Upinzani bila kubadili siasa mtapata hasara kubwa Kwa Samia..

Upinzani bila kubadili siasa mtapata hasara kubwa Kwa Samia..

Hakuna kitu kinaamua siasa kama 'wakati'..
Wanasiasa wazuri ni wale wanaojua nyakati zinavyobadilika na kwenda na wakati uliopo ...

Watanzania walikuwa wamechoshwa mno na siasa za Magufuli...na uongozi wake kiujumla..
Kubanwa Uhuru wa kuongea
Kufokewa na kukaripiwa
Kutoa matamko Kwa ukali..
Kuzungumza Peke yake..
Kutokukosolewa ..
Kukosekana Kwa mijadala na majadiliano..
Na mengi yaliyoenda na hayo..

Ujio wa Samia umebadili siasa Kwa ujumla..
Samia hafoki anaongea Kwa upole na kushawishi ..
Anazungumzia mazungumzo na mijadala..
Hazuii kukosolewa badala yake anakaribisha kukosolewa Kwa serikali yake..

Kikubwa zaidi ni Mwanamke ..
Watu wanamtazama Kwa 'kumhurumia'..
Na kumpa 'all benefits of the doubts'..
Na kuelewa kuwa anapambana na mfumo dume...
Watu wengi wanaju hii nchi ngumu na wanajua Samia atahangaika kuweza kumudu ...still wanafarijika na 'kurudi Kwa Uhuru wa kuongea na kukosoa'..

Sasa kama wapinzani wanafikiri siasa za kumshambulia Rais na serikali yake zinalipa bado kama enzi za JK watakuwa wanakosea sana....
Sana Sana wataonekana 'hawana adabu'
Na wanajaribu 'kumuonea' 'Rais Mwanamke' baada ya 'kidume ' JPM
'kuwakomesha hadi wakaufyata'..

Siasa za kipindi hiki zinahitaji ubingwa wa hoja kwenye mijadala ya kistaarabu..bila
Kuwa 'boa' wananchi ambao walishachoshwa na Magufuli Sana Sana wanataka 'mzunguko' wa hela urudi kama ule wa JK....

Kuleta siasa za ulalamishi..
Siasa za uwana harakati.
Na siasa za Ku target watu na kuwashambulia bila kujua ..'role halisi' ya hao watu ni siasa ambazo zinakuwa 'outdated ' so fast...

Watu wanampenda Samia sio Kwa sababu ni kiongozi bora.. wanampenda Kwa sababu wanaona 'nafuu inakuja'
Upinzani ukicheza siasa za kuleta 'distraction'wakati watu wanasubiri nafuu ije ..hasira za wananchi zinaweza washukia wao.....

Siasa inaendana na nyakati.. wapinzani wanasoma nyakati??
NAKED truth umeandika
 
Uko sawa kuhusu mapungufu ya watawala sana tuu, lakini kwa mimi ambaye nilishiriki uchaguzi na kuufuatilia ki utafiti na kwa vigezo, naona bado sana kwa upinzani kipigiwa kura za ushindi.

Nilitumia muda wa kutosha kupita kanda ya Magharibi na kuungana na watafiti wengine Kaskazini ambako ni nyumbani.

Matokeo:
Mwendazake katika utawala wake aliweza kuaminiwa na kuwaunganisha vizuri kanda ya Magharibi, Mara, Mwanza, Simiyu,Shinyanga, Geita, Kagera, kigoma, Tabora, Rukwa, Katavi na Songwe, Ruvuma, Mtwara, Iringa, Morogoro. Na alifanikiwa kuwaunganisha watanzania wanaoishi sehemu mbali mbali nchini mwetu lakini wana asili ya Mikoa hiyo. Kama ilivyo kawaida ya kisiasa upinzani kwa hizo jamii bado upo.

