Upinzani bila kubadili siasa mtapata hasara kubwa Kwa Samia..

Upinzani bila kubadili siasa mtapata hasara kubwa Kwa Samia..

Hili suala la tume na Katiba mpya ni kelele za viongozi wenu ambao hawana dhamira ya dhati ya kuiondoa CCM, ni baadhi ya visingizio ambavyo hawata kosa kuwa navyo hata ikipatikana hiyo Tume. Jambo moja rahisi sana mkuu; Hivi fedha ambazo CDM wamekusanya kama Ruzuku from 2015-2020 wamefanyia nini cha maana (Katika kukijenga chama)? Maana ilikuwa fedha nyingi mnoo, kwa upinzani serious ile fedha ingewatengenezea msingi mzuri sana maana huwezi fanya siasa bila fedha

Wasioitaka CCM ni wananchi

Kwa tulipofika huhitaji fedha wala chochote kumshawishi mwananchi kuipigia kura chama pinzani,sababu tayari asilimia kubwa ya watanzania wameshakinaiwa na CCM


Tume ya uchaguzi,dola na mengine ndio yanayoendelea kuiweka CCM madarakani & nothing rather than that ushahidi tosha ni chaguzi kuu 2020
 
Wasioitaka CCM ni wananchi

Kwa tulipofika huhitaji fedha wala chochote kumshawishi mwananchi kuipigia kura chama pinzani,sababu tayari asilimia kubwa ya watanzania wameshakinaiwa na CCM


Tume ya uchaguzi,dola na mengine ndio yanayoendelea kuiweka CCM madarakani & nothing rather than that ushahidi tosha ni chaguzi kuu 2020
You are right about 2020, lakini je kutoitaka tu CCM inatosha? Ok assume tume iwe fair, kuna mbadala wa ccm kwa sasa?
 
Yaani kifo cha JPM kimezika kabisa upinzani

Kisiasa walitakiwa wanyakue agenda zake na kumlazimisha mama aendelee nazo....walikurupuka vibaya

wangekosoa uhuru wao tu wa siasa na wananchi angehamia upande wa upinzani....na kuiacha CCM inajizoa zoa
Kofia naiinua, sikudhani kama unao muono wa ndani kama huu, nilifikiri ni sisi wa chache sana wenye kutafakari na kuona. Asante.
 
Kwanza elewa. Mimi siko kwenye siasa kwa namna yoyote. Natoa maoni yangu kama raia asiye na chama wala upende wowote kwenye siasa za Tanzania. Upande wangu ni ''haki na fursa sawa kwa kila raia''. Kingine: naamini nchi inaweza kuendeshwa kwa mfumo wa chama kimoja na ikaenda vizuri iwapo wananchi wanajitambua na siyo woga! Kinachotakiwa ni wananchi kujua haki zao. Hili la kusema watanzania wengi ni waoga na hawajitambui ni kitu kilicho dhahiri na siyo tusi hata kidogo. Ni ukweli mchungu. Ila ''chawa'' wanaoishi kwa siasa kama wewe hili ni faida kwako hivyo hutataka liondoke. Bila hata kuzungumzia siasa, kuna haki nyingi za msingi zinakiukwa lakini wananchi wengi wamelala fofofo kama hakuna kinachotokea. Wewe hutakubali kwa sababu ujinga wetu wananchi ndiyo kula yako.
The reverse is true, uwerevu wa wananchi ndio faida yako.

Swali pana hapa ni huo uwerevu uwe kwenye nini? Hakuna siku binadamu akawa mwereu kwa kila jambo.
 
Andiko lako liko vizuri sana lakini kuna mahali umeteleza mkuu
 
Umeongea ukweli..japo sina wasiwasi. Upinzani upo na watu smart sana kama Mbowe
Siku Mbowe akiwa smart, nitarudi upinzani kabla jua halija chomoza.

Wewe mwana siasa uliye pevuka lazima ufahamu kuwa Mwendazake alikuwa na constituency yake, na kwa hiyo kisiasa lazima uirithi.
Chadema ina mpango gani kisiasa kufaidika na kifo cha Mwendazake?

