Vