa ukijua watoto watakuwa Masikini, hiyo IPO hivyo
Kama itatokea wakawa matajiri hiyo tunaita Exceptional.

Sasa wewe unasema kwenu wote mnadegree na mmoja anadiploma licha ya kuwa wazazi wenu hawajasoma na ni Masikini, angalia na Ndugu wa Mama zako na Baba zako ipo hivyo, angalia majirani zako ipo hivyo, angalia jamii yako ipo hivyo.

Sio umezaliwa njombe huko Kwa vile kuna baridi ndio useme Tanzania ni nchi ya Baridi, watu watakuona hamnazo!

Kuhusu single mother, Mimi sijaandika vibaya nimeandika ukweli na kuweka jamii ikae sehemu yake.
Huwezi tumia mfano wa mtu mmoja kujumuisha na kuzima mifano elfu iliyopo kwenye jamii.
Huyo Rafiki yako ni moja Kati ya waliobahatika tuu Ila wengi WA Vijana wanalalamika katika Jambo hilo.

Ndio maana nikakuambia wewe ni Wale wanatumia 1/100
Sisi ndio wengine tunatumia 99/100

Sasa wewe na Degree yako kama hujui mambo madogo Kama haya itakuwa unashangaa mno.

Vinginevyo uniambie umetumia hisia zaidi katika hili, lakini kama ni akili basi huu mi mtihani
 
Kanuni inasema kila mtu atapata wa kufanana
Mluu mimi naomba nijenge hoja katika hii kanuni ya "kilw mtu atapata wa kufanana nae"

Neno kufanana ni neno pana ambalo hatutakiwi kulitafsiri kwa kulifinya hhata kidogo.

Kwa sababu neno kufanana upsna wake inaweza kuwa kufanana kiumri,
Inaweza kuwa kufanana kwa rangi
Inaweza kuwa kufanana kwa tabia
Inaweza kuwa kufanana kwa dini
Inaweza kuwa kufanana kwa idadi ya watoto mliokuwa nao
Inaweza kuwa kufanana kwa urefu.
Inaweza kuwa kufanana kwa unene.
Inaweza kuwa kufanana kwa hali za kipato.
Inaweza kuwa kufanana kwa makabila.
Inaweza kuwa kufanana kwa level za elimu
kufanana kwa idadi ya ndoa mlizowahi kufunga nakadhaalika.

Mkuu hizo zote hapo juu ni tafsiri zinazoingia kwenye neno kufanana.

So ni dhaahir kwamba utakapooa mtu ambaye mumefanana kwa jambo fulani maana yake kuna mambo mengi kinyume na hayo mtatofautina tu.

Mfano kijana ambae hajaoa anaoa mke ambaye hajawahi kuolewa kwa kudai tu anaoa mtu aliyefanana nae,

hapo huyu mtu katafuta mke anayefanana nae kwa mujibu wa idadi ya ndoa alizozipitia huko nyuma na akaona kwamba huyu hajawahia kuolewa kama yeye.

Lakini mbali ya kufanana hhuko hao watu kwa idadi ya ndoa za nyuma bila shaka watatofautiana kwa mambo mengine mengi

Mfano wa mambo ambayo wanaweza kutofautina ni hadhi ya familia,kipato,elimu,rangi,kimo,aina ya kazi,tabia n.k

Sasa kama hii fomula ingekuea inamata basi leo watu wasingeishi pamoja ama ingekuwa dunia yote ni taabu tupu kwa sababu hatufanani kwa yote na wala hatutofautiani kwa yote.

Nikirudi kwenye point yangu ni kwamba kuoa single mother sio tatizo kwa sababu huwenda mkatofautiana kwenye ishu ya idadi ya watoto
lakini mkafanana kwenye ishu ya tabia,kabila,levo ya elimu,hadhi ya familia na hayo mliyofanana yakawafanya muiishi vizuri kwenye ndoa kuliko hayo mliyotofautina.
 
Mluu mimi naomba nijenge hoja katika hii kanuni ya "kilw mtu atapata wa kufanana nae"

Neno kufanana ni neno pana ambalo hatutakiwi kulitafsiri kwa kulifinya hhata kidogo.

Kwa sababu neno kufanana upsna wake inaweza kuwa kufanana kiumri,
Inaweza kuwa kufanana kwa rangi
Inaweza kuwa kufanana kwa tabia
Inaweza kuwa kufanana kwa dini
Inaweza kuwa kufanana kwa idadi ya watoto mliokuwa nao
Inaweza kuwa kufanana kwa urefu.
Inaweza kuwa kufanana kwa unene.
Inaweza kuwa kufanana kwa hali za kipato.
Inaweza kuwa kufanana kwa makabila.
Inaweza kuwa kufanana kwa level za elimu
kufanana kwa idadi ya ndoa mlizowahi kufunga nakadhaalika.

Mkuu hizo zote hapo juu ni tafsiri zinazoingia kwenye neno kufanana.

So ni dhaahir kwamba utakapooa mtu ambaye mumefanana kwa jambo fulani maana yake kuna mambo mengi kinyume na hayo mtatofautina tu.