Mwendazake, aliichukua Constituency ya Chadema, watu wa chini wote kimaisha na kibiaashara lakini hakuwapa manufaa ya kuridhisha, hapo ndio chama kinazoa wanachama na wafuasi.
 
Suala ka katiba mpya binafsi naamini ni suala la wananchi au watu wasio na maslahi kabisa ya kisiasa kama kina Warioba.

Nakuhakikishia, hata leo CHADEMA au ACT wakifanikiwa kuingia madarakani kwa katiba hii hii ya 1977, hawataibadilisha. Zitabaki danadana tu.

Hakuna mwanasiasa mwenye madaraka asiyependa madaraka makubwa kama hayo yaliyomo kwenye katiba ya 1977.

Mimi naamini zaidi kwenye madaraka na maamuzi ya wananchi.
Mkaruka unakosea kutumia wishful thinking kwa jambo ambalo imekuwa ajenda yao toka vyama vya siasa vianzishwe.

Kwa katiba ya sasa vyama vya upinzani havitaweza kutawala kwa amani bila kufanya system overhaul na system overhaul itawezekana tu kwa kufanya mabadiliko makubwa ya kikatiba.

Vyama vya upinzani vikiingia madarakani ni lazima vitafanya hayo mabadiliko ili viweze kutekeleza sera zake.
 
Samia kasema atakutana na wapinzani..
Sio Sisi wananchi wa mitandaoni..
Atakapo kutana nao wao ndo Wana nafasi ya kuweka maombi ya wananchi ..na kum influence Samia kuelekea agenda za wananchi..

Sisi tutabaki kupiga kelele Tu huku mitaani na mitandaoni lakini wao wapinzani Wana nafasi kubwa zaidi baada ya Rais kusema atazungumza nao
Ipo tofauti, lakini ni kidogo sana. Wenye kutoa maoni kwenye mitandao na uongozi wa vyama vya upinzani. A symbiotic relationship.
 
Mimi ni mtu ambae niko open minded, napendela majadiliano ya hoja zaidi.

Nikikukabi leo haina maana kua nitakukubalia daima, mimi sina upenzi na haina maana kua nikikuponda leo basi nitakuponda daima.

Napenda kuona watu wanajenga hoja based on facts and not assumptions or hearsay.

Sasa mtu anapokuja na kuandika uharo eti watanzania walimchoka JPM unajiuliza hao watanzania ni wapi, hawa waliokua wanaandamana hadi kufa kuuona mwili wake?

Maana ukisema watanzania halafu hukuweka specific ni watanzania gani maana yake umewasemea watanzania wote wanaokadiliwa kua 60 million, hilo jambo sio sahihi.

Kwa mfano mimi binafsi sikua nampenda JPM lakini mama yangu alikua anampenda, sasa siwezi kusema kisa mimi simpendi basi Watanzania wote walikua hawampendi, huo ni utaahira. Na usemi ama uandishi wa kitaahira kama huo ndio haukubaliki.
Mkuu huku mwisho umemalizia vizuri na kwa uhalisia.

Sisi wakazi wa Wilaya ya Hai, vijana wengi ni wapenzi wa Chadema lakini ni ukweli usio na kigugumizi chochote ya kuwa wazazi wetu wengi wanaipenda CCM.
Na tunaishi na wazazi wetu na tunafurahia maisha.
 
Wasioitaka CCM ni wananchi

Kwa tulipofika huhitaji fedha wala chochote kumshawishi mwananchi kuipigia kura chama pinzani,sababu tayari asilimia kubwa ya watanzania wameshakinaiwa na CCM


Tume ya uchaguzi,dola na mengine ndio yanayoendelea kuiweka CCM madarakani & nothing rather than that ushahidi tosha ni chaguzi kuu 2020
Usiwasemee wananchi unaweza ukawa sio sahihi.
 