Maeneo yaliyokuwa na upinzani kabla:

Tunadanganyana sana humu kwenye mitandao, lakini wapiga kura waliokuwa wanaishi mkoa wa Kilimanjaro walikuwa na mawazo tofauti na sisi tunaishi nje ya Mkoa wa Kilimanjaro lakini tuna asili ya huko.

Wao walihamishia kura zao CCM, sisi tukiwa bado upinzani na tulio wataka wawe wabunge, huko majimboni, wao walikuwa hawawataki na hii ilikuwa wazi kwenye majimbo mengi tu.

Na hata maelezo ya wizi wa kura wananchi wa mkoa wa Kilimanjaro ambao wanaishi Kilimanjaro hawaelewi hilo. Na hili ni kuanzia Same mpaka Siha.

Upinzani lazima upiganie kura za Mwendazake uzirithi ili kuchukua nchi. Tutabeza, tutadhihaki lakini ukweli unabaki kuwa kuna kura za kupoteza kama hatuto tupia jicho na kuzipata kura za Mwendazake.

Sent using Jamii Forums mobile app
Hivi mnatumiaga viungo gani kufikiri hadi kuandika hivi...kama huu ujinga ulioandika una ukweli kwanini mlitumia bunduki ujinga huu ambizianeni huko kwenye korido zenu

Sent from my Nokia 8.1 using JamiiForums mobile app
 
Ukimkosoa Mama kwa hoja hana ujanja wowote , pamoja na yote huyu ni miongoni mwa walioharibu Katiba mpya hadharani na gizani , faili lake lipo , tunamwangalia tu atakachofanya
Halafu mtoa mada ajue tunaonekana kufurahia uwepo wa Mama sio kwa sababu tunampenda au tunamkubali hapana,Bali tunafurahi Chinjachinja muasisi wa Wasiojulikana hayupo madarakani.

Kama vile sio kwamba watu walifurahi kwa sababu kafa,hapana,kwa sababu kila mtu atakufa.
Tulichofurahia Ni Mtu katili yule kuondoka madarakani.
Tungeweza kufurahia kuondoka kwake madarakani hata ingekua kwa
Kupinduliwa,
Kuugua na kushindwa kuendelea na majukumu yake,
Kujiuzulu,
Kushindwa uchaguzi,
Kutoroka nchi,
Ama vinginevyo ilimradi angeondoka kwenye kiti kile mtu dhalimu yule.

Mtoa mada hajui upinzani up tu mioyoni mwa watu,Kuna watu Hatuipendi CCM tu Kama tusivyompenda shetani.
Kama wanaamini mama anapendwa Basi uchaguzi ujao uwe wa haki.Tume huru na Katiba mpya waone mziki wake.

Wamesahau kwama hata wakati Jiwe anaingia madarakani alipewa kila aina ya sifa,lakini Leo kafa kaitwa kila aina ya Jina baya.

Leo namsifu Mama kwa sababu anafuta Mambo ya Jiwe ila siku ya Uchaguzi msimamo wangu Ni Chadema wasimamishe kitu chochote Mimi nitakipigia kura. Ninaposema kitu namaanisha kitu kweli,awe mtu ama gogo ilimradi limesimamishwa na CDM nitalipigia kura.
Kuendelea kuichagua CCM Ni kuendelea kuwachagua akina Lusinde,msukuma,Ndugai na wajinga wengine.Tuanchotaka sisi Ni kubadilisha kabisa Mfumo.
 
Huo ndiyo ukweli husika na Chadema haina chochote cha kubadilisha kama walivyomkabili dikteta ndiyo hivyo hivyo wamkabili Mama kama ATADEMKA atajijua yeye na maccm yake masuala ya kuongoza nchi kwa uwazi, haki na kuheshimu sheria za nchi ikiwemo Katiba, Bunge na mahakama pia kupatikana kwa Katiba mpya na Tume huru ya uchaguzi kabla ya 2025 yote hayo HAYAKWEPEKI.
Watu tunamfurahia Mama kwa sababu Tulishamchoka MAGUFULI na Siasa zake za kikatili,
Ukweli ni kwamba CCM imechokwa kuliko kitu chochote duniani.
Kama mtoa mada anaamini Mama anapendwa waruhusu Katiba Mpya na Tume huru ya uchaguzi.

