Ukristo na Uislamu ni Dini mbili zisizofanana kabisa

Ukristo na Uislamu ni Dini mbili zisizofanana kabisa

Utume wa Musa ni karne nyingi sana, haikuwa rahisi kugundua moja kwa moja kama ni yeye ndio aliandika au watu aliokuwa nao
Sasa kama ilikuwa ngumu, kwanini yanafanyiwa kazi maandiko yake na huku mnajua wazi ya kuwa hakuna hakika yake ?
 
Labda hii watu hawajui. Leo si tunazungumzia dini zetu, let's go.

Kuna tofauti ya watu walioandikwa kwenye Biblia na Koran, hilo kwanza ulijue. Ibrahim unayemsoma kwenye Biblia si Ibrahim unayemsoma kwenye Koran.

Ibrahim wa kwenye Biblia baba yake anaitwa Terah ila wa kwenye Koran anaitwa Azar. Kasome Quran 6:74.

Kwenye Biblia wana Yesu, kwenye Koran wana Issa. Huyu Issa hakusulubiwa msalabani, ila Yesu alisulubiwa. Ndugu zangu, hawa ni watu wawili tofauti.

Kuna MUNGU (Almighty GOD) kwenye Biblia na kuna Allah kwenye Koran

So watu wa huku ni tofauti na wa kule. Kwa Biblia, Ishmael anajulikana kama mtoto wa kijakazi, ila kwa Kuran ni tofauti.

So mkikaa na kuzungumza, cha kwanza jueni mnawazungumzia watu wa sehemu tofautitifauti.

Mfalme Suleiman wa Bible alikuwa holy na baadaye akaanguka dhambini ila wa kwenye Kuran alikuwa anaongea mpaka na majini. So mkiwa mnawasoma watu wa kwenye Bible, msije kufikiri ni watu walewale wa kwenye Kuran, sio hivyo.

Musa wa kwenye Biblia alipewa Amri 10 za MUNGU, Musa wa kwenye Koran hakupewa amri 10 zozote.

Biblia inamtambua Samson kama jamaa aliyebarikiwa nguvu na uwezo wa kupambana na udhaifu wake ni kukata nywele zake, ila hakuna kisa cha namna hiyo kwenye Quran.

Biblia imeorodhesha mitume na manabii wengi wakitoka katika chimbuko la wayahudi, wakati Quran haiwazungumzii wayahudi katika chimbuko la unabii.

Ndio maana ukimsoma mtu wa huku, unaona tofauti kubwa na mtu wa kule.

Kuran imemtambua Adam kama mtume, ila kwa Biblia imemtambua kama mtu wa kawaida tu, mtu aliyeumbwa mwanzoni kabisa.

So mlifahamu hilo, sio mnakaa kwenye vijiwe vya kahawa mnabishana weeee meaningwhile watu mnaowazungumzia ni tofauti.

Historia ya Matukio ikitofautiana basi jua kabisa hao ni watu tofauti kabisa.

Hivyo ni vyema kila mtu abaki na anachokiamini, muda au siku ya kiama ndio ukweli utadhihirika nani alikuwa sahihi na nani alikuwa muongo.
Mhaya , Uko vizuri sana
 
Hakuna uthibitisho wa kutokuwepo Mungu kwa vile Hayupo kwa namna yoyote ile ya kuthibitishika yupo.

Huu ni uthibitisho tosha kwamba hayupo.

Ukiweza thibitisha yupo.
Hivi huwa unaelewa unachokiandika ? Unajua kama hakuna maana ?

Kitu ambacho hakijawahi kuwepo wewe unakijuaje ? Hivi una akili kijana ? Kisome ulicho kiandika uone kama kina maana.

Usiniambie nithibitishe ya kuwa hayupo wakati wewe umeshindwa kuthibitisha kutokuwepo na kutuambia unajuaje kutokuwepo kwa kitu ambacho hakijawahi kuwepo. Hivi unafikiri unachokiandika ?

Ili ujue kutokuwepo kwa kitu lazima kutanguliwe na kuwepo kwake au ujue kwa hakika kabisa ya kuwa hicho kitu hakipo.

Sasa wewe vyote huna. Halafu unakuja kuandika ujinga na utoto. Tetea hoja yako sio maneno matupu.
 