Kwa sasa hatuna Wapinzani kabisa na naona watatoka ndani ya CCM km ilivyokuwa G55
kweli Mpinzani unadai Hotuba ya mama Samia ilikuwa dk 1 tu kuzungumzia upinzani?
unadai ulipwe mafao na gari yako iliyopigwa risasi na kuzuiliwa, ufutiwe kesi km huna umuhimu baki Ubelgiji
Mpinzani unadai Magufuli kachukiwa kwa kifo cha Ben Saanane wakati walioumizwa ni wengi, tuna ndugu zetu walifukuzwa kazi kwa uonevu, Vyeti fake, umri bado, ukabila nk
Wapinzani watatoka ndani ya CCM km kina Nape, Gambo nk
Katiba mpya na Tume bado muda upo kwa sasa Wapinzani wa kweli waanze na makosa ya mwendazake lkn kwa CHADEMA bado nasema hakuna
Gambo hana nguvu km Lema kwa wananchi, lkn kwa sasa ndiye atakuwa mpinzani anayeleta mabadiliko kwa Wananchi wa Arusha, sio maandamano
cc

BAK

 
wapinzani waliingiza emotion issue ya JPM, na wakasahau siasa ni wakati JPM kaondoka nao😂
Kweli kabisa na sasa hivi wataongozwa na Jemedari Shibuda sio kila mmoja aende akanywe chai au kuelza matakwa yake binafsi, nirudishiwe shamba langu au mafao yangu. Agenda zote zipitie kwa John Shibuda au Francis Mutungi
 
You are right about 2020, lakini je kutoitaka tu CCM inatosha? Ok assume tume iwe fair, kuna mbadala wa ccm kwa sasa?

Binafsi naona awamu iliyopita haikufanikiwa kuua upinzani hata kama juhudi zote zilizofanywa kuanzia 2015 mpaka 2020 na ndio maana ndio maana kulihitajika msaada mkubwa wa tume na dola ili kupata kiti

Upinzani unatokana na madhaifu yanayotokana na mtawala ambapo kwa hapa kwetu bado mtawala ana madhaifu mengi sana ambayo hata hafahamu anaanzia wapi kuyarekebisha

Kwahiyo penye chaguzi huru na haki bado mtawala anaachia nchi kwa upinzani huu huu ambao mnadhani kua ume expire
 
Mkuu huku mwisho umemalizia vizuri na kwa uhalisia.

Sisi wakazi wa Wilaya ya Hai, vijana wengi ni wapenzi wa Chadema lakini ni ukweli usio na kigugumizi chochote ya kuwa wazazi wetu wengi wanaipenda CCM.
Na tunaishi na wazazi wetu na tunafurahia maisha.
Kabisa.

Na huwezi kusema eti kwa kua wewe humpendi ama sio shabiki wa ccm basi watanzania wote sio mashabiki wa ccm wakati unajua kabisa kuna wengine tena ndugu zako wanaipenda ccm.
 
Hakuna kitu kinaamua siasa kama 'wakati'..
Wanasiasa wazuri ni wale wanaojua nyakati zinavyobadilika na kwenda na wakati uliopo ...

Watanzania walikuwa wamechoshwa mno na siasa za Magufuli...na uongozi wake kiujumla..
Kubanwa Uhuru wa kuongea
Kufokewa na kukaripiwa
Kutoa matamko Kwa ukali..
Kuzungumza Peke yake..
Kutokukosolewa ..
Kukosekana Kwa mijadala na majadiliano..
Na mengi yaliyoenda na hayo..

Ujio wa Samia umebadili siasa Kwa ujumla..
Samia hafoki anaongea Kwa upole na kushawishi ..
Anazungumzia mazungumzo na mijadala..
Hazuii kukosolewa badala yake anakaribisha kukosolewa Kwa serikali yake..

Kikubwa zaidi ni Mwanamke ..
Watu wanamtazama Kwa 'kumhurumia'..
Na kumpa 'all benefits of the doubts'..
Na kuelewa kuwa anapambana na mfumo dume...
Watu wengi wanaju hii nchi ngumu na wanajua Samia atahangaika kuweza kumudu ...still wanafarijika na 'kurudi Kwa Uhuru wa kuongea na kukosoa'..

