Uzeeni mwanaume ana uhitaji wa ndoa zaidi kuliko mwanamke. Chukua hatua

Uzeeni mwanaume ana uhitaji wa ndoa zaidi kuliko mwanamke. Chukua hatua

Ukishaishi na mwanamke miaka 5 kama sikosei na kukawa na uthibitisho huo, huyo ni mkeo.
Kama hukosei !!!!

Ninavyojua kwenye kudai haki katika mambo yanayohusu ndoa, cheti cha ndoa ni muhimu maana hilo ndio kinatambulisha kuwa fulani n mkeo
 
Sijui wewe unaishi kwenye jamii gani lakini jamii ninayoishi mimi ina kina mama waliotuzaa, wadada tuliokua nao na wadogo zetu wa kike. Tunaona changamoto wanazopitia.

Kwaiyo agenda potofu za ubinafsi na ubaguzi zinazolenga kudhoofisha jinsia fulani na kuchochea separation kwenye jamii siwezi kuacha kuzikemea.

Ndoa ni kitu cha hiyari, unaona haikufai achana nayo, waachie inayowafaa. Binafsi naona muunganiko wa watu either official or unofficial ni jambo jema linalojenga umoja kwa sababu opposite yake ina mabaya mengi kuliko mazuri!
Basi anza na waroman kwa kuleta upadri na usista acha kujitoa ufahamu
 
Kama hukosei !!!!

Ninavyojua kwenye kudai haki katika mambo yanayohusu ndoa, cheti cha ndoa ni muhimu maana hilo ndio kinatambulisha kuwa fulani n mkeo
Kama sikosei nikimaanisha sina hakika na muda unaokidhi hilo takwa.

Ukishaishi nae kwa muda unaokidhi hayo matakwa ana haki zake, tena kama umezaa nae ndo kabisa. La muhimu ni kuwa makini, usiishi na malaya anayekuuzia mwili wake otherwise wasiwasi utatoka wapi?
 
Ukiwa umezeeka, ukipata mwanamke anaejitambua atakurudisha ujanja na USO utanga'aa kama wa mtoto mdogo. Utafurahiya maisha. Ukikosea USO utakunjamana kama ngozi ya goti na utakufa mapema.
 
Na huyo mke hazeeki unazeeke wewe tu?

Sent using Jamii Forums mobile app
Anazeeka ndo maana unashauriwa umzidi mkeo umri. Sio lazima ila inashauriwa hivyo. Mwanaume wa miaka 70 anahitaji huduma ya mwanamke kuliko mwanamke wa miaka 50 anavyohitaji huduma ya mwanaume.

Yaani wewe ukiwa na miaka 70, unamuhitaji mwanamke kuliko mwanamke wa miaka 50 anavyomhitaji mwanaume.
 
Ukiwa umezeeka, ukipata mwanamke anaejitambua atakurudisha ujanja na USO utanga'aa kama wa mtoto mdogo. Utafurahiya maisha. Ukikosea USO utakunjamana kama ngozi ya goti na utakufa mapema.
Mada iishie hapa
 
Usiombe uwe mzee halafu huna pesa ukuweka akiba ya hata vijumba vya kupanga.
Mke uwalisha sumu watoto utabakia mwenyewe ndani unahesabu bati.
Ukiwa na pesa utachukua dogo dogo wa kudoea urithi wakati ukifa.
 
So unaweza kukubaliana tu na mwanamke pasipo kuungana??
Kuungana ukimaanisha nn? Unaweza kufunga ndoa na mwanamke kwa makubaliano ya kipindi maalum. Mfano, Tunafunga ndoa kwa ajili ya watoto wetu, wakfika miaka 5 tunaachana.

Unajua sisi tumeionganisha ndoa na dini ndo sababu tunaiona kama adhabu. Mfano ukatolikini hakuna kuachana hata kama umeoa mchawi sasa hapa ni hatari.
 
Kuungana ukimaanisha nn? Unaweza kufunga ndoa na mwanamke kwa makubaliano ya kipindi maalum. Mfano, Tunafunga ndoa kwa ajili ya watoto wetu, wakfika miaka 5 tunaachana.

