UPDATES: Elimu kwa umma ambayo ni jambo la msingi na endelevu
Tukisoma Kitabu cha Nukuu za Kiswahili za Mwalimu uk 150

Mwl JK Nyerere aliwahi kusema,


" Tumwombe sana MWENYEZI Mungu atusaidie kuishi ili TUJIFUNZE MAMBO MENGI ZAIDI juu ya Maajabu yake katika Ulimwengu huu TUNAOISHI na tujipatie faida za maisha hayo sisi wenyewe, watoto wetu na nchi yetu."





M M KAHINGA
🙏🏽🙏🏽🙏🏽🙏🏽🙏🏽
 
Sawa tafuta na Ile nukuu anayosema Wazanzibar wanazingua sababu ya Udini sababu ya Uislamu, ukiipata Audio itapendeza zaidi
 
Utamaduni wa kufuatisha akili za watu wajinga tuuangamize ili elimu sahihi iisaidie nchi kusonga mbele

Nakumbuka Tarehe 20/06/2024 Mheshimiwa Elibariki Kingu Mbunge wa Jimbo la Singida Magharibi
Alisema. Ukweli lazima tuuseme na Umuhimu wa kuusema Ukweli ni kuweza kulisaidia Taifa ( ili) liweze kuwa na Mtazamo ambao ni sahihi. Kutoka Mtazamo ambao sio sahihi ambao unaweza ukajengwa katika mazingira tu ya kijamii , kiuchumi, ama mazingira mengine ya kisiasa.

Mwisho wa kunukuu Mheshimiwa Rais Dkt Samia Suluhu Hassan Akiwa katika Kongamano la Wana Tasnia ya habari Nakumbuka Tarehe 18/06/2024 Alisema Mimi Binafsi siamini katika Ukiritimba wa Mawazo au fikra .
Yaani Monopoly of ideas Ninaamini katika kusikiliza Sauti na Mawazo ya ( watu) wenzangu
Mwisho wa kunukuu

Tutoe fikra na Mawazo yetu kwa Mujibu wa katiba ya Jamhur ya Muungano wa Tanzania 1977 toleo 2005 uk 23 Ibara 18(a) na 19(1) kwa Maana ya Uhuru wa Mawazo huku tukizingania ibara 09 a b f na h.
Ilani ya CCM ibara 110(c) bila kuacha uk 01 ibara 04. Vitendo vya kutokujali katiba na Maandiko ya kimfumo limekuwa tatizo sugu ndani ya nchi na kupelekea watu Wajinga kuwapotosha Makundi ya Watu walio wengi ambao wanatakiwa kusaidiwa ili wawe na Elimu ya kujielewa wanufaike na Taifa lao

Askofu Dkt Benson Kalikawe Bagonza Askofu wa KKKT Dayosisi ya Karagwe Akitoa hotuba Tarehe 08/03/2022
Alisema Utamaduni wa kutojali Katiba una nguvu kuliko nguvu ya Katiba . Mazoea ya kutoheshimu Katiba yana nguvu kuliko Katiba. Mwisho wa kunukuu Leo hii nchi kwetu Matatizo mengi tuliyo nayo yametokana na Changamoto nyingi zikiwemo za Ukosefu wa Elimu sahihi ya kila sekta.

Matokeo ya Changamoto hii yamewaibuwa Watu Jasiri wasiokuwa na Elimu ya kile wakisemacho . Hao ndiyo Baadhi wanajiita Wanasiasa kwa kigezo Cha kuvaa sare za kisiasa tu huku vichwani wakiwa zero . Hapa nikimaanisha hawajuwi lolote lile kuhusu ilani , katiba , Kanuni miongozo na Taratibu. Watu Hawa hawana research yeyote Zaidi ya Ujasiri wa kujiropokea na kutengeneza wafuasi kwa njia za hila na Rushwa.

Makada wenye Uelewa wamekuwa kimya huku wakishuhudia upotoshaji ukiendelea. Hatuwezi kukubali Mambo haya. Ni lazima Sasa Wapotoshaji tuwape Elimu. Shekhe Amir Farid. Akitoa Mawaidha. Akiwa Wilaya ya Chake Chake Huko Pemba. Nakumbuka Tarehe 20/06/2024 Alisema, Pahali popote Wewe Tafuta Elimu tu. Elimu ndizo zinazotufungua Mwanaadamu.

Elimu ndiyo inayokupa Mwanga. Mwisho wa kunukuu. Viburi na Jeuri ya Baadhi ya Viongozi miongoni mwetu kumepelekea haki kupotea miongoni mwetu huku tukijifanya ni watu Waumini wenye Imani ya kimungu huku tukipendelea watu na kuwabagua wengine kwa Hali zao kiasi kwamba hata wakipaza sauti hatuwasikilizi kwa vile viburi vilivyo tufunika na kutusahaulishia Uwepo wa maamrisho ya Mwenyezi Mungu kiasi kwamba hatuna hofu Tena ya kuwa ipo siku tutahesabiwa.

Shekhe Othman Khamis Juma Imam Masjid Mtoro Nakumbuka Tarehe 29/03/2022 Alisema Mwambie Mwenyezi Mungu katika mema ya Dunia akuondolee kiburi Mwenyezi Mungu katika mema ya Dunia hii ( mwambie) akuondolee kiburi Na badala yake (muombe ) akupe Unyenyekevu Wote walio nyenyekea Wakajishusha
Wakaondoa kiburi hao ndiyo waliofanikiwa ( Kiroho) Binaadamu wote wanampenda mtu Mnyenyekevu
Na Binaadamu wote hawampendi ( mtu) Mwenye kiburi Kila mtu akikutambuwa unacho kiburi , Kiwe Cha Mamlaka , Utawala Kiwe Cha pesa Kiwe Cha nguvu mwilini ( Kiburi) kiwe kitakavyokuwa Madhali ni Jeuri

Ni kiburi Basi ( ujuwe) watu hawakupendi Hata Kama unaona ( watu wako ) wanakupigia makofi ukiwepo ujuwe ( ni watu) waongo TU. Hakuna Mwenye Mapenzi na Wewe hapo. Mwisho wa kunukuu Niwaombe viongozi wenye Tabia hizi Msione hatusemi Roho zetu zinaumia Ila tunawapigia makofi tu ilimradi Mambo yaende
Lakini lazima mjuwe Mnavyowalinda Waliojipatia vyeo kinyume na Matakwa ya Utaratibu Watu wasio stahili kwa Mujibu wa Maandiko ya kimfumo Mnapowalinda mjuwe mnachuma dhambi kubwa Na Tabia hizi hatuzipendi

Na mnapowaandama mafukara na watumishi wa Umma huku mkiwalinda waovu wengine Tabia hizi hatuzipendi na tunakuwa hatuwapendi hata Ninyi kwa Tabia hizo chafu zilizo Kinyume na Viapo vyenu.
Tukatae Sasa kuwalea watu wasiokijuwa Chama Cha Mapinduzi kwa kuwaondoa kwenye vyeo walivyo vikalia huku wakiwa hawajuwi lolote lile kuhusu ilani Katiba Kanuni miongozo na Taratibu zetu.

Sisi Kama Chama tunaunda Serikali na kuisimamia Serikali kutekeleza yaliyo ndani ya ilani Tunapokuwa na Viongozi ndani ya CCM waliovalia Kama makada wakiwa hawaijuwi ilani wala katiba, Kanuni miongozo na Taratibu Tujiulize Tabia hizi ni za Uzalendo au Sio za Uzalendo!?! Tusome katiba ya CCM 1977 toleo 2022 ibara 5(4) ili kwenda kusoma Kitabu Cha Binaadamu na Maendeleo Cha Mwalimu Julius Kambarage Nyerere uk 17-21 kwa msisitizo wa kuyaishi maneno na kuyafanyia kazi Nakumbuka Tarehe 28/05/2024 Mheshimiwa Paul Christian Makonda Mkuu wa Mkoa wa Arusha Alisema Nilisha sema hivi siku zote , siku zote , tusijitetee na kuwatetea (watu) walio tuingiza mahali pabovu.

Hatuwezi kulindana kwa Makosa tuliyoyafanya Mwisho wa kunukuu Padre Dkt Charles Kitima Katibu Mkuu wa Baraza la Maaskofu Tanzania (TEC) Nakumbuka Tarehe 16/06/2024 Alisema Tukubali tuanze kuandaa mfumo wa kujirekebisha Kama tunataka tujirekebishe, tujirekebishe Kama tumeona kitu hakiendi sawa Sisi tutasema
Kwa sababu itakuwa ni laana mbele ya Mwenyezi Mungu Mnajuwa watu wanaenda kutumbukia shimoni halafu (wenye macho) mnakaa kimya Hapana Hapana

Mwisho wa kunukuu

Kidumu Chama Cha Mapinduzi

Mathias Mugerwa Kahinga

🙏🏿🙏🏿🙏🏿🙏🏿🙏🏿🙏🏿🙏🏿
 
WATU WAZALENDO WANA AKILI NA HOFU YA MUNGU
WATU WASIO WAZALENDO
HAWANA HOFU YA MUNGU
WAKIONA HATA MAOVU YANAFANYIKA
WAO HUJITIA UCHIZI KUYATETEA

Tuisaidie nchi kwa kusema sema Ukweli hata tukitishwa vipi Sisi Tuufie Ukweli tunaouamini ili vizazi visizidi kupotoshwa na kupotezwa kifikra.
Mchungaji Richard Hananja
Akiongea na Wana habari
Nakumbuka Tarehe 17/02/2024
Alisema
Na Mimi siachi kusema hata watu watukane vipi ujuwe.
Hata wasemeje
Hiyo ( kusema saana) kufuru
Mimi Niko tayari hata kufungwa lakini nitasema
Kufuru ( nitaianika )kabisa yaani.
Kufuru ( ifahamike)
Mwisho wa kunukuu
Nakumbuka Tarehe 17/06/2021
Mheshimiwa Steaven Masato Wasira
Mkongwe wa Siasa za Kitanzania
Ex Waziri
Akifanya Mahojiano na Zumari
Alisema
Nitumie nafasi hii kuwaambia Watanzania kwamba Mwalimu ( Julius Kambarage Nyerere) alikuwa anathamini saana neno linaloitwa Ukweli
Ukimueleza Ukweli na ukadhibitisha kwamba Ukweli ule unaousema unatoka moyoni na kwamba unawatetea watu ambao Shida Yao inaonekana dhahiri Mwalimu ( Nyerere) alikuwa anaheshimu Sana Ukweli.
Mwisho wa kunukuu
Tusome Katiba ya CCM 1977 toleo 2022 ibara 5(4)
Mheshimiwa Nape Mosses Mnauye
Waziri wa habari Mawasiliano na Technology
Akiwa katika Kongamano la Majadiliano ya Ripoti ya Tume ya Haki Jinai
Nakumbuka Tarehe 19/07/2023
Alisema
Tukosoane turekebishane tutoe maoni bila ( ya) kutukanana.
Mwalimu ( Julius Kambarage Nyerere) alitufundisha
Tushindane kwa hoja bila kupigana.
Kosoeni
Toeni maoni ( ila) Msidharirishe Wala msitukanane
Mwisho wa kunukuu
Tuendelee kupeana Elimu iliyo sahihi ili kuiendea Mitazamo iliyo sahihi yenye Ucha Mungu usio na mionekano ya hila za Kinafiki.
Watu wenye akili
Na Machawa wasio na akili
Huhitilafiana Mitazamo kuhusu Uzalendo
Mzalendo kwa nchi yake
Kwanza ana Nidhamu kwa wenzake bila kujali vipato vyao au Hali za kwa ujumla.
Akikubaliana na Watanzania wenzake kutii ilani katiba Kanuni miongozo na Taratibu huwa anafanya hivyo with respect na kukaa mbali na Aina yeyote ya hila au janja janja.
Shekhe Hilal Shawej ( kipozeo)
Akiongea mbele ya Mufti wa Tanzania
Nakumbuka Tarehe 20/02/2024
Alisema Mbora wa watu ni yule ( mtu) Mwenye kuwafaa watu
Mwisho wa kunukuu
Mzalendo ana Nidhamu kwa kauli Chanya za Viongozi wa Dini
Halazimishi Viongozi wa Dini wamsomee maandiko tu ayapendayo Yeye
Mzalendo hujiepusha kufuru za namna hiyo
Mzalendo akitaka Uongozi
Hujipa muda kuangalia Ilani katiba , kanuni miongozo na Taratibu zinavyo elekeza na huziishi
Mzalendo akiwanyooshea vidole
Mafukara
Na Watumishi wa Umma
Huwanyooshea pia vidole watu wa Chama kwa kuheshimu kiapo Chake Cha kuitii katiba ambayo ndani yake inamkataza kuwa mtu Mbaguzi na Mpendeleaji.
Mzalendo ana hofu ya kumhofu Mwenyezi Mungu
Na anakuwa anaenenda katika Mafundisho ya Dini kwa imani yake
Mheshimiwa Rais wa Zanzibar
Dkt Hussein Mwinyi
Akiongea mbele ya Professor Abubakar Bin Zuber Bin Ally Bin Mbwana
Mufti na Shekhe Mkuu wa Tanzania
Nakumbuka Tarehe 24/02/2024
Alisema
Mafundisho ya Dini yetu yanatufunza Umuhimu wa kila Mara kumuelekea Mwenyezi Mungu ikiwa ni namna mojawapo ya kutambuwa uwepo wake.
Mwisho wa kunukuu
Mzalendo halisi
Hawi na pupa ya kupindisha pindisha mambo ili apate Yeye na wafuasi wake huku kundi kubwa likiishi Kama liko Jahanam
Mtume wetu Mohammad SAW Alitufundisha kuwalisha watu na kuwapenda
Hivi inakuwaje upendo wetu tunauonyesha kwa watu wengine huku Wanaccm wenzetu wakiteseka kwa ugumu wa maisha !??!!
Tubadilike Sasa
Tuwe Wazalendo
Mzalendo Hana hila ila ana ucha Mungu na anawasikiliza Viongozi wa Dini na kutii hotuba , Mahubiri na Mawaidha Yao
Nakumbuka Tarehe 24/02/2024
Professor Abubakar Bin Zuber Bin Ally Bin Mbwana
Mufti wa Tanzania
Akiongea mbele ya Muwakilishi wa Rais Samia
Dkt Hussein Mwinyi
Alisema
Sisi tuna Mashekhe
Si Kama tulijikuta Mashekhe hivi hivi tu
Tuna Mashekhe
Kuna wenzetu wengine hawana Mashekhe
Hao shauri Yao Kama hawana Mashekhe
Mtu Ambaye Hana Shekhe lazima atakuwa na Shekhe Mwingine
Yaani haiwezekani
Kitu lazima kiwe na Mbadala
Kama huna Shekhe lazima uwe na kitu kingine .
Mbaye Hana Shekhe
Shekhe wake ni Sheitwaan.
Mwisho wa kunukuu
Ndani ya CCM watu wauchukiao Ukweli huku wakiwa wameapa kufuata na kutii ilani katiba Kanuni miongozo na Taratibu watu Hawa wakuikaji wa Maksudi wa Taratibu zetu Mashekhe wao ni Mashetani ndiyo maana hata wakielezwa Ukweli wanachukia .
Wanajawa na hasira
Kushiba washibe wao na hasira za shibe wawe nazo wao hao ndiyo watu Wapumbavu wakaao na hasira vifuanu mwao.
Mchungaji Christopher Mwakasege
Akitoa Mahubiri Tarehe 23/02/2024
Alisema
(Je) hujasoma kwenye Biblia !?
Hasira hukaa kifuani mwa (mtu) Mpumbavu
Mwisho wa kunukuu
Tuachane na kujifanya watu wenye hasira wakati Mali tunazozitafuna Kuna haki pia za familia fukara zilizo jitolea kwa njia Mbali Mbali kuimarisha Chama.
Mtu
Mzalendo kila anachokula anawawaza na Mafukara Kama wamepata riziki .
Mtu Asiyekuwa na Uzalendo.
Ni Jeuri
Hawapendi Maskini Bali anatumia Wala Ubwabwa na walamba visingizio kufanya hila ili azidi kuwaumiza hao Mafukara wasio na Watetezi
Mtu Asiyekuwa Mzalendo Hana maishani mwake neno liitwalo huruma
Wanavyoumia Mafukara na kupaza Sauti Yeye hukerekwa na hutamani kuwaongezea Machungu huku akijionyesha Kama vile anawasaidia lakini hawasaidii.
Mtu asiye Mzalendo hata akisikia Kuna kiongozi anawaonea Mafukara Yeye hachukuwi hatua za kisheria
Hukaa kimya kana kwamba hasikii lolote.
Mheshimiwa Getrude Mongella
Ex Rais wa Bunge la Africa
Na Mwanasiasa Mkongwe
Akihojiwa na kipindi Cha Zumari
Nakumbuka Tarehe 04/11/2022
Alisema
Mwalimu (Nyerere) alikuwa na Ubinaadamu wa Aina fulani.
Alikuwa kila Mara anajali utu anajali watu watoke kwenye dhiki
Na alikuwa ni mtu Mwenye huruma.
Mwisho wa kunukuu
Mtu Asiyekuwa Mzalendo
Ana Tamaa ya kula yeye bila kuwajali wenzake
Ana Chuki binafsi
Anapendwa sifa hata Kama Anaboronga boronga Mambo.
Maneno yake yaliyo mengi yamechanganyika na hila na Uongo mwingi ulifunikwa na viini macho vya vijineno vyente mfananio Kama wa Ukweli
Akikosolewa ana hasira nyati anasubiri
Akiongea huongea Kama mtu Rahimu ila ushetani wake hudhihirika kwa matendo yake ya hovyo yenye Dalili na Mambo ya Kinafiki Kama yaliyo ainishwa kwenye Vitabu vitakatifu.
Hapendi maneno yaitwayo
Haki na Usawa.
Kuwaonea Mafukara na kuwapa vitisho ndiyo Raha yake.
Tujipime tujiangalie
Mimi na Wewe
Kwa kumuogopa Mwenyezi Mungu
Tuko kundi gani !?!?
Tujitathmini Sisi wenyewe
Self assessment yetu Sisi wenyewe Kama Chama kuliko kusubiri Wapinzani kutukosoa
Tuyaone Mapungufu yetu na kwa hofu ya kumhofu Mwenyezi
Waliokanyaga ilani katiba Kanuni miongozo na Taratibu wakapata vyeo watoke
Watu hao
Sio Wazalendo na Sio Waaminifu kwa mifumo ya nchi
Watu Waaminifu na wenye uelewa kuhusu Chama wamejaa
Tuwatumie hao kukirudisha Chama kwenye njia yake na Huu ndiyo utakuwa ukombozi kwa Wanaccm wengine wanaogandamizwa kwa kuwahofu watu wachache wasio na Utii kwa mifumo ya Chama
Mungu atuongoze tudhamirie bila Unafiki kuyarekebisha yanayotutia aibu kwa jamii.
Haiwezekani Sisi Wanaccm kwa Mujibu wa katiba ya CCM 1977 toleo 2022 uk 03 ibara 5(14) tunapambana kuondoa Umaskini kwa Wanajamii huku Sisi kwa Sisi tukiwa hatusaidiani kwa lolote Wala chochote na hatuko tayari kumsaidia mtu Mwenye ubunifu wowote huku tukitangaza kuwasaidia wengine wenye ubunifu ambao Sio Wanaccm
Mheshimiwa Rais Dkt Samia Suluhu Hassan
Mwenyekiti CCM Taifa
Rais wa Jamhuri Ya Muungano wa Tanzania
Akiwa katika Kongamano la Wana Tasnia ya habari
Nakumbuka Tarehe 18/06/2024
Alisema
Tujitathmini ( Sisi) wenyewe.
Self assessment
Yetu wenyewe
Ya sekta yetu
Kuliko tungetafuta ( mtu baki) atufanyie assessment angetuandika vibaya saana kwa haya ambayo Sisi wenyewe ndani tumeyaona
Lakini tumejitathmini wenyewe
Tumekuwa Wakweli
Mwisho wa kunukuu
Tusome katiba ya CCM 1977 toleo 2022 uk 02-05 ibara 05(2)(7)(8)(9)(10)(11) uk 06 ibara 07 na 08 (1)(2)(6) uk 10-11 ibara 15(1)(2)(3)(4)(5)(6)(7) turudi uk 07 ibara 12(1)(a) ili twende uk 152 vifungu (1)(2)(3)(5)(6)(7)(8)(9)
Ilani ya CCM 2020 -2025 uk 01 ibara 04 na uk 08 ibara 10 na 11