Sasa kama wapinzani wanafikiri siasa za kumshambulia Rais na serikali yake zinalipa bado kama enzi za JK watakuwa wanakosea sana....
Sana Sana wataonekana 'hawana adabu'
Na wanajaribu 'kumuonea' 'Rais Mwanamke' baada ya 'kidume ' JPM
'kuwakomesha hadi wakaufyata'..

Siasa za kipindi hiki zinahitaji ubingwa wa hoja kwenye mijadala ya kistaarabu..bila
Kuwa 'boa' wananchi ambao walishachoshwa na Magufuli Sana Sana wanataka 'mzunguko' wa hela urudi kama ule wa JK....

Kuleta siasa za ulalamishi..
Siasa za uwana harakati.
Na siasa za Ku target watu na kuwashambulia bila kujua ..'role halisi' ya hao watu ni siasa ambazo zinakuwa 'outdated ' so fast...

Watu wanampenda Samia sio Kwa sababu ni kiongozi bora.. wanampenda Kwa sababu wanaona 'nafuu inakuja'
Upinzani ukicheza siasa za kuleta 'distraction'wakati watu wanasubiri nafuu ije ..hasira za wananchi zinaweza washukia wao.....

Siasa inaendana na nyakati.. wapinzani wanasoma nyakati??
Unaogopa sana demokrasia wewe.
 
Hakuna kitu kinaamua siasa kama 'wakati'..
Wanasiasa wazuri ni wale wanaojua nyakati zinavyobadilika na kwenda na wakati uliopo ...

Watanzania walikuwa wamechoshwa mno na siasa za Magufuli...na uongozi wake kiujumla..
Kubanwa Uhuru wa kuongea
Kufokewa na kukaripiwa
Kutoa matamko Kwa ukali..
Kuzungumza Peke yake..
Kutokukosolewa ..
Kukosekana Kwa mijadala na majadiliano..
Na mengi yaliyoenda na hayo..

Ujio wa Samia umebadili siasa Kwa ujumla..
Samia hafoki anaongea Kwa upole na kushawishi ..
Anazungumzia mazungumzo na mijadala..
Hazuii kukosolewa badala yake anakaribisha kukosolewa Kwa serikali yake..

Kikubwa zaidi ni Mwanamke ..
Watu wanamtazama Kwa 'kumhurumia'..
Na kumpa 'all benefits of the doubts'..
Na kuelewa kuwa anapambana na mfumo dume...
Watu wengi wanaju hii nchi ngumu na wanajua Samia atahangaika kuweza kumudu ...still wanafarijika na 'kurudi Kwa Uhuru wa kuongea na kukosoa'..

Sasa kama wapinzani wanafikiri siasa za kumshambulia Rais na serikali yake zinalipa bado kama enzi za JK watakuwa wanakosea sana....
Sana Sana wataonekana 'hawana adabu'
Na wanajaribu 'kumuonea' 'Rais Mwanamke' baada ya 'kidume ' JPM
'kuwakomesha hadi wakaufyata'..

Siasa za kipindi hiki zinahitaji ubingwa wa hoja kwenye mijadala ya kistaarabu..bila
Kuwa 'boa' wananchi ambao walishachoshwa na Magufuli Sana Sana wanataka 'mzunguko' wa hela urudi kama ule wa JK....

Kuleta siasa za ulalamishi..
Siasa za uwana harakati.
Na siasa za Ku target watu na kuwashambulia bila kujua ..'role halisi' ya hao watu ni siasa ambazo zinakuwa 'outdated ' so fast...

Watu wanampenda Samia sio Kwa sababu ni kiongozi bora.. wanampenda Kwa sababu wanaona 'nafuu inakuja'
Upinzani ukicheza siasa za kuleta 'distraction'wakati watu wanasubiri nafuu ije ..hasira za wananchi zinaweza washukia wao.....

