Upangaji wa Makao Makuu Dodoma. Nani aliamuru Ikulu izungukwe na Makazi ya Watu?

Upangaji wa Makao Makuu Dodoma. Nani aliamuru Ikulu izungukwe na Makazi ya Watu?

Ni vile watu hawaelewi utendaj kazi wa Intelijensia.

Hao unaosema ni Wananchi wamezunguka IKULU una uhakika ni Wananchi/Raia wa kawaida?.

Humo kuna Nyoka kama wote.

Mbili huwezi rundika Viongoz ktk sehem moja ni risk kama itafanyika shambulio la Anga.

Tatu huna uhakika kama RAIS anakaa IKULU.. sio kila muda anakuwepo pale.

Nne Chamwino imewekwa strategically kwa kuzingatia Environmental factors.

Tano RAIS mwenyewe hapapendi Dodoma, hivyo hakaagi sana huko.

Sita, Wazo lako la kuwa DODOMA ni mji wa kisenge senge nimekubaliana na ww, ule mji ni wakipumbavu lingebaki Bunge tu kule. Tunadhalilisha Taifa.
 
Watanzania kama sio kukosa exposure basi ujinga unatutesa sana na kuna siku utakuja kutugharimu sana

Wiki iliyopita nilikuwa Dodoma nimeangalia namna ya Jiji la Dodoma lilivyopangwa na kusema kweli nimesikitika sana.

Hii nchi kuna siku yatatukuta ya Haiti wahuni wanaingia kwenye makazi ya Rais kufanya umafia na kutokomea bila hata kukamatwa alafu ndo tunakuja kuunda tume kujua tatizo kumbe hatushughulishi akili zetu kwa wakati sahihi.

Nani aliyesema Chamwino kwenye Ikulu pazungukwe na Makazi ya watu binafsi? Waliopendekeza hili hawakuona hatari yake?

Nani alipendekeza Mji wa Serikali ujengwe Mtumba na sio Chamwino?

Kwa sehemu nyingi duniani makazi ya Rais yanazungukwa na Ofisi Kuu za Serikali na hata makazi ya viongozi wa Kiserikali na sio watu binafsi. Kujenga mji wa Serikali sehemu tofauti alafu kuweka ikulu kwenye makazi ya watu hawakuona hili linaweza kuleta matatizo siku moja?

Kiuhalisia Mji wa Serikali na Makazi ya Viongozi wa Serikali vyote vilitakiwa kuwepo Chamwino na kuzungukwe na kambi za Jeshi ila kwa Dodoma haya hayajafanyika

La kunichekesha zaidi ni Jengo la Bunge. Hili Jengo lipo sehemu ya ajabu kabisa. Nje kuna vibanda vya chips na makazi holela. Inafika hadi wabunge wanakosa sehemu za kupaki magari na mwishowe kusababisha msongamano mkubwa sana kipindi cha Bunge.

Kusema kweli kwa watu wasio na akili wataifurahia Dodoma ila kwa wenye akili na wanaoona mbali Dodoma itakuja kuligharimu sana Taifa siku za mbeleni mbeleni!
Makazi yenyewe ya raia waliozunguka ikulu hayajaplaniwa vizuri yani yamejengwa hovyo wasije wasumbua baadae kuanza kuwatoa.
 
Ni vile watu hawaelewi utendaj kazi wa Intelijensia.

Hao unaosema ni Wananchi wamezunguka IKULU una uhakika ni Wananchi/Raia wa kawaida?.

Humo kuna Nyoka kama wote.

Mbili huwezi rundika Viongoz ktk sehem moja ni risk kama itafanyika shambulio la Anga.

Tatu huna uhakika kama RAIS anakaa IKULU.. sio kila muda anakuwepo pale.

Nne Chamwino imewekwa strategically kwa kuzingatia Environmental factors.

Tano RAIS mwenyewe hapapendi Dodoma, hivyo hakaagi sana huko.

Sita, Wazo lako la kuwa DODOMA ni mji wa kisenge senge nimekubaliana na ww, ule mji ni wakipumbavu lingebaki Bunge tu kule. Tunadhalilisha Taifa.
Kuhusu wananchi wa kawaida kuzunguka maeneo yale hilo nina uhakika nalo maana nilikuwa maeneo yale . Hata Halmashauri ya Jiji wamepima viwanja na wanaviuza kwa watu mbalimbali maeneo yale.

Mbili ni safe zaidi kwa Ofisi Kuu ya nchi kuzingukwa na Ofisi za Serikali na Makazi rasmi ya viongozi na watumishi wa serikali kuliko kuwa otherwise.

Nchi nyingi duniani nilipofika iko hivyo. Ikulu ipo karibu na Bunge, Wizara na Makazi ya wafanyakazi wa Serikali na viongozi
 
Kwa mawazo yako kitendo cha Ikulu kuwa karibu na Makazi ya Watu ndiyo inakuwa rahisi kuingilika? Hivi ulishajaribu kwenda hapo Ikulu?