Hivi huwa unaelewa unachokiandika ? Unajua kama hakuna maana ?

Kitu ambacho hakijawahi kuwepo wewe unakijuaje ? Hivi una akili kijana ? Kisome ulicho kiandika uone kama kina maana.

Usiniambie nithibitishe ya kuwa hayupo wakati wewe umeshindwa kuthibitisha kutokuwepo na kutuambia unajuaje kutokuwepo kwa kitu ambacho hakijawahi kuwepo. Hivi unafikiri unachokiandika ?

Ili ujue kutokuwepo kwa kitu lazima kutanguliwe na kuwepo kwake au ujue kwa hakika kabisa ya kuwa hicho kitu hakipo.

Sasa wewe vyote huna. Halafu unakuja kuandika ujinga na utoto. Tetea hoja yako sio maneno matupu.
Wewe ndio huna akili unasema kitu kipo halafu huwezi kuthibitisha kipo?

Ukishindwa kuthibitisha kitu kipo ni kwamba hakipo.

Usicho elewa ni nini?

Wewe unasema Mungu yupo halafu huwezi kuthibitisha kwamba yupo?

Una puyanga puyanga tu kama mtu aliyerukwa akili.
 
Sijawahi kuwa na hasira na makafir ila makafir huwa wanasumbuliwa sana na dini ya haki kila siku lazima warushe uzi zaidi ya mmoja kuhangaika na uislamu ila hukuti muislamu mwenye muda huo,dini yetu imejotosheleza and we are very proud, hushangai hadi kufunga tu ramadhani pia makafir wanapna wivu kama kwaresma hakuna?
images (19) (1).jpeg
 
Wewe ndio huna akili unasema kitu kipo halafu huwezi kuthibitisha kipo?

Ukishindwa kuthibitisha kitu kipo ni kwamba hakipo.

Usicho elewa ni nini?

Wewe unasema Mungu yupo halafu huwezi kuthibitisha kwamba yupo?

Una puyanga puyanga tu kama mtu aliyerukwa akili.
Nimecheka sana, kuthibitisha uwepo wa Mungu ni jambo rahisi sana na jepesi mno. Na muda wowote nalifanyia.

Wewe soma ulichokoandika kisha uonyeshe kama kina maana, ukiweza kuonyesha ya kuwa kina maana, Mimi naacha kujadili huu mjadala.

Unapojenga hoja hakikisha unaweza kuitetea, huwezi kusema eti ushahidi au uthibitisho wa kuwa Mungu hayupo ni sababu hajawahi kuwepo ? Sasa swali linakuja kitu ambacho hakijawahi kuwepo wewe unajuaje kama hakipo au umekidiriki vipi ? Unaruka ruka.

Ili uone kati yangu Mimi na wewe nani anapuyanga, ni wewe ujibu maswali niliyokujibu kuuliza.
 
Qur'an Ina matatizo zaidi ya kiuandishi, iliandikwa au kukusanywa miaka zaidi ya 100 baada ya Mtume kufariki, wakati Biblia ilikuwa imekamilika au baadhi ya vitabu vyake viliandikwa miaka 30-40 baada ya Yesu kupaa. N walioandika waliishi naye; walimjua na kimfahamu Yesu.
Ndiyo maana Qur'an Waislamu and wengine hawaijui , kazi yao ni kufunga na kuswali na kusikiliza mawaidha tu. Hata waliotafsiri mengine wamepotosha baadhi ya maandiko. Mtu mwenybhekima atasoma na kuchambua. Mwislamunhna uhakika kam akifa atakwenda mbinguni, sababu hata Mtume mwenyewe hajui. Angalia Yesu alizungumza kwa ujasiri sana. " Nilipo Mimi nanyi mtakiwepo"
Qur'an imeandikwa miaka 100 toka kufariki mtume 😂.

Unaweza kuthibitisha hiki
 
Ukishindwa kuthibitisha kitu kipo ni kwamba hakipo.
Kushindwa kuthibitisha kitu kipo ni kwamba hakipo. Hii akili ya wapi kijana ? Yaani Falsafa na Logic zinawafanya muwe wavivu sana kufikiri.

