Ulioa au kuolewa ukiwa na umri gani?

Ulioa au kuolewa ukiwa na umri gani?

Hao hawajawahi kuwa na point mbele yangu mkuu kwa sababu nimeshatangulia nalijua pori liko vipi,hata mimi nilikuwa na akili kama zao lakini zenye tafakuri kubwa na nilikuwa najua kwamba uanaume ni ku-face realty.

Mimi kwa kiasi kikubwa maisha yangu nimelelewa na binamu yangu (Mungu Mwenyezi amrehemu) ndoa yake ilivunjika nikiwa naiona mwaka 2001 wakiwa na miaka 12 ndani ya ndoa na nazijua shida alizopitia hadi anakufa but still nimekuja kuoa na nina maisha tulivu standard kwa umri nilio nao.

Nasisitiza shida za ndoa zipo na raha za ndoa zipo mtu asiseme ndoa mbaya kisa amefumaniwa na mkewe nae huyo mkewe akalipiza kisha akajaza vijana sumu kwamba ndoa ni mbaya,hasha.

Sasa hivi una miaka mingapi? Kwenye ndoa?

Pengine inakusubiria ufikishe miaka 12 ndio ndoa ivunjike!!!! Laana inasaka 12 years
 
Kipindi ukiwa na umri gani ndo uliamua KUOA AU KUOLEWA?

✨Ulimpata wapi your partner?


HAPO ONGEZEA ULIMPATA WAPI HUYO MWENZA WAKO?
Nimeolewa mwaka 1975,
Nikiwa na Miaka 20
Nilimpata kanisani, sio mchungaji ila tukikutana kanisani, tukapenda, mpaka sasa ndoa ya Miaka 48 na wajukuu 10, mjukuu WA mwisho yupo form 4
Mungu NI mwema
 
28 yrz wife 25 tupo mwaka wa kumi with 3 kids,tuna jumla ya miaka 18 ya kimahusiano.humo mna miaka ya uvulana na usichana na miaka ya mahusiano serious kisha kumi ya ndoa na familia,namshukuru Mungu kwa hili.

Juzi weekend nilikuwa namtania wife namwambia tumeshatoboa sisi ni wa kufa na kuzikana alifurahi sana maana yeye ndiye aliyetengeneza mazingira ya ndoa sikuwa tayari wakati huo but leo (japo sijawahi kumwambia na sitakaa nimwambie kwa sababu zangu binafsi) namshukuru kama siyo yeye kuna vitu naona kabisa nisingekuwa navyo.

Vijana oeni,maisha ni haya haya kila mtu ameandikiwa kikombe chake cha mwenzako hutakinywa na yeye chako hatakinywa msi-copy matukio ya ndoa mkayafananisha huko ni kudanganyana.

Hongera mkuu kwa experience nzuri ila kwenye ushauri tutachanganya na zetu pia 🙏🏽🙏🏽
 
Nimeoa nikiwa na miaka 27 mke wangu akuwa na 24, mpk sasa nina miaka ya ndoa 7 na nmebarikiwa watoto watatu mungu ni mwema nafuraia maisha ya ndoa sana. Wito wangu kwa vijana wa kataa ndoa msipende kusikiliza maneno mara eti kataa ndoa hapana ndoa ni jambo zuri sana tafuta mtu ambae mnaendana fanyeni maisha yangu ni ayo tu.

Sent from my vivo 2015 using JamiiForums mobile app
 
28 yrz wife 25 tupo mwaka wa kumi with 3 kids,tuna jumla ya miaka 18 ya kimahusiano.humo mna miaka ya uvulana na usichana na miaka ya mahusiano serious kisha kumi ya ndoa na familia,namshukuru Mungu kwa hili.

Juzi weekend nilikuwa namtania wife namwambia tumeshatoboa sisi ni wa kufa na kuzikana alifurahi sana maana yeye ndiye aliyetengeneza mazingira ya ndoa sikuwa tayari wakati huo but leo (japo sijawahi kumwambia na sitakaa nimwambie kwa sababu zangu binafsi) namshukuru kama siyo yeye kuna vitu naona kabisa nisingekuwa navyo.

Vijana oeni,maisha ni haya haya kila mtu ameandikiwa kikombe chake cha mwenzako hutakinywa na yeye chako hatakinywa msi-copy matukio ya ndoa mkayafananisha huko ni kudanganyana.
Hongera sana mkuu
 
Mwanangu nitapokonya kutoka kwa mama yake, na matunzo nitampa mama yangu kwaajili ya mwanangu.

Sent from my vivo 2015 using JamiiForums mobile app
yaani Mama yako kakulea wewe na ndugu zako kawafikisha ukubwani mkiwa na afya njema, badala mumpe muda sasa na yeye apumzike uzeeni kwake na ninyi ndiyo mumtunze, ndiyo kwanza mnaenda kumbebesha tena jukumu la kulea wajukuu..!!

afadhali basi iwe imetokea mambo ambayo yapo juu ya uwezo wenu hiyo inaeleweka, lakini unaenda 'kumpokonya' mtoto kwa mama yake unampelekea hekaheka tena bibi wa watu, hivi huwa hamna huruma na wazazi wetu..?
 
Back
Top Bottom