Taratibu za kuingia pale ni ngumu mno sasa sijui wewe hofu yako ni ipi? Au Rais hatakiwi kuonekana na Wananchi wa kawaida? Kama suala ni usalama wa Rais akiwa Ikulu bado upo kwani ulinzi wake ni mkubwa mno..
 
D
Kwa mawazo yako kitendo cha Ikulu kuwa karibu na Makazi ya Watu ndiyo inakuwa rahisi kuingilika? Hivi ulishajaribu kwenda hapo Ikulu?

Taratibu za kuingia pale ni ngumu mno sasa sijui wewe hofu yako ni ipi? Au Rais hatakiwi kuonekana na Wananchi wa kawaida? Kama suala ni usalama wa Rais akiwa Ikulu bado upo kwani ulinzi wake ni mkubwa mno..
Dar tu naskia Manji alijenga jengo karibu na ikulu naskia Serikali walichukua floo zote za juu.

Kwa Dar ikulu yetu imezungukwa na Ofisi za Serikali na nyumba ambazo zinasemwa ni za watumishi wa Serikali/ za serikali.

How comes Dodoma inapangwa tofauti?
 
Mkuu Yoda heshima kwako bora ibaki hapo hapo gharama za hama hama ni kubwa sana mkuu
Sasa hivi ni kama serikali iko Dodoma na Dar es Salaam na hali inaweza kudumu hata miaka 30 ijayo au ikawa ya kudumu milele. Kwenye maisha ni vyema pia kujiepusha na kitu kinaitwa "sunk cost fallacy".

Sunk cost fallacy ni ile hali ya kuogopa kuachana na mpango, uamuzi au biashara fulani hata kama kufanya hivyo ndio uamuzi wa busara zaidi hali ilipofika kwa sababu tu umewekeza sana katika huo mpango/uamuzi/biashara.Badala yake unabaki tu ukifariji kisaikolojia kuendelea labda ipo siku faida au tija itapatikana huku ukizidi kupoteza, kuumia au kupata hasara.
 
Kuhusu wananchi wa kawaida kuzunguka maeneo yale hilo nina uhakika nalo maana nilikuwa maeneo yale . Hata Halmashauri ya Jiji wamepima viwanja na wanaviuza kwa watu mbalimbali maeneo yale.

Mbili ni sehemu zaidi kwa Ofisi Kuu ya nchi kuzingukwa na Ofisi za Serikali na Makazi rasmi ya viongozi na watumishi wa serikali kuliko kuwa otherwise.

Nchi nyingi duniani nilipofika iko hivyo. Ikulu ipo karibu na Bunge, Wizara na Makazi ya wafanyakazi wa Serikali na viongozi
Mfn Nchi gani?

Hapo ni swala muda, kwanza kbs majengo na baadhi ya shughuli hazitafanyika maeneo hayo ikumbukwe kuwa IKULU yenyewe haijakamilika 100% ktk swala la ujenzi
 
D

Dar tu naskia Manji alijenga jengo karibu na ikulu naskia Serikali walichukua floo zote za juu.

Kwa Dar ikulu yetu imezungukwa na Ofisi za Serikali na nyumba ambazo zinasemwa ni za watumishi wa Serikali/ za serikali.

How comes Dodoma inapangwa tofauti?
Kupanga ni kuchagua, sidhani kama hilo suala lipo kikanuni au kisheria kwamba Ikulu lazima zifanane!

Kama suala ni usalama wa Rals hata Ikulu izungukwe na Makazi ya Watu hakuna athari yoyote na kama kuna njama dhidi yake hata azungukwe na Kambi za Jeshi au Ofisi za Serikali bado haitasaidia.

Wewe mwenyewe kuna sehemu kwenye maandishi yako umekiri kuwa Rais wa Urusi alikoswakoswa licha ya Ikulu yake kuwa mazingira ambayo wewe unaamini ni salama.
 
Mfn Nchi gani?

Hapo ni swala muda, kwanza kbs majengo na baadhi ya shughuli hazitafanyika maeneo hayo ikumbukwe kuwa IKULU yenyewe haijakamilika 100% ktk swala la ujenzi
Marekani, Urusi, China, India Nigeria, Rwanda na Afrika Kusini
 
Architecture inaweza ikawa sio hoja sana. Ila kupima viwanja na kuwauzia watu maeneo karibu na ikulu kabisa itakuja kutufanya tuwe tunawaza vizuri siku si nyingi sana
Usanifu nao ni hoja, si sawa kujenga ofisi kuu ya Serikali katika karne hii kwa sanifu ya Seraseni ya mwaka 1922. Tunashauriwa kutunza majengo ya zamani, lakini katika ujenzi mpya ni vema kuangalia wakati wa Sasa na ujao
 
Fire Fire Fire my comrade,all I hear is facts. Let's keep spitting facts later generations gonna understand.
 
Usalama kwa kiongozi mkuu unapaswa kuwa sawa mahali popote pale
Hata pale Chamwino usalama upo licha kuwa na Makazi ya Watu, alafu lazima utambue kuwa kile unachokiona karibu na Makazi ya Watu ni ukuta ambao ni zaidi ya kilometa 20.
 
Back
Top Bottom