Unajua sisi tumeionganisha ndoa na dini ndo sababu tunaiona kama adhabu. Mfano ukatolikini hakuna kuachana hata kama umeoa mchawi sasa hapa ni hatari.
Huoni kama kufunga ndoa kwa mkataba ni sawa na kutokuoa tu.
 
Wanaume tunapozeeka tunarudi kuwa watoto,

Wanaume husema "men age like a wine" wakiamini kua kadri wanavyokua ndivyo wanakuwa na mvuto zaidi kwa kuwa wanajijenga kiuchumi, ila ukweli ni kuwa kadri mwanaume anavyokua ndio anakuwa na uhitaji wa ndoa zaidi( kuwa na mwanamke atakayemjali.)

Huwa watu wanawacheka single mother, lakini ukweli ni kuwa single mother akishakuza, basi anakula maisha. Kazi kwa mwanaume

Kwa mfano..

1. Mtoto wa kiume hawezi kumhudumia baba yake fully, coz ana familia na anabidi atoke akatafute.
2. Mtoto wa kike hawezi kumhudumia baba yake,
3. Kaka au mdogo wako wa kiume hawezi kukuhudumia.
4. Mdada wa kazi hawezi kuhudumia mwanaume (mzee) ipasavyo.
4. Ni rahisi bibi kuishi single na wajukuu au hata mwenyewe na maisha yakaenda kuliko babu

Kiumbe pekee anaeweza kukusaidia ni mke wako.

Mwanaume usisubiri uzeeke ndio uoe, utaleta mgogoro kwenye familia bure

IMG_7889.jpg
 
Huoni kama kufunga ndoa kwa mkataba ni sawa na kutokuoa tu.
Unachanganya tafsiri ya ndoa. Weka dini pembeni. Sheria inasema ndoa ni nn? Ukumbuke watumishi wa dini yako huwasainisha mkataba wa serikali pia, sema kipengele kinachowekwa tiki ni kile cha kudumu(milele) ila mkataba ni ule ule wanaosaini wanaoenda kufunga kwa mkuu wa wilaya kwa kipengele cha miaka kadhaa. Na wote mnatambulika kama wanandoa katika kipindi hicho mlicho katika ndoa. Tofauti ni ww umesaini mkataba wa mpaka kifo, mwenzako amesaini miaka kadhaa halafu watajua kuwa waendelee au la.
 
So kulingana na maelezo yako hapo inamaana umechukulia assumption zifuatazo:

1. Mwanaume lazima awe mgonjwa akifika uzeeni

2. Mwanaume ana mwili mbovu unaochoka haraka kuliko wa mwanamke.

3. Mwanamke hawezi kuumwa akawa mgonjwa wa kutegemea misaada.

4. Mwanaume mzee ni sawa na mtoto mchanga.

5. Jamii humtenga mwanaume anayezeeka.

6. Hakuna taasisi au watu au wasamalia wema wanaweza kumsaidia mwanaume anapofika uzeeni.

So kimsingi umetumia assumptions ambazo zimetokana na mapokeo ya historia za maisha ya wazee wetu kujijibu kuhusu uhalisia wa maisha na kutengeneza matarajio yako kuhusu future ya wanaume wote. HUU NI UBATILI.

1. Unaweza kuwa na mke na familia wakafariki wote kwa ajali au ugonjwa then ukarejea kuwa bila kuwa na mtu. So usiweke guarantee kuwa maisha yako yanakuwa assured sababu upo na mke na watoto ujana wako.

2. Wanawake hutumia survival instinct na techniques kuishi sababu wanajijua hawana uwezo wa kupambana na changamoto za kiasili katika nature. Nitakufafanulia hapa kidogo.

Mwanamke uzuri wake huwa upo kati ya miaka 15 na hauwezi vuka 40 especially akiwa ameshapata watoto mara kadhaa so anajua hakuna mwanaume wa hadhi ya juu na mwenye pesa atamtamani katika umri huo na kutoa pesa na mali zake in exchange for kids and bills zake.