Kidumu Chama Cha Mapinduzi






Mathias Mugerwa Kahinga.
 
KIONGOZI ASIPOTENDA UADILIFU NA UAMINIFU
AJUWE
ANAJISAFISHIA NJIA YA KUMPELEKA JAHANNAM

Nakumbuka Tarehe 26/07/2023
Mheshimiwa Rais Dkt Samia Suluhu Hassan
Akiongea katika Mkutano wa Wakuu wa nchi za Africa katika kituo Cha Mikutano Cha Kimataifa Cha Julius Nyerere -. JNCC
Alisema,
Mwasisi wa Taifa huru la Africa Kusini Hayati Mzee Nelson Mandela alisema , na Mimi namnukuu
Education is most powerful weapon you can use to change the World.
Akimaanisha kuwa Elimu ndiyo silaha yenye nguvu Zaidi inayoweza kutumika kubadilisha Ulimwengu.
Mwisho wa kunukuu
Tusome katiba ya CCM 1977 toleo 2020 uk 06 ibara 08 vifungu vidogo 1,2,5,,6, uk 10-11 ibara 15 vifungu vidogo 1,2,3,4,6,na 7.
uk 07 ibara 12 kifungu kidogo 1,a ili tukasome uk 151kifungu 1,2,3,6,na 08.
Tusome Kitabu cha The Political Parties act Chapter 258 uk 11kifungu Cha 6A vifungu vidogo1,2, na 5
Tukidumu katika kuelimishana tutaondoa Ujinga endelevu unaowatesa wengi na kuwapelekea kuishi kimazoea kinyume na Matakwa ya ilani ya CCM 2020 uk 01 ibara 04.
Ukiwa Kiongozi ni lazima ufahamu ya kuwa Kuna watu unao waongoza na Walio wengi ni Mafukara
Cheo kinalevya
Unaanza kuwaona Maskini Kama uchafu .
Unatoa Rushwa kwa Wajumbe ili upendelewe upate Cheo Kisha unasimama Hadharani kwa Maskini ukijifanya ni Mtu wa ibada
🤔🤔🤔
Unajifanya Kama hujielewi unawapendelea watu Waovu na kuwazibia wenye kustahili
🤔🤔🤔
Siku yako inakuja.
Watu wanalia fulani katoa taarifa za Uongo kupata cheo Wewe unachukulia powa na una uwezo wa kusema japo neno
Subiri siku yako.
Tukisoma Kitabu cha Maandiko ya Sunnah za Mtume Mohammad SAW Kiitwacho Muntakhabu Ahadith uk 770 kifungu cha 160
Maandiko yanasema
Abu hurairah Radhiallahu Anhu amesimulia kuwa Rasulullahi Swallallahu Alaihi Wasallam amesema,
Kama mtu yeyote amepewa Uamiri juu ya Watu kumi au Zaidi lakini hakufanya Uadilifu kwao , Basi atakuja siku ya Kiama akiwa amefungwa minyororo na pingu.

Mwisho wa kunukuu

Umefika wakati Sasa kuongeza nguvu katika kutoa Elimu ili watu wawakatae Viongozi wanaotoa fedha kupata Vyeo.
Madhara ya wanunua Vyeo tumeisha yaona
Maskini wanalia huku walionunua Vyeo Wakiwa wanalindwa.
Ndiyo maana nitaendelea kuwahimiza Viongozi wa Kitaifa
Naomba waniite niwaonyeshe fedha ilipo ili tuanze kuwainua Wanaccm kiuchumi wasitumike kwa visingizio vya kuitwa Wajumbe kupitisha Watoa Rushwa na kuwafanya Viongozi kwa kuwafokea Maskini.
Kisha tunatoka mbele ya Jamii na kuonekana kana Kwamba hatuna changamoto ndani yetu.
Mtu Mwenye njaa Hana Uadilifu Wala Uaminifu kwa ile njaa inavyompeleka puta.
Nakumbuka Tarehe 25/04/2022
Comrade Abdulrahman Omary Kinana
Makamu wa Mwenyekiti CCM Taifa
Akiwa ziarani Tanga
Alisema,
Tusikubali tukamchaguwa mtu kwa sifa ya kununua kwa hela.
Au kwa kutoa Rushwa.
Hatuwezi tukakataa Rushwa nje ya CCM wakati ndani ya CCM kuna Rushwa.
NI lazima tukatae Rushwa
Rushwa si sifa ya mtu kuwa Kiongozi.
Kuwa na fedha mfukoni haiwezi kuwa sifa.
Na mtu anayetaka kununua uongozi Hana sifa.
Anataka njia ya mkato

Mwisho wa kunukuu

Katika Ulimwengu wa kiroho nilipata kuonyeshwa
Diwani akijihusisha na Rushwa za Wazi kabisa na akapewa Udiwani.
Pia kwenye Ulimwengu wa kiroho
Nilimuona Mwenyekiti Wa Serikali ya Mtaa akitokea Upinzani Kama leo
Akatoa Rushwa ya Milioni tano huku Chini na akapeleka. million nne juu .
Akatengenezewa kadi za ssseem usiku mmoja na kesho akapitishwa na vikao husika akawa Mwenyekiti wa Serikali ya Mtaa .
Sasa ameanza kujisahau na kuwatusi Wafia Chama kwani anaamini Sasa ni Mwendo wa kumwaga mihela kupata Cheo.
😳😳😳😳😳😳
NI lazima Sasa tueneze Elimu ili kuukimbiza Ujinga unao wapelekea watu kuamini kuwa anayetoa fedha ndiye Kiongozi sahihi.
Huu ndiyo Ujinga unaotuletea Viongozi wasio na Maono .
Nakumbuka Tarehe 23/04/2022
Mheshimiwa Jennista Mhagama
Akiwa Waziri wa nchi ofisi ya Rais Menejimenti Utumishi na Utawala Bora
Alisema
Mheshimiwa Hayati Baba wa Taifa alitukumbusha saana kupiga Vita Maradhi Ujinga na Umaskini.
Mama Samia Suluhu Hassan anaendelea kuthibitisha anatembea kwenye nyayo za Baba. Wa Taifa katika Vita hivyo dhidi ya Maradhi Ujinga na Umaskini ili kuleta ustawi kwa Taifa.
Mwisho wa kunukuu.
Nakumbuka Tarehe 26/07/2023
Professor Kitila Alexander Mkumbo
Waziri wa Mipango na Uwekezaji
Akifanya Ziara Kigoma alisema
Rais huyu ni Muungwana saana
NI Muungwana saana

Mwisho wa kunukuu

Kwa kuyazingatia haya yote Naomba nikutane na Viongozi wa Kitaifa ili tujadiliane .
Wanaccm wengi wako kimya naonyeshwa katika Ulimwengu wa kiroho wamewekwa kwenye mifuko ya wale Walio finance kuwaka walipo.
Tuwakatie minyororo kwa kuwawezesha kiuchumi
Huu ndiyo ucha Mungu
Tusaidiane Sasa Miradi na ubunifu ninao
Chama CCM chetu.
Serikali ni CCM
Tunakwama wapi .
Niitene nionyeshe fedha zilipo.
Ili tuondoe Omba omba inayotumika kutuletea Viongozi wenye mapungufu ya kiutaratibu wasio na Vision Baadhi.


Kidumu Chama Cha Mapinduzi

Mathias Mugerwa Kahinga
🙏🏿🙏🏿🙏🏿🙏🏿🙏🏿
 
Maandishi mengi mno... we use to call this Flood
 
Mkuu, unataka tukae kusoma kitabu chote hicho? Jamani ebu kuweni serious angalau kidogo basi!
 
Utamaduni wa kufuatisha akili za watu wajinga tuuangamize ili elimu sahihi iisaidie nchi kusonga mbele

Nakumbuka Tarehe 20/06/2024 Mheshimiwa Elibariki Kingu Mbunge wa Jimbo la Singida Magharibi
Alisema. Ukweli lazima tuuseme na Umuhimu wa kuusema Ukweli ni kuweza kulisaidia Taifa ( ili) liweze kuwa na Mtazamo ambao ni sahihi. Kutoka Mtazamo ambao sio sahihi ambao unaweza ukajengwa katika mazingira tu ya kijamii , kiuchumi, ama mazingira mengine ya kisiasa.

Mwisho wa kunukuu Mheshimiwa Rais Dkt Samia Suluhu Hassan Akiwa katika Kongamano la Wana Tasnia ya habari Nakumbuka Tarehe 18/06/2024 Alisema Mimi Binafsi siamini katika Ukiritimba wa Mawazo au fikra .
Yaani Monopoly of ideas Ninaamini katika kusikiliza Sauti na Mawazo ya ( watu) wenzangu
Mwisho wa kunukuu

Tutoe fikra na Mawazo yetu kwa Mujibu wa katiba ya Jamhur ya Muungano wa Tanzania 1977 toleo 2005 uk 23 Ibara 18(a) na 19(1) kwa Maana ya Uhuru wa Mawazo huku tukizingania ibara 09 a b f na h.
Ilani ya CCM ibara 110(c) bila kuacha uk 01 ibara 04. Vitendo vya kutokujali katiba na Maandiko ya kimfumo limekuwa tatizo sugu ndani ya nchi na kupelekea watu Wajinga kuwapotosha Makundi ya Watu walio wengi ambao wanatakiwa kusaidiwa ili wawe na Elimu ya kujielewa wanufaike na Taifa lao

Askofu Dkt Benson Kalikawe Bagonza Askofu wa KKKT Dayosisi ya Karagwe Akitoa hotuba Tarehe 08/03/2022
Alisema Utamaduni wa kutojali Katiba una nguvu kuliko nguvu ya Katiba . Mazoea ya kutoheshimu Katiba yana nguvu kuliko Katiba. Mwisho wa kunukuu Leo hii nchi kwetu Matatizo mengi tuliyo nayo yametokana na Changamoto nyingi zikiwemo za Ukosefu wa Elimu sahihi ya kila sekta.

Matokeo ya Changamoto hii yamewaibuwa Watu Jasiri wasiokuwa na Elimu ya kile wakisemacho . Hao ndiyo Baadhi wanajiita Wanasiasa kwa kigezo Cha kuvaa sare za kisiasa tu huku vichwani wakiwa zero . Hapa nikimaanisha hawajuwi lolote lile kuhusu ilani , katiba , Kanuni miongozo na Taratibu. Watu Hawa hawana research yeyote Zaidi ya Ujasiri wa kujiropokea na kutengeneza wafuasi kwa njia za hila na Rushwa.

Makada wenye Uelewa wamekuwa kimya huku wakishuhudia upotoshaji ukiendelea. Hatuwezi kukubali Mambo haya. Ni lazima Sasa Wapotoshaji tuwape Elimu. Shekhe Amir Farid. Akitoa Mawaidha. Akiwa Wilaya ya Chake Chake Huko Pemba. Nakumbuka Tarehe 20/06/2024 Alisema, Pahali popote Wewe Tafuta Elimu tu. Elimu ndizo zinazotufungua Mwanaadamu.

