Uteuzi: Rais Samia ateua Mshauri wa Sheria na Mshauri wa Mabadiliko ya Tabianchi na Mazingira

Uteuzi: Rais Samia ateua Mshauri wa Sheria na Mshauri wa Mabadiliko ya Tabianchi na Mazingira

Huyu Masaju kama sijakosea alikuwa ndio Naibu Mwanasheria mkuu wa serikali awamu ya 4 na baada ya Werema kutoka akashika usukani yeye.

Kiufupi hiki cheo cha Mshauri wa Rais mambo ya sheria hakina tofauti kubwa kimajukumu na Mwanasheria Mkuu wa Serikali maana huyo ndiye mshauri wa serikali na Rais kwa mambo yote ya Kisheria. Kwa lugha nyingine tunaweza kusema Mama ameona Feleshi hatoshelezi
 
Anashauri kuhusu tabia nchi na mazingira Rais wapi na ili afanye nini ?, Kwanini ushauri wake asiupeleke huko kwa wadau ili wautungie sheria na mikakati ? Au kama vipi Rais anapenda sana hii Topic aingie Youtube na kusoma makala mengi tu Online... (At least gharama itakuwa ni bundle na sio package atakayopewa huyu mdau)
Umeongea kienyeji sana. Climate change au mabadiliko ya tabianchi ni mada Muhimu sana kwa sasa! Lazima Mkuu wa nchi apate ushauri maridhawa!
Tatizo naliona kwa huyo mteuliwa!
 
Asa mwanasheria mkuu wa serikali na waziri wa katiba na sheria watafanya kazi gani
 
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan amefanya uteuzi kama ifuatavyo:-

1. Amemteua Jaji George Masaju kuwa Mshauri wa Rais, Masuala ya Sheria (Advisor to the President – Legal Affairs). Jaji Masaju ni Jaji wa Mahakama Kuu Kanda ya Dodoma. Uteuzi huu umeanza tarehe 20 Aprili, 2023; na

2. Dkt. Richard Stanslaus Muyungi kuwa Mshauri wa Rais, Masuala ya Mabadiliko ya Tabianchi na Mazingira (Advisor to the President – Climate Change and Environment). Kabla ya uteuzi huu Dkt. Muyungi alikuwa Meneja wa Mazingira, katika Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO). Uteuzi huu umeanza tarehe 19 Aprili, 2023.View attachment 2595400
Huyu si ndo yule alikuwa anabanwa na lisu na kudai hata akipewa ushauri wa bure na huyo mwanasheria hawezi kuupokea
 
Hii nchi ngumu sana!!yaani wanaofaidi matunda ya nchi ni wale wale tu!!utafikiria kuwa ndio wenye haki miliki na nchi!!akitoka hapa utasikia yupo pale!!Afrika tuna safari ndefu sana tena isiyo na matumaini!!
Matunda gani yaho ndugu!
 
Anna Makinda alikuwa Speaker mzuri sana
 
Hii nchi ngumu sana!!yaani wanaofaidi matunda ya nchi ni wale wale tu!!utafikiria kuwa ndio wenye haki miliki na nchi!!akitoka hapa utasikia yupo pale!!Afrika tuna safari ndefu sana tena isiyo na matumaini!!
hamna jema hata kidogo! Sasa ww anakujulia wap ili akuteue! Ndo shida ya wakosoaji weusi! Humu tu umeingia na jina bandia! Halafu unataka nini sijui! Au na ubandia wako umefanya kitu gan cha kuonekana chenye manufaa kwa nchi ? Achen hzo bhana
 
Hii nchi ngumu sana!!yaani wanaofaidi matunda ya nchi ni wale wale tu!!utafikiria kuwa ndio wenye haki miliki na nchi!!akitoka hapa utasikia yupo pale!!Afrika tuna safari ndefu sana tena isiyo na matumaini!!
hamna jema hata kidogo! Sasa ww anakujulia wap ili akuteue! Ndo shida ya wakosoaji weusi! Humu tu umeingia na jina bandia! Halafu unataka nini sijui! Au na ubandia wako umefanya kitu gan cha kuonekana chenye manufaa kwa nchi ? Achen hzo bhana
 
Back
Top Bottom