Ukristo na Uislamu ni Dini mbili zisizofanana kabisa

Ukristo na Uislamu ni Dini mbili zisizofanana kabisa

Labda hii watu hawajui. Leo si tunazungumzia dini zetu, let's go.

Kuna tofauti ya watu walioandikwa kwenye Biblia na Koran, hilo kwanza ulijue. Ibrahim unayemsoma kwenye Biblia si Ibrahim unayemsoma kwenye Koran.

Ibrahim wa kwenye Biblia baba yake anaitwa Terah ila wa kwenye Koran anaitwa Azar. Kasome Quran 6:74.

Kwenye Biblia wana Yesu, kwenye Koran wana Issa. Huyu Issa hakusulubiwa msalabani, ila Yesu alisulubiwa. Ndugu zangu, hawa ni watu wawili tofauti.

Kuna MUNGU (Almighty GOD) kwenye Biblia na kuna Allah kwenye Koran

So watu wa huku ni tofauti na wa kule. Kwa Biblia, Ishmael anajulikana kama mtoto wa kijakazi, ila kwa Kuran ni tofauti.

So mkikaa na kuzungumza, cha kwanza jueni mnawazungumzia watu wa sehemu tofautitifauti.

Mfalme Suleiman wa Bible alikuwa holy na baadaye akaanguka dhambini ila wa kwenye Kuran alikuwa anaongea mpaka na majini. So mkiwa mnawasoma watu wa kwenye Bible, msije kufikiri ni watu walewale wa kwenye Kuran, sio hivyo.

Musa wa kwenye Biblia alipewa Amri 10 za MUNGU, Musa wa kwenye Koran hakupewa amri 10 zozote.

Biblia inamtambua Samson kama jamaa aliyebarikiwa nguvu na uwezo wa kupambana na udhaifu wake ni kukata nywele zake, ila hakuna kisa cha namna hiyo kwenye Quran.

Biblia imeorodhesha mitume na manabii wengi wakitoka katika chimbuko la wayahudi, wakati Quran haiwazungumzii wayahudi katika chimbuko la unabii.

Ndio maana ukimsoma mtu wa huku, unaona tofauti kubwa na mtu wa kule.

Kuran imemtambua Adam kama mtume, ila kwa Biblia imemtambua kama mtu wa kawaida tu, mtu aliyeumbwa mwanzoni kabisa.

So mlifahamu hilo, sio mnakaa kwenye vijiwe vya kahawa mnabishana weeee meaningwhile watu mnaowazungumzia ni tofauti.

Historia ya Matukio ikitofautiana basi jua kabisa hao ni watu tofauti kabisa.

Hivyo ni vyema kila mtu abaki na anachokiamini, muda au siku ya kiama ndio ukweli utadhihirika nani alikuwa sahihi na nani alikuwa muongo.
Okay nilitaka kukujibu kwa hoja ila umemaliza vizuri..tuendelee kuishi na imani zetu maana hata hizi dini ni tofauti na imani za mababu zetu ni vile hatujui tmetupwa kwenye uwanja wa masbindano tusiyoyajua ila imani zetu ndizozitatuokoa kutoka katika vita na mashindano ya mataifa.
Niwaachie quiz ndogo but very wide
"Kwanini dini zimetoka kwa mataifa ya wazungu na kwanini sio taifa moja mean urabuni islam and European Christ?"
 
Kushindwa kuthibitisha kitu kipo ni kwamba hakipo. Hii akili ya wapi kijana ? Yaani Falsafa na Logic zinawafanya muwe wavivu sana kufikiri.

Kushindwa kuthibitisha uwepo wa kitu Kuna sababu kadhaa miongoni mwa sababu ni kutokuwa na elimu juu ya kitu husika.

Lakini Kuna vitu vingine uwepo wake ni lazima, na unajithibitisha wenyewe. Mfano uwepo wa simu, unathibitisha uwepo wa Msanifu wa simu hiyo.