Elimu ndiyo inayokupa Mwanga. Mwisho wa kunukuu. Viburi na Jeuri ya Baadhi ya Viongozi miongoni mwetu kumepelekea haki kupotea miongoni mwetu huku tukijifanya ni watu Waumini wenye Imani ya kimungu huku tukipendelea watu na kuwabagua wengine kwa Hali zao kiasi kwamba hata wakipaza sauti hatuwasikilizi kwa vile viburi vilivyo tufunika na kutusahaulishia Uwepo wa maamrisho ya Mwenyezi Mungu kiasi kwamba hatuna hofu Tena ya kuwa ipo siku tutahesabiwa.

Shekhe Othman Khamis Juma Imam Masjid Mtoro Nakumbuka Tarehe 29/03/2022 Alisema Mwambie Mwenyezi Mungu katika mema ya Dunia akuondolee kiburi Mwenyezi Mungu katika mema ya Dunia hii ( mwambie) akuondolee kiburi Na badala yake (muombe ) akupe Unyenyekevu Wote walio nyenyekea Wakajishusha
Wakaondoa kiburi hao ndiyo waliofanikiwa ( Kiroho) Binaadamu wote wanampenda mtu Mnyenyekevu
Na Binaadamu wote hawampendi ( mtu) Mwenye kiburi Kila mtu akikutambuwa unacho kiburi , Kiwe Cha Mamlaka , Utawala Kiwe Cha pesa Kiwe Cha nguvu mwilini ( Kiburi) kiwe kitakavyokuwa Madhali ni Jeuri

Ni kiburi Basi ( ujuwe) watu hawakupendi Hata Kama unaona ( watu wako ) wanakupigia makofi ukiwepo ujuwe ( ni watu) waongo TU. Hakuna Mwenye Mapenzi na Wewe hapo. Mwisho wa kunukuu Niwaombe viongozi wenye Tabia hizi Msione hatusemi Roho zetu zinaumia Ila tunawapigia makofi tu ilimradi Mambo yaende
Lakini lazima mjuwe Mnavyowalinda Waliojipatia vyeo kinyume na Matakwa ya Utaratibu Watu wasio stahili kwa Mujibu wa Maandiko ya kimfumo Mnapowalinda mjuwe mnachuma dhambi kubwa Na Tabia hizi hatuzipendi

Na mnapowaandama mafukara na watumishi wa Umma huku mkiwalinda waovu wengine Tabia hizi hatuzipendi na tunakuwa hatuwapendi hata Ninyi kwa Tabia hizo chafu zilizo Kinyume na Viapo vyenu.
Tukatae Sasa kuwalea watu wasiokijuwa Chama Cha Mapinduzi kwa kuwaondoa kwenye vyeo walivyo vikalia huku wakiwa hawajuwi lolote lile kuhusu ilani Katiba Kanuni miongozo na Taratibu zetu.

Sisi Kama Chama tunaunda Serikali na kuisimamia Serikali kutekeleza yaliyo ndani ya ilani Tunapokuwa na Viongozi ndani ya CCM waliovalia Kama makada wakiwa hawaijuwi ilani wala katiba, Kanuni miongozo na Taratibu Tujiulize Tabia hizi ni za Uzalendo au Sio za Uzalendo!?! Tusome katiba ya CCM 1977 toleo 2022 ibara 5(4) ili kwenda kusoma Kitabu Cha Binaadamu na Maendeleo Cha Mwalimu Julius Kambarage Nyerere uk 17-21 kwa msisitizo wa kuyaishi maneno na kuyafanyia kazi Nakumbuka Tarehe 28/05/2024 Mheshimiwa Paul Christian Makonda Mkuu wa Mkoa wa Arusha Alisema Nilisha sema hivi siku zote , siku zote , tusijitetee na kuwatetea ( watu) walio tuingiza mahali pabovu.

Hatuwezi kulindana kwa Makosa tuliyoyafanya Mwisho wa kunukuu Padre Dkt Charles Kitima Katibu Mkuu wa Baraza la Maaskofu Tanzania ( TEC) Nakumbuka Tarehe 16/06/2024 Alisema Tukubali tuanze kuandaa mfumo wa kujirekebisha Kama tunataka tujirekebishe, tujirekebishe Kama tumeona kitu hakiendi sawa Sisi tutasema
Kwa sababu itakuwa ni laana mbele ya Mwenyezi Mungu Mnajuwa watu wanaenda kutumbukia shimoni halafu ( wenye macho) mnakaa kimya Hapana Hapana

Mwisho wa kunukuu


Kidumu Chama Cha Mapinduzi

Mathias Mugerwa Kahinga

🙏🏿🙏🏿🙏🏿🙏🏿🙏🏿🙏🏿🙏🏿
We mwanaccm kweli? We siyo chawa? Wanaccm hawanaga ushauri wa hivyo bwana. Wana kazi moja tu ya kusifu na kuabudu
 
KIONGOZI ASIPOTENDA UADILIFU NA UAMINIFU
AJUWE
ANAJISAFISHIA NJIA YA KUMPELEKA JAHANNAM

Nakumbuka Tarehe 26/07/2023
Mheshimiwa Rais Dkt Samia Suluhu Hassan
Akiongea katika Mkutano wa Wakuu wa nchi za Africa katika kituo Cha Mikutano Cha Kimataifa Cha Julius Nyerere -. JNCC
Alisema,
Mwasisi wa Taifa huru la Africa Kusini Hayati Mzee Nelson Mandela alisema , na Mimi namnukuu
Education is most powerful weapon you can use to change the World.
Akimaanisha kuwa Elimu ndiyo silaha yenye nguvu Zaidi inayoweza kutumika kubadilisha Ulimwengu.
Mwisho wa kunukuu
Tusome katiba ya CCM 1977 toleo 2020 uk 06 ibara 08 vifungu vidogo 1,2,5,,6, uk 10-11 ibara 15 vifungu vidogo 1,2,3,4,6,na 7.
uk 07 ibara 12 kifungu kidogo 1,a ili tukasome uk 151kifungu 1,2,3,6,na 08.
Tusome Kitabu cha The Political Parties act Chapter 258 uk 11kifungu Cha 6A vifungu vidogo1,2, na 5
Tukidumu katika kuelimishana tutaondoa Ujinga endelevu unaowatesa wengi na kuwapelekea kuishi kimazoea kinyume na Matakwa ya ilani ya CCM 2020 uk 01 ibara 04.
Ukiwa Kiongozi ni lazima ufahamu ya kuwa Kuna watu unao waongoza na Walio wengi ni Mafukara
Cheo kinalevya
Unaanza kuwaona Maskini Kama uchafu .
Unatoa Rushwa kwa Wajumbe ili upendelewe upate Cheo Kisha unasimama Hadharani kwa Maskini ukijifanya ni Mtu wa ibada
🤔🤔🤔
Unajifanya Kama hujielewi unawapendelea watu Waovu na kuwazibia wenye kustahili
🤔🤔🤔
Siku yako inakuja.
Watu wanalia fulani katoa taarifa za Uongo kupata cheo Wewe unachukulia powa na una uwezo wa kusema japo neno
Subiri siku yako.
Tukisoma Kitabu cha Maandiko ya Sunnah za Mtume Mohammad SAW Kiitwacho Muntakhabu Ahadith uk 770 kifungu cha 160
Maandiko yanasema
Abu hurairah Radhiallahu Anhu amesimulia kuwa Rasulullahi Swallallahu Alaihi Wasallam amesema,
Kama mtu yeyote amepewa Uamiri juu ya Watu kumi au Zaidi lakini hakufanya Uadilifu kwao , Basi atakuja siku ya Kiama akiwa amefungwa minyororo na pingu.

Mwisho wa kunukuu

Umefika wakati Sasa kuongeza nguvu katika kutoa Elimu ili watu wawakatae Viongozi wanaotoa fedha kupata Vyeo.
Madhara ya wanunua Vyeo tumeisha yaona
Maskini wanalia huku walionunua Vyeo Wakiwa wanalindwa.
Ndiyo maana nitaendelea kuwahimiza Viongozi wa Kitaifa
Naomba waniite niwaonyeshe fedha ilipo ili tuanze kuwainua Wanaccm kiuchumi wasitumike kwa visingizio vya kuitwa Wajumbe kupitisha Watoa Rushwa na kuwafanya Viongozi kwa kuwafokea Maskini.
Kisha tunatoka mbele ya Jamii na kuonekana kana Kwamba hatuna changamoto ndani yetu.
Mtu Mwenye njaa Hana Uadilifu Wala Uaminifu kwa ile njaa inavyompeleka puta.
Nakumbuka Tarehe 25/04/2022
Comrade Abdulrahman Omary Kinana
Makamu wa Mwenyekiti CCM Taifa
Akiwa ziarani Tanga
Alisema,
Tusikubali tukamchaguwa mtu kwa sifa ya kununua kwa hela.
Au kwa kutoa Rushwa.
Hatuwezi tukakataa Rushwa nje ya CCM wakati ndani ya CCM kuna Rushwa.
NI lazima tukatae Rushwa
Rushwa si sifa ya mtu kuwa Kiongozi.
Kuwa na fedha mfukoni haiwezi kuwa sifa.
Na mtu anayetaka kununua uongozi Hana sifa.
Anataka njia ya mkato

Mwisho wa kunukuu

Katika Ulimwengu wa kiroho nilipata kuonyeshwa
Diwani akijihusisha na Rushwa za Wazi kabisa na akapewa Udiwani.
Pia kwenye Ulimwengu wa kiroho
Nilimuona Mwenyekiti Wa Serikali ya Mtaa akitokea Upinzani Kama leo
Akatoa Rushwa ya Milioni tano huku Chini na akapeleka. million nne juu .
Akatengenezewa kadi za ssseem usiku mmoja na kesho akapitishwa na vikao husika akawa Mwenyekiti wa Serikali ya Mtaa .
Sasa ameanza kujisahau na kuwatusi Wafia Chama kwani anaamini Sasa ni Mwendo wa kumwaga mihela kupata Cheo.
😳😳😳😳😳😳
NI lazima Sasa tueneze Elimu ili kuukimbiza Ujinga unao wapelekea watu kuamini kuwa anayetoa fedha ndiye Kiongozi sahihi.
Huu ndiyo Ujinga unaotuletea Viongozi wasio na Maono .
Nakumbuka Tarehe 23/04/2022
Mheshimiwa Jennista Mhagama
Akiwa Waziri wa nchi ofisi ya Rais Menejimenti Utumishi na Utawala Bora
Alisema
Mheshimiwa Hayati Baba wa Taifa alitukumbusha saana kupiga Vita Maradhi Ujinga na Umaskini.
Mama Samia Suluhu Hassan anaendelea kuthibitisha anatembea kwenye nyayo za Baba. Wa Taifa katika Vita hivyo dhidi ya Maradhi Ujinga na Umaskini ili kuleta ustawi kwa Taifa.
Mwisho wa kunukuu.
Nakumbuka Tarehe 26/07/2023
Professor Kitila Alexander Mkumbo
Waziri wa Mipango na Uwekezaji
Akifanya Ziara Kigoma alisema
Rais huyu ni Muungwana saana
NI Muungwana saana

Mwisho wa kunukuu

Kwa kuyazingatia haya yote Naomba nikutane na Viongozi wa Kitaifa ili tujadiliane .
Wanaccm wengi wako kimya naonyeshwa katika Ulimwengu wa kiroho wamewekwa kwenye mifuko ya wale Walio finance kuwaka walipo.
Tuwakatie minyororo kwa kuwawezesha kiuchumi
Huu ndiyo ucha Mungu
Tusaidiane Sasa Miradi na ubunifu ninao
Chama CCM chetu.
Serikali ni CCM
Tunakwama wapi .
Niitene nionyeshe fedha zilipo.
Ili tuondoe Omba omba inayotumika kutuletea Viongozi wenye mapungufu ya kiutaratibu wasio na Vision Baadhi.


Kidumu Chama Cha Mapinduzi

Mathias Mugerwa Kahinga
🙏🏿🙏🏿🙏🏿🙏🏿🙏🏿
Kongole.
Umeandika mambo mengu sana ya msingi, lakini hitimisho lako/kibwagizo chako cha "kidumu chama cha mapinduzi" kinaondoa maana nzima ya hoja zako.

Muasisi,muendelezaji na mnufaika wa yote uliyoyalalamikia ni hicho chama ambacho wewe unataka kiendelee kudumu huku unapingana na matokeo ya kudumu kwake!!

Hujui unataka kuelekea Kusini,Kaskazini, Magharibi au Mashariki!!!
 
Nakumbuka tarehe 27/05/2024.

Mheshimiwa Rais Paul Christian Makonda, Mheshimiwa Rais wa Mkoa wa Arusha, akiwa Monduli.

Nawaomba wananchi, msiwe na woga. Sema kwa ujasiri mkubwa. Ilimradi hamumuonei mtu wala hamumsingizii mtu.

Tunataka haki iwe msingi wa mafanikio.

Mwisho wa kunukuu.

Tusome Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania 1977, toleo la 2005, Ibara ya 34(4), Ibara ya 35(1), Ibara ya 18(a), na 19(1), Ibara ya 09(a, b, f, na h).

Ilani ya CCM Ibara ya 110(c), Ibara ya 04 uk. 01, na Ibara ya 10 na 11 uk. 08.

Machawa ni watu wajinga. Hawaelewi kwamba Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania 1977, toleo la 2005, inawapa jukumu la kuchukua hatua dhidi ya uvunjifu wa katiba na sheria za nchi.

Tuwape elimu ili wabadilike kifikra. Waache kuwachukia wanaoibua maovu. Pia waache kuwapa ushirikiano watu waovu kwa vigezo vya malipo ya ubwabwa na rushwa.

Wakumbuke ilani inayotekelezeka sasa uk. 01, Ibara ya 04, inakataza watu kufanya kazi kwa mazoea.

Wakati ni huu kwa machawa kuonyesha uchamungu wao usio na unafiki na kuwa wazalendo wa kweli kwa kutenga muda wao kujisomea ili kujua mifumo ya nchi itakayowaondolea aibu na fedheha ya kusimama hadharani kutetea ujinga na upumbavu kwa vigezo vya kulipwa ubwabwa na buku jero.

Kidumu Chama Cha Mapinduzi.

Mathias Mugerwa Kahinga

🙏🏿🙏🏿💪🏿💪🏿👆🏿👆🏿
 
NAWAPENDA SANA VIONGOZI WETU WA DINI ZOOTE

NATAKA NIWAASE ILI NIWAEPUSHE NA KUTIWA MOTONI SIKU YA KIAMA.

KABLA YA KUMSIFIA MWANASIASA YEYOTE, TUULIZENI WANASIASA WENYEWE ILI MSIENDELEE KUCHUMA DHAMBI NA KUIPOTOSHA JAMII ISIYOKUWA NA UELEWA WA ELIMU YA SIASA.

Nilisikika nikitema nyongo ya Mamba katika Ulimwengu wa Kiroho huko Ndotoni, nikikemea tabia ya baadhi ya viongozi wa kidini kuacha neno la Mungu na kuipenda siasa zaidi kuliko Mwenyezi Mungu, huku wakisifu na kuchagua aya za kusema ili kunogesha wale wanaojipendekeza kwao.

Nikaanza kutema nyongo:

Viongozi wakuu kabisa wa kitaifa wakisifiwa sina shaka kwao kwa sababu kiongozi mkuu kazi yake ni kutoa muelekeo na kuchukua hatua kwa wale wanaokaidi muelekeo ule. Viongozi wakuu tayari wameelekeza watu watendewe haki, kwa nini haki inatendeka kwa kuangalia koo, familia, uswahiba, ujamaa, na muhali?