Nakuhakikishia Samia hawezi kwenda kinyume na matakwa ya CCM,na moja ya takwa kubwa la CCM Ni dhuluma kwa kila Jambo.

Mama mtago wake Ni mdogo tu,ama awe upande wa CCM ama awe upande wa wananchi.

Ikiwa Kikwete mwanasiasa nguli ndani ya CCM walimdhibiti suala la Katiba mpya ingawa yeye ndio alielianzisha likamshinda na heshima yake ikashuka sembuse Mama mchanga katika Siasa?

Kama CCM wanajiamini kuwa mama anapendwa waruhusu Katiba na Tume ili chaguzi ziwe za haki waone mziki wa Upinzani.
Mimi nimeichoka CCM katika maisha usione hivi,hata wanipe Lori la fedha ntawasaliti tu.
 
Hivi mnatumiaga viungo gani kufikiri hadi kuandika hivi...kama huu ujinga ulioandika una ukweli kwanini mlitumia bunduki ujinga huu ambizianeni huko kwenye korido zenu

Sent from my Nokia 8.1 using JamiiForums mobile app
Broo umeandika kitu kizito Sana ,CCM huwa kweli wanaondolewa asilimia 95 ya akili wanabakishiwaga asilimia 5 tu kwa ajili ya kupeleka chakula mdomoni badala ya puani,ya kukumbuka kuvaa nguo na kwa ajili ya dharula ndogondogo Kama kuvukia barabara na vitu Kama hivyo.
Uchaguzi mkuu huu uliopita ndio umewavua nguo CCM na dunia nzima ikaona.
Yaani hadi Mimi mfuasi wa Upinzani nikawa naona aibu Mimi.
 
Huo ndiyo ukweli husika na Chadema haina chochote cha kubadilisha kama walivyomkabili dikteta ndiyo hivyo hivyo wamkabili Mama kama ATADEMKA atajijua yeye na maccm yake masuala ya kuongoza nchi kwa uwazi, haki na kuheshimu sheria za nchi ikiwemo Katiba, Bunge na mahakama pia kupatikana kwa Katiba mpya na Tume huru ya uchaguzi kabla ya 2025 yote hayo HAYAKWEPEKI.
Swadakta
 
  • Nzuri
Reactions: BAK
Narubongo,

..Upinzani lazima wabadili mwenendo na ajenda zao baada ya kifo cha Magu na ujio wa Mama Samia.

..CCM nao lazima wajipange upya kutokana na mazingira ya kisiasa baada ya kifo cha Mwenyekiti wao.

..Nakubalina na mtoa mada kwamba, Mama Samia, kutokana na haiba na jinsia yake, anaweza kupata huruma na heshima fulani toka kwa wananchi. Na nakubaliana na mtoa mada kwamba wapinzani wanapaswa kulielewa hilo na kutafuta namna bora ya ku-deal na Rais na Mwenyekiti wa CCM wa aina hiyo.

..Mama Samia naye anapaswa kuelewa kwamba wananchi wana mategemeo fulani naye. Hii HESHIMA ambayo wanampa asiitumie vibaya. Kwa mfano, nini kitatoke ikiwa Mama Samia ataanza kutawala kwa mkono wa chuma kama Magufuli? Siamini kama wananchi wanategemea uhuni-uhuni, ukatili, na ubaguzi, na mambo mengine ya hovyo aliyokuwa nayo Magufuli ktk utawala wa Mama Samia.

..Je, ktk utawala wa Mama Samia ikitokea mpinzani mwingine akaumizwa kama alivyoumizwa Tundu Lissu wananchi watamchukuliaje Mama Samia na utawala wake? Je, ikitokea wapinzani wakaanza kufanyiwa vurugu, na dhuluma, na vyombo vya dola na mahakama, wananchi wataendelea kumheshimu Mama Samia? Je, kundi la WASIOJULIKANA likiendelea kutamba wananchi watatulizwa na kauli ya upole za Mama Samia?