So mwanamke anapambana tokea usichana wake kuhodhi rasilimali ambazo atakuja zitumia baadae akishachuja. Na hili anafanikiwa kwasababu kuna mifumo ameshaimanipulate ili hili lifanikiwe mfano kwenye maswala ya kidini kisheria na kijamii ameweza kutengeneza utaratibu kuwa akiolewa basi watoto na mali za mumewe zote ni mali zote atavihodhi. Ukutaka kujua hili mwambie mkeo unataka muuze kila kitu muhamie sehemu mpya uone roho yake ipo wapi.

So, hii inamfanya mwanamke kuwa makini katika maisha yake ili kupata mali na mwisho kabisa kupata watoto ambao wewe utawasomesha kwa bidii ili waje kumtunza yeye uzeeni wewe ukiwa unapambana na magonjwa kama kisukari, pressure, ukimwi, kansa ambayo ni matokeo ya wewe kutumia takriba miaka 40 ya ujana wako kumhangaikia yeye na watoto wake na kusahau kuwa ukishachoka yeye hakuhitaji tena anachotaka ufe ili usimsumbue na watoto wake aache kula raha wakae kukuuguza.

3. Mwanaume kufika umri mkubwa na kuwa tegemezi kwa mkewe na watoto ni matokeo ya poor planning na resources wastage tokea ujana wote.

Wanaume tunatumia zaidi ya miaka 40 ya ujana wetu pengine na zaidi kuwapambania watu ambao wakisikia tumestaafu tumechakaa hawataweza tuhangaikia kwa miaka hata mitano 5 kabla hawajaanza tuombea tufe maana tunakuwa mzigo wa kudumu kwao jambo ambalo hawapo tayari kulibeba.
Imagine kumhudumia mzee wa kuanzia miaka 60 ambaye hana pesa na anakutegemea kama mtoto utaweza? Miaka 60 akihudumiwa vizuri anaweza fika hata miaka 120 akiwa na nguvu za kutembea mwenyewe na kuongea ni chakula tu na matibabu mazuri. Sasa hii ni kitu ambayo mkeo hatokuwa tayari kuona inatokea maana itabidi mojawapo afe ili watoto au mtoto asiwe na mzigo mkubwa sana wa kuhudumia wazazi wawili ndio maana umri huu akina mama ndio huwa wanaanza kukengeuka na kuwageuka wanaume zao kwa watoto na kuanza figisu za kuwafitini watoto na baba zao ili wao waishi vizuri na ombi kubwa la mwanamke mzee ni mume wake atangulie mbele za haki ili yeye apumzike aishi kwa starehe uzeeni pake.

4. Nikuulize je umeshawahi kuhoji ulaji wako na namna unacheki afya yako katika umri wako huu wa ujana? Jukumu la afya yako si la mkeo wala watoto wako, ni jukumu lako binafsi. Therefore, usitegemee mkeo afanye kazi hii aache kujitazama afya yake kwanza maana yeye anajijali zaidi kuliko wewe.
Ipo hivi mkeo atakupikia chakula ule unenepe asifiwe anamtunza mumewe but nini hutokea kwa mtu anayenenepeana na kujaza mafuta mwilini mwake? Kisukari, pressure, stroke siku za baadae, na mengineyo ni matokeo ya kutozingatia afya na haya huja kutokea uzeeni huko umri wa kuanzia miaka 60+ ndipo haya maradhi huanza kazi.

But wakati wako wa ujana ukiwa makini na life style yako kwenye diet yako yaani chakula gani unakula,umakini na unywaji wa madawa makali hovyo ambayo huchosha figo na ini lako na moyo wako especially viagra, painkillers kali kama ibuprofen,pombe kali kila siku,dawa za nguvu za kiume etc, mazoezi ya mwili, kuwa makini na nani unalala nae kitandani kupunguza risk za magonjwa yatayodhoofisha mwili kupitia madawa ya kuyatibu, namna unapumzika na kulala, unadeal vipi na stress za mahusiano na kuzikomeshaje mfano unaishi na mwanamke anayekusumbua kichwa na si muelewa why upo nae sasa na anakuzeesha mwili na kukuchosha akili piga chini.