Kushindwa kuthibitisha uwepo wa kitu Kuna sababu kadhaa miongoni mwa sababu ni kutokuwa na elimu juu ya kitu husika.

Lakini Kuna vitu vingine uwepo wake ni lazima, na unajithibitisha wenyewe. Mfano uwepo wa simu, unathibitisha uwepo wa Msanifu wa simu hiyo.

Sasa unaposema Mungu hayupo kwa sababu hakuwahi kuwepo, ho sentensi Haina maana. Sasa unajengaje hoja kwa kitu ambacho hakina maana ? Huu ni uzwa zwa.
 
Ni sawa Kuwa watu wawili wanaweza kuwa Jina zaidi ya Moja?
Au hilo unabisha?
Ndio inawezekana kuwepo watu wawili tofauti kabisa wenye jina linalofanana... Kitu kinachofanya watu hawa wawili kusemekana kuwa ni mtu mmoja ni kufanana kwa matukio au historia yao... Ila wasipofanana tu matukio basi hao sio mtu mmoja... Mfano Yesu na Issa ni watu wawili tofauti kabisa kwa sababu historia zao hazifanani.

Kwenye Biblia kuna watu wamekosewa mara nyingi sana Unakuta kwenye Agano jipya baba yake kaandikwa jina jingine na kwenye agano la kale baba yake jina jingine...
Taja hayo majina yaliyokosewa kwenye biblia. Au leta huo mfano

Hakuna Mtu aliyekuwa akiitwa Yesu na wala kwenye Majina ya kiyahudi hakuna jina Linaloitwa Yesu.
Yesu ni tafsiri tu ya kiswahili
Jina "Yesu" ni tafsiri ya Kiswahili ya jina la Kigiriki "Ἰησοῦς" (Iēsous), ambalo lenyewe ni tafsiri ya jina la Kiebrania "ישוע" (Yeshua) au "יְהוֹשֻׁעַ" (Yehoshua), linalomaanisha "Yahweh anaokoa" au "Yahweh ndiye wokovu."

Kama ilivyo kwa majina mengine ya kiebrania yaliyotafsiriwa kuja kiswahili kama Yohana, Musa, Petro na mengineyo. Kitu pekee kinachofanya jina hilo kudhiriisha huyo mtu ni mfanano wa historia na matukio yao
Sarai mkewe Abramu akamtwaa Hajiri Mmisri mjakazi wake, baada ya kukaa Abramu katika nchi ya Kanaani miaka kumi, akampa Abramu mumewe, awe mkewe."
Hajiri kipindi anaolewa alikuwa bado kijakazi, na hata hakupata haki zote kama mke. Hata mtoto wake hakufanywa mwana mkuu machoni pa Ibrahim badala yake Mke wake Sarah baada ya kuzaa ndio isaka akafanywa mtoto mkuu machoni pa baba.

Waislamu wao wanaelezea historia ya Ibrahim na Ismail katika muktadha tofauti. Na kufanya watu hawa wasifanane na wa kwenye biblia. Historia ya Abrahim wa biblia na Ibrahim wa Quran inaelezea watu hawa katika utofauti hivyo hawawezi kuwa mtu mmoja
 
Qur'an Ina matatizo zaidi ya kiuandishi, iliandikwa au kukusanywa miaka zaidi ya 100 baada ya Mtume kufariki, wakati Biblia ilikuwa imekamilika au baadhi ya vitabu vyake viliandikwa miaka 30-40 baada ya Yesu kupaa. N walioandika waliishi naye; walimjua na kimfahamu Yesu.
Ndiyo maana Qur'an Waislamu and wengine hawaijui , kazi yao ni kufunga na kuswali na kusikiliza mawaidha tu. Hata waliotafsiri mengine wamepotosha baadhi ya maandiko. Mtu mwenybhekima atasoma na kuchambua. Mwislamunhna uhakika kam akifa atakwenda mbinguni, sababu hata Mtume mwenyewe hajui. Angalia Yesu alizungumza kwa ujasiri sana. " Nilipo Mimi nanyi mtakiwepo"
Kwanini unaandika Uongo ?

Tuwekee tatizo Moja tu la kiuandishi ambalo lipo katika Qur'an.