..Kwa mtizamo wangu fursa na agenda za kisiasa zipo kwa kila upande. Kinachotakiwa ni kila upande kujipanga kuzitumia fursa hizo. Vilevile ni vizuri mazingira ya kisiasa yakawa ya HAKI SAWA kwa kila mwenye nia ya kufanya siasa hapa Tanzania.
 
Soma vizuri, hakuna kiongozi aliyewahi kukubalika na watu wote wakati wote, lakini pia hakuna kiongozi aliyekataliwa na watu wote wakati wote.

Kama ulimchoka wewe, hilo una uhakika nalo 100% na atakayekupinga ana matatizo. Lakini kusema alishachokwa na wengine, ni jambo lenye ukweli kwa assumptions na hypothesis, lakini ukubali wapo waliompenda hasa wenye maisha duni na yeye siku zote alijitafsiri kuwa hao ndio kipaumbele chake na hasira zake ziliwashukia wakwepa kodi na wala rushwa na waonevu ikiwemo wanyonyaji mpaka kwenye madini kule.

Sasa u-balance, usilazimishe kuwa kila mtu alimchoka, ulimchoka wewe.
Jiwe alichokwa na watu wenye akili timamu na wanaojielewa.
 
CDM wao hata kwenye uchaguzi walizunguka nchi kuomba kura wakiingia madarakani wapunguze madaraka ya raisi wayarejeshe kwa wananchi.

Wamekuwa wakipigania kupunguza chain ya wanasiasa kwenye utawala kwa kuondoa mfumo wa wakuu wa wilaya wa kuteuliwa na wakurugenzi waajiriwe na halmashauri zenyewe on merits badala ya wanasiasa.

Wewe huoni hili lingeleta tija kwenye usimamizi wa raslimali za wananchi?
You guys have you ever had an engagement on policy issues with politicians of Tanzania? .

I am a very close friends to many in opposition ? I also have many politicians pro government, for smooth operation of my businesses, I seldom engage both on political issues and governance .

This engagement has led me to believe that, there is a thin line separates both.

Together tuimarishe serikali yetu, nafikiri sio kweli kabisa tutakuwa salama opposition wakitawala.
Tulichagua opposition Hai, uongozi wote kwa miaka 20, Kwa tulioyapitia leo wakazi wanaoishi Hai wanamwita Sábaya kijana wao.

Watanzania echos zimebadilika sana.
 
Naona umeandika vitu vingi vingine umepatia vingine umekosea.

Ufisadi; hii hoja yako ime-base kwamba palipo na watawala lazima wizi uwepo, kwako kama CCM wanaiba, na upinzani lazima wataiba pia, ukazungumzia utafunwaji wa ruzuku ku-justify hii hoja yako.

Hivi yule CAG anavyotoa hati safi kwa baadhi ya vyama huwa ni maigizo yale?, siamini hilo. CAG anakuwa ameridhishwa na matumizi ya ruzuku ndio maana anafanya vile, sasa kama hawa jamaa wana hati safi, nini kinawashinda wakiongoza nchi wasiwe clean pia? wapewe nafasi badala ya kuwahukumu kabla.

Tena umezungumzia kiongozi wa upinzani kukaa madarakani muda mrefu kama kigezo kingine cha kutafuta upigaji, hapa nako nakupinga, kiongozi anakaa muda mrefu madarakani kwa kuchaguliwa na wajumbe wa chama chake, kama ana sifa mbovu kwanini wamchague?

Ukweli ni kwamba wanaridhishwa na utendaji wake ndio maana wanaendelea kumchagua, au kama una ushahidi wa kiongozi "aliyepiga" na bado anaendelea kuchaguliwa niambie, sio rumours za mtaani, hizo hazikosekani.

