feyzal
JF-Expert Member
- Apr 20, 2016
- 7,683
- 15,128
Hii biashara niliiweza sema mauzauza yaliniangusha ila mbinu zangu ziliganikiwa sana mwanzo.Biashara ya mgahawa imetuumiza wengi sana.
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Hii biashara niliiweza sema mauzauza yaliniangusha ila mbinu zangu ziliganikiwa sana mwanzo.Biashara ya mgahawa imetuumiza wengi sana.
Yeah mkuu.Daah huenda ungeendelea sahivi ungekuwa mbali sana mkuu
Miwili kasoro ni biashara pekee haikuniangaisha mpaka nilishangaa ila zingine dah.Mafanikio ndani ya mda gani mkuu
Vipi kwa sasa mbona huendelei kuifanya?Yeah mkuu.
Ulikuwa unachukua mzigo kutoka wapi kupeleka wapi! Ulianza na mtaji kias gani?Miwili kasoro ni biashara pekee haikuniangaisha mpaka nilishangaa ila zingine dah.
kuna post nimeeleza uko juuVipi kwa sasa mbona huendelei kuifanya?
mzigo kutoka songea kuja dsm,nilianza na laki 1 na elfu 30 hapo kila kitu.Ulikuwa unachukua mzigo kutoka wapi kupeleka wapi! Ulianza na mtaji kias gani?
Ok!! nashukuru sana kiongoziSorry mkuu nilikua maporini huko network shida, kuhusu mtaji wa dagaa hata 500k unaanza kwasababu gunia la debe 10 linarange 180k-250k kutokana na upatikanaji wa dagaa unaweza kuanza hata na gunia mbili kama hupeleki mbali sana ila kama upo vizuri 1m ni mtaji mzuri zaidi, kuhusu usalama visiwani upo tuu cha muhimu fanya kilichokupeleka basi na usimkopeshe mvuvi hela ila biashara ya dagaa kwangu mimi changamoto lilikua somo kama unaanza tafuta kwanza wateja then ndo ingia mzigoni. Mwanza soko lipo kirumba ila pale hakuna biashara kuna madalali wapuuzi sana sikushauri.
Mkuu una madini,, ni biashara ipi hyo ilikua na ilikuaje tupe madini kdogoNaelewa hiyo situation. Mimi mwenyewe mkimbiaji mzuri wa biashara ila ili usikimbie biashara inabidi ujue sana mchezo wake ulivyo kabla hujaingia, usubiri kupata real experience uko.
Usiende na assumption kwamba kuna hela wakati hujui utaipataje. Usiende na assumption kwamba mzigo utatoka, mauzo yatakuwepo. Nenda na kutafuta profit sio kuonekana uko busy.
Mfano kwenye mgahawa umetumia kwa hesabu za haraka umetumia:
1kg mchele 2300
¼ nyama 2250
Viungo 1000
Mafuta 700
Misc. 250
Gas 1000
Jumla 7500.
Hapo ukiuza kama mtoa msaada unauza sahani tano @ 2000 unapata 10,000.
Gross profit ni 2500 yani hapa umeuza kama mpuuzi bado hujalipa vibarua. Sasa how comes unatumia 200,000 unapata 150,000?
Biashara ya wazi kabisa hii, ulijiuliza ukajua kwanini au uliamua ukimbie kama kawaida yako? Mimi biashara niliyokimbia naweza nikaiandikia kitabu kwanini niliacha, maelezo kibao. Na najua kwanini wanaoifanya hawawezi toboa, na sikukutana na yeyote aliyetoboa.
Embu itolee ufafanuzi hyo sentensi"Biashara yako iwe chini ya kampuni"[emoji106]Mimi ninachoona siyo Kila biashara inanafaa
+Nashauri biashara yako ya kwanza iendane na profession yako(una ujuzi mwingi zaidi hapa) mfano mfamasia afungue famasi etc
+Kingine it takes time aisee......inaonekana Tanzania kuchomoka ni wastani wa miaka mi tatu hivi
+Ukiweza kwepa Kodi kwepa sana ......hizi Kodi sijui malipo ya nn yanakula gharama sana
+Biashara yako iwe chini ya kampuni ...ni rahisi zaidi kudeal na kampuni kuliko jamaa wa mtaani tu.hata serikali inafanya kazi na makampuni
+Hakikisha biashara yako haiweke rehani mtaji wako(Kwa mfano kwenye kukopesha etc)
+Chagua biashara ambayo mteja analipa kwanza ndipo anapata huduma na siyo anapata huduma halafu malipo baadaye
Nawaza hivo tu....
Unafanya biashara gani na wapi tupe maujuziBiashara tamu jaman mimi hata uniambie uniajiri kwa 5m kwa mwezi sikubali ninamwaka wa 3 sasa, kwenye biashara na sijawahi juta
Biashara ya kununua mazao ya chakula ya msimu na kuuza. Ile ambayo kuna jamaa kakushawishi uanze sijui uende Mtwara sijui wapi Kusini uko.Mkuu una madini,, ni biashara ipi hyo ilikua na ilikuaje tupe madini kdogo
Kiufupi biashara yoyote yenye mahusiano na kilimo sio lelemama unatakiwa uwe na roho ya mamba.Biashara ya kununua mazao ya chakula ya msimu na kuuza. Ile ambayo kuna jamaa kakushawishi uanze sijui uende Mtwara sijui wapi Kusini uko.