Sasa unaposema Mungu hayupo kwa sababu hakuwahi kuwepo, ho sentensi Haina maana. Sasa unajengaje hoja kwa kitu ambacho hakina maana ? Huu ni uzwa zwa.
Wewe umeweza kuthibitisha Mungu yupo?

Unabaki kusema Mungu yupo ilhali wewe mwenyewe hujathibitisha Mungu yupo?

Unataka mimi nithibitishe Mungu hayupo ilhali wewe umeshindwa kuthibitisha yupo!

Hivi wewe unafikiri sawasawa kweli?

Nakwambia hivi ukishindwa kuthibitisha kwamba Mungu yupo, Ni kwamba hayupo kwa namna yoyote ile ya kuthibitishika yupo.

Ninyi wavaa kobazi mna matatizo ya akili.
 
Ina maanisha kila mtu aliyejisikia aliandika biblia?na haiwezi kuwa ni maneno ya mungu
Tuanzie hapo kwanza.... Kwani unamaanisha nini ukisema "Maneno ya Mungu"

Neno la mungu ni ujumbe wowote kutoka kwa Mungu kupitia kwa mtu yeyote.

Biblia iliandikwa kwa uwezo wa Roho mtakatifu kupitia manabii na wanafunzi wa yesu na wafuasi wake. Na maneno hayo hayakutungwa tu, bali yalishuhudiwa na watu... Nimekupa mfano Agano Jipya linakitabu cha Luka, Mathayo, Yohana ambao wote wameandika vitabu vyao lakini vinafanana maandiko... Ingekuwa kila mtu kajiandikia tu si maandiko hayo yanatofautiana!
 
Kwanini unaandika Uongo ?

Tuwekee tatizo Moja tu la kiuandishi ambalo lipo katika Qur'an.

Unaposema iliandikwa au kukusanywa, hapa umeonyesha wazi ya kuwa Qur'an huijui. Qur'an imeandikwa yote na kukamilika hata Mtume hajafa. Alivyo kufa Mtume ndio ikakusanywa na haikupita hata miaka 20. Hii miaka 100 umeipata wapi ?
Acha uongo
 
MKuu Hapa umedanganya Saana..
Hakuna Hata mwandishi mmoja kwenye Biblia ni authenification yaani hakuna aliyemuona yesu wala hakuna aliyeonana na waandishi wa Biblia..
Biblia Yote ni Pseudepigrapha...
Ni uhandishi kwa 3rd Part..
Na naweza kukuthibitishia hivyo..
Na Quran hivyo hivyo
Wewe ndio umepotoka.... Injili ya yesu agano jipya imeandikwa na Mathayo, Luka na Yohana ambao kimsingi ni wanafunzi wa Yesu na walikuwa nae nyakati nyingi na Biblia inasema hivyo

Kijana uje na facts za maana
 
Tuonyeshe alitupiga fix wapi ?
Unbelievers are enemies of Allah and they will roast in hell. - 41:14

Kama alisema ukweli kwa nini hapa aagize tena wauawe?

Fight unbelievers who are near to you. 9:123
 
Hakuna mfuasi hata mmoja wa Yesu aliandika Biblia..
Kama unaweza nithibitishie
Mkuu narudia tena Biblia ni muunganiko wa vitabu vilivyoandikwa na watu tofauti... Yani maandiko yao yaliunganishwa na kuitwa biblia, na biblia imeandikw nyakati tofauti tofauti, kuna agano la kale lililoandikwa kabla ya Yesu na yesu alilikuta, na kuna agano jipya ambalo limeandika injili ya Yesu kristo... Biblia imeandikwa sio kwa pamoja bali kwa kukusanya maandiko kutoka kwa manabii wa kale, wanafunzi wa yesu na wafuasi wa Mungu
 
Yeremia hakuwa nabii
Unazungumzia katika Dini gani? Ndio maana na sema uislamu na ukristo ni dini zisizofanana

Katika Ukristo, Yeremia alikuwa nabii katika historia ya Israeli na katika Biblia. Yeye ni moja ya manabii mashuhuri wa Agano la Kale, aliyejulikana kwa unabii wake na ujumbe wa kiroho aliowasilisha kwa watu wa Israeli.