Siasa inaendana na nyakati.. wapinzani wanasoma nyakati??
Nimeipenda hii!.
P
 
Mkaruka unakosea kutumia wishful thinking kwa jambo ambalo imekuwa ajenda yao toka vyama vya siasa vianzishwe.

Kwa katiba ya sasa vyama vya upinzani havitaweza kutawala kwa amani bila kufanya system overhaul na system overhaul itawezekana tu kwa kufanya mabadiliko makubwa ya kikatiba.

Vyama vya upinzani vikiingia madarakani ni lazima vitafanya hayo mabadiliko ili viweze kutekeleza sera zake.
Kama sera zipi hizo zinazohitaji system overhaul ??
 
Binafsi naona awamu iliyopita haikufanikiwa kuua upinzani hata kama juhudi zote zilizofanywa kuanzia 2015 mpaka 2020 na ndio maana ndio maana kulihitajika msaada mkubwa wa tume na dola ili kupata kiti

Upinzani unatokana na madhaifu yanayotokana na mtawala ambapo kwa hapa kwetu bado mtawala ana madhaifu mengi sana ambayo hata hafahamu anaanzia wapi kuyarekebisha

Kwahiyo penye chaguzi huru na haki bado mtawala anaachia nchi kwa upinzani huu huu ambao mnadhani kua ume expire
Uko sawa kuhusu mapungufu ya watawala sana tuu, lakini kwa mimi ambaye nilishiriki uchaguzi na kuufuatilia ki utafiti na kwa vigezo, naona bado sana kwa upinzani kipigiwa kura za ushindi.

Nilitumia muda wa kutosha kupita kanda ya Magharibi na kuungana na watafiti wengine Kaskazini ambako ni nyumbani.

Matokeo:
Mwendazake katika utawala wake aliweza kuaminiwa na kuwaunganisha vizuri kanda ya Magharibi, Mara, Mwanza, Simiyu,Shinyanga, Geita, Kagera, kigoma, Tabora, Rukwa, Katavi na Songwe, Ruvuma, Mtwara, Iringa, Morogoro. Na alifanikiwa kuwaunganisha watanzania wanaoishi sehemu mbali mbali nchini mwetu lakini wana asili ya Mikoa hiyo. Kama ilivyo kawaida ya kisiasa upinzani kwa hizo jamii bado upo.

Maeneo yaliyokuwa na upinzani kabla:

Tunadanganyana sana humu kwenye mitandao, lakini wapiga kura waliokuwa wanaishi mkoa wa Kilimanjaro walikuwa na mawazo tofauti na sisi tunaishi nje ya Mkoa wa Kilimanjaro lakini tuna asili ya huko.

Wao walihamishia kura zao CCM, sisi tukiwa bado upinzani na tulio wataka wawe wabunge, huko majimboni, wao walikuwa hawawataki na hii ilikuwa wazi kwenye majimbo mengi tu.

Na hata maelezo ya wizi wa kura wananchi wa mkoa wa Kilimanjaro ambao wanaishi Kilimanjaro hawaelewi hilo. Na hili ni kuanzia Same mpaka Siha.

Upinzani lazima upiganie kura za Mwendazake uzirithi ili kuchukua nchi. Tutabeza, tutadhihaki lakini ukweli unabaki kuwa kuna kura za kupoteza kama hatuto tupia jicho na kuzipata kura za Mwendazake.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kama sera zipi hizo zinazohitaji system overhaul ??
Unaposema unahitaji kuleta utawala bora lazima uanze na katiba.

Unaposema uboreshe mifumo ya haki za binadamu lazima uanze na katiba.

Katiba inasema nchi ni ya ujamaa na kujitegemea unatekeleza vipi sera za kibepari bila kuondoa kwanza hiyo blah blah ?

Ndiyo maana ccm wanaendesha nchi kwa mihemko na matamanio binafsi ya rais kwa sababu sera zao zote hazina msingi wa kikatiba.

Unaposema utaleta taasisi imara utaunda vipi taasisi imara bila kuwa na katiba inayoweka misingi ya taasisi imara ?
 
Back
Top Bottom