Ile biashara inataka uwe na elimu kubwa na uzoefu wa mazingira na mazao husika. Ukiwa nje unaona ni mahindi tu, ukiingia field unakutana na mahindi yana namba sijui H30 na ngapi, mara punje ina pumba nyingi mara inatoa kiini kikubwa mara imepinda katikati hivyo gunia halina uzito sana.
Hujaja kwenye mpunga uko utakutana na mbegu zaidi ya nane na huwezi zijua kichwakichwa.
In short tuseme ni biashara ambayo unatakiwa uwe mtu wa kijijini kukekule, sio umetoka Kigamboni wajomba zako wanauza CD na mitumba eti unakurupuka kuuza mpunga. Utaijulia wapi kalima wangu, Zambia, salo, mbawa mbili na India?
Mpaka unakuja kujua mchezo umechoma mtaji tiyari. Ukija kuujua serikali inazuia mazao kuuzwa nje, msimu unaofuata serikali inanunua michele kutoka Pakistan bei inashuka sokoni.
Nilikaa hata msimu haukuisha nikala kona. Kila niliyekutana naye kachoka. Wenye faida ni wanaonunua na kuweka store. Sasa wewe na 10M yako ukiiweka store then ukafanye nini. Nikatimua mbio
Alikuwa anapigwa lakini hakuchunguza kabla ya kukata tamaa.Naelewa hiyo situation. Mimi mwenyewe mkimbiaji mzuri wa biashara ila ili usikimbie biashara inabidi ujue sana mchezo wake ulivyo kabla hujaingia, usubiri kupata real experience uko.
Usiende na assumption kwamba kuna hela wakati hujui utaipataje. Usiende na assumption kwamba mzigo utatoka, mauzo yatakuwepo. Nenda na kutafuta profit sio kuonekana uko busy.
Mfano kwenye mgahawa umetumia kwa hesabu za haraka umetumia:
1kg mchele 2300
¼ nyama 2250
Viungo 1000
Mafuta 700
Misc. 250
Gas 1000
Jumla 7500.
Hapo ukiuza kama mtoa msaada unauza sahani tano @ 2000 unapata 10,000.
Gross profit ni 2500 yani hapa umeuza kama mpuuzi bado hujalipa vibarua. Sasa how comes unatumia 200,000 unapata 150,000?
Biashara ya wazi kabisa hii, ulijiuliza ukajua kwanini au uliamua ukimbie kama kawaida yako? Mimi biashara niliyokimbia naweza nikaiandikia kitabu kwanini niliacha, maelezo kibao. Na najua kwanini wanaoifanya hawawezi toboa, na sikukutana na yeyote aliyetoboa.
Asante kwa Madini Mkuu.Uvumilivu
Biashara yoyote inahtaji uvumilivu,unaweza ukahisi hamna wateja eneo ulilofungua biashara lakini si kweli wateja wapo na ni hao hao unaowaona wanapita nnje ya biashara yako.
TABIA ZA WATEJA
Wateja wana tabia ya kusikiliziana,anataka aone nani anakuja dukani kwako ndio na yeye aje, Usijali wala usikate tamaaa...
endelea na Promo utawaona mmoja mmoja anakuja.
"Chelewa kufunga Wahi kufungua" Huu ni moja ya Uchawi namba 1 kwa biashara Mpya.
Amini nakwambia kuna biashara unapatia location,mtaji na kila kitu ukiona wateja hawaji jua kuna eneo unakosea usikimbulie kuifunga na kubadlisha.
Usiuze bidhaa 1 dukani kwako hata kama n huduma,usitoe moja toa na zngine za kuvuta wateja.
Binafsi naweza fungua Barber Shop ya kunyoa mtu 20,000 lakini katka branding zangu matangazo na sticker ntaongezea
VIFURUSHI NA VOCHA ZINAPATIKANA
watu watakua wanakuja nunua vocha na vifurushi,wale wateja wasikiliziaji watajua wenzao wanaingia kunyolewa kumbe mtu kafata vocha,akija kunyoa siku ananyolewa vizuri Ana NASA.
Mengi ya kuandika,ila kama mtaji unao usiruhusu biashara ikushinde.
Mkuu wewe unafanya biashara gan na umetoa kais gan? Au umeandika tii ili watu waingie mkenge?Business inahitaji nidhamu pamoja na commitment ya kutosha.. ukiachana na hayo Kuna watu Wana vichwa vya biashara. Yaani hata auze pipi automatically anatoboa tu.. wewe mwenzangu na Mimi unaweka mamilioni unaambulia patupu.
Vipo vingi vya kufanya na unaweza kutoboa kimya kimya bila hata kushirikisha nguvu ya Giza. Muhimu cheza na location, misimu, aina ya watu wanaokuzunguka, angalia nini ukifanya unakuwa free zaidi halafu jikite kwanza hapo hatua nyingine itafata mumo kwa mumo