Viongozi wangu wa Simba, ondoeni kirusi Chasambi ndani ya timu yetu, msikilizeni akimsifia Max Nzengeli na kudai Simba hakuna role model wake

Chasambi ananifurahisha anavyopambana akiwa ndani ya uwanja ila nikimuangaliaga na kumsikiliza nje ya uwanja kuna kitu hakijawahi kukaa sawa kwangu.

Yeye ni mdogo sana kutoa kauli kama hiyo, msilinganishe na kauli za kila Mayele au Aucho ambazo kwanza hazifanani na kauli yake ila pia tayari walikuwa ni wazoefu na wana mamlaka ya kutoa kauli walizotoa. Pia naamini walizitoa hizo kauli zao msimu ukiwa umeisha siyo katikati ya vita ya ubingwa.

Pia kawadharau wachezaji wenzake wote kwa kusema hakuna mchezaji anayemuinspaya katika timu nzima. Tatu unaenda kumbig up mchezaji wa timu shindani ambaye uko katika mbio naye za ubingwa.

Labda ni ukosefu wa elimu ila inarudi kule kule, ana chembechembe za dharau.

Mwenzake Karabaka kapigwa pini na inawezekana kabisa ni kwa ujinga kama huu.
 
Kumbe angesema role model wake ni Mutale🤣🤣
 
Comrade jitahidi ujifunze somo la fair play kwenye michezo. Hizi mambo za Yanga na Simba zisitugeuze kuwa misukule. Hakuna kosa wala kirusi hapo! Huo ni mtazamo wake. Hivyo unatakiwa uuheshimu.
 
Kumbe angesema role model wake ni Mutale🤣🤣
Anaweza kuwa Mutale kwani shida iko wapi? Mnapenda kukariri majibu na kuyatumia hata katika maswali yasiyohusika. Sasa Mutale ameingiaje hapa?
 
Basi mumchagulie nyinyi huyo role model wake.
 
Comrade jitahidi ujifunze somo la fair play kwenye michezo. Hizi mambo za Yanga na Simba zisitugeuze kuwa misukule. Hakuna kosa wala kirusi hapo! Huo ni mtazamo wake. Hivyo unatakiwa uuheshimu.
Fair play haihusiani na mambo ya nje ya uwanja. Nyie ndiyo mmejifunzia mpira kwenye viwanja vya mduara.
 
Wewe utakuwa utopolo ndiyo mna akili kisoda. Unamzuiaje mtu kutoa maoni yake?
 
Usingeandika tusingejuwa UPUMBAVU wako. Ila Chasambi kasema ukweli, timu ni Mukwala, Mutale, na Mpanzi wenyewe wanajitafuta sasa watakuwaje kioo kwake.
 
Comrade jitahidi ujifunze somo la fair play kwenye michezo. Hizi mambo za Yanga na Simba zisitugeuze kuwa misukule. Hakuna kosa wala kirusi hapo! Huo ni mtazamo wake. Hivyo unatakiwa uuheshimu.
Kama ulisoma hilo somo basi ulifeli.
Fairness kwa wachezaji wenzake,kwa viongozi na mashabiki haikuwepo.
Hata hivyo wanasimba waache kuochukulia kauli hii kwa umakini.Waendelee kujifunza kijana alitaka kupeleka ujumbe gani.

Sent from my Infinix X626 using JamiiForums mobile app
 
Huyu dogo kapuyanga kwa umri wake na uwezo wa kisoka ilitakiwa afahamu siasa za usimba na uyanga. Bado ni kijana mdogo sana kutoa Diss kama ile... kwamba pale simba anakochezaa kuna mchezaji anayemvutia...??? Shida sio kumtaja max... inshu ni kubeza wachezaji wenzake.. ambayo ushiriako wao ndo unamfanya dogo aonekane.... Real atakuwa anajuta sasa hivi.... na ukikosa kuaminiwa na hizi timu mbili ndo unashuka hivyo... alipuyanga big time
 
Nawaomba viongozi wa Simba toeni wachezaji mamluki kama chasambi hachelewi kuiuza Simba kwa utopolo yanga
 
Dogo Ni Yanga ILa Yupo Simba Kw Sbb Amesajiliwa Tu
 
Amechagua kilichokuwa chema. Anastahili pongezi kuliko kutishwa mzigo wa lawama, kisa tu eti amekuwa mkweli.
 
Garnacho anasema role model wake ni Ronaldo muda wapo wote timu ya taifa na Messi.
Hujui kua Garnacho kacheza na Ronaldo pia Man U , sasa huyo Chasambi kacheza na max wapi?

Na kwanini asingetaja tuu max direct bila kuhusisha wachezaji wa simba
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…