Unatafuta msaidizi wa nyumbani? Kwa Million 100 jipatie Optimus Robot kutoka kwa Elon Musk

lindo anaweza kuingia

nilijaze chaji likae huko nje lipambane na vibaka lionje joto ya jiwe
Mengine yanalima shambani ila likiishiwa chaji linadondoka chini na jembe inabidi ukaliokote ujitwike kichwani ukalichaji
 
Sasa hivi wanamezeshwa akili ila ipo siku wataanza kutumia akili zao kufanya maamuzi yao wenyewe. Au kichaa mmoja atayabadili akili yaanze kufanya anachotaka yeye.
Hata mimi nimewaza ivo vipi haya Maroboti yakawa mengi let say Tanzania yakawa kama maroboti 50m...ghafla yakahakiwa mfumo wao si itakuwa kisanga.
 
Kama linauzwa $30,000 ambayo ni Million 100. Kwanini maboss wasinunue.

Maana kumuajiri mtu kwa mshahara wa Mil 3 kwa mwezi, na bado jumamosi na jumapili na sikukuu haji. Na akija anafanya kazi saa 2 hadi saa 9 tu.
Hapo bado hajakuibia. 😂
 
Sasa hivi wanamezeshwa akili ila ipo siku wataanza kutumia akili zao kufanya maamuzi yao wenyewe. Au kichaa mmoja atayabadili akili yaanze kufanya anachotaka yeye.
Si hamuyachaji tu au mnatoa betri tuone yatafanya nini? Mnakuza na kuhofia vitu vya hovyo sana.
 
Hayachoki wapi au mi sijui. Si yanatumia umeme au yanachajiwa? Labda mi nipo zama za giza sijui yanajiendeshaje.
 
Hata wafanye nini bado hawawezi shindana na binadamu uumbaji wa Mungu.

Hao majamaa hayana ule mguso wa kibinadamu ambao ni muhimu sana.
 
Sijui tumejiandaaje kuanza kucompete ajira na aga maroboti.

Msijisumbue, Tanzania hawana UWEZO WOWOTE juu ya maroboti, nani atoe $30,000?

Bakhresa ana wafanyakazi 100, anawalipa 15,000 kwa siku
100 x 15,000 x siku 360(mwaka 1) = TSHS 540,000,000
Marobot 50 x $30,000(tsh 82,500,000) = tsh 4,125,000,000
Hujaweka

Matengenezo​
Services​
replacement​
Haya mabo hayahusu Tanzania achen Propaganda​
 
Watu tutapigwa chini vibaya mno.....marobot yawekwe ndani, Elon tuonee huruma baba.
 
Huyu jamaa anapenda Kiki sana ni Copy paste maarufu tu. Robot kama haya yamejaa kibao Japan, Taiwan na Asia ya mbali ila husikii hizi kelele, na sio Trial yanafanya kazi kabisa, Hotel zake zilikua maarufu sana wakati wa Korona.
 
Wanitengenezee roboti la kulima eka zangu kumi za mahindi, naliacha huko shambani baada ya siku mbili najua atakuwa ameshamaliza shamba lote kwa kulima
 
Si hamuyachaji tu au mnatoa betri tuone yatafanya nini? Mnakuza na kuhofia vitu vya hovyo sana.
Technolojia inazidi kubadilika mkuu, sasa hivi kuna robot ikifika percent fulani inaenda yenyewe kwenye charging port yake na kutulia, (Nitakuwekewea video clip).

Nadhani unafahamu 'Wireless reverse charging' juzi hapa china kampuni ya xiaomi wamezindua wireless charger inakaa ofisini nyinyi simu zenu zinajichaji moja kwa moja huku mkitumia.

Inshort wewe wakati ukitaka kufikiri hivyo wao tayari washachukua control ya kila kitu ingawa isiwe wakati wetu lkn kuna jarida moja 60's liliwahi kuandika ipo siku moja mtu ataweza kuongea huku akitembea na simu isiyo na wire kwani ilionekana kama kitu cha kusadikika na wengine walikufa kabla ya kushuhudia hilo likiwezekana.
 
Ni fursa hiyo kwa kaka Mbowe na CHADEMA kununua maroboti kwa ajili ya kufanya maandamano maana watanzania ni waoga zaidi ya kunguru, hata kudai haki zao tu hawawezi.
 
Huyu jamaa anapenda Kiki sana ni Copy paste maarufu tu. Robot kama haya yamejaa kibao Japan, Taiwan na Asia ya mbali ila husikii hizi kelele, na sio Trial yanafanya kazi kabisa, Hotel zake zilikua maarufu sana wakati wa Korona.
Nilikua najua yanafanya zile programmed activities kumbe ya aweza ata kusikiliza mfano ukase a nataka bia aina flani na likaenda lenyewe kuleta?

Basi jamaa kilichom’beba ni press.
 
Kwanini sisi hapa JF tusimpe heshima ya Dokta Elon Musk🤣😂
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…