Uzi wa sehemu za gharama nafuu kulala kwa wanaokwenda kwenye saili Dodoma

Uzi wa sehemu za gharama nafuu kulala kwa wanaokwenda kwenye saili Dodoma

Mkuu, hivi Hostel za UDOM huwa inawezekana wanaruhusu watu wa Saili kulala?


Kuna wazo hapa limenijia, hivi kwanini Chuo Kikuu UDOM kisingeanzisha utaratibu maalumu wa kuongea na Wanafunzi wao, ambao watakuwa tayari vyumba vyao vitumike kwa wanaofanya Saili kisha mapato yanayopatikana yawe ni sehemu ya ada yao ya Hostel na Chuo kipate kidogo!

Kuliko kuacha watu wateseke mitaani, naliona hili kupunguza sana gharama za wanaokwenda kufanya Saili na hata hao wanafunzi kupunguza au kuepuka kabisa kulipa ada za Hostel.
Wazo zuri sana, kazi kwao kwa wahusika
 
Hzo Hostel za Udom wanalipia pesa ngapi..?
Akalale hostel za UDOM, Humanity/ social. Au aende COED, ng'hong'hona Au alale nanenane stand, mbona pazuri tu. Au aende uswahilini huko mailimbili nk
Na ukizingatia vikao vya kamati za bunge vimeanza, dodoma inafurika 😀😀🙌
 
Hahahaa, access ya mrija wa Asali kutokana na Tozo zetu tunaitafuta kwa udi na uvumba sana. Nchi ni yetu sote na keki ya Taifa ni haki ya kila mmoja wetu. Tupambane kwa njia yeyote tunayoona inafaa

Hahaha, ni kweli Mkuu.
 
Hahaha, nakumbuka miaka hiyo kuna jamaa nilipewa stori yao, wao waliona ni bora wakakeshe club na wengine bar.

Hayo makundi yote mawili hakuna hata mmoja alipata kazi kwenye saili husika.

Ubora wa usingizi nao ni sehemu kubwa ya maandalizi ya mtihani.
 
Wakuu, sio vibaya wakati tunasubiri wenye uzoefu wa sehemu nzuri za kulala, tukaendelea kutaja na magari au namna rahisi zaidi za kufika Dodoma kwenye Saili.
 
A1982C2F-7710-41D8-ADAF-34672B9D21A9.jpeg
 
Wakuu, sio vibaya wakati tunasubiri wenye uzoefu wa sehemu nzuri za kulala, tukaendelea kutaja na magari au namna rahisi zaidi za kufika Dodoma kwenye Saili.

Mimi naanza na Shabiby, inasemekana kwa hii route ni magari ya uhakika sana na yanafanya vizuri.

Wewe huwa unatumia mabasi au mbinu gani kufika Dodoma?
 
Sikieni sasa kama huna kabisa hela, kuna guest moja bei ni 5k choo nje, na 7k(self) kama sijasahau, hii ipo karibu kabisa na Chuo yani unakiona chuo kile pale na unaweza ukatembea kabisa ila kuna mwendo.

Jinsi ya kufika: ukifika stend ya Mabasi panda gari zinazoenda mjini saba saba, ukifika mjini panda hiace zinazoenda ntyuka eeh ndio jina ilo ilo sijakosea.... shuka mwisho wa gari alafu nenda mbele barabara inapoelekea upande wa kulia utaiona iyo guest ni Local flani ila kama huna hela inaweza kufaa.
 
Sikieni sasa kama huna kabisa hela, kuna guest moja bei ni 5k choo nje, na 7k(self) kama sijasahau, hii ipo karibu kabisa na Chuo yani unakiona chuo kile pale na unaweza ukatembea kabisa ila kuna mwendo.

Jinsi ya kufika: ukifika stend ya Mabasi panda gari zinazoenda mjini saba saba, ukifika mjini panda hiace zinazoenda ntyuka eeh ndio jina ilo ilo sijakosea.... shuka mwisho wa gari alafu nenda mbele barabara inapoelekea upande wa kulia utaiona iyo guest ni Local flani ila kama huna hela inaweza kufaa.
Inaitwaje mkuu
 
Wewe huwa unatumia mabasi au mbinu gani kufika Dodoma?

Sina gari maalum, huwa naangalia bei ya nauli, kama natokea Dar kwenda Dom napanda gari yoyote inayoenda Dom au kupita Dom.

Ila magari kama Champion, Mshikamano, Kapricon(nishawahi kulipanda) siwezi kuyapanda yamechoka sana
 
Back
Top Bottom