5. Unatabia gani za kifedha katika haya maisha yako. Mfano unatumia vipi mapato yako yote hadi ukifika uzeeni ukose hata mia unaanze kulaumu watu kuwa ukiwasaidia au kuwasomesha na wao sasa wanakutenga.

Muda wako wa miaka ya utafutaji yaani kuanzia miaka 10 hadi 50+ itumie kuweka mpango wako wa pembeni ambao haumhusu mkeo wala watoto wako. Mkeo akijua umekwisha maana na kile kidogo atataka kiwe chake na akishakihodhi wewe kwake utakuwa ni threat ambayo atatakiwa kuitokomeza ili akitumie kwa uhuru bila bugudha.

Nyakati hizi ukiishi kwa mifumo ya babu na baba zetu ya kuhudumia bibi na mama zetu kwa asilimia 200% , kisha bado ujitoe kwa ukoo wako na ukoo wa mkeo, then tegemea matokeo yale yale ya kufika miaka 60+ ukiwa hoi na kukosa msaada sababu binadamu hupenda kusaidiwa ila sio kusaidia. Roho yako nzuri iwekeze kwako kwanza kwa 90% then 10% uwekeze nje yako. Nasema hivi kwasababu usijekutegemea kuna mtu atakumbuka huruma zako na kujitoa na yeye ajitoe kwa kadiri ile ile kama yako hiyo sahau.

Imagine ukitumia 90% kwenye mipango yako ya kuwekeza. Sio unapokea mshahara unampa mkeo apange matumizi. Unaokota milioni kumi unampa mkeo apange matumizi, ndugu utakuja juta. Why usiweke mkakati wa biashara ili kuongeza mapato, kuwa na bodaboda, kuwa na bajaji, kuwa na mradi wowote ambao wewe ndie utaratibu kila kitu. Ili pesa yako ianze kukua ukifika by the age 50+ account yako iwe na not less than 400milions in savings na huko mtaani una vitega uchumi ambavyo vipo active. Ukipewa kiinua mgongo chako inakuwa kama ela ya vocha tu.

Hii itakupa maisha marefu na mambo ya kufanya uzeeni na utaishi bila stress za kipato wala kuhangaika na watoto. Wacha watoto wadeal na mama yao maana ndio investment yake. Wewe unafocus na chakula, mazoezi na kuendelea kusimamia baishara zako bila stress. Utaona kama huo umri wa utu uzima ukifika hizi story za sijui nani atakutunza utakutana nazo.

Kuna mengi ambayo tunakosea kama wanaume then tuna assume kuwa ni namna maisha yalivyo au ni nature while si kweli. Ukipanga maisha yako yaende kwa mfumo fulani ndivyo itakuwa hivyo hivyo hadi uzeeni.

So kama utaishi kwa kutapanya kile unachokitafuta kwa jasho la damu then utegemee uzeeni kuna sehemu utapata sapoti then jua unajiandaa kuumia. Mwisho wa siku utajua hujui. Jiandae mapema mazingira ya kustaafu ili uishi kwa starehe baadae sio kuanza kuwaza waza na kupata msongo wa mawazo uzeeni.
 
Usichukue mifano ya walioshindwa ukaifanya ndio asili ya maisha.

Mwanaume jitunze afya yako, fanya mazoezi kula vizuri, acha nyama choma na bia zisizo na mpangilio, kula matunda, kunywa maji, kula mboga mboga.

Kwa hali yoyote usiwe na uzito wa kufika kg. 90 jitahidi sana ucheze kwenye 80 hadi 60+, utaishi maisha mazuri sana.

Magonjwa yetu mengi na kuchoka kwetu kwa kasi kunatokana na ulaji mbovu hasa wakati tukiwa na miaka 30 - 45.

Wakuu tujali sana afya zetu ikiwa ni pamoja na afya ya akili.
No one can give a better comment like this kwenye hii mijadala sijui kwann huwa watu hawafikirii namna hii.
 