Nasema hivyo kwa sababu wanaopaswa kutenda haki na kuipigania ni pamoja na yeyote aliyeapa kuilinda, kuihifadhi, na kuitetea katiba na sheria za nchi kwa mujibu wa Ibara ya 26(2) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania 1977 toleo 2005 huku akizingatia ilani ya CCM Ibara 04 uk. 01, inayosomwa kwa pamoja na uk. 161-168 kwa msaada wa kuhuisha Ibara 10 na 11 uk. 08.

Viongozi wakuu wa kitaifa wanakemea ubaguzi na upendeleo. Kwa nini wasaidizi wa viongozi hao wanasikia vilio vya mafukara na watumishi wa umma kuhusu maonezi yao lakini wanakaa kimya? Wanasikia watu wametoa taarifa za uongo na kupata vyeo lakini wanakaa kimya. Watu wameuza ofisi ya chama, wahusika wa kuchukua hatua wako kimya. Watu wamewapakazia wenzao taarifa za uongo mitandaoni na kwenye TV, ila wanaopaswa kuchukua hatua wako kimya. Wanaccm wana maisha magumu, ilibidi wasaidiwe ili nao waweze kuwasaidia wananchi, ila badala ya wanaccm kusaidiwa, wanatumiwa kama vyombo vya kuvulia samaki kuwaneemesha waliowaweka kwenye vyeo huku wanaccm wakiishi na kufa wakiwa mafukara kabisa.

Viongozi wengi wana nyadhifa zilizotokana na wanaccm hawa mafukara, ila wakishapata vyeo hivyo huvitumia kuwaneemesha wengine. Wanakufuru mpaka kufikia kuvunja katiba, kanuni, miongozo na taratibu kuwaneemesha wasio stahili, walio kinyume na utaratibu, na kuwalinda kwa kutengeneza matisho ya kuwaziba midomo mafukara na watumishi wa umma huku wakitaka wanasiasa hao kwa mauozo haya waendelee kusifiwa na kutukuzwa kama ni watu wema kwenye jamii huku wakiwa hawajutii wala kujisikia vibaya kusigina maandiko walioyoapa kwa kushika vitabu vitakatifu vya Mwenyezi Mungu mbele ya jamii.

Viongozi wa dini mkumbuke, sehemu kubwa ya jamii ndani ya nchi haina uelewa mkubwa kuhusu siasa na pia maandiko ya kiimani. Hivyo, ni busara kwa viongozi wa dini nyie kuwa mnakumbusha maelekezo na makatazo ya Mwenyezi Mungu kila mtu kwa imani yake na kukemea tabia mbovu mtakazokuwa mnaiona kwa baadhi ya viongozi. Ila mkitaka kusifu, waulizeni walio chini kabisa ili kupata ukweli halisia na sio kusifu tuuu.

Nakumbuka tarehe 22/03/2023, Shekhe Msellem Bin Ally akitoa ufafanuzi na uchambuzi wa Qur'an Tukufu alisema: Waswahili husema sadaka huanzia nyumbani, kwa hiyo wewe kama unacho uanze na msaada kwa watu wako kwanza nyumbani. Au umsaidie maskini ambaye ana shida kubwa (maskini ambaye) anakaribia kula udongo kwa sababu ya dhiki na njaa.

Mwisho wa kunukuu.

CCM ngazi za chini tuna sura za ucheshi na tabasamu zilizoghubikwa na maisha magumu ya mwanaukome. Posho zinatoka kwa baadhi ya vyeo, kwingine ni mswaki tu. Hatuna ofisi za kutosha. Hatuna maji safi na salama maeneo baadhi. Hatuna vyoo maeneo baadhi. Watu wanawekwa kwenye vyeo kinyume na matakwa ya utaratibu na wanalindwa wadumu pale huku haya yote yakiwa ni kufuru mbele ya Mwenyezi Mungu.

Nimeandika sana nikiomba nisikilizwe. Ninao ubunifu, sisikilizwi. Wanasaidiwa watu baki ila sisi tulioumia kuwaweka baadhi ya viongozi hapo walipo hatusikilizwi tena. Tumekuwa kama kalai lililotumika kujenga ghorofa na baada ya ghorofa kukamilika kalai lile likatupwa stoo kama ni uchafu sasa.

Watu wasio wajali wenzao twawezaje kuwasifia? Ni jambo baya lisilokuwa na ucha Mungu ndani yake kuwaambia Watanzania wenzetu tutawaondolea umaskini huku sisi wenye jukumu hilo tukiwa hatusaidiani wala hatuna mpango wa kusikiliza sauti zinazopazwa huku chini zikililia kusikilizwa maono yao na kushikwa mkono.

Tusome kwa tafakuri katiba ya CCM 1977 toleo 2022 uk. 06 Ibara 07 na 08 (1)(2)(6), uk. 02-03 Ibara 5(14) kwa msisitizo. Watu wasiozingatia haya twawezaje kuwasifia kama vile ni watenda haki? Uadilifu na uaminifu uko wapi kwa matendo haya ya kutuacha na ugumu wa maisha na kisha kusaidia wengine kabisa kwenye fani zingine huku sisi tulioshindia pande la muhogo kuwaweka hao madarakani tukiendelea kupiga miayo?

Tukisoma Kitabu Cha Sunnah za Mtume Mohammad SAW Kiitwacho Muntakhab Ahadith uk. 768, maandiko matakatifu yanatueleza: Awf Bin Malik Radhiallahu Anhu amesimulia kuwa Rasullullah Swallallahu Alaihi Wasallam amesema kama mnataka nitakujulisheni ni nini uhakika wa Imarah (utawala). Nikamuuliza kwa sauti ya juu mara tatu: "Ni nini ewe Rasullullah?" Akasema: "Kwanza ni lawama, pili ni majuto, na tatu ni adhabu kwenye siku ya kiama, isipokuwa yule atakayefanya uadilifu, na vipi mtu anaweza kufanya uadilifu kuhusiana na jamaa zake."

Mwisho wa kunukuu.

Tunaachana na njaa. Tunatumiana kwa mipango ya safu. Hatujali katiba, kanuni, miongozo na taratibu. Twawezaje kusema tunatenda uadilifu? Uaminifu wetu mbele ya jamii uko wapi? Viapo vyetu ya kuiahidi jamii kutenda haki viko wapi? Kwa nini tunawasifia watu wanaowaumiza wanyonge na kuwaneemesha watu wengine ambao hawakuumia kusaka dola?

Tukisoma Kitabu Cha Muntakhab Ahadith uk. 806, maandiko matakatifu yanatueleza: Abdurahman Bin Abi Bakra Radhiallahu Anhuma amesimulia kuwa mtu mmoja alimsifu mtu mwingine mbele ya Mtume Swallallahu Alaihi Wasallam, na yule aliyesifiwa pia alikuwepo. Mtume Swallallahu Alaihi Wasallam akasema: "Ole wako, umekata shingo ya ndugu yako." (Mtume akarejea haya mara tatu). "Kama mmoja wenu ni lazima asifu, na akaona hilo kuwa ni la lazima na pamoja na kumjuwa huyo (kuwa ni mtu mwema), basi na aseme tu: Nafikiri fulani ni mtu mwema, Allah atamuhesabu (na Allah pekee kwa hakika ndiye anayejuwa ikiwa ni mwema au muovu). Siwezi kumsifu mtu yeyote mbele ya Allah kwa uhakika" (Bukhari).

Mwisho wa kunukuu.

Sisi tunaosifu watu wasiostahili kusifiwa kwa tabia zao za kukiuka katiba, kanuni, miongozo na taratibu tunamfuata Mtume gani? Imani yetu kwa Muumba wetu ikoje?

Shekhe Msellem Bin Ally akitoa ufafanuzi na uchambuzi wa Qur'an tarehe 18/05/2024, alisema Aya 102 sura ya tatu Allah amewaagiza waumini kwa sababu ndiyo wanaomsikia maagizo
 
UTII KWA MAMLAKA ZA KIDUNIA NI MPANGO WA MUNGU

Watanzania wenzangu, tujifunze upendo wa kweli wa kutochukiana tunapojadiliana mambo ya msingi. Tukiendelea kunyamazia mambo ya msingi, Mungu wetu atatuangamiza sote kwa uzembe na ujinga wa kukosa kutumia fikra na elimu alizoturuzuku.

Tukisoma Maandiko Matakatifu kutoka Kitabu cha Muntakhab Ahadith, ukurasa wa 693, yanasema:

Urs bin Umairah Radhiallahu Anhu amesimulia kuwa Rasulullahi Swallallahu Alaihi Wasallam amesema:"Hakika Allah hawaadhibu watu wote kwa makosa ya waasi wachache, hadi hawa waasi waendelee kuasi na wale watiifu pamoja na kuweza kuwazuia, wasiwazuie. Kwa hili Allah huamrisha kuangamizwa wote watiifu na waasi."

Mamlaka zilizopo duniani zinaongozwa na wanadamu ambao pia ni viumbe wa Mwenyezi Mungu. Viumbe hawa Mungu wetu anawataka kutenda haki kwa wanaowaongoza na sio vinginevyo. Tawala zilizokwenda kinyume na maagizo ya Mungu, Mungu aliwaangamiza watawala hao.

Sisi watawaliwa tunapaswa kutii mambo halali yanayotuza uwepo wa Mungu kwa kufuata sheria husika zilizopo nchini na si vinginevyo.

Tusome Ilani ya CCM 2020, kurasa 161 - 168.

Nakumbuka siku ya Mashindano ya Qur'aan 2019, Rais wetu mpendwa Dkt John Pombe Joseph Magufuli alisema,ninamnukuu:"Ninawasihi viongozi wa dini na madhehebu yote nchini kuendelea kutufundisha sisi waumini wenu maandiko ya Mwenyezi Mungu na pia kutuhimiza kuyaishi."

"Kumcha Mungu kuna baraka zake."

Mwisho wa kunukuu.

Watanzania wenzangu ni lazima ifike mahali tupaze sauti ili wale baadhi ya watu tuliowaamini ambao wako kinyume na matakwa ya sheria zetu za nchi wakae pembeni kwani mara nyingi viongozi wasiotenda haki ni wafuasi wa Ibilisi wako pale kubomoa na sio kunenga. Na baadhi yao wanaamini kabisa sheria zilizopo nchini ni kwa ajili ya makapuku na sio wao. Hii ni dhana potofu na kamwe hatuwezi kuitii.

Tukisoma Maandiko Matakatifu kutoka Kitabu cha Muntakhab Ahadith, ukurasa wa 760, yanasema:Ali Radhiallahu Anhu amesimulia kuwa Rasulullahi Swallallahu Alaihi Wasallam amesema:"Hakuna utiifu kwa yeyote kwa kumuasi Allah, utiifu ni katika mema tu."

Mara nyingi watawaliwa huburuzwa sana kwa uzembe wao wa kukosa kujisomea na kujua haki zao kikatiba. Tusome katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania 1977, toleo la 2005, ukurasa wa 17, ibara ya 08 (1)(a)(b)(c).

Niliwahi kusoma Kitabu cha "The Amazing Results of Positive Thinking" ukurasa wa 19, mwandishi Dr. Norman Vincent alisema:"Sometimes there are strong negative elements in our lives that we refuse to clean out. We make feeble effort to put POSITIVE FORCE TO WORK, but they get stymied behind NEGATIVE forces."

Ni lazima tubadili mawazo yetu kwa kujiepusha na matendo ya kibaguzi na kiupendeleo ili tuweze kutenda haki kwa viumbe vya Mwenyezi Mungu ili siku ya kiama tusije kuishia motoni.

Utawala wa haki na usawa ndiyo Mungu anatuagiza watawaliwa kuutii na si vinginevyo. Tusome Kitabu cha Mwongozo wa CCM 1981, kurasa 138 - 139, kifungu cha 159 - 162.

Tukisoma Maandiko Matakatifu kutoka Kitabu cha Muntakhab Ahadith, ukurasa wa 617, kifungu cha 342, yanasema:Abu Hurairah Radhiallahu Anhu amesimulia kuwa Rasulullahi Swallallahu Alaihi Wasallam amesema:"Kuna alama tatu za mnafiki, anapozungumza husema uongo, na anapoahidi huenda kinyume, na anapoaminiwa hufanya hiyana."

Tukisoma Biblia Takatifu, Warumi 13:1, Maandiko Matakatifu yanasema:"Kila mtu na aitii mamlaka iliyo kuu kwa maana hakuna mamlaka isiyotoka kwa Mungu na hiyo iliyopo imeamriwa na Mungu."

Tukisoma Maandiko Matakatifu kutoka Kitabu cha Muntakhab Ahadith (Green Cover), ukurasa wa 773, kifungu cha 169, yanasema:Irbadh bin Sariyah Radhiallahu Anhu amesimulia kuwa Rasulullahi Swallallahu Alaihi Wasallam amesema:"Muabuduni Allah na wala msimshirikishe na chochote. Na watiini wale waliopewa mamlaka ya mambo yenu. Msizozane na Amiri (kiongozi) kuhusu amri zake, hata kama ni mtumwa mweusi. Shikamaneni vizuri na Sunna mnazozijuwa za Mtume wenu na Makhalifa wake waongofu, waliobarikiwa kwa uongofu na ishikeni kwa magego yenu njia ya haki."

Watanzania wenzangu, vitendo vya kibaguzi na kiupendeleo vinawanyima haki na usawa watu waadilifu na waaminifu. Ni lazima tuvikemee nchi hii ni ya kwetu sote sio ya watu wachache wanaojiona ni haki yao kula vizuri huku walio wengi wakila makombo.

Tuinuane wote, mwenye dalili za uelewa asaidiwe. Hii ndiyo haki. Nimepambana miaka mitano kuwezeshwa ili nijenge vyoo vya CCM na ofisi pasipo kuomba fedha za CCM ila nimegonga mwamba. Viongozi wengi hawainui watu wa chini wakati wao waliinuliwa na watu vile vile. Roho mbaya.

Tukisoma Maandiko Matakatifu kutoka Kitabu cha Muntakhab Ahadith, ukurasa wa 291, yanasema:Allah Subhanahu Wataala anasema, "Wala msichanganye haki na batili na mkaficha haki hali mnajuwa."

Na tukisoma tena ukurasa wa 118, Maandiko Matakatifu yanasema:"Ili kunufaika moja kwa moja kutoka kwa Allah Taala ni lazima kuamini kuwa mafanikio kamili katika dunia hii na Akhera yako katika kutii maagizo yake katika njia iliyoonyeshwa na Rasulullahi Swallallahu Alaihi Wasallam."

Tukisoma tena Maandiko Matakatifu, ukurasa wa 119, yanasema:Allah Subhanahu Wataala anasema, "Na atakaye mtii Allah na Mtume wake bila shaka amefanikiwa mafanikio makubwa."

Watanzania wenzangu ni wazi kuwa hatuwezi kuwa wote viongozi. Haiwezekani. Wale tunaowatanguliza mbele tunawaomba wawe wasikivu kwa watu wa chini. Waache majivuno na kujisikia kuwa wao ni bora kuliko tulio huku chini. Tunapolia vilio vyetu viwaguse watusaidie, vinginevyo wakienekeza kiburi wajue siku wakifa watafikia motoni, moto ambao kuni zake ni hao watu wenye kiburi na kujisikia bora kuwadharau wenzao.

Wazo likitoka huku chini linapuuzwa hadi lisemwe na mtu wa familia fulani superior ndio linasikilizwa. Viburi. CCM tuna miradi mingi na sisi tunaishi na uhai wa CCM huku chini tunajitolea wala hatuna posho. Pesa za CCM na maruzuku zimejaa tele, kwanini mwanachama wa CCM japokuwa akiomba tu kuwezeshwa bila kuomba fedha hasaidiwi?

Watu wako tayari kumuinuamtu ambaye hakuwahi kujitolea kukipigania chama kuliko mwanachama mfia chama. Hii ni dhambi kuwaumiza wanyonge.

