USHAURI: Rais Samia suluhisho pekee kwa Bandari Tanzania ni hili

USHAURI: Rais Samia suluhisho pekee kwa Bandari Tanzania ni hili

Tukipata serikali inayotumia akili tatizo la bandarini litapungua sana sana. Kulivyo na maendeleo ya teknolojia siyo rahisi kukosa solution. Bora waingie mkataba na kampuni yenye weledi ifanye utafiti wa kina na kuja na suluhisho la uendeshaji wa bandari (siyo waingie ubia).
Utafiti gani wakati shida inajulikana? Suala ni kufanya maamuzi tu
 
Nani kakwambia kipindi cha Mwalimu hakukuwa na ufisadi?

Unafikiri viwanda alivyovikuta na kuvianzisha pamoja na mashirika yalikufa kipindi gani?
Nimesema haukuwa wa kutisha kama sasa. Halafu tunazungumzia bandari na siyo sehemu nyingine. BTW ufisadi upo kila wakati hata kwa nchi zilizoendelea lkn tofauti ni level na namna unavyoshughulikiwa.
 
Kujua shida, na kujua namna ya kutatua shida ni vitu viwili tofauti. Ndiyo maana kina Samia wanadhani dawa ni kutumbua na wewe unadhani dawa ni uwekezaji.
Shida Bandari sio watu! Shida Bandari ni nature ya biashara yenyewe! Best performing ports worldwide zinaendesha kwa ubia between private sector na serikali! hata huko kwenye mataifa yqliyoendelea wanafanyq ivo

You need to know Bandari ni biashara yenye ushindani sana duniani
 
Nimesema haukuwa wa kutisha kama sasa. Halafu tunazungumzia bandari na siyo sehemu nyingine. BTW ufisadi upo kila wakati hata kwa nchi zilizoendelea lkn tofauti ni level na namna unavyoshughulikiwa.
Unaweza nipa statistics kuwa haukuwa wa kutisha?
 
Inasemekana chama Cha kijani kinaweka makada wake huko bandarini kwa maslahi ya kichama wakitaka mpunga wanaupata kirahisi can
Hiki chama uwepo wake Ni hatari kwa maendeleo ya Tanzania.
Hii ndo source ya shida zote nchini..

#MaendeleoHayanaChama
 
ujinga unauonesha wewe!

Unaotolewa hapa ni ushauri kutatua tatizo lililoshindikana kutatua! Kama unaona Bandari ya Dar haina msongamano wewe sitakiwi hata kukujibu humu maana unaonekana umejaa ujinga tu na kupinga pinga! Toka huko uliko na siku njoo Dar toka masaki hadi Posta njia ya coco beach utaona msongamano wa meli. Nenda pita Mandela Road hadi chalinze uone msongamano wa maloli alafu rudi humu
Wewe rekodi yako inafahamika vizuri hapa. Huna la maana la kushauri, na bila shaka huna uwezo wa kushauri chochote cha maana.
 
Amani iwe nanyi
Leo Rais wa JMT amemtumbua Mkurugenzi wa Bandari Ndug Erick Hamis.

Pamoja na kumtumbua Rais Samia amelalamika juu ya efficiency ya Mamlaka yetu ya Bandari na kusema kuwa Mamlaka hii ingekuwa inafanya kazi vizuri ingeweza kuchangia hata nusu ya mapato ya Bajeti yetu. Ni kweli kabisa naungana na Rais Samia kwenye hili!

Mfupa wa Bandari ni mfupa uliowashinda Marais karibu wote waliowai kutawala Tanzania! Hii imekuwa kawaida kila Rais mpya akiingia au Waziri Mkuu mpya akiteuliwa sehemu ya kwanzq kwenda kulalamika na kutumbua imekuwa Mamlaka ya Bandari Tanzania.

Kwa kumbukumbu zangu kuanzia kwa Mkapa, Kikwete, Magufuli hadi sasa Samia, Bandari hapajawai kupoa.

