Unadhani kwanini vijana wanapenda sana kuajiriwa serikalini kuliko kampuni binafsi?

Unadhani kwanini vijana wanapenda sana kuajiriwa serikalini kuliko kampuni binafsi?

Watu wanaogopa
Sekta binafsi asiporidhishwa tu na hali ya kibiashara nchini kesho yake press conf anafunga biashara au kuuza kwa mtu mwingine 😀😀😀😀
 
Asikwambie mtu Ajira ya serikali ndio ajira hizi zingine za sector binafsi ajira iko mikononi mwa mtu, siku yoyote na muda wowote unaweza kupoteza ajira, mbaya zaidi inapofika kipindi ambacho mkataba wako wa kazi ukiwa unakaribia kuisha muda wote unakuwa na mawazo endapo kama mwajiri atakuongezea mkataba au lah, sasa hizi pressure huwa za kifala sana kwa wafanyakazi. Ajira ya maana ni ya serikali tu huo ndio ukweli.
 
Ukiwa na uoga wa maisha Serikalin panakufaa Ila sidhani Kama naweza kushawishika kufanya kazi serikalin labda vitengo nyeti. Zipo sehemu private Zina ubabaishaji lakini siyo zote. Yapo mashirika yamenyooka na hayana ubabaishaji na mshahara ukiingia unakuta akaunti imenona siyo mshahara wa serikali pesa ya nyanya
 
Ukiwa na uoga wa maisha Serikalin panakufaa Ila sidhani Kama naweza kushawishika kufanya kazi serikalin labda vitengo nyeti. Zipo sehemu private Zina ubabaishaji lakini siyo zote. Yapo mashirika yamenyooka na hayana ubabaishaji na mshahara ukiingia unakuta akaunti imenona siyo mshahara wa serikali pesa ya nyanya
Mkuu private ni pasua kichwa najua sasa hivi huwezi kukubali kwasababu unakula keki ya taifa ila mabadiliko ya uongozi yanaweza ya kakufanya ukachukia kazi anakuja boss mpya anasema fulani simtaki bila sababu unaanza kuundiwa zengwe,

mara unatia kampuni hasara na kusingiziwa kila kosa hata kama hujafanya wewe wakati mwingine mpaka wafanyakazi na viongozi wanaweza wa kakutenga na kuku dharau vile vile mkataba wa short term kwa private ndio chanzo cha ajira kuwa chungu mpaka umnyenyekekee mtu ila kila mtu na choise yake mkuu kikubwa mpunga uingie kwenye account.
 
Ajira ni serikalini tu ,huko kwingine ni uhuni tupuuuu...

Ndio maana vijna tunapigania ajira serikali ,hata kama mshahara ni laki 3 ....

Ukishaingia mwenye mfumo wa serikali ni security kubwa Sana ,huwezi fukuzwa kazi kirahisi kabisa ...!
 
Private upate makampuni yanayojielewa kama TCC,Twiga Cement,TBL au International NGO utakula maisha sana.ila private kwenye vijikampuni uchwara vya wachina au wahindi hapo hakuna kitu aisee.
 
Je nini mtazamo wako juu ya wahitimu wengi wa vyuo kupenda kuajiriwa serikalini ilhali kampuni binafsi ndio zinazoongoza kwa kulipa mishahara minono ?

Mtu yuko radhi kuacha kazi kwenye kampuni binafsi yenye mshahara wa 1.5M na kwenda kupoke basic salary ya 900k serikalini

Je ni job security au fursa za mikopo ukiwa unafanya kazi serikalini ?

Au kuna sababu nyingine ya msingi inayopelekea vijana kupenda kuajiriwa serikalini ?

Embu
Uukiniuliza hili swali nakujibu simple. Vijana ni wavivu pili upigaji last kwa mtu binafsi huwo muda hupati. End
 
Private upate makampuni yanayojielewa kama TCC,Twiga Cement,TBL au International NGO utakula maisha sana.ila private kwenye vijikampuni uchwara vya wachina au wahindi hapo hakuna kitu aisee.
Ndugu hata hayo makampuni uliyoyataja bado chenga tu Ndugu, kuna jamaa yetu alikuwa TBL alipatwa na redundancy yeye na wengineo wenye umri kuanzia 45+ katika hiyo kampuni, na hao wote walikuwa skilled labour, kitu kingine hayo mashirika hayana zile pension za kila mwezi baada ya kustaafu, ukishapewa chako biashara ndio imeisha sasa hali hiyo ajira ya serikali bado ni bora sana ina faida nyingi zinazoonekana na zisizo onekana.
Wabbilah Tawafiq
 
ni bora yaogopeshe kuliko kufanya kazi sekta binafsi, sekta binafsi muda wowte na saa yoyote unakalia kuti kavu. AJIRA NI SERIKALINI, AJIRA NI SERIKALINI, AJIRA NI SERIKALINI............................................................
Kwahiyo mi ninayetaka kuacha ualimu nikapige mishe zingine means sitofanikiwa?
 
Kwahiyo mi ninayetaka kuacha ualimu nikapige mishe zingine means sitofanikiwa?
Ndugu nakushaori usiache hiyo kazi ya ualimu wala usidanganyike na wala usidanganywe hata kidogo kuacha kazi, cha msingi unaweza kupiga hizo mishe zingine huku ukiwa unaendelea na ajira yako. Wakati tuko kanda ya ziwa miaka minne nyuma kuna mwalimu kama wewe aliachaga kazi serikalini akaingia katika NGOs ya watu wa Wamerekeni hapa na pale lile shirika likafunga ofisi kulingana na sera za mwendazake hiyo ilikuwa mwaka 2020, mpaka hivi tunavyokwambia jamaa bado yupo kwenye kuti kavu na uamuzi aliouchukua kipindi kile mchizi anajuta sana. Kiongozi kama umeajiliwa serikalini usiache kazi eti ukajiajiri, usiache kazi serikalini eti uende sekta binafsi huo ni uchawi Comrade nakuhusia tulia hapo ulipo usishawishike kuacha kazi serikalini, wewe uliona ajira gani mwajiliwa hata kama akipatwa na maradhi ya muda mrefu ya kumfanya ashindwe kufika ofisini lakini bado ataendelea kulipwa ili mradi kuwe tu na taarifa zake katika ofisi husika je kwa sekta binafsi hili suala linawezekana? ajira ni serikalini, ajira ni serikalini, namalizia tena AJIRA NI SERKALINI......................................................................................
 
Nyumba nimejenga japo ndogo je hata biashara ikinishinda nina cha kuogopa? Au sababu ni mwanamke bas siwez kufight nikasuccess
AKILI KICHWANI MWAKO KIONGOZI LAKINI MENGI NILIYOYAONA KWA WATU WA KARIBU SIWEZI NIKAMSHAURI MTU AACHE AJIRA YA SERIKALI KWA KIPINDI HIKI YANGU NI HAYO..............................................................................
 
Back
Top Bottom