Unaposema iliandikwa au kukusanywa, hapa umeonyesha wazi ya kuwa Qur'an huijui. Qur'an imeandikwa yote na kukamilika hata Mtume hajafa. Alivyo kufa Mtume ndio ikakusanywa na haikupita hata miaka 20. Hii miaka 100 umeipata wapi ?
 
Biblia inajumuisha maandiko yaliyoandikwa na waandishi mbalimbali katika kipindi tofauti cha historia ya dini ya Kiyahudi na Kikristo. Haijaandikwa moja kwa moja na nabii mmoja maalum. Badala yake, inajumuisha maandiko yaliyoandikwa na manabii, wataalamu wa dini, wanahistoria, na waandishi wengine, ambao waliandika kwa kuzingatia ufunuo, uzoefu wa kidini, na matukio ya kihistoria. Kwa mfano, katika Agano la Kale, vitabu vingi vinavyohusishwa na nabii kama vile Isaya, Yeremia, na Ezekieli, wanasemekana kuwa na sehemu ya maandiko yaliyojumuishwa katika Biblia. Katika Agano Jipya, vitabu vya Injili vilivyoandikwa na wanafunzi wa Yesu pamoja na barua za mitume ni sehemu ya maandiko yaliyojumuishwa katika Biblia.
kumbe biblia sio maneno ya yesu!...ahsante mkuu
 
wakati Biblia ilikuwa imekamilika au baadhi ya vitabu vyake viliandikwa miaka 30-40 baada ya Yesu kupaa. N walioandika waliishi naye;
Kitabu kiliandikwa ndani ya miaka hiyo.

Kisha utuambie hao walio andika ni kina nani na je walimuona Yesu ?
 
kumbe biblia sio maneno ya yesu!...ahsante mkuu
Wakristo Wana Historia tu na maisha ya Yesu ila hawana matini ya neno kwa neno ya Mafundisho ya Yesu.

Halafu walivyo pewa mtihani hawana muda wa kuyahakiki maandiko yao na kujua yapi sahihi na yapi sio sahihi. Wame kaa kaa tu.
 
Samahani Mkuu Unajua maana Ya Torati au Torah?
Kama unajua nadhani hautakuwa na shaka mtu akisema Musa alipewa Torati..
Katika ukristo torati ni kitabu kinachomuelezea Musa.... Musa wa biblia na musa wa Quran ni watu wawili tofauti....

Quran haielezei Amri kumi za MUNGU ambazo ni nguzo za ukristo. Mikasa inatofautiana uwezi kusema mtu huyo ni mmoja kaka
 
Ndiyo maana Qur'an Waislamu and wengine hawaijui , kazi yao ni kufunga na kuswali na kusikiliza mawaidha tu. Hata waliotafsiri mengine wamepotosha baadhi ya maandiko. Mtu mwenybhekima atasoma na kuchambua. Mwislamunhna uhakika kam akifa atakwenda mbinguni, sababu hata Mtume mwenyewe hajui. Angalia Yesu alizungumza kwa ujasiri sana. " Nilipo Mimi nanyi mtakiwepo"
Sasa kutokuijua ni jambo la mtu binafsi. Wewe Biblia unaijua au Wakristo wote wanaijua Biblia ?

Sababu hii ni elimu, lazima utoe juhudu kutaka kuijua ndio unaijua ukizembea huwezi kuijua.
 
Wakristo Wana Historia tu na maisha ya Yesu ila hawana matini ya neno kwa neno ya Mafundisho ya Yesu.

Halafu walivyo pewa mtihani hawana muda wa kuyahakiki maandiko yao na kujua yapi sahihi na yapi sio sahihi. Wame kaa kaa tu.
Mud aliwapiga fix mkajaa
 
Quran haielezei Amri kumi za MUNGU ambazo ni nguzo za ukristo. Mikasa inatofautiana uwezi kusema mtu huyo ni mmoja kaka
Nani aliwaambia ya kuwa amri kumi za Mungu ni nguzo za Ukristo ?

Shida yenu Ukristo ni dini isiyo kuwa na misingi yenyewe haikamiliki mpaka itumie maandiko yasiyo wahusu. Mfano wa kumbukumbu la Taurati. Taurati haikuletwa kwa Wakristo sababu Mpaka Yesu anaondoka hapakuwa na Ukristo duniani.
 
Back
Top Bottom