Mfano kijana ambae hajaoa anaoa mke ambaye hajawahi kuolewa kwa kudai tu anaoa mtu aliyefanana nae,

hapo huyu mtu katafuta mke anayefanana nae kwa mujibu wa idadi ya ndoa alizozipitia huko nyuma na akaona kwamba huyu hajawahia kuolewa kama yeye.

Lakini mbali ya kufanana hhuko hao watu kwa idadi ya ndoa za nyuma bila shaka watatofautiana kwa mambo mengine mengi

Mfano wa mambo ambayo wanaweza kutofautina ni hadhi ya familia,kipato,elimu,rangi,kimo,aina ya kazi,tabia n.k

Sasa kama hii fomula ingekuea inamata basi leo watu wasingeishi pamoja ama ingekuwa dunia yote ni taabu tupu kwa sababu hatufanani kwa yote na wala hatutofautiani kwa yote.

Nikirudi kwenye point yangu ni kwamba kuoa single mother sio tatizo kwa sababu huwenda mkatofautiana kwenye ishu ya idadi ya watoto
lakini mkafanana kwenye ishu ya tabia,kabila,levo ya elimu,hadhi ya familia na hayo mliyofanana yakawafanya muiishi vizuri kwenye ndoa kuliko hayo mliyotofautina.

Umenena sahihi!

Unapozungumzia ufanano hapo lazima watu waelekeane walau Kwa 70%
Sio tuu kisa dini moja ndio mmefanana.
Mpaka pawe na ufanano watu huangalia percentage kubwa ya ufanano ikizidi 70%-100 hao wanafanana

Ikiwa 40-60 wapo nusu Kwa nusu.

Nasisitiza zaidi, ikiwa kijana bado ni mdogo na ndio anataka kuingia kwenye ndoa afuate ushauri wangu, aoe kijana mwenzake ambaye Naye ni mdogo ambaye hajawahi kuolewa wala hajawahi kuzaa.

Siongei Kwa ubaya bali Kwa wema tuu.
Tena Kwa dunia ya sasa ushauri wangu ndio unanguvu zaidi na unapaswa kufuatwa Kwa sababu wanadamu wengi wameharibika.

Na Mwanamke Kama anamtoto ninamshauri atafute mume mkubwa na mwenye watoto kama yeye, au Mgane tena aliye na uwezo angalau.
Sio kuwapa Vijana wawatu shida na misongo ya mawazo
 
why does it feel like you have taken everything so personally? By the way mimi sio muandishi wa huu uzi, nimecomment tu so I don't see why you had to reply to my comment specifically.

Try not taking everything for their literal meaning, same article can carry a different concept/understanding based on each reader's perception. So take a deep breath and relax, life is too short to take everything so serious. Uwe na mchana mwema ndugu.

Tatizo baadhi ya watu ishu ikiandikwa Kwa jamii wanaichukulia personal.
Ni Sawa na mchungaji au Sheikhe awe anasema Walevi au wezi alafu mtu mwenye tabia hizo aanze kurusha mawe.

Yeye anazungumzia 1/100
Mimi nazungumzia 99/100
Alafu haoni tofauti
 
Hiyo namba 9 nilijaribu kuifanya kwakweli mpaka Leo imeniachia maumivu ingawa wakati mwingine Mungu Kuna watu kawaanda kwaajiri ya kutetea wanyonge ila huwa tunapigwa vita Sana, wapo ambao hutiwa uchizi, wapo ambao huuwawa na kujeruhiwa,kwenye maisha kama unajihisi unaamani ya kutosha basi usijaribu kuwachokonoa binadamu utajuata kuzaliwa utaiona Dunia Chungu

Usiwe Funza kwenye ridhiki za watu, watakuuwa Watu wabaya Sana.
 
Umenena sahihi!

Unapozungumzia ufanano hapo lazima watu waelekeane walau Kwa 70%
Sio tuu kisa dini moja ndio mmefanana.
Mpaka pawe na ufanano watu huangalia percentage kubwa ya ufanano ikizidi 70%-100 hao wanafanana

Ikiwa 40-60 wapo nusu Kwa nusu.

Nasisitiza zaidi, ikiwa kijana bado ni mdogo na ndio anataka kuingia kwenye ndoa afuate ushauri wangu, aoe kijana mwenzake ambaye Naye ni mdogo ambaye hajawahi kuolewa wala hajawahi kuzaa.

Siongei Kwa ubaya bali Kwa wema tuu.
Tena Kwa dunia ya sasa ushauri wangu ndio unanguvu zaidi na unapaswa kufuatwa Kwa sababu wanadamu wengi wameharibika.

Na Mwanamke Kama anamtoto ninamshauri atafute mume mkubwa na mwenye watoto kama yeye, au Mgane tena aliye na uwezo angalau.
Sio kuwapa Vijana wawatu shida na misongo ya mawazo
Jee mwanaume akiwa na mtoto halafu Binti Hana mtoto hii Iko okey
 
why does it feel like you have taken everything so personally? By the way mimi sio muandishi wa huu uzi, nimecomment tu so I don't see why you had to reply to my comment specifically.

Try not taking everything for their literal meaning, same article can carry a different concept/understanding based on each reader's perception. So take a deep breath and relax, life is too short to take everything so serious. Uwe na mchana mwema ndugu.
mwenzako kapanic aisee, yuko deep
 
Back
Top Bottom