Hapo kwenye haki za binadamu napo umetumia mfano wa wengine kuwahukumu wengine, this to me is not fair, kwa mawazo yako haya ni sawa na una "play some sort of mind games" kuwaambia watu kuliko kuwapa hao wapinzani bora tubaki na hii CCM yetu, nop.
Naamini kama ungekuwa na close personal engagement na pande zote mbili na ukawa mkweli naamini usingeandika uliyo andika. Kuna taabu kubwa. Njia aliyoitumia Mwendazake sikuipenda, lakini nia na ujasiri wake kutaka kupunguza matatizo ya integrity namuunga mkono.

Wengine hatuzungumzi kwa kufikiri au kushawishiwa, tuna mabinti na vijana wa kuwazaa katika highest echelon in government leadership.

We have to revisit our ethos.
 
Watu tunamfurahia Mama kwa sababu Tulishamchoka MAGUFULI na Siasa zake za kikatili,
Ukweli ni kwamba CCM imechokwa kuliko kitu chochote duniani.
Kama mtoa mada anaamini Mama anapendwa waruhusu Katiba Mpya na Tume huru ya uchaguzi.

Nakuhakikishia Samia hawezi kwenda kinyume na matakwa ya CCM,na moja ya takwa kubwa la CCM Ni dhuluma kwa kila Jambo.

Mama mtago wake Ni mdogo tu,ama awe upande wa CCM ama awe upande wa wananchi.

Ikiwa Kikwete mwanasiasa nguli ndani ya CCM walimdhibiti suala la Katiba mpya ingawa yeye ndio alielianzisha likamshinda na heshima yake ikashuka sembuse Mama mchanga katika Siasa?

Kama CCM wanajiamini kuwa mama anapendwa waruhusu Katiba na Tume ili chaguzi ziwe za haki waone mziki wa Upinzani.
Mimi nimeichoka CCM katika maisha usione hivi,hata wanipe Lori la fedha ntawasaliti tu.
Acha uwongo, wakupe Lori la pesa bado huipendi, kwa hiyo wewe siasa ni ushabiki na sio maisha? Hufai kuchangia hapa unatupotezea muda na kujaza kurasa tuu.
 
Hakuna kitu kinaamua siasa kama 'wakati'..
Wanasiasa wazuri ni wale wanaojua nyakati zinavyobadilika na kwenda na wakati uliopo ...

Watanzania walikuwa wamechoshwa mno na siasa za Magufuli...na uongozi wake kiujumla..
Kubanwa Uhuru wa kuongea
Kufokewa na kukaripiwa
Kutoa matamko Kwa ukali..
Kuzungumza Peke yake..
Kutokukosolewa ..
Kukosekana Kwa mijadala na majadiliano..
Na mengi yaliyoenda na hayo..

Ujio wa Samia umebadili siasa Kwa ujumla..
Samia hafoki anaongea Kwa upole na kushawishi ..
Anazungumzia mazungumzo na mijadala..
Hazuii kukosolewa badala yake anakaribisha kukosolewa Kwa serikali yake..

Kikubwa zaidi ni Mwanamke ..
Watu wanamtazama Kwa 'kumhurumia'..
Na kumpa 'all benefits of the doubts'..
Na kuelewa kuwa anapambana na mfumo dume...
Watu wengi wanaju hii nchi ngumu na wanajua Samia atahangaika kuweza kumudu ...still wanafarijika na 'kurudi Kwa Uhuru wa kuongea na kukosoa'..

Sasa kama wapinzani wanafikiri siasa za kumshambulia Rais na serikali yake zinalipa bado kama enzi za JK watakuwa wanakosea sana....
Sana Sana wataonekana 'hawana adabu'
Na wanajaribu 'kumuonea' 'Rais Mwanamke' baada ya 'kidume ' JPM
'kuwakomesha hadi wakaufyata'..