Yeremia alizaliwa karibu mwaka 650 KK na alitumikia kama nabii kwa karibu miaka 40, akihubiri ujumbe wa Mungu kwa watu wa Yuda, hasa wakati wa kipindi cha kushuka kwa ufalme wa Yuda kwa mikono ya Wababiloni. Alikuwa na jukumu la kuonya watu kuhusu hukumu za Mungu na kuwahimiza kurekebisha njia zao ili kuepuka msiba.

Maisha na unabii wa Yeremia yameandikwa katika kitabu cha Biblia kinachoitwa "Kitabu cha Yeremia," ambacho kinaelezea jinsi alivyohubiri na kushuhudia kipindi cha kisiasa na kiroho cha taifa la Yuda. Yeremia alikuwa nabii aliyejitolea sana kwa Mungu, akifanya kazi yake kwa uaminifu licha ya upinzani na mateso aliyopata.
 
Kuna mwamba anaitwa Mfalme Constantine mkuu, mtawala wa kwanza wa dola ya Roma kuingiza Ukristo kwenye serikali ya Roma na yeye mwenyewe kuingia kwenye Ukristo. Huyu ndiyo master mind wa biblia, sehemu kubwa ya mpangilio wa vitabu vya agano jipya vilipangwa kwa maelekezo yake. Vitabu vya agano la kale vingi ni hadithi za maisha ya wayahudi na sheria za dini ya kiyahudi (Judaism).

Malengo ya mtawala Constantine katika kuunda biblia ilikuwa ni kutengeneza ushawishi wa kisiasa kupitia dini ya kiyahudi lakini waongeze udambwidambwi mwingine ili kunogesha kwa kuweka agano la kale na jipya. Baadhi ya wasomi na watafiti wa elimu ya dini wanaamini kwamba sehemu kubwa ya hadithi za agano jipya ni za kutungwa na watawala wa dola ya Roma kwa maslahi yao ya kisiasa katika kujenga ushawishi ulimwenguni.
Ndicho kilichopelekea Ukristo kuwa na madhehebu ambayo unayoyaona leo... Watu walianza kujitenga na kutengeneza madhehebu mengine baada ya kuona ukristo unapotoka kutoka katika asili yake halisi
 
Ndio maana wadudu(finyofinyo) wanaweza kujitokeza wenyewe tu kwenye Nyama bila kuhitaji muumbaji.
Hao wadudu unaowazungumzia ni funza waliotagwa na nzi.... Leo hii wewe ukioza ukiwa nje ya dunia uwezi kutoa funza kwa sababu kule hakuna nzi... Au nyama ukiifungia kwenye chombo ambacho mdudu hawezi kuingia basi nyama itaoza bila kuwa na hao wadudu... Huo sio muujiza
 
Wakati ulipokuwa mchungaji ulikuwa unamhubiri mungu yupi?
Ulitumia kitabu gani?
Mkuu Nyakati za zamani zikishapita Ndo kipindi ambacho mtu akikumbuka Hujiona Jinsi gani alivyokuwa Mjinga..

Kwa mfano Huwezk waambia Wana wa Israel wale vyakula Vilivyo Najisi ambavyo walikula wakiwa misri wavile hivyo hovyo wakiwa Kanaani wakati Mungu amewapa maagizo ya KOSHER
 
Wazungu wameshtukia kama walikuwa wanapigwa , hakuna mungu anabariki mashoga, hakuna mungu watatu na mungu hajawahi kuwa na mtoto, mungu gani anateswa na yeye anamlilia mungu? Does it make sense kweli
Ndio shida ya kutokusoma maandiko ya biblia... Huo ushoga hata kwenye Sodoma na Gomorrah kwenye biblia ulikuwepo ukapelekea mungu kushusha gharika la moto katika miji hiyo...