Hoja yangu kuu kwenye hili ni kwamba inawezekana sana bado hatujajua shida ni nini hasa pale Bandarini na kwa uelewa wangu mdogo napenda leo nimshauri Mhe Rais mambo ya kufanya na naamini kama nilivyoshauri kuhusu Ngorongoro na ikafanyika na sasa imefanikiwa basi nashauri juu ya hili la Bandari na naamini ikifanyika itafanikiwa

1. Lazima tukubali kuwa Bandari ya DSM haiwezi kuwa efficient kwa sababu imekuwa finyu kuhimili idadi ya mizigo, Meli na Magari kiushindani

2. Lazima tukubali kuwa Serikali haiwezi kuendesha bandari kwa ufanisi tunaoutaka katika dunia hii ya ushindani. Bandari kubwa zote duniani na zinazofanya vizuri kwenye soko la ushindani kuanzia Dubai, Hong Kong, Singapore, New York na nyinginezo, zinaendeshwa either kwa sehemu kubwa na private sector au kwa ubia baina ya Serikali na Private Sector

Hivyo ili kufanikiwa kupata ufanisi hapa Tanzania kwenye sekta ya Bandari , Lazima tutake tusitake, tufanye yafuatayo

a. Kwa haraka sana, Ijengwe Bandari ya Bagamoyo ambayo iwe na Gati zisizopungua 40. Bandari hii iendeshwe na Private sector with exception kwenye masuala ya Ulinzi, Usalama na Kodi

b. Sekta binafsi wapewe pia fursa ya kujenga Miundombinu ya Reli na barabara kuunganisha Bandari ya Bagamoyo na Jiji la Dar es Salaam ikiwemo reli ya kati SGR na TAZARA

c. Bandari za DSM, Tanga, Mwanza na Kigoma na Mtwara ziendeshwe kwa ubia na Private sector. Serikali isimamie masuala ya kodi , ulinzi na usalama tu!

d. Barabara ya Mandela Road( dsm) itanuliwe kuwekwa njia 8 kutokea Bandarini hadi Ubungo na utanuzi wa njia 6 uendelee kutoka Kimara hadi Ubungo. Hii ni ili kuleta ufanisi wa usafirishaji mizigo katika Jiji la Dsm. Ikiwezekana Private sector washirikishwe kwenye hili.

e. Kulikuwa na Mpango wa Kujenga Barabara ya Malori kutokea Bandarini hadi Chalinze. Mpango huu ufufuliwe na barabara hii ijengwe hata kwa kutumia Private sector! Fedha zitarudi haraka sana hata kwa toll tax!

Nchi kubwa duniani ziliona hili na wakaamua kufanya! Hata kwa Tanzania Serikali iking'ang'ania kuendesha bandari kila siku mtaishia kushikana uchawi na kutumbuana!

Ni suala la kuamua tu na wakati ni sasa
Tatizo la nchi hii ni akili ndogo za viongozi wetu. Tutafanya sana siasa za kutumbua watu kwani ni rahisi sana kutumbua lakini siasa za maendeleo zina watu wake na kwa bahati mbaya watu hao hawako kwenye siasa za nchi hii. Huwezi kuniambia huyu mama atafanya MAENDELEO kwa nchi hii!
 
Tatizo la nchi hii ni akili ndogo za viongozi wetu. Tutafanya sana siasa za kutumbua watu kwani ni rahisi sana kutumbua lakini siasa za maendeleo zina watu wake na kwa bahati mbaya watu hao hawako kwenye siasa za nchi hii. Huwezi kuniambia huyu mama atafanya MAENDELEO kwa nchi hii!
Kwa nini asiweze kufanya? mbona anafanya maendeleo sehemu nyingi tu?
Kikubwa apewe ushauri mzuri na sahihi tu
 
Kwa nini asiweze kufanya? mbona anafanya maendeleo sehemu nyingi tu?
Kikubwa apewe ushauri mzuri na sahihi tu
Ni mtu wa kawaida sana kama akina Nyerere, Mwinyi, Mkapa, Kikwete na Magufuli. Hakuna lolote walilofanya la pekee watu hawa ndio maana nchi yetu ni ya kawaida tu.
 
Ni mtu wa kawaida sana kama akina Nyerere, Mwinyi, Mkapa, Kikwete na Magufuli. Hakuna lolote walilofanya la pekee watu hawa ndio maana nchi yetu ni ya kawaida tu.
Maendeleo ni process! Roma haikujengwa kwa siku moja! Kikubwa ni kufanya maamuzi sahihi kwa wakati sahihi
 
Back
Top Bottom