Yesu mwenyewe alisema watu wanaoa kwasababu ya tamaa siyo kuleana uzeeni na akatoa angalizo kama unaweza kujizuia Bora usioe

Sent from my TECNO KC8 using JamiiForums mobile app
 
Kuna ukweli katika hili.

Sijawahi kutana na mbabu single ambaye yupo sawa psychologically. Mwisho wa siku "all we need is to be needed". Na watoto huwa ni mama, akiondoka anaondoka nao, akiwepo na wao wapo. So you can imagine how hard it can get if you find yourself lonely at late 60 huko. No energy, no partner to cuddle, no f*cking family! Only brick walls around you.

Japo wanawake wanazingua sana lakini we need them. It's Nature!
Loneliness ni matokeo ya namna gani unatumia muda wako na unafanya nini na muda wako wa ziada. Sasa wewe mtu miaka yote ulikuwa muajiriwa wa serikali unatoka nyumbani asubuhi ukitoka job unapitia Bar kula bata jioni unarudi unakaa dakika chache na mkeo then unalala ndio mfumo wako wa maisha.

Ukifika umri wa uzee na umestaafu, marafiki baadhi wamehama makazi labda wamehamia makazi yao ya kustaafu nje ya mji, wewe umehamia makazi yako mapya pengine, mkeo sasa ataanza kujishughulisha na biashara kuchangia kipato hivyo muda mwingi hatakuwa nyumbani. Watoto watakuwa wameanza chuo au kumaliza na kuanza kujitegemea na wamehama nyumbani.

So basically muda huu hautakuwa na ratiba ya kueleweka utakuwa tu upo free muda mwingi na hauna ramani. Utaanza kukaa na madogo kijiweni ambao hamtawezana kwenye mijadala na pengine watakupuuza. Na vile hauna hata hela utashindwa hata kukaa bar kupiga kinywaji kidogo utaboreka sana ndio hapo sasa mnaanza kusema upweke unauwa.

Ila kama utakuwa na mfumo wa tofauti wa kupanga maisha ili muda huo ukifika ukukute una shughuli unafanya na haupo idle yaani unakuwa ni mtu mwenye shughuli zako huo upweke unatokea wapi kwa mfano.
 
Uwongoo..
Siku hizi mwanamke ukiwa mzee anakusaidia ufe mapema atawale miradi...
Mimi binafsi babu yangu alikuwa mwalimu na alistaafa 1996..

Bibi yangu alikufa kitambo ila babu yangu babu anaonekana kama si mzee kabisa na anaishi pekee yake anapika mwenyewe na kazi ndogo ndogo za hapo kwake na nguo anamashine yake ya kufua licha ya kwangu ana watoto 9 wa kuzaa lakini kila mtoto anapambana na hali yake na wamesambaa na wengine ni wagonjwa, sisi wajukuu hatuna msaada sana kwake tunapambana na hali zetu kifupi hatutegemei hata kidogo...

Kipindi bibi yupo kuliko na magomvi sana hapo kwa babu..
hivyo usiwe na wazo hilo eti ndoa ni muhimu mzeeni
Watu hii mifano huwa hawazungumzii ili tuingie mkenge tuishi Maisha ya kipuuzi.
 
Unachanganya tafsiri ya ndoa. Weka dini pembeni. Sheria inasema ndoa ni nn? Ukumbuke watumishi wa dini yako huwasainisha mkataba wa serikali pia, sema kipengele kinachowekwa tiki ni kile cha kudumu(milele) ila mkataba ni ule ule wanaosaini wanaoenda kufunga kwa mkuu wa wilaya kwa kipengele cha miaka kadhaa. Na wote mnatambulika kama wanandoa katika kipindi hicho mlicho katika ndoa. Tofauti ni ww umesaini mkataba wa mpaka kifo, mwenzako amesaini miaka kadhaa halafu watajua kuwa waendelee au la.
Understood.
 
  • Thanks
Reactions: Tsh
Back
Top Bottom