Kwa kifupi biblia ilishatabiri hayo matukio yote, yesu mwenyewe ananukuliwa akisema nyakati za mwisho watatokea manabii wa uongo, watu watatumia jina la MUNGU kufanya maovu... Kwa mkristo anayejua dini vizuri hawezi kushtuka, na hili unabii utimie lazima yatokee haya tunatoyashuhudia leo.

Kuhusu kuwa na watoto, hili nilishazungumzia... Sio kila baba ni mpaka akuzae... Kwani baba yako wa kambo kakuzaa, mbona unamuita baba... Uumbaji ni jambo tosha la kumuita MUNGU Baba mkuu. Bila yeye wewe si kitu.

Kuhusu kuteswa Yesu, ni jambo lililo kwisha kupangwa, yani Yesu alitabiriwa kuwa atakuja na atakufa msalabani kwa dhambi zetu ili tujue ni jinsi gani MUNGU anatupenda mpaka anamtoa Yesu msalabani ili tuweze kumuamini... Ule ni utabiri hata malaika Gabriel alimwambia Mariam mama yake yesu kuhusu habari za yesu
 
Hao wadudu unaowazungumzia ni funza waliotagwa na nzi.... Leo hii wewe ukioza ukiwa nje ya dunia uwezi kutoa funza kwa sababu kule hakuna nzi... Au nyama ukiifungia kwenye chombo ambacho mdudu hawezi kuingia basi nyama itaoza bila kuwa na hao wadudu... Huo sio muujiza
Kuna watu wako hai na wanaoza viungo vyao na kutoa wadudu.

Je hao wadudu wanaletwa pia na nzi?
 
Mkuu Nyakati za zamani zikishapita Ndo kipindi ambacho mtu akikumbuka Hujiona Jinsi gani alivyokuwa Mjinga..

Kwa mfano Huwezk waambia Wana wa Israel wale vyakula Vilivyo Najisi ambavyo walikula wakiwa misri wavile hivyo hovyo wakiwa Kanaani wakati Mungu amewapa maagizo ya KOSHER
Sijaona jibu la swali mkuu.
 
Kama haujui vitu uwe unauliza. Uslam na Ukristu ni kama Harrier na Lexus au Nissan Dualis na Nissan Qashqai.

Ngoja nikupe ufananio.

1. Amri kumi za MUNGU walizopewa wakristo ndizo hizo hizo wanazofata na kushika waislam. Kama unabisha niambie wapi sio kweli.

2. Dini zote zina siku maalumu ya ibada, yaani Jumapili na ijumaa.

3. Dini zote wanatoa sadaka siku za ibada na siku za kawaida wanahimizwa kufanya zaka na sadaka binafsi.

4. Dini zote zinatumia lugha za kigeni yaani English,latin na kiarabu

5. Dini zote zinahimiza kutenda mema na kupiga vita uovu na ubaya.

6. Dini zote zina muabudu MUNGU, na zinamlaani shetani.

7. Dini zote zina vitabu vikuu yaani Bible na Msaafu vyenye mafundisho na kanuni za kale zenye maudhui ya kisasa.

8. Dini zote zinaamrisha maisha kuanza na Ndoa.

9. Dini zote zina role model figure yaani Mitume Yesu na Mohamed.

Hapo ni kwa machache tu nimekulistia ili ujionee kuwa kuna vitu vingi hizi dini zipo common na zinamuingiliano.
 
Mathayo alikuwa ni nani kwa Yesu ? Je alimuona Yesu ?
Nimeshasema mara kadhaa mathayo ni mwanafunzi wa Yesu, sasa wewe ni mwanafunzi alafu ushindwe kumuona mwalimu wako.... Sio alimuona tu, bali alitembea nae na kula nae

Ebu uliza swali lenye mantiki
 
Back
Top Bottom