Vijana wenzangu tusiogope kuoa, ndoa tamu

Vijana wenzangu tusiogope kuoa, ndoa tamu

Wakuu Ndoa ni tamu ndiyo ndoa ni tamu kwan kuna mtu anabisha kwenye hilo

Emu fikiria unaamshwa asubuhi upate cha asubuhi baada ya hapo unasindikizwa bafuni kuoga. Muda huo nguo zinapigwa pasi ukimaliza mke anakusaidia kujiandaa ukimaliza unakunywa chai yako safi. Dah baada ya hapo anakuaga kwa maneno matam na yenye kukutia moyo unapoenda kutafuta riziki.

Kila baada ya masaa 2 lazima haakikishe hali yako huko, ukirudi unapokelewa vizuri na maneno ya pole na ahsante. Jaman hayo ni baadhi ya mazuri ya ndoa nawashangaa mnaogopa kuoa. Mwanamke anakupa ushauri mzuri naukiufuata lazima tu ufanikiwe. Mke ndo anakuwa wa kwanza kuufariji pale unapokuwa na stress hakika tabasamu lake tu ni tiba ya mambo mengi kwangu

Vijana wenzangu tusiogope kuoa tafuta yule unaempenda na yeye anakupenda hakika siku zote hitajutia kuoa

Namalizia ndoa tamu mke ni faraja ni chanzo cha mafanikio yako.

Usiogope kuoa
Umpate mwenye akili zake timamu sasa ndiyo utafurahia, ila ndoa ni zaidi ya hayo
 
Sawa mkuu ila nina bro ni Tiss na bado kabambikiwa mtoto unafanya mchezo nn😅😅😅
😂😂Huyo Tiss katika taaluma ila katika kanjanja za maisha ya mahusiano kala buyu.Wanawake tuishi nao kwa akili,hiv viumbe bhana ni vya ajabu ndio maana tuwe makini sana na hakuna kuendekeza hisia hapo lazima upate mke sahihi
 
Ndoa bila maombi mnadumbukia shimoni, maana sio mpango wa shetani maana anaichukia na ni lazima awapaitishe kwenye miba na mtachukiana utazani mlilazimishwa kupendana wakati mlichaguana kwa akili zenu wenyewe
 
😂😂Huyo Tiss katika taaluma ila katika kanjanja za maisha ya mahusiano kala buyu.Wanawake tuishi nao kwa akili,hiv viumbe bhana ni vya ajabu ndio maana tuwe makini sana na hakuna kuendekeza hisia hapo lazima upate mke sahihi
Hahahha mwamba itakuwa kapigwa kitu cha PyongYang maana hajielewi nyumba 3 kamuandikia mwanamke zote yeye analewa K vant tu kwa stress
 
Tatizo hiki kizazi cha [emoji216].Mnaendekeza zinaa na inapelekea kuoa wasio wa kuoa.Katika suala la kuoa inabidi uwe FBI au USALAMA WA TAIFA kumchunguza mwanamke wa kuoa
Tatizo linaanzia hapo, wengi tunabebana hivyo hivyo
 
Back
Top Bottom