Siasa za kipindi hiki zinahitaji ubingwa wa hoja kwenye mijadala ya kistaarabu..bila
Kuwa 'boa' wananchi ambao walishachoshwa na Magufuli Sana Sana wanataka 'mzunguko' wa hela urudi kama ule wa JK....

Kuleta siasa za ulalamishi..
Siasa za uwana harakati.
Na siasa za Ku target watu na kuwashambulia bila kujua ..'role halisi' ya hao watu ni siasa ambazo zinakuwa 'outdated ' so fast...

Watu wanampenda Samia sio Kwa sababu ni kiongozi bora.. wanampenda Kwa sababu wanaona 'nafuu inakuja'
Upinzani ukicheza siasa za kuleta 'distraction'wakati watu wanasubiri nafuu ije ..hasira za wananchi zinaweza washukia wao.....

Siasa inaendana na nyakati.. wapinzani wanasoma nyakati??

Kwa maelezo haya najiuliza kama “upinzani” una muhimu kwenye siasa za Tanzania. Je, wananchi/Watanzania tunahitaji kuwa na wanasiasa wa upande wa upinzani? Je, tunahusika, tunaelewa na tuna interest na masuala wanayoyapambania?

Au ni vikundi vya wanasiasa wenye maslahi yao binafsi wanayoyatafuta serikalini na inabidi watumie mbinu na mikakati maalum kutushawishi Wananchi tuwaunge mkono ilhali sisi tunaelekea kuwa “more sympathetic” na Rais na serikali yake?

Kama ni hivyo, hatuna haja na upinzani. They might as well close shop and look for other vocations.

LAKINI kama upinzani ni muhimu na unahitajika isipokuwa vyama vya upinzani vilivyopo sio makini, basi tuhamasishane kuanzisha upinzani makini badala ya kuhangaika kutoa ushauri kwa failures (if that’s the concern). Hakuna mwenye monopoly na upinzani.

Huwa sioni sawa kuona wengi wakichukulia “upinzani” kama brand na shughuli ya kina Mbowe, Lissu, Zitto, Lema, n.k. pekee.

Inatolewa kauli kama “wasipobadili namna wanavyofanya siasa kuna hatari watatoweka au watakuwa irrelevant kwenye siasa za Tanzania”! Au, even worse: “...upinzani utakuwa irrelevant Tanzania”! So what? Je, hao wakipotea ndio mwisho wa upinzani Tanzania? Kama itakuwa hivyo (upinzani ukiwa irrelevant) tatizo liko wapi?
 
Hakuna kitu kinaamua siasa kama 'wakati'..
Wanasiasa wazuri ni wale wanaojua nyakati zinavyobadilika na kwenda na wakati uliopo ...

Watanzania walikuwa wamechoshwa mno na siasa za Magufuli...na uongozi wake kiujumla..
Kubanwa Uhuru wa kuongea
Kufokewa na kukaripiwa
Kutoa matamko Kwa ukali..
Kuzungumza Peke yake..
Kutokukosolewa ..
Kukosekana Kwa mijadala na majadiliano..
Na mengi yaliyoenda na hayo..

Ujio wa Samia umebadili siasa Kwa ujumla..
Samia hafoki anaongea Kwa upole na kushawishi ..
Anazungumzia mazungumzo na mijadala..
Hazuii kukosolewa badala yake anakaribisha kukosolewa Kwa serikali yake..

Kikubwa zaidi ni Mwanamke ..
Watu wanamtazama Kwa 'kumhurumia'..
Na kumpa 'all benefits of the doubts'..
Na kuelewa kuwa anapambana na mfumo dume...
Watu wengi wanaju hii nchi ngumu na wanajua Samia atahangaika kuweza kumudu ...still wanafarijika na 'kurudi Kwa Uhuru wa kuongea na kukosoa'..

Sasa kama wapinzani wanafikiri siasa za kumshambulia Rais na serikali yake zinalipa bado kama enzi za JK watakuwa wanakosea sana....
Sana Sana wataonekana 'hawana adabu'
Na wanajaribu 'kumuonea' 'Rais Mwanamke' baada ya 'kidume ' JPM
'kuwakomesha hadi wakaufyata'..

