Uzi wa sehemu za gharama nafuu kulala kwa wanaokwenda kwenye saili Dodoma

Uzi wa sehemu za gharama nafuu kulala kwa wanaokwenda kwenye saili Dodoma

Sikieni sasa kama huna kabisa hela, kuna guest moja bei ni 5k choo nje, na 7k(self) kama sijasahau, hii ipo karibu kabisa na Chuo yani unakiona chuo kile pale na unaweza ukatembea kabisa ila kuna mwendo.

Jinsi ya kufika: ukifika stend ya Mabasi panda gari zinazoenda mjini saba saba, ukifika mjini panda hiace zinazoenda ntyuka eeh ndio jina ilo ilo sijakosea.... shuka mwisho wa gari alafu nenda mbele barabara inapoelekea upande wa kulia utaiona iyo guest ni Local flani ila kama huna hela inaweza kufaa.
Kutoka hapo hamna usafiri hata wa Bajaj kwenda UDOM?
 
Usafiri upo sabasaba utapanda daladala au bajaji wewe tu

Asante sana.

Hata hivyo nilikusudia kutoka mikoani kwenda Dodoma. Kwa mfano Shabiby inatoka Dar es Salaam kwenda Dodoma. Vivyo hivyo kama ingefaa tungetaja na mabasi ya kutoka mikoa mingine yenye ubora na gharama zenye ahueni.

Hatuwezi amini, lakini kuna watu huu route ya Dom hawajawahi kuienda hata mara moja, na hawajui magari gani ni mazuri.
 
Sikieni sasa kama huna kabisa hela, kuna guest moja bei ni 5k choo nje, na 7k(self) kama sijasahau, hii ipo karibu kabisa na Chuo yani unakiona chuo kile pale na unaweza ukatembea kabisa ila kuna mwendo.

Jinsi ya kufika: ukifika stend ya Mabasi panda gari zinazoenda mjini saba saba, ukifika mjini panda hiace zinazoenda ntyuka eeh ndio jina ilo ilo sijakosea.... shuka mwisho wa gari alafu nenda mbele barabara inapoelekea upande wa kulia utaiona iyo guest ni Local flani ila kama huna hela inaweza kufaa.

Mkuu, asante sana. Nakuahidi malipo ya huu wema utayaona kwa mambo yako kukunyookea zaidi.
 
Sina gari maalum, huwa naangalia bei ya nauli, kama natokea Dar kwenda Dom napanda gari yoyote inayoenda Dom au kupita Dom.

Ila magari kama Champion, Mshikamano, Kapricon(nishawahi kulipanda) siwezi kuyapanda yamecho sana

Nashukuru sana Mkuu, naamini kwa hili jibu lako la uzoefu na wengine watakuwa makini kwenye kuchagua.
 
Chimbo lingine ni kwenye hostel za veta hapo Dodoma karibu na Bunge
Ni pahala salama kabisa kwa bei nafuu sana

Mkuu, tunashukuru sana. Hivi pale kwenye zile hosteli ni mpaka koneksheni au ni yeyote akifika getini anaweza kujielezea akapata huduma.

Vipi makadirio yake ya gharama kwa kulala usiku mmoja, yanaweza kufika kiasi gani?
 
Ondoka jioni kwenu ufike dom alfajiri siku ya usahili. Jioni unageuza kama umetoka kapa

Wazo zuri sana, hili si linamaanisha kupanda malori yale ya IT na magari binafsi?
 
Wazo zuri sana, hili si linamaanisha kupanda malori yale ya IT na magari binafsi?
Sidhani kama ni nzuri kujiandaa na interview za utumishi nafikiri ni vyema ukaenda mapema ili hata akili iwe imetulia na lodge za bei rahisi zipo makulu pale karibu na udom utumishi
 
Wazo zuri sana, hili si linamaanisha kupanda malori yale ya IT na magari binafsi?
Sidhani kama ni nzuri kujiandaa na interview za utumishi nafikiri ni vyema ukaenda mapema ili hata akili iwe imetulia na lodge za bei rahisi zipo makulu pale karibu na udom utumishi
 
Sidhani kama ni nzuri kujiandaa na interview za utumishi nafikiri ni vyema ukaenda mapema ili hata akili iwe imetulia na lodge za bei rahisi zipo makulu pale karibu na udom utumishi

Aisee, ni kweli mkuu. Asante sana.
 
Ndugu Mwifwa na wengine wote, asanteni sana kwa ule ushauri chanya, wakati mdogo wangu kwenye tangazo la kuitwa kwenye Usaili yupo lakini kwenye mfumo wa Utumishi akaunti yake ilikuwa kimya. Hatimaye ameona mabadiliko, na amepewa Namba pamoja na maelekezo ya venue.


Balaa liko kwenye ujasiri wa kwenda kuwania nafasi moja kati ya Sita miongoni mwa walioitwa 2455.


Japo kuna binti namfahamu, alipita na kupata kazi kwenye zaidi ya watu 1000 waliokuwa wanapigania nafasi 1 ya uhandisi na hana koneksheni wala pesa.
 
Mm nin kak angu huwa nafika ddm ila nalazimik kutafuta guest kwa maana sielewi kwann huwa anipeleki kwake

Sent from my Infinix X650 using JamiiForums mobile app
Wewe lala guest kwa ndugu sio, hata mi dodoma Nina ndugu, mikoa mingi Nina ndugu lakini nikienda nafikia Lodge, tunaonana mitaani kusalimiana narudi Lodge kulala, mambo ya kulala Kwa ndugu utakuja gombanisha mtu na mkewe au mumewe bure
 
Ndugu Mwifwa na wengine wote, asanteni sana kwa ule ushauri chanya, wakati mdogo wangu kwenye tangazo la kuitwa kwenye Usaili yupo lakini kwenye mfumo wa Utumishi akaunti yake ilikuwa kimya. Hatimaye ameona mabadiliko, na amepewa Namba pamoja na maelekezo ya venue.


Balaa liko kwenye ujasiri wa kwenda kuwania nafasi moja kati ya Sita miongoni mwa walioitwa 2455.


Japo kuna binti namfahamu, alipita na kupata kazi kwenye zaidi ya watu 1000 waliokuwa wanapigania nafasi 1 ya uhandisi na hana koneksheni wala pesa.
Ahsante sana mkuu kwa mrejesho, mtie moyo asiogope hawezi kujua lolote laweza kutokea.

Nasikia wanaofika oral wana probability kubwa ya kupata nafasi hata kama hawatapata hiyo nafasi wanayoipambania maana huwa wanawekwa kwenye kanzidata na nafasi zikipatikana wanapangiwa.

Placement ya tarehe 19/7/2022 wote walifaulu oral ila hawakuapata nafasi kwa kipindi hicho na zilipopatikana wakapangiwa vituo.

Kuna jamaa namfahamu kwenye hiyo placement alifanya oral ya NHC ila hakupata nafasi ndipo akaja kupangiwa RUWASA.

Kwa hiyo nguvu iliyopo kwa dogo aielekeze kwenye kujitahidi angalau afike Oral.
 
Back
Top Bottom