Ulipokea vipi Msiba wa Hayati Magufuli?

Ulipokea vipi Msiba wa Hayati Magufuli?

Kawaida tu tena ilikua night kama saa tano au sita nipo ferry napiga tangawizi na stori kibao kwenye kativii basi akaja dem toka kwenye pantoni wakati tunaenda geto akaniambia rais kafa sikumtilia maanani nikasema stori zote nitapata kesho jioni kwenye kahawa na kweli jioni nikaenda kupata stori nzima na yale niliokua siyajui japo sikutilia maanani stor za kahawa uongo mwingi na ferry kila mtu unamuhofia kuropoka watu wanajichunga sana
 
Nilikua nipo Lodge na Mwanadada Fulani mzuriiii amenona mapaja kwelikweli.

Nikiwa nmeshapiga kamoja, tupo kwenye mchakato wa Cha pili, TV ikiendelea ,ghafla Samia huyo!!.

Kiukweli hata kupiga shooo nilishindwa, Moyo ukatetemeka, nguvu siku nazo huku machoz yananitoka, na ukiwaa yaaan kulala sikulala na shooo ikaishaaa Asubuhi tukasepa.



Kwann niliumia ? Niliwaza ,hivi ndivo tunarudi kwenye Tanzania ya miaka 10 nyuma?....japo zilikua nihisia, ila ndio kumbe nilikua kweli
 
Sikua na huzuni yoyote wala furaha kwasababu hakukua na ukaribu wowote kati yangu na yeye wala uhusiano wa kindugu, ugumu na wepesi wa maisha yangu haujawahi kutatuliwa na rais yoyote zaidi ya Nyerere aliyetupatia huduma za afya na elimu bure.

Maisha ni mapambano yako mwenyewe na sio rais I aliyoko madarakani, hats yeye Magufuli alihimiza sana watu kufanya kazi,kwa maana nyingine hakutaka watu wamtegemee yeye.
 
Alikuwa ni kiongozi mbaya kupindukia. Japo alikuwa muuaji na katili, kiasi cha kila mpenda haki kupendelea kutokuwa na kiongozi wa namna ile, lakini nilisikitika kupokea taarifa za kifo chake. Ni jambo jema mwovu aendelee kuishi, ajutie uovu wake au abadilike na kuuchukia uovu wake wa kale. Nilipoisikia habari ile, nilishtuka, nikaamka. Nilikaa kimya kwa dakika, nikajawa na simanzi. Maana kwa kweli pamoja na kuwaaumiza watu wengi, haikuwahi kutokea akilini mwangu kufikiria kuwa, aheri afe. Ningependelea aondoke kwenye uongozi lakini siyo kufa. Lakini basi kwa kuwa ilitokea, mapenzi ya Bwana yalitimia kwa kipimo cha hekima yake Mungu.

Vyovyote iwavyo, kifo chake ni fundisho kubwa kwetu tulio hai. Cha kujiuliza, sisi tunafanya nini tofauti na uovu wake? Tunafanya nini sambamba na mazuri yake, hata kama yakiwa machache? Kuna wengine ni fundisho kubwa kwao mara mbili zaidi maana wakati wa utawala wake, walitenda uovu mwingi wakiamini yupo wa kuwalinda kwenye uovu wao.

Wapo waliomkufuru Mungu, hata wakamwita Magufuli ni Mungu, wengine wakasema ni zaidi ya Yesu, na wengine wakasema eti Mungu amshukuru Magufuli. Na wote sasa hivi wamebakia kama kondoo wasio na mchungaji.

Hii ilikuwa ni kufuru kubwa. Mbaya zaidi hata marehemu mwenyewe hakuwakemea. Mwalimu Nyerere alipopambwa kupita kiasi, alimaka na kusema, 'mmeniita mchongameno nimenyamaza, mmeniita Haambiliki nimenyamaza, lakini hili la Musa, kuniita Musa, hapana, sitaki kusikia'. Yaani Mwalimu aliona kuwa yeye hafanani wala kumkaribia kwa chochote nabii Musa aliyewaongoza wana wa Israel toka utumwani Misri. Nabii Musa alikuwa mwanadamu, lakini mwalimu aliona bado Nabii Musa ni mkubwa mno kuweza kufananishwa naye. Marehemu alilinganishwa na Mungu, yeye akakaa kimya. Lilikuwa kosa kubwa.

Kifo chake ni fundisho kwetu kuwa Mungu hana ushirika na mwanadamu yeyote katika Umungu wake. Tunafundishwa kuwa Mungu hana mwanzo wala mwisho. Kifo hiki kilitufundisha kuwa hata uwe na nini, wewe bado ni mwanadamu, unafanana na wanadamu wenzako katika kuzaliwa na kufa.

Tuendelee kuomba, Mungu atujalie hekima ya kujifunza kupitia kifo hiki, na wala kifo hiki kisitufanye kuzidi kumkosea yeye Mungu au wanadamu wenzetu.
Umenikumbusha Yule mzee aliposema..tumuombe Mungu amshukuru Magufuli..
 