Siasa za kipindi hiki zinahitaji ubingwa wa hoja kwenye mijadala ya kistaarabu..bila
Kuwa 'boa' wananchi ambao walishachoshwa na Magufuli Sana Sana wanataka 'mzunguko' wa hela urudi kama ule wa JK....

Kuleta siasa za ulalamishi..
Siasa za uwana harakati.
Na siasa za Ku target watu na kuwashambulia bila kujua ..'role halisi' ya hao watu ni siasa ambazo zinakuwa 'outdated ' so fast...

Watu wanampenda Samia sio Kwa sababu ni kiongozi bora.. wanampenda Kwa sababu wanaona 'nafuu inakuja'
Upinzani ukicheza siasa za kuleta 'distraction'wakati watu wanasubiri nafuu ije ..hasira za wananchi zinaweza washukia wao.....

Siasa inaendana na nyakati.. wapinzani wanasoma nyakati??
As usual, you have never disappointed Ndugu The Boss
 
Naamini kama ungekuwa na close personal engagement na pande zote mbili na ukawa mkweli naamini usingeandika uliyo andika. Kuna taabu kubwa. Njia aliyoitumia Mwendazake sikuipenda, lakini nia na ujasiri wake kutaka kupunguza matatizo ya integrity namuunga mkono.

Wengine hatuzungumzi kwa kufikiri au kushawishiwa, tuna mabinti na vijana wa kuwazaa katika highest echelon in government leadership.

We have to revisit our ethos.
What is "closed personal engagement"?

Nipinge nilichoandika hapo kwa hoja, kuwa na mabinti serikalini kwangu sio hoja, ni kujimwambafai.
 
Hivi mnatumiaga viungo gani kufikiri hadi kuandika hivi...kama huu ujinga ulioandika una ukweli kwanini mlitumia bunduki ujinga huu ambizianeni huko kwenye korido zenu

Sent from my Nokia 8.1 using JamiiForums mobile app
Kila unavyo chambua kwa kudhania kudhania huwezi kujua hali halisi.
Furahisha jukwaa, lakini sisi hutukuwataka wabunge tulio letewa. Sijui sehemu nyingine lakini mkoani kwetu hata uchaguzi ufanyike leo kama wagombea wa upinzani ni wale wale matokeo bado yatabaki hivi hivi.
 
Broo umeandika kitu kizito Sana ,CCM huwa kweli wanaondolewa asilimia 95 ya akili wanabakishiwaga asilimia 5 tu kwa ajili ya kupeleka chakula mdomoni badala ya puani,ya kukumbuka kuvaa nguo na kwa ajili ya dharula ndogondogo Kama kuvukia barabara na vitu Kama hivyo.
Uchaguzi mkuu huu uliopita ndio umewavua nguo CCM na dunia nzima ikaona.
Yaani hadi Mimi mfuasi wa Upinzani nikawa naona aibu Mimi.
Pole sana.
 
What is "closed personal engagement"?

Nipinge nilichoandika hapo kwa hoja, kuwa na mabinti serikalini kwangu sio hoja, ni kujimwambafai.
Kutoheshimu utawala bora upo katika public institutions ( the very meaning ya public institution, iwe CCM, CHADEMA, CUF na vyama vingine ) zote, tumekosa ubunifu wa kutatua matatizo ya kijamii bila kuumizana kimwili, kiihisia na kiuweredi. ( kwenye chama hata kama um elimika vipi, hutakiwi na mwenyekiti wewe ni mjinga tuu. Na kilaza kapendwa na mwenyekiti ili amlalie basi yeye ana maarifa na akili nyingi)

Uchu wa madaraka na pesa upo wa hali ya juu mno kiasi wahitaji hawataki kufuata njia za kiustaarabu kufikia wanacho kitaka.