Tukisoma Maandiko Matakatifu kutoka Kitabu cha Muntakhab Ahadith (Green Cover), ukurasa wa 483, yanasema:Abu Darda Radhiallahu Anhu amesimulia kuwa Nimemsikia Rasulullahi Swallallahu Alaihi Wasallam akisema:"Nitafuteni miongoni mwa wadhaifu, kwani mnaruzukiwa na kusaidiwa kutokana na wadhaifu wenu."

Wanachama wa CCM wa chini ni sisi huangaika huku ngazi za chini kusaka dola ila dola ikipatikana tunasahauliwa. Tumechoka na ukapuku. Tuwezesheni nasi tuifurahie nchi yetu. Tuache kiburi na dharau, tujengeeni basi japo kumbi za mikutano na vyoo.

Tukisoma Maandiko Matakatifu kutoka Kitabu cha Muntakhab Ahadith (Green Cover), ukurasa wa 483, yanasema:Harithah bin Wahab Radhiallahu Anhu amesimulia kuwa Nimemsikia Rasulullahi Swallallahu Alaihi Wasallam akisema:"Je, niwajulisheni watu wa Peponi? Kila aliye dhaifu na mwenye kudharauliwa, lakini kama akiapa juu ya jambo lolote kwa jina la Allah, Allah huifanya kiwe hivyo. Na je, niwajulisheni watu wa motoni? Kila mkaidi, mwenye majivuno na kiburi."

Huu wosia ninaoutoa kwa viongozi wa CCM. Munueni wanyonge wote tuliosimama mstari wa mbele kupambana kwa ajili ya Chama na si wale mnaowataka wenyewe ambao hawakipiganii chama wala kujitoa kwa hali na mali.

Ukiacha Chama na Viongozi, tuangalie masheikh, maustadh, mapadri na wachungaji mnaowapenda watu, msiwabague watu bali muwainue. Na nyie watu mnaoenda kuomba msaada kwa masheikh, maustadh, mapadri na wachungaji, mkisaidiwa msiwasahau.

Mungu anapenda wanyenyekevu.

Niseme tu kuwa Chama cha Siasa na Dini vinategemea wafuasi. Kiongozi anayemnyanyasa mfuasi asiyemjali, huyo kiongozi ni Kibaraka wa Ibilisi na hafai kuongoza watu.

Mungu Ibariki Tanzania, Mungu Wabariki Viongozi Wenye Hekima.

Wenu katika ujenzi wa Taifa,Ndugu Mwanachama Mpenda Haki


 
UONGOZI NI MWEPESI SANA.

NI KUFANYA MAAMUZI KUTENDA HAKI NA USAWA

KWA YALE TUNAYOKUBALIANA KUYAFUATA NA KUYATIMIZA PASIPO VITENDO VYA KIBAGUZI NA KIUPENDELEO.

Nakumbuka niliwahi kusoma Kitabu cha HOW SUCCESSFUL PEOPLE THINK uk 96

Mwandishi John C Maxwell aliwahi kumnukuu William Feather Mtunzi wa The business of life akisema,

" Before it can be SOLVED, a problem MUST BE clearly DEFINED."
" Too many people RUSH to solutions and as a RESULT they end up SOLVING THE WRONG PROBLEM."

Mwisho wa kunukuu

Tukisoma Kitabu cha 21 Irrefutable laws of leadership uk 75

Mwandishi John C Maxwell anatukumbusha,

" A leader's good Character BUILDS TRUST among his FOLLOWERS.
But when a leader BREAKS TRUST, he FORFEITS HIS ability to lead "

Mwisho wa kunukuu.



SIAMINI KATIKA HILO

KUMTANGULIZA MUNGU

NA KUFUATA TARATIBU HUSIKA

UKIJIEPUSHA NA VITENDO VYA KIBAGUZI NA KIUPENDELEO

NI WAZI UTAKUWA KIONGOZI BORA WA MFANO WA KUIGWA.

LEO HII KWA MAKSUDI TUNASHUHUDIA WATU ( BAADHI YA VIONGOZI WAKIZISIGINA KATIBA KANUNI MIONGOZO NA TARATIBU TULIZOJIWEKEA NA KUKUBALIANA KISHA NI HAO HAO BAADHI WANASIMAMA NA KUPAMBANA HADHARANI KUWASAIDIA MASWAHIBA ZAO

WENYE MAPUNGUFU MAKUBWA YA KISHERIA.

NIULIZE TU KIDOGO HAPA.

Katiba na vitabu vyetu vyote vya KISHERIA

Vinatamka WAZI

HAKUNA Mtu YEYOTE aliyeko JUU YA SHERIA.

Utakuta watu wametoa TAARIFA KWA MFANO WATU WA HUKU CHINI UTAKUTA WAMEOELEKA TAARIFA JUU KUWA MTU FULANI HAFAI.

WALE WA JUU BAADHI WANAKAA NA MTUHUMIWA KISHA WANAANDAA VIKAO WANAMPITISHA HUKU WAKIJUWA

HAFAI NA WANANCHI WAMELALAMIKA.

NAJIULIZA

WALE WAJUMBE WASOMI HUWA HAWAELEWI YA KUWA HAKUNA MTU ALIYE JUU YA SHERIA?

BADALA YA KUTOA USHIRIKIANO NA WATOA TAARIFA( WAFICHUA MAOVU)

NI HAO HAO HUANZA KUPANGA ZENGWE KUMWANGAMIZA ALIYETOA TAARIFA HUKU WAKISHIRIKI KUMPA CV ZA HOVYO MARA YULE KICHAA nk.

Nilichojifunza

UKIWA kiongozi MWAMINIFU MWADILIFU MPENDA HAKI NA USAWA NI LAZIMA UJIANDAE KWA LOLOTE KWANI WATU WALIO WENGI

WANAPENDA RUSHWA NA UNAFIKI NDIYO FARAJA KWAO.

TUNASOMA YESU KRISTO ALIJARIBU KUTUKOMBOA WANADAMU ILA ALIPATA SHIDA KUTOKA KWA KIZAZI CHA WAFUASI WA IBILISI.

MTUME (SAW) NAYE ALIPOTULETEA NENO
WAFUASI WA IBILISI WALIPINGA NA WALIMPIGA HADI WAKAMNG' OA MENO.

SOMO UKIWA MTENDA MEMA NA MFUASI WA MUNGU LAZIMA UJIANDAE KISAIKOLOJIA.


TUNAISHI KATIKA DUNIA AMBAYO Watu wabaya HUTAMANI SANA KUONEKANA WEMA MACHONI MWA JAMII PASIPO WAO KUELEWA KUWA JAMII

IMEELIMIKA NA INAONA KILA KITU ILA IKO KIMYA.



TUENDELEE KUREKEBISHANA KWA KUAMBIZANA UKWELI ILI TUBADILIKE. TUUIMARISHE UMOJA WETU NA DEMOKRASIA YA KWELI.

Nakumbuka Aug 2020

Mzee Joseph Butiku aliwahi kusema

Ninamnukuu,

" Demokrasia maana yake kwa neno jepesi la Kiswahili ni nafasi ya Wananchi kushiriki katika KUFIKIRI, KUFIKIRI, kutoa mawazo yao WAZIWAZI na kutenda katika kutekeleza yale ambayo WANAKUBALIANA, The right to participate."

Mwisho wa kunukuu

Watanzania tunapokubaliana wote kufuata SHERIA ni lazima iwe hivyo.

Tunapoingiza UBAGUZI NA UPENDELEO tunazisigina katiba zetu na kuzigalagaza HOVYO HOVYO kisha ni sisi sisi tunaanza KUWALAUMU MAHAKAMA Wakati sote kila mtu akitimiza WAJIBU WAKE Wa KUZILINDA SHERIA ambazo MIONGONI MWETU tumeapa KUZILINDA .

Tumfurahishe Mungu kwa kuwa wakweli.

Nakumbuka February 2020
Jaji Mkuu wa Tanzania
Professor Ibrahim Hamisi Juma

Alisema, ninamnukuu,

" Neno uamuzi wa Mwisho unaozungumzwa , maana yake nini, Maana yake ni kwamba KILA TAASISI YA UMMA INAGUSA HAKI SIO MAHAKAMA, Jambo linakuja LIMEHARIBIKA NDIYO linakuja Mahakamani."

Mwisho wa kunukuu

Nilivyomuelewa IKIWA WOTE TUTAHESHIMU MAANDIKO YETU NA KUTENDA HAKI ,KILA MTANZANIA KWA NAFASI ALIYOPO KUITENDEA HAKI NA KUJISOMEA YALE TULIYOKUBALIANA
HUKO MAHAKAMANI TUTAPUNGUZA MSONGAMANO .

Nakumbuka February 2020
Mzee Joseph Butiku alisema
Ninamnukuu,

" Chama imara Serikali imara inasimamia itikadi yake BILA KUBABAIKA, HICHO ndicho Chama IMARA na MSOME DOCUMENTS ZA CHAMA,
MSISEME MANENO YENU TUU, Mnaamka kila mtu ana la kwake,
SOMENI MAANDIKO YA CHAMA YAKO YAMEANDIKWA , SIO kila mtu ana la kwake, kila mtu ana la kwake" .

Mwisho wa kunukuu
Watanzania ifike Mahali tuone AIBU KUWAONEA WENZETU KWA MATUMIZI MABAYA YA MADARAKA YETU.

Niliwahi kusoma Kitabu cha HOW SUCCESSFUL PEOPLE THINK uk 170

Mwandishi John C Maxwell aliwahi kumnukuu Mkufunzi wa Kimarekani Horace Mann akisema,
" Be ashamed TO DIE until you have won some victory for humanity."

Mwisho wa kunukuu.

Tusome katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania 1977 uk 27 ibara 26 (1)(2) na uk 20 ibara 13(4)(5).

Tusome katiba ya CCM 1977 uk 01 - 03 ibara 05 (16)(17) na uk 05 ibara 08 (1)(2)

Tusome Kitabu cha Kanuni za Uongozi na Maadili Toleo 2017 uk 02 kifungu cha (iv)

Tuishi na WENZETU KWA SISI WENYEWE KUWA MIFANO YA KUIGWA NA SIO KUTANGULIZA UKALI.

Niliwahi kusoma Kitabu cha The 21 Irrefutable laws of leadership uk 248

Mwandishi John C Maxwell aliwahi kuandika,
"Learn to lead not just for yourself, but for the people who follow behind you.
And as you reach the highest levels DON'T FORGET to take others with you to be the leaders of tommorow."

Tusome Kitabu cha Kanuni za Fedha na Mali za Chama na Jumuiya zake uk 165 kifungu 14:3

Tukisoma Kitabu cha HOW SUCCESSFUL PEOPLE THINK uk 163

Mwandishi John C Maxwell anatukumbusha

" People with humility don't think less of themselves,
They just think of themselves less."

Tusome Kitabu cha Azimio la Arusha uk 04 kifungu cha (i)

Tukisoma Kitabu cha The 21 Irrefutable laws of leadership uk 212

Mwandishi John C Maxwell aliwahi kuandika,

" When you become a leader, YOU LOSE THE RIGHT to think about yourself."

Tusome Ilani ya CCM 2020 uk 161 - 168.
Nakumbuka February 2020
Mzee Joseph Butiku alisema,

Ninamnukuu,

"Naomba MSOME manaake, mara NYINGI sisi tunasahau KUSOMA SOMA. Kila mtu anapenda KUSEMA Mambo ya kwake,
Ni tabia nzuri ya KUFIKIRI lakini vile vile ni VIZURI KUFUATA MISINGI."

Rais wetu Mpendwa Dkt John Pombe Joseph Magufuli akiwa Mlale RUVUMA
Tarehe 08/04/2019 alisema

Ninamnukuu,

" Ni lazima Sisi Kama Taifa tufike Mahali TUJIULIZE
TUACHE UNAFIKI,
Kama Mahali TULIKOSEA ni lazima MAKOSA yale TUYABADILISHE,
Ni lazima kwa sababu sisi wote ni Watanzania."

Watanzania wenzangu kwa UMOJA WETU tukiamua kabisa KUMTANGULIZA MUNGU na TUKAAMUA kuyafuata maamrisho yake BILA UNAFIKI WA KUPENDELEANA NA KUBEBANA NINA UHAKIKA NCHI YETU ITAKUWA ZAIDI YA LIBYA WALIVYOKUWA.
SISI TUNA MALI NYINGI MNO HATUNA HAJA YA KUUKUMBATIA UNAFIKI.
TUTENDE HAKI NA USAWA
HUU NDIYO UONGOZI BORA NA SAFI WENYE KUACHA ALAMA ILIYO NJEMA.

TUWE WEMA TUUCHUKIE UNAFIKI KWANI UNATUJENGEA CHUKI HAUTENDI HAKI NA WATANZANIA WENGI WAMEAMKA NA WANAJIELEWA

TUSIWABURUZE

Tukisoma Maandiko Matakatifu ya Mwenyezi Mungu kutoka Kitabu cha Muntakhab Ahadith uk 372

Maandiko Matakatifu yanasema,

" Abu Hurairah Radhiallahu Anhu amesimulia kuwa Rasulullahi Swallallahu Alaihi Wasallam amesema,

" Yule ambaye anamkumbuka Allah KWA WINGI ANAOKOLEWA kutokana na UNAFIKI."


KIDUMU CHAMA CHA MAPINDUZI




Mathias Mugerwa Kahinga
🙏🏿🙏🏿🙏🏿🙏🏿🙏🏿🙏🏿🙏🏿

"
 

Wapo Baadhi ya Viongozi Walio Wengi Wasio Stahili Kuwa na Vyeo​

Wapo baadhi ya viongozi wengi wasio stahili kuwa na vyeo. Ndio walio vikalia vyeo vya kumuinua fukara. Itakuwa miujiza kwa fukara kuwa na maisha bora.

Nilisikika katika ulimwengu wa kiroho nikiunguruma kama simba kuwapinga wale wote wenye vyeo walioapa kuihifadhi, kuilinda, na kutetea Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya mwaka 1977, toleo la 2005, ikiwa ni pamoja na sheria zingine ndani ya nchi.

Watu wanatoa rushwa na inakuwa ni dhahiri, lakini watoa rushwa hao kununua vyeo wanalindwa kwa nguvu zote. Tumesahau kwamba tuliapa kutokuwa wabaguzi wala wapendeleaji. Watu wanapeana vyeo kiswahiba na sio kiuwezo wa kutenda kazi. Wanakula vinono na wao ndio wenye hasira kali kuliko mtu yule mwenye maisha ya dhiki tangu uhuru.

Tunatamka kulisaidia bara la Afrika huku tukiwa tu sisi tunao ongea lugha moja hatujasaidiana. Ubunifu tunao lakini watu hawatusaidii kwa hofu ya kwamba tukifanya vizuri wao watapoteza vyeo wavipendavyo kwa ajili ya kuvifanyia matanuzi. Hawana huruma kabisa.

Mfano miongoni mwetu, watu wamepata vyeo kutokana na wanavosema mafukara, ila kwa sasa wamewatema hao mafukara hadi nyakati za uchaguzi ndio watawaona tena kuwa na maana na sio sasa.

Nakumbuka kuna nyakati Pastor Sunbella Kyando wa The Reality of Christ Church alisema, "Saa nyingine mtu unaangalia kwenye eneo la siasa, machozi yanakutoka. Kuna wakati mwingine kuna vitu hatukutakiwa kuomba, kwa sababu tunaomba kwa sababu kuna watu walitakiwa wakae kwenye hayo maeneo (ya siasa) na hawajakaa, na inatugharimu kuanza kumuomba Mungu rehema. Lakini laiti tunge simamisha watu ambao wamekaa kwenye ufalme (watu hao) wangefanya vinavyotakiwa kufanyika."

Mwisho wa kunukuu.

Utaona baadhi ya viongozi wakijinasibu kama watu wanaomjuwa Mwenyezi, lakini matendo yao yako kinyume kabisa. Ni kama wamevaa ngozi ya mwanakondoo huku wao wakiwa ni mbwa mwitu. Hawana msaada hata kwa mawazo mema yanayoweza kuinua hali za wanavosema mafukara.

Nimebuni miradi tele. Nimehangaika huu ni mwaka wa 15. Nina kiu ya kuacha alama ndani ya jamii. Mimi sisikilizwi, ila machawa wakiongelea mambo yasiyo ya maana wanapongezwa na kuitwa wakale kwenye mahoteli makubwa.

Tumefika mahali ambapo mtu akitamka neno Mwenyezi Mungu tu, basi anaonekana kama ni mcha Mungu kumbe ni mnyambilisi. Hana msaada wowote kwa mafukara zaidi ya kuwatumia kwa maslahi yake binafsi.

Mheshimiwa Philipo Isdor Nzabayanga Mpango, Makamu wa Rais wa Tanzania, nakumbuka tarehe 29/06/2021 katika mkutano wa BAKWATA ufanyikao kila baada ya miaka mitano alisema, "Mimi naamini kwa dhati kabisa, kama watu wakishika mafundisho ya dini zao vizuri (naamini) maovu mengi yatapungua sana. Na ndio maana napenda kurejea ombi langu ninalolitoa mara kwa mara (pale) ninapokutana na viongozi wa dini zote kwamba muisaidie serikali kujenga jamii yenye maadili mema."

Mwisho wa kunukuu.

Uadilifu wa viongozi kwa jamii uko ndani ya viapo vyao na ndani ya miiko ya uongozi. Katika uongozi umchao Mwenyezi Mungu, huwa na masikio makubwa kusikiliza vilio vya watu mafukara, na kiongozi anayelalamikiwa na mafukara kwa kutotenda haki hutolewa.

Sasa hivi kuna vyeo visivyogusika. Mfano, M/kiti wa mtaa, diwani, mbunge. Utakuta watu maeneo baadhi katika ulimwengu wa kiroho mafukara wamewachoka watu fulani na katiba inakataza kubebana ila waovu wanabebwa na kulipwa posho.

Kwa mazingira haya, viongozi wa dini watakuwa hawana la kuamua bali kusubiri huruma za wenye viapo kuchukua hatua.

Padre Dkt Faustine Kamugisha wa Kanisa Kuu la Bukoba, Jimbo la Bukoba, nakumbuka tarehe 27/05/2022 alisema, "Shetani ni mpiga maneno. Anaitwa baba wa uongo. Lakini Yesu anafanya vitu vinaonekana."

Mwisho wa kunukuu.

Watu wamekuwa wabaya. Wanajisikia kumuumiza fukara na mtumishi wa umma huku watu wenye vinasaba nao wakiwa wanalalamikiwa na mafukara na hakuna hatua zinazochukuliwa.

Mheshimiwa Mwanaidi Ally Khamis, akiwa Naibu Waziri wa Maendeleo ya Jamii Jinsia na Makundi Maalumu, nakumbuka tarehe 27/05/2022 alisema, "Tatizo letu tumekuwa waoga wananchi. Hata sijui tunatishwa na kitu gani ambacho kinatupa hofu tusiweze kuyaeleza yale mambo ambayo yanatokea katika mitaa yetu."

Mwisho wa kunukuu.

Ujasiri wa kusema tunao na wala sisi sio waoga ila kama unasema halafu hakuna hatua zinazochukuliwa, maana yake sisi wasemaji tunafitinishwa na hao tuwasemao wasiochukuliwa hatua.

Mfano tu huko Nkiwanzeeezaa kuna diwani wananchi wanamlalamikia kwa kuwabaka mabinti wa shule za msingi na sekondari katika ulimwengu wa kiroho, kuwabaka mabinti na kuwaonyesha wapambe zake katika ulimwengu wa kiroho, kuuza madawa ya kulevya katika ulimwengu wa kiroho, kutembea hovyo hovyo kama kuku wa mdondo na wake za watu katika ulimwengu wa kiroho, kuwadhulumu mayatima nyumba katika ulimwengu wa kiroho, kudanganya chama kwa kutoa taarifa za uongo ili apate cheo, kupata udiwani kinyume na matakwa ya katiba ya chama katika ulimwengu wa kiroho, na mengine mengi lukuki ya hovyo ikiwa na kutokusoma mapato na matumizi maeneo yote aliyowahi kuwa kiongozi tokea kuzaliwa kwake katika ulimwengu wa kiroho.

Ajabu na kweli, bado diwani huyu yuko madarakani. Kwa hali hii, watu wasemeje katika ulimwengu wa kiroho?

Diwani amefika mahala anaogopa. Hawezi tena kuitisha mkutano wa hadhara kwa hofu ya kuzomewa na kudhalilika kwa jinsi alivyochokwa na wananchi.

Mheshimiwa Albert John Chalamila, Mkuu wa Mkoa wa Dar, nakumbuka tarehe 21/11/2023 alisema, "Sisi viongozi aliotuteuwa (Mheshimiwa Rais kumsaidia kazi), tukifanya vitu vya hovyo na watumishi wenzetu, (tujuwe) wananchi wanamchukia Rais aliyetuteuwa sisi. Tukifanya matendo mema, matendo ya huruma, matendo yanayogusa watu (inakuwa) ni sifa kwa Rais wetu."

Mwisho wa kunukuu.

Tuonyeshe sifa njema kwa Rais kwa kuchukua hatua kwa mujibu wa viapo vyetu na kwa kuizingatia katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya mwaka 1977, toleo la 2005, ibara 34(4), ibara 35(1), ibara 26 yote, na ibara 9 a, b, f, h.

Shekhe Walid Alhad Kawambwa, Kaimu Shekhe Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, akitoa mawaidha tarehe 13/03/2023 alisema, "Vyeo hivi vinaharibu watu hasa ikiwa ulikuwa unavitaka tangu zamani. Kuna watu wamepagawa kwa mazoea mazoea tu kisha Mungu akawaonja, akawapa madaraka. Wao wenyewe hawakujua kama ule ni mtihani. Wakapiga mbizi katika bahari ya kujitahidi, lakini wakatoka katika bahari hiyo hawakulowa hata tone moja."

Maneno haya yanataka darsa ndefu wakati hatuna. Mwisho wa kunukuu.

Nakumbuka tarehe 21/11/2023, Mheshimiwa Albert John Chalamila, Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, alisema, "Wananchi na ninyi iko siku pia mtanielewa vizuri, kwamba Mkuu wa Mkoa ni Mkuu wa Mkoa wa aina gani. Kwanza napenda uwazi, halafu nachukia ubabaishaji, na ninaweza nikakukurupukia hadharani bila hata haya kwa umri wako, kwa umbile lako, na kwa umbo lako. Kwa hiyo nikisikia mahali kuna ubabaishaji, kuna rushwa zisizoangalia haki za watu, hakuna commitment, watu wanakuwa hawana huruma, inakuwa ni mbaya. Mimi kwenye mazingira kama hayo

Tumuunge Mkono Mheshimiwa Rais kwenye Vita vya Kupambana na:​

  • Umaskini
  • Ujinga
  • Maradhi
Hasa ujinga, tukiuchekea utatuangamiza. Tumeishajua ujinga ni adui, tusiuchekee chekee.

Mheshimiwa sana, kiongozi mstaafu, mkuu wa majeshi mstaafu, mwenye hofu ya Mungu kwa vitendo, mcha Mungu wa kweli, Mheshimiwa Venance Salvatory Mabeyo, akifanya mahojiano katika eneo la Itega - Dodoma alisema:

"Adui huwezi kumchekea. Si ndiyo? Basi, adui ukimchekea chekea atakumaliza wewe kabla hujammaliza."
Mwisho wa kunukuu.

Tuache kuwachekea maadui. Wanatumaliza kifikra mpaka baadhi yetu hatuonyeshi heshima kwa katiba, kanuni, miongozo na taratibu.

Naye Shekhe Walid Alhad Kawambwa, Kaimu Shekhe Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, akitoa mawaidha tarehe 13/03/2023 alisema:

"Basi nimeona nimalize kwa maneno hayo."
Mwisho wa kunukuu.

Nikashtuka kutoka ndotoni nilipokuwa naota, nikiwa mwili umeishiwa nguvu huku nikisema blabla hazifai. Kila kiongozi anaposema asimamie kauli zake zifanyike kwa vitendo, ikiwemo kuchukua hatua kwa vitendo.

Kidumu Chama Cha Mapinduzi.

Mathias Mugerwa Kahinga
 
ELIMU KWA UMMA LIWE NI JAMBO LA MSINGI NA ENDELEVU KUTOKA KWA KILA MMOJA WETU ILI KULINUSURU TAIFA LISIZIDI KUANGAMIA

Nilisikika katika ulimwengu wa kiroho huko ndotoni nikiunguruma kama simba aliyeshika windo. Nikaanza:

Katika maisha yetu ya kila siku tunakutana mara kwa mara na baadhi ya watu wajinga ambao wanao ujasiri wa kuuamini ujinga wao na kufanya jitihada za kuueneza ujinga ule kwa jamii ili ukubalike kuwa ndiyo mfumo sahihi wa kimaisha. Wanaamini kabisa ujinga ule unaweza kulisaidia taifa.

Tunalo jukumu sasa la kulinyoosha taifa na kuwapa watu elimu ili wasiendelee kupotoka kwa ujinga unaozagaa unaopelekea watu kuishi kama vipofu wakukataa ukweli na kuukumbatia uongo. Tumefika mahala ambapo mtu mkweli anachukiwa na mtu muongo anashangiliwa. Kuna watu ukiwaangalia wana mionekano kama wanaona ila katika ulimwengu wa kiroho ni vipofu kwani tayari hawaioni kweli bali batili imewawekea wingu machoni mwao.

Pastor Sunbella Kyando wa The Reality of Christ Church akitoa mahubiri, nakumbuka tarehe 22/09/2021 alisema:

"Usipokuwa na maarifa unakuwa blind."
Mwisho wa kunukuu.

Katiba ya CCM 1977 toleo 2022 ukurasa 10-11 ibara 15(3)(6), ukurasa 07 ibara 12(1)(a) ili kwenda ukurasa 152 vifungu (3)(6)(8). Yote hii ni kuonyesha ni kwa jinsi gani elimu inastahili kupewa kipaumbele kwa kuipata na kisha kuwaelimisha wengine.

Mheshimiwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan nakumbuka tarehe 12/08/2022 akiwahutubia wananchi katika Uwanja wa Samora - Iringa alisema:

"Ndugu wananchi, elimu ni msingi wa maisha na maendeleo kwa kila taifa."
Mwisho wa kunukuu.

Tuielimishe jamii ielewe mifumo ya nchi na tuisisitize jamii kuitii mifumo huku na sisi waelimishaji tukiwa mstari wa mbele kuyatenda hayo tuyaelimishayo kwa vitendo.

Professor Joyce Ndalichako akiwa Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu kazi, ajira, vijana na watu wenye ulemavu nakumbuka tarehe 20/07/2022 alisema:

"Masuala ambayo yanahusiana na elimu, tutaimarisha utoaji wa elimu kwa umma ili watu wawe na uelewa na wasiwe na hisia potofu."
Mwisho wa kunukuu.

Tukisoma Ilani ya CCM 2020 ukurasa 229 ibara 181, ibara 182, ukurasa 124 ibara 78, ukurasa 128 ibara 80, ukisomwa na ukurasa 08 ibara 10 na 11 kwa msisitizo.

CCM inatambua kuwa raslimali watu ndiyo nyenzo muhimu ya maendeleo ya kijamii na kiuchumi. Aidha, CCM inaamini kuwa elimu bora ndiyo nyenzo muhimu ya kuijenga, kuilea na kuendeleza raslimali watu ili ziweze kuchangia kikamilifu katika ujenzi wa taifa.

Mwisho wa kunukuu.

Tusome Ilani ya CCM 2020 ukurasa 152 ibara 102, ukurasa 299-300 ibara 252(e). Ilani ya CCM 2020 ukurasa 04-05 ibara 07 ili kupata uhalali wa kwenda kusoma Ilani ya CCM 2015 ukurasa 296 ibara 188 huku tukizingatia ibara 177 ukurasa 230.

Mheshimiwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan nakumbuka tarehe 13/05/2022 katika maadhimisho ya miaka 10 ya Tanzania Human Rights Defenders Network (THRDC) alisema:

"Elimu kwa umma ni muhimu sana kwa sababu mtakapoelimisha umma, kazi yetu (watetezi wa haki) itakuwa ndogo sana ya kutetea watu. Hizo rights hazitavunjwa sana. Kila mtu atakuwa anajua wajibu wake unavyokaa wa kikatiba, haki yake, wajibu wake. Kwa hiyo, rights hazitavunjwa sana. Kwa hiyo, ongezeni hilo la elimu kwa umma."
Mwisho wa kunukuu.

Wanachama wa CCM ni lazima tujielimishe sana ili tukwepe tabia inayoshamiri ya sisi mafukara kulishwa ubwabwa na kupewa buku jero huku wanaotupatia vitu hivyo wakijenga migorofa na mijumba ya maana huku sisi tukiaminishwa kuwa ni watu wa kutumiwa tu na kulishwa ubwabwa huku maisha yakitupa kichapo na kuishi kama tuko dampo tumetupwa. Mwl. Nyerere mwenyewe alikuwa msomi na hakukubali wajanja wachache wawa brain wash walio wengi.

Wewe usiyesoma unayefurahia kulishwa ubwabwa, unawezaje kujisifu kuwa unamfuata Baba wa Taifa Mwl. Nyerere wakati matendo yako ni matendo ya hovyo ya kuchukia mambo ya elimu na kujiweka katika kutumia hisia binafsi kuwaongopea wenzio.

Professor Issa Shivji nakumbuka tarehe 13/04/2022 katika hafla ya uzinduzi wa vitabu kwenye kuadhimisha miaka 100 ya kuzaliwa kwa Baba wa Taifa, Shule ya Uongozi Kibaha alisema:

"Mwl. (Nyerere) mwenyewe alikuwa msomi. Alikuwa mwanazuoni mwenye kipaji kikubwa. (Mwl. Nyerere) alikuwa anasoma sana."
Mwisho wa kunukuu.

Na ninyi wasomi mnaojifanya mmesoma, onyesheni ni kwa jinsi gani mnaweza kuwainua wanachama wa CCM mafukara na sio kututisha na Kiingereza kingi huku mkiwa hamfanyi jitihada zozote za kuwainua wanachama wenzenu wanaoaibika na kuitwa ombaomba.

Mheshimiwa Albert John Chalamila wakati huo akiwa Mkuu wa Mkoa wa Kagera nakumbuka tarehe 03/09/2022 alisema:

"Sitaki Kiingereza wala sitaki makaratasi, nataka namna gani utakavyoitumia elimu yako kuibadilisha kuwa maendeleo."
Mwisho wa kunukuu.

Mheshimiwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan katika hafla ya kukabidhi magari kwa mamlaka za maeneo ya utekelezaji kwa shughuli za TASAF Tanzania Bara na Zanzibar, nakumbuka tarehe 01/06/2022 alisema:

"Naomba sana, mbali ya kazi mnayoifanya, fanyeni kazi ya elimu kuwatoa watu kwenye umaskini wa fikra na waishi maisha ambayo yanaeleweka."
Mwisho wa kunukuu.

Elimu itasaidia hata mabinti zetu ndani ya chama kuto kutumiwa hovyo kwa maslahi ya wajanja. Wanu Hafidh Ameir, Mwenyekiti wa Wanawake Initiative Foundation Zanzibar na mtoto wa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan, nakumbuka tarehe 19/06/2022 alisema:

"Elimu ndiyo nyenzo muhimu itakayomsaidia kijana, hususan msichana, kuendesha maisha yake na kuepuka unyanyaswaji."
Mwisho wa kunukuu.

Mfano, diwani wa Nkiwansensaaaa asiye na elimu hutumia hila kuwahadaa mabinti wa shule za msingi na sekondari, na wengine huwatoa mimba guest na wengine kuwapiga picha za utupu na kisha kuonyesha wapambe zake. Akiulizwa, diwani huyu hujibu:

"Wasichana wananitaka wenyewe, sasa nifanyeje?"
Diwani amesahau kiapo cha maadili alichokiapa. Mabinti hawa tukiwapa elimu watajielewa na kamwe hawatachezewa tena. Tukimpenda Mwenyezi Mungu, tutapenda maamrisho yake. Mwenyezi Mungu anatutaka pia tuikamate sana elimu.

Apostle Deonis Mutalemwa Bushir wa ECG Church nakumbuka tarehe 26/05/2022 akitoa mahubiri akiongelea maagizo ya Yesu Kristo kwa wanadamu alisema (Mathayo 12:50):

"Kwa maana yeyote atakayefanya mapenzi ya Baba yangu aliye mbinguni, huyo ndiye ndugu yangu na umbu langu na mama yangu."
Mwisho wa kunukuu.

Mwenyezi Mungu anataka tusome tuwe na elimu ili udugu wetu na Yesu Kristo ushamiri. Sisi baadhi tumeikataa elimu, tumejiweka rehani kwa watoa ubwabwa. Tunajichekesha hovyo kwa wenye fedha na kuwachukia wanaotukumbusha haki zetu zilizo ndani ya katiba, kanuni, miongozo na taratibu. Tumemkufuru Mwenyezi Mungu na kuzifurahia kufuru zetu kwa ujinga wa kulikataa neno la Mungu.

Biblia Takatifu Hosea 4:6:

"Watu wangu wanaangamizwa kwa kukosa maarifa, kwa kuwa wewe umeyakataa maarifa, mimi nami nitakukataa wewe."
Mwisho wa kunukuu.

Biblia Takatifu Mithali 4:13:

"Mkamate sana elimu, usimuache aende zake, mshike maana yeye ni uzima wako."
Mwisho wa kunukuu.

Sasa wewe jitie wazimu kamata sana ubwabwa na buku jero, watajirisha wajanja ili ukifa ukafikie jahannam kwa ujinga wa kupangwa safu na kuzikubali kama umerogwa kwa kukosa elimu ya katiba, kanuni, miongozo na taratibu. Mtume Mohammad SAW aliambiwa asome, na baada ya kusoma akatuambia umma wake tuende mpaka Uchina kuitafuta elimu.

Wewe vitabu vya chama viko, huvisomi, ukalia kuendekeza ubwabwa na besenga, unatajirisha watu wenye roho mbaya wasio kufikiria wewe wala familia yako kwa ujinga tu ulio uendekeza wa kuto kusoma na kuujuwa ukweli.

Mheshimiwa Ridhiwani Kikwete akiwa Naibu Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, nakumbuka tarehe 29/08/2022 alisema:

"Ninafikiri hata kwenye Qur'an, mtanisahihisha mashekhe wangu kama nitakosea, aya ya kwanza iliyoshushwa ni kwamba Mtume wetu (Mohammad SAW) anaelekezwa kwamba asome."
Mwisho wa kunukuu.

Wewe unayelishwa ubwabwa na kupewa buku jero bila kusoma katiba, kanuni, miongozo na taratibu, unamfuata mtume gani wewe!?!?

Uhuru wako umeuweka rehani kijinga kijinga mpaka uamuliwe cha kufanya na watu walioiteka akili yako kwa ujinga tu huku wakikuongopea na kijicheo kitokanacho na rushwa kisicho na uhalali wa wananchi walio wengi.

Umekubali kuwa mtumwa kwa ujinga wa kukataa kujibidiisha kujuwa maandiko ya chama na kuyaishi. Tusome katiba ya CCM 1977 toleo 2022 ukurasa (i), kisha ukurasa (iv)-(vi), then ukurasa 02 ibara 5(4) ili kupata uhalali wa kwenda kusoma kitabu cha Nukuu za Kiswahili za Mwalimu ukurasa 148.

Mwl. Nyerere aliwahi kunukuliwa akisema:

"Elimu ni kama mlima mkubwa unaofika mawinguni. Kila unavyopanda, ndivyo unavyoona vizuri zaidi upeo wa macho yako. Tusipoazimia kujielimisha, tutaachwa nyuma. Tena uhuru wetu utategemea tu hutuma za watu wengine na mataifa mengine (na wala) sio uwezo wetu sisi wenyewe."
Mwisho wa kunukuu.

Nikashtuka kutoka ndotoni huko katika ulimwengu wa kiroho huku nikiwa nafoka foka hovyo, someni nyie! Tusikubali kufokewa wala kutishwa. Uongozi ni unyenyekevu. Ukiona kiongozi anakufokea, anakutisha, kinyume na alivyoapa, huyo ujue ni mbwa mwitu aliyevaa ngozi ya mwanakondoo.

Kidumu Chama Cha Mapinduzi

Mathias Mugerwa Kahinga
 
TUSIDANGANYANE KAMWE PESA NDIYO SABUNI YA ROHO.

Niliwahi kusoma Kitabu cha Nukuu za Kiswahili za Mwalimu uk 199

Mwl JK Nyerere aliwahi kusema,

" ....Mchungaji ambaye kondoo ni mali yake ATAPIGANA NA MBWA MWITU, ijapo anajuwa ni hatari kubwa."

Wanaccm wenzangu tubadilike tuache kupoteza muda wetu KUAMINISHANA UJINGA ya kwamba pesa ni IBILISI sio Kweli. Badala yake mijadala yetu kichama iliyo mingi ILENGE KUIMARISHA PATO LA CHAMA NA SISI WANACHAMA KUWA NA MAPESA TELE MIFUKONI MWETU. Tukifanya hivi tutakuwa tunatekeleza siasa safi ZA KIUTU na tutakuwa tunamfurahisha Mungu wetu kwa KUWAJAZA MAPESA WENZETU KAMA TUNAVYOPENDA KUJAZA MAPESA MIFUKONI MWETU WALE WAJANJA WABINAFSI WACHACHE. TUSEME TUSIKIKE TUACHE UBUBU.

Niliwahi kusoma Kitabu cha 100 Ways to Motivate yourself uk 10

Mwandishi Steve Chandler aliwahi kuandika,

"All of our thoughts and feelings won't matter anymore when we are on our DEATH BEDS . What will matter is the actions we took and the different that it made.

Wanaccm wenzangu tusimame tuache UOGA wa kijinga na wa kipumbavu tuseme UKWELI kwani tulio wengi TUNAUMIA SANA NA HALI ZA BESENGA NA OMBA OMBA ZITOKANAZO na hali ya UFUKARA, UMASKINI NA UDUNI wa kukosa michongo ya kupata fedha kwani WAJANJA WACHACHE TUNAOWAAMINI NA KUWAPA NYADHIFA mara nyingi WANATUACHA SOLEMBA NA KUJALI NAFSI ZAO NA VIKARAGOSI VYAO.

Niliwahi kusoma Kitabu cha Build Self confidence uk 09

Martin Luther King aliwahi kusema,

" If a man hasn't discover something, that he will die for, he isn't fit to live."

Wanaccm wenzangu katiba yetu ya CCM 1977 toleo 2017 uk 143 inatutaka tuseme UKWELI Daima.

Niliwahi kusoma Kitabu cha How successful People Think uk 80

Mwandishi John C Maxwell aliwahi kuandika,

" The truth will set you free - But first it will make yuo ANGRY."

Wanaccm wenzangu wenye UWEZO na NYADHIFA WAONEENI HURUMA WANACCM WENZENU MASKINI NA MAFUKARA , MSIWACHUKULIE POWA KUWATUMIA KAMA MAJAMNVI KUWAKANYAGA ILI MPATE VYEO VYENU MJITAJIRISHE NA NAFASI ZENU HUKU WENZENU WAKIBAKI HOE HAE MKIENDELEA NA TABIA HIYO YA KUBANIANA NA KUJINUFAISHA MTAISHIA JAHANNAM.

Neno la Mungu Biblia Takatifu Wafilipi 2 ; 4 - 5 linasema,

Kila mtu asiangalie Mambo yake mwenyewe, bali kila mtu aangalie Mambo ya wengine.

Iweni na nia hiyo ndani yenu ambayo ilikuwamo pia ndani ya KRISTO YESU.

Katiba ya CCM 1977 toleo 2017 uk 1 ibara 5(1)

Malengo na madhumuni ya CCM ni kushika DOLA.

Hii maana yake ni KUSHIKA FEDHA ILI TUWEZE KUYATEKELEZA YALE TULIYO AHIDI KWA WATANZANIA ikiwa ni pamoja na KUUONDOA UMASKINI KABISA.

DOLA tukishaipata Wachache WANAISHI VIZURI WALIO WENGI WANACCM WANAKUWA HOE HAE.

Hakuna japo katenda kokote kuletwa HALMASHAURI ZA CCM NGAZI ZA SHINA HADI WILAYA , tunaanza KUWANUFAISHA WALIOKUWA WAKITUPONDA NA KUTUTEMEA MATE.HALI YA OMBAOMBA NA BESENGA INASHAMIRI KANA KWAMBA TUNA LAANA YA KUPAMBANIA KUSHIKA DOLA.

Ilani ya CCM uk 235 kifungu 187 kinatutaka tubuni miradi ila miradi ikibuniwa PESA YOTE INAPAA JUU HUKU CHINI ZERO.

Tukisoma Kitabu cha Sera ya CCM ya kujitegemea kimapato na kiuchumi 2014 kinahimiza wanaccm wanaweza kuingia UBIA NA CCM ili wasaidie kuinua pato la CCM ila bado tunabaniana na matokeo UFUKARA HUU TUTAENDELEA KUWA NA VIONGOZI NGAZI YA KATA NA JIMBO WALIO WENGI WAJANJA WAJANJA WENYE VIPATO HARAMU ILA WENYE UFINYU WA UPEMBUZI WA MAMBO MAKUBWA NA NDIYO MWANZO WA KUDUMAZWA WANACCM MAFUKARA WENYE UPEO MPANA WA KULETA MAGEUZI MAKUBWA KIUCHUMI NDANI YA CCM.

Wanaccm WAFIA CHAMA imefika mahali tumekuwa kama BURUDOZA LA KUCHONGA BARABARA ILA BARABARA ILE IKIKAMILIKA , BURUDOZA HUBEBWA NA KUFICHWA ILI LISIHARIBU LAMI japo liliumia kufyeka miti na mamibuyu makubwa.

Tukisoma Kitabu cha Binadamu na Maendeleo uk 19

Mwl JK Nyerere aliwahi kuandika,

" Wanachama wa Chama cha kisiasa ni muhimu sana kuliko watu wengine kama anafanya kazi yake na watu wanamkubali kama mmoja wao na wanamuendea Wakati wa shida, mawazo, ushauri na utatuzi."

Na tukisoma tena uk 134 Mwl JK Nyerere anaandika,

Kutafuta Maendeleo kwa njia za kibepari KUNAPINGANA na haki za Binadamu na heshima kwa wote.
Ubepari watu wengi watafanya kazi ila watu wachache WATANUFAIKA kwa jasho lao. WACHACHE watakula KARAMU nzuri na walio wengi WATAKULA MAKOMBO.

Pia tusome MWONGOZO WA CCM 1981 uk 104 kifungu 110.

Tukisoma tena Kitabu cha MWONGOZO WA CCM 1981 uk 103 kifungu 108

" Serikali ndicho Chombo kikuu cha Utekelezaji wa siasa ya chama.
Chama kinaiongoza Serikali na VYOMBO VYAKE.

Kwa msingi huu SISI WAONGOZAJI WA SERIKALI TUNAKWAMA WAPI WAKATI TUNA VYEO VIKUBWA ILA NI MAFUKARA KIVIPATO.

Niwaombe MAKADA mlio Serikalini tusaidieni WANACCM NASI TUCHANGAMKE MIFUKONI kwani Daima tuko bega kwa bega kwenye mapambano ya KUSAKA DOLA, TUURUDIE UPENDO WA MUNGU TUOMBEANE KILA MTU AWE NA FEDHA SIO DHAMBI KWA WANA CCM KUENDESHA PIKI PIKI NA MAGARI KWA WALIO WENGI.

WACHACHE MSITUNYANYASE MTUINUE ILI TUACHANE NA NTIMA NYONGO.

Niliwahi kusoma Kitabu cha Nukuu za Kiswahili za Mwalimu uk 244

Mwl JK Nyerere aliwahi kusema,

....kila mtu hupenda fedha nyingi na hakuna mtu yeyote, tangu Waziri mpaka kibarua ambaye hapendi pato lake lizidi kuongezeka kila siku.

Tukisoma tena Kitabu cha Nukuu za Kiswahili za Mwalimu uk 229

Mwl JK Nyerere aliwahi kusema,

" Watu wa juu wasipojali tofauti iliyopo BAINA YA HALI ZAO NA HALI ZA WATU WA CHINI, Basi hapo ni kuwahimiza watu wa Tanganyika kufanyakazi ni kuwahimiza WAWAFANYIE KAZI WATU WA JUU.

Tusome pia Kitabu cha Awamu ya Tatu ya Mradi wa kuimarisha chama ili tuone Comrade JM Kikwete uk 07 alivyoandika.

Awamu hii tunaye Mwenyekiti CCM Taifa Comrade John Pombe Joseph Magufuli ambaye anaumiza kichwa ili TANZANIA ISONGE MBELE KIMAENDELEO TUSIMCHOSHE NA SISI HUKU CHINI TUFUNGULIANE MIKANGO YA RIZIKI TUSIBANIANE TUKAMTUKUZA SHETANI KWA KUENDEKEZA UBINAFSI.

Tukisoma Kitabu cha Sera ya CCM ya kujitegemea kimapato na kiuchumi 2014 uk 19

Maamuzi mbalimbali ya Halmashauri KUU YA Taifa, yamedhihirisha suala la chama kujikwamua kiuchumi kupitia vyanzo vya MAPATO vya uhakika limejadiliwa mara nyingi sana na kuelekeza hatua za kuchukuliwa ila BADO halijafanikiwa kupata Utekelezaji wa kukidhi azma hii katika ngazi mbalimbali.

Tukisoma Kitabu cha Nukuu za Kiswahili za Mwalimu uk 255

Mwl JK Nyerere aliwahi kusema,

" Wachache wanapoonekana wazi wazi wakiogelea katika UTAJIRI wa wizi na magendo na unyonyaji, wakati wengine wanakabiliana na dhiki ya Kweli Kweli, si rahisi kulinda umoja na si rahisi kwa Serikali kufanikiwa katika jitihada zake za kufufua uchumi wetu.

Tukisoma tena Kitabu cha Nukuu za Kiswahili za Mwalimu uk 238

Mwl JK Nyerere anasema,

" Mipango yetu ni mizuri, lakini Utekelezaji wake ni mbaya siku zote."

Mwl JK Nyerere anatusisitiza tena kwenye Kitabu cha Nukuu za Kiswahili za Mwalimu uk 176

".....kama mnao uwezo wa KUTAJIRIKA, nawaombeni, " fanya wote tutajirike" Hivi mtajirike peke yenu, tutajirike wote. " Wapi ni rahisi watu wachache kutajirika".

Niliwahi kusoma Kitabu cha The Power of your Subconscious Mind uk 112

Mwandishi Dr Joseph Murphy Ph D DD aliwahi kuandika,

" You are not here to live in a hovel, dress in rags and go hungry, you should be happy, prosperous and successful.
Do not ever regard money as EVIL OF FILTHY. If you do you cause it to take wings and fly away from YOU. Remember that you loose what YOU CONDERM.
YOU CAN NOT ATTRACT WHAT YOU CRITICISE.

Tukisoma tena Kitabu cha The Power of your Subconscious Mind uk 110

Mwandishi DrJoseph Murphy Ph D DD aliwahi kuandika,

" It is your right to be rich. You are here to lead the abundant life and be happy , radiant, and free.
You should, therefore have all the money you need to lead a full happy and prosperous life.

Makada walio ndani ya CCM na MAKADA WALIO SERIKALINI ILI KUHAKIKISHA ILANI INATEKELEZEKA , TUPENDANE, TUJALIANE TUSIZIBIANE RIZIKI , TUPEANE MICHONGO ALIYESHIBA AMKUMBUKE MWANACCM FUKARA NA OMBA OMBA ILI JITIHADA ZIWEPO TUKWAMUANE KWENYE LINDI LA UFUKARA.HUU NDIYO UPENDO WA DHATI USIO NA UNAFIKI NDANI YAKE.

Tukisoma Biblia Takatifu Wagalatia 5; 14- 15 Neno la Mungu linasema ,

" Maana Torati yote imetimilika katika Neno moja , nalo ni hili , UMPENDE JIRANI YAKO KAMA NAFSI YAKO.

Lakini MKIUMANA NA KULANA, ANGALIENI MSIJE MKAANGAMIZANA.

Tukisoma Qur aan Tukufu Kitabu cha Fadhila za Sadaqaat uk 566, Neno la Mola wetu linatuasa,

" Enyi watu mliopewa starehe za Dunia ambayo HAITADUMU, kumbukeni ni UPUMBAVU MTUPU KUDANGANYWA na kivuli kinachotembea.

Tukisoma Kitabu cha Fadhila za Sadaqaat uk 832 - 833 Neno la Mungu wetu linatueleza

" Ewe MPUMBAVU uliyepumbazwa na furaha za Dunia hii, ! Tafadhali FIKIRIA na uchukue amali njema kutoka Dunia hii ili zikufae huko Akhera!".

Tukisoma Qur aan Tukufu Kitabu cha Tarjuma ya Sahih Al Bukhari uk 24 kifungu (13)

Amehadithia Anas (RAA) kwamba Mtume SAW amesema,

" Haijakamilika imani ya mmoja wenu mpaka AMPENDELEE nduguye lile ajipendelealo NAFSI YAKE."

Wanaccm wenzangu, Maendeleo yetu nyakati za zingine yanachochewa na VIONGOZI WACHA MUNGU WASIO WABINAFSI, TUNAELEKEA KWENYE CHAGUZI HIVI KARIBUNI, WATIA NIA TUWACHUJE KWA UMAKINI ILI TUWAPATE WAKWELI WASIO MATAPELI WALE WAONGO WAMETUUMIZA MNO KWA AHADI ZAO ZA KITAPELI TUMRUDIE MUNGU KWA KUWAKATAA VIONGOZI WAONGO. TUNAPOKUBALI KUONGOZWA NA MTU MUONGO NI WAZI TUNAKUBALI KUWA CHINI YA UTAWALA WA SHETANI NA MUNGU WETU AMETUKATAZA KUWA MARAFIKI NA SHEITWANI.

Tukisoma Qur aan Tukufu Kitabu cha Tarjuma ya Sahih Al Bukhari uk 90 Kifungu (30)

Alisema (SAW) Tafadhali na shahada wa UONGO, " akaendelea kukiri mara tatu kauli hiyo"

Tukisoma Qur aan Tukufu Juzuu 7 al an am (6) Kifungu 32

" Na maisha ya Dunia hii si kitu ila mchezo tu na UPUUZI. Na bila shaka nyumba ya Akhera ni bora zaidi Kuliko hii Dunia kwa wale wamchao Mwenyezi Mungu. Basi hamtii akilini haya mnayoambiwa ?"

Mungu awe nasi na atuingoze TUUKATAE UBINAFSI TUWE WAMOJA TUINUANE KIVIPATO TUSICHORANE

AMEEEEN

M. M. Kahinga.
🙏🏽🙏🏽🙏🏽🙏🏽🙏🏽
 
TABIA MBOVU NA CHAFU ZA BAADHI YA WATU WAJIITAO WANASIASA ZA KUVUNJA NA KUSIGINA MIFUMO YA NCHI NA KISHA KUPEANA VYEO VYENYE HARUFU YA RUSHWA LAZIMA TUPAZE SAUTI TUKOMESHE UJINGA HUO

Mheshimiwa Rais Dkt Samia Suluhu Hassan ana nia njema na nchi hii. Tatizo letu Baadhi tunapenda ku act Kama tuna Nidhamu huku tukiwa hatuna Nidhamu kwenye utekelezaji wa Viapo vyetu juu ya kuhifadhi
Kulinda na kutetea katiba na Sheria za nchi na Huu ndiyo Unafiki unao ligharimu Taifa letu lililo changanyikana na kuwachukia watu wenye akili kwa Ukweli wao wa kutaka ilani itekelezwe Kama ilivyoandikwa.

Mheshimiwa Rais Dkt Samia Suluhu Hassan akiwa Nkasi Namanyere nakumbuka Tarehe 15/07/2024 alisema lazima tuangalie Kama tumetekeleza kwa kiasi gani Ilani ya Uchaguzi. Mwisho wa kunukuu.

Tusome Ilani ya CCM 2020-2025 uk 161-168 uk 01 ibara 04 kwa mazingatio ya uk 08 ibara 10 na 11. Hapa tunabaini. Vitendo vya kufumbia macho watu wanaohujumu Mifumo na kujipatia vyeo vinapelekea kuinajisi ilani ambayo ni Mkataba Kati yetu na Wanaanchi ambao tuliwaahidi Utawala Bora usiokuwa na Matabaka ya Ubaguzi na Upendeleo wenye kudharau Mifumo ya nchi.

Comrade Mary Chatanda Mwenyekiti UWT CCM TAIFA kiongea Mbele ya Makamu Mwenyekiti wa CCM nakumbuka Tarehe 25/05/2024 alisema nikiwa na Jambo ( huwa Mimi) sipendi nikae nalo hata Kama nitaendelea kusema sema akini (beno Hilo) nikilitoa (nikalisema) litanisaidia angalau kupata pumzi. Mwisho wa kunukuu

Rushwa kila kukicha inazidi kuota mizizi ndani ya nchi huku Sisi tukiwa hatutendi haki ya kuchukuwa hatua kwa Mujibu wa katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania 1977 toleo 2005 ibara 26(2) kwa Maana ya kuitendea haki ibara 09 a,b,f, na h. Pia hatuitendei haki ilani ya CCM inayosisitiza Utawala Bora na kukataza watu kufanya kazi kwa mazoea.

Haiwezekani Kiongozi labda Diwani fulani yuko kwenye Cheo Kinyume na utaratibu wa kimfumo halafu analindwa na kulipwa posho kwa vile ni mtu muaminifu na Muadilifu. Kumbe Nya ng"au kabisa.

Mtu aliye Kinyume na utaratibu wa kimfumo anapodumu madarakani inakuwa Haina tofauti na kumchukuwa Jambazi Muuaji asiye na Mafunzo yeyote ya kipolice na Kisha kumkabidhi kituo Cha police awaongoze Askari Police Waadilifu na waaminifu huku ukitegemea kupata Matokeo Chanya ya kupunguza au kuutokomeza kabisa uhalifu.

Hizi zinakuwa ni Ndoto za alinacha Comrade Mary Chatanda Mwenyekiti UWT CCM Taifa nakumbuka Tarehe 25/05/2024 alisema nimeona niliseme hili (ili) niweze kupona nisiposema nitakufa nalo naweza kupata pressure bila sababu. Mwisho wa kunukuu.

Tusome ilani ya CCM 2020-2025 ibara 110(c) Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania 1977 toleo 2005 ibara 18(a) na 19(1) kwa Maana ya Uhuru wa Mawazo. Mtu paaap anakuja sssem haijuwi ilani anafundishwa tu kutamka neno. Utekelezaji wa ilani anafunishwa tu kutamka

Katiba Kanuni miongozo na Taratibu akiwa haelewi na Wala hajuwi yaliyomo kwenye vitabu hivyo
Tunawezaje kutenda haki kwa mafukara ikiwa nguvu zetu tunazielekeza kwenye kulinda Uovu usiohitaji Police Mpelelezi kufanya upelelezi!

Comrade Abdulrahman Omar Kinana Makamu Mwenyekiti CCM Taifa Bara Akiwa katika wiki ya Wazazi huko Katavi Katika Kongamano la Malezi na Maadili nakumbuka Tarehe 11/07/2024 alisema mtu Mwenye Maadili ni mtu mzuri ni mtu Muungwana, bi mtu anaye jiheshimu na kuheshimu wenzake mtu ambaye amejaa sifa, mtu Mwenye Maadili. Kwa hiyo Sisi sote (Wanaccm na Watanzania kwa ujumla) Tunatakiwa kuwa na Uadilifu katika Maisha yetu ya kila siku.

Katika Jamii yetu tunayoishi Mambo yako wazi ila tunaoneana aibu kuchukuwa hatua Na tunaona fahari na raha kutangaza kuwachukulia hatua Mafukara na Watumishi wa Umma ambao kimsingi hawasemi kwa Kuogopa kupoteza ajira zao.

Ni lazima mazongira ya hovyo Kama haya yenye harufu Mbaya na Chafu zenye viashiria vya Rushwa na kuto kutenda haki tuyakomeshe kabisa kwa kupaza sauti bila ya kuchoka. Rushwa na kuto kutenda haki ni Mambo yanayoleta sifa Mbaya tusiyo isitahili mbele ya Jamii.

Maneno yetu kuhusu haki yanazidi kupishana na uhalisia wa maisha tunayoyaishi huku tukiwa hatutilii maanani hata viapo tulivyo apa kwa Mwenyezi Mungu vya kutenda haki bila ya ubaguzi Wala Upendeleo na kibaya Zaidi hata watu wenye akili wenye kutueleza Ukweli tumeanza kuwaona Kama Maadui zetu huku tukiwa tumeapa kusema kweli na kujiepusha na fitna kwa Mujibu wa katiba ya CCM 1977 toleo 2022 uk 152 kifungu Cha 08.

Nakumbuka Tarehe 11/07/2024 Mheshimiwa Rais Paul Christian Makonda, Mheshimiwa Rais wa Mkoa wa Arusha
Nakumbuka Tarehe 11/07/2024 Akizungumza na Wanajeshi na Askari Police Alisema Hatutaki tujipe image ambayo (Sisi) hatuna na (vile vile) hatutaki tufiche Mapungufu yetu lakini Basi tusipewe sifa (yeyote ile) ambayo hatuna. Rushwa Haina Dini na Wala Haina kabila na (vile vile Rushwa) Haina Taasisi

Hayati Rais Dkt John Pombe Joseph Magufuli Rais wa Tanzania Awanu ya Tano Nakumbuka Tarehe 15/October/2019 Alisema Nilipokuwa nikipewa kazi hii ya Urais nilisema Mimi najipa kazi ya kutumbuwa Majipu .
Kwa sababu nilijuwa (ni wapi) nchi hii imefikia wapi kwenye suala la Rushwa.

Watu wa Tanzania kwa Mujibu wa katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania 1977 toleo 2005 ibara 26(1) uk 27 inatukumbusha. Kila mtu ana Wajibu wa kufuata na kuitii katiba hii na Sheria za Jamhuri ya Muungano.
Tukirudi uk 18 ibara 09 a,b ya katiba inasomeka kwamba utu na haki nyinginezo zote za Binaadamu zinaheshimiwa na kuthaminiwa. Kwamba Sheria za nchi zinalindwa na kutekelezwa.

Tukisoma Sheria ya nchi inayosimamia Vyama vya siasa inavitaka Vyama kufuata maandiko ya Vyama vyao kiukamilifu. Maandiko ya Vyama ni Kama vile ilani katiba Kanuni miongozo na Taratibu zingine. Watu wanavunja Taratibu hizi wanapata vyeo na Ushahidi uko wazi.

Wanaenda maofisini kufanya kazi za kuwahimiza watu wawe Waadilifu na waaminifu huku Viongozi hao wao wakiwa Manya ng'au yanayolindwa kwa nguvu za Rushwa. Kwa Hali hii tutawezaje kuwa Wacha Mungu?
Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania 1977 toleo 2005 uk 20-21 ibara 13(1)(4)(5) inatueleza watu wote ni sawa mbele ya Sheria na katiba inakataza Taasisi yeyote au mtu yeyote kumbagua mtu kwa Aina yeyote.

Tujiulize Vitendo vya kuwachukulia hatua Mafukara na Watumishi wa Umma huku tukiwaacha Viongozi wanajulikana wazi kabisa kuwa walipata vyeo Kinyume na utaratibu Sio ubaguzi huo? Tukisoma katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania 1977 toleo 2005 uk 18 ibara 09 Inatueleza wamba Aina zote za dhulma , vitisho, ubaguzi, Rushwa, uonevu au Upendeleo zinaondolewa nchini.

Mwisho wa kunukuu maandishi ya katiba tujiulize kufumbia macho uovu ulio wazi kabisa wa kuwalinda waliopindisha Taratibu na kujihusisha na kuwananga na kuwatangaza Mafukara na Watumishi wa Umma
Je, huu Sio uonevu na Upendeleo wa wazi uliojaa ubaguzi? Tujiulize hivi Sisi Baadhi tunaoapa kuwa wasikivu na Watii kwa katiba na Sheria za nchi huku tukitamka maneno tukiwa timamu wenye akili zetu kuhifadhi, kulinda
na kutetea katiba na Sheria za nchi.

Hivi tunapokuwa hatuhifadhi hatulindi, hatutetei tunapendelea na kubagua watu kwa kuchukuwa hatua kibaguzi baguzi Je na Sisi hatustahili kushitakiwa. Au Sisi tuko Juu ya Sheria Kama viwanda vinavyotengeneza Sigara zinazo wauwa watu huku zikipewa Ulinzi wa kuzalishwa na watu walioapa hadharani huku wakiwa wameshika vitabu vitakatifu Vya Mwenyezi Mungu wakimuahidi Mwenyezi Mungu kufanya kazi Kinyume na viapo vyao?

IGP Camillus Wambura Mkuu wa Jeshi la Police Tanzania Nakumbuka Tarehe 15/07/2024 Alisema Matendo mengi (ni) ya Ajabu Saana. Kwa hiyo Mimi vitu ambavyo ni vya msingi ni ( kwamba) Jamii yetu ibadilike. Jamii yetu iache matendo ya kihalifu. Jamii yetu iache taarifa za Uongo tuzingatie Maadili. Mwisho wa kunukuu
Wakili Jasiri Msomi mheshimiwa Peter Madeleka, Ex Police Officer Nakumbuka Tarehe 15/07/2024 Alisema
Siasa ndiyo kila kitu kwenye maisha ya Mwanaadamu Mahitaji ya kisiasa ndiyo yanayo amuwa namna gani tujiendeshe Kama nchi.

Mheshimiwa Rais Dkt Samia Suluhu Hassan Akiwa Ziarani Rukwa Akizindua Barabara ya Sumbawanga -Matai -Kasanga Akiwa Wilaya ya Kalambo Nakumbuka Tarehe 16/07/2024 alisema (Nitoe wito kwa Watumishi wa Umma) kuhakikisha wanafanya kazi njema na kutoa huduma njema kwa Wananchi ambao ndiyo Waajiri wetu .
Ambao ndiyo wametuweka katika nafasi tulizo nazo.

Tusome Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania 1977 toleo 2005 uk 17 ibara 08(1)(a)(b)(c)(d)
Nikashtuka katika Ulimwengu wa kiroho huko ndotoni nikiwa kimya

Kidumu Chama Cha Mapinduzi

Mathias Mugerwa Kahinga

🤔🤔🤔🤔🤔🤔🤔🤔🤔
 
Back
Top Bottom