Aisee ninakumbuka ulikuwa wakati wa UE aisee nililia mtu mzima nikapoteza ufanisi siku hiyo kwenye mtihani.it was the saddest day.
Wewe ulikuwa na upendo zaidi ya mama janet aliyekuwa anatabasamu siku mwili unaagwa chato?
 
Wakati tukiwa kwenye kipindi cha Kumbu kumbu cha musiba wa hayati Dr John Pombe Magufuli Rais wa JMT awamu ya tano tuambizane wewe ndugu yangu huko uliko taarifa za musiba ulizipataje na ulipokea vipi msiba mzito wa kuondokewa na rais wa Tanzania?

Ilikuwa ni habari ya kusikitisha kwa Watanzania kwa mara ya kwanza kumpoteza Rais Kipenzi akiwa madarakani na pengine Afrika mashariki nzima.
Ilikua ni habari ya kusikitisha lakini kwa muda mchache tulisahau na kumshukuru Mungu kwa kutuletea mkombozi wa Tanzania Rais Samia Suluhu aliyekuja kuimboa Tanzania kiuchumi, kisiasa na kijamii
 
Wakati tukiwa kwenye kipindi cha Kumbu kumbu cha musiba wa hayati Dr John Pombe Magufuli Rais wa JMT awamu ya tano tuambizane wewe ndugu yangu huko uliko taarifa za musiba ulizipataje na ulipokea vipi msiba mzito wa kuondokewa na rais wa Tanzania?

Ilikuwa ni habari ya kusikitisha kwa Watanzania kwa mara ya kwanza kumpoteza Rais Kipenzi akiwa madarakani na pengine Afrika mashariki nzima.
Mbona huulizinwa MKAPA ambazo ulikuwa wa ghafla?
Wa huyu tuliambiwa na Waziri Mkuu kwamba yuko fiti anafanya shughuuli kama kawaida! mnamtaka aende Kariakoo mmuone huko?
Daah hii ni wiki Moja mbaya sana!
 
Alikuwa ni kiongozi mbaya kupindukia. Japo alikuwa muuaji na katili, kiasi cha kila mpenda haki kupendelea kutokuwa na kiongozi wa namna ile, lakini nilisikitika kupokea taarifa za kifo chake. Ni jambo jema mwovu aendelee kuishi, ajutie uovu wake au abadilike na kuuchukia uovu wake wa kale. Nilipoisikia habari ile, nilishtuka, nikaamka. Nilikaa kimya kwa dakika, nikajawa na simanzi. Maana kwa kweli pamoja na kuwaaumiza watu wengi, haikuwahi kutokea akilini mwangu kufikiria kuwa, aheri afe. Ningependelea aondoke kwenye uongozi lakini siyo kufa. Lakini basi kwa kuwa ilitokea, mapenzi ya Bwana yalitimia kwa kipimo cha hekima yake Mungu.

Vyovyote iwavyo, kifo chake ni fundisho kubwa kwetu tulio hai. Cha kujiuliza, sisi tunafanya nini tofauti na uovu wake? Tunafanya nini sambamba na mazuri yake, hata kama yakiwa machache? Kuna wengine ni fundisho kubwa kwao mara mbili zaidi maana wakati wa utawala wake, walitenda uovu mwingi wakiamini yupo wa kuwalinda kwenye uovu wao.

Wapo waliomkufuru Mungu, hata wakamwita Magufuli ni Mungu, wengine wakasema ni zaidi ya Yesu, na wengine wakasema eti Mungu amshukuru Magufuli. Na wote sasa hivi wamebakia kama kondoo wasio na mchungaji.

Hii ilikuwa ni kufuru kubwa. Mbaya zaidi hata marehemu mwenyewe hakuwakemea. Mwalimu Nyerere alipopambwa kupita kiasi, alimaka na kusema, 'mmeniita mchongameno nimenyamaza, mmeniita Haambiliki nimenyamaza, lakini hili la Musa, kuniita Musa, hapana, sitaki kusikia'. Yaani Mwalimu aliona kuwa yeye hafanani wala kumkaribia kwa chochote nabii Musa aliyewaongoza wana wa Israel toka utumwani Misri. Nabii Musa alikuwa mwanadamu, lakini mwalimu aliona bado Nabii Musa ni mkubwa mno kuweza kufananishwa naye. Marehemu alilinganishwa na Mungu, yeye akakaa kimya. Lilikuwa kosa kubwa.

Kifo chake ni fundisho kwetu kuwa Mungu hana ushirika na mwanadamu yeyote katika Umungu wake. Tunafundishwa kuwa Mungu hana mwanzo wala mwisho. Kifo hiki kilitufundisha kuwa hata uwe na nini, wewe bado ni mwanadamu, unafanana na wanadamu wenzako katika kuzaliwa na kufa.

Tuendelee kuomba, Mungu atujalie hekima ya kujifunza kupitia kifo hiki, na wala kifo hiki kisitufanye kuzidi kumkosea yeye Mungu au wanadamu wenzetu.
Nikifupisha habari yako kwa neno moja ni kuwa
ulifurahi
 
Back
Top Bottom