Watu wanajali matokea bila kujali process. Suala na kupata matokeo tuu kitakiwacho, Matumizi ya elimu na ujuzi imekuwa sio kitu muhimu kama unapata matokeo.

Viongozi wote wamekuwa miungu watu katika hizo taasisi za umma.
Uhusiano mzuri hautegemei uwezo wako wa akili bali hali ya kipesa na instruments zinazo kulinda na Ushabiki.

Kuna ubinyaji wa demokrasia katika vyama vyote na ni kundi dogo walilokubaliana ndilo linalo tawala chama na sio uongozi uliochaguliwa.

Matumizi ya pesa yamekuwa yapo kufuata kiongozi atakavyo na sio kufuatana na mahitaji halisi ya chama.

Na mengine mengi tuu.
 
Mimi naona tuna upinzani imara sana, maana hawajabadilika no matter what. Wanaonekana wanahoja nzuri na ni wazalendo. Kwa sababu kama ingekuwa upinzani wanaangalia tumbo tu, hivi sasa hawana ubunge wala uwaziri vivuli,tusingewaona wakiwa na mission yoyote kisiasa wangesambaa.
Kuhusu kukosoa sidhani kama kunastaha kwenye kukosoa,kukosoa ni kukosoa tu. Hakuna lugha nzuri katika kukosoa jambo la msingi wasikilizwe penye tija parekebishwe.
Mfano mmoja ni Nape amekosoa maamuzi ya spika kuwabakisha wabunge bila kujali kwamba walifukuzwa na vyama vyao, ccm wamekuwa mbogo. Point ni Haijalishi umekosoaje,inategemea na utashi wa aliyekosolewa.
 
Kutoheshimu utawala bora upo katika public institutions ( the very meaning ya public institution, iwe CCM, CHADEMA, CUF na vyama vingine ) zote, tumekosa ubunifu wa kutatua matatizo ya kijamii bila kuumizana kimwili, kiihisia na kiuweredi. ( kwenye chama hata kama um elimika vipi, hutakiwi na mwenyekiti wewe ni mjinga tuu. Na kilaza kapendwa na mwenyekiti ili amlalie basi yeye ana maarifa na akili nyingi)

Uchu wa madaraka na pesa upo wa hali ya juu mno kiasi wahitaji hawataki kufuata njia za kiustaarabu kufikia wanacho kitaka.

Watu wanajali matokea bila kujali process. Suala na kupata matokeo tuu kitakiwacho, Matumizi ya elimu na ujuzi imekuwa sio kitu muhimu kama unapata matokeo.

Viongozi wote wamekuwa miungu watu katika hizo taasisi za umma.
Uhusiano mzuri hautegemei uwezo wako wa akili bali hali ya kipesa na instruments zinazo kulinda na Ushabiki.

Kuna ubinyaji wa demokrasia katika vyama vyote na ni kundi dogo walilokubaliana ndilo linalo tawala chama na sio uongozi uliochaguliwa.

Matumizi ya pesa yamekuwa yapo kufuata kiongozi atakavyo na sio kufuatana na mahitaji halisi ya chama.

Na mengine mengi tuu.
Naona unataka kuingilia maamuzi ya wengi kwa kuleta mashinikizo yako. Huyo mwenyekiti anapigiwa kura na wajumbe anashinda, sasa hapo huelewi kitu gani? tatizo mnataka mnaemkubali nyie ndio awe halafu yule anayekubalika na wengi asiwe, hiyo sio demokrasia.

Unaposema kuna kundi dogo linalotawala chama na sio uongozi uliochaguliwa wakati tunaona kura zinapigwa na mshindi anatangazwa na washindani wake, unataka kulazimisha rushwa ndio inatumika, nikikuuliza ushahidi wa hilo unao sijui kama utanipa jibu sahihi, kwangu kiongozi anaetumia rushwa ni yule asiekubalika, wengine record zao zinawabeba.
 
Back
Top Bottom