Pre GE2025 Upendo Peneza aeleza sababu za kuondoka kwake CHADEMA

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)
Sahihi, yeye anasema hizo fedha 1.5 kwa wabunge wa viti maalum, na lako tano kwa Kila mbunge wa jimbo walizokuwa wanachangishwa zikafika 5b+, waliambiwa zitatumika kuwezesha wagombea wakati wa uchaguzi wa 2020. Lakini hawakuziona wakati wa uchaguzi ule. Na maelezo yake hayanyooki.
 
Ni wajinga tu ndio wanawaelewa watu wanaotoka upinzani na kurudi/kwenda CCM wakati CCM ni ile ile na mambo yake ni yale yale.
 
Huyu akatibiwe....ni mgonjwa anateseka KISAIKOLOJIA

Kama anamme au mchepuko basi kuna shida mahala kwenye drilling

Inawezekana huko aliko unga juhudi wana mbutuwa butuwa alicho ahidiwa HAKIONI

Ushauri tu akae kimya Ajitafakari mbele na nyuma kuliko kila mala KUTAPIKA kwenye Media....huko ni kujutia Maamuzi...
 
Usimwamini mwanasiasa

Hauwezi Kuwa smart ukatoka Chadema na kuhamia Ccm , labda for self-interest I agree with her Ila in national interest I don't agree with her.


MTU pekee ambaye alikuwa ni hazina na anaipambania nchi ni zitto kabwe tu. Ndo maana mpaka Leo amesimama Imara.
 
Mwanasiasa Upendo Peneza anasema wakati anaingia CHADEMA kilikuwa chama cha kawaida kabla ya yeye kukisaidia kukua kwa kasi.

Pia soma: Upendo Peneza ahamia CCM, awananga CHADEMA



===

Kama tunakwenda Tanga nilikuwa nauliza kama kuna nafasi kwenye gari. Ili kwenda kwenye hizo operesheni Sangara nafasi ya gari ilikuwa haikosekani. Nilikuwa nachukua pocket money ambayo nilikuwa napewa na wazazi wangu

Pia nilikuwa na marafiki ambao niliwaambia kuwa nimejiunga na siasa walikuwa wakinisapoti. Nilikuwa nikienda kwenye safari najilipia chumba cha kulala (hotel). Najihudumia kila kitu ili lengo nipate hiyo nafasi ya kushiriki na nafasi ya kuonekana.

Nilianza kupewa kazi ya kutangaza mkutano kwenye gari na kuita watu. Unaitwa watu waje kwenye mkutano lakini ukifika uwanjani hakuna watu na kipindi hicho CHADEMA ilikuwa haijakua kiasi hicho. Baadaye ndio Mwenyekiti anakuja na chopa na watu wanakuja kusikiliza ujumbe.
 
Ni kweli, alipoulizwa kuhusu kuhamia ccm aliishia kutoa majibu ya kujiumauma na sifa zile zile za kichawa. Hakuna uwezekano wa yeye kuiponda ccm hadharani akiwa ndani ya ccm, kama ambavyo hajawahi kuiponda cdm hadharani akiwa ndani ya cdm. Kwa Sasa lazima aongee lugha itakayompa nafasi ndani ya ccm. Na sisi humo humo ndio tunaokota ya kweli.
 
Unaamini mtu anaweza kuhamia CCM ya sasa Toka CDM Ili akaseme Kweli yote?
Sitegemei aseme kweli yote, lakini hakuna uwezekano wa yeye kuongea uongo yote.
 
Mwanasiasa Upendo Peneza anasema wakati anaingia Chadema kilikuwa chama cha kawaida kabla ya yeye kukisaidia kukua kwa kasi.
View attachment 2991345


Huyo anajishusha Sana with nothing

Kama alifika hatua ya kuwa Mbunge maana yake alibidi kutoendeshwa na tumbo bali Akili.


Mambo anayoongea ni utoto.

Kanuni za Maisha zipo wazi kuwa ili ufanikiwe hauwezi kujitenga na neno 'Sacrifice'

Good leader 'Eat last'
 
Amesema kuhusu pesa walizokuwa wanachangishwa wao kama wabunge, hawafahamu zimetumika kufanya Nini. Na ni kweli hizi pesa zimekuwa zikitolewa porojo. Huyu Upendo kwakuwa ana hasira ataongea mengi ya hasira, lakini humo ndani tutapata ukweli.
Kwa nini hakusema haya hadharani wakati akiwa CHADEMA?
Huu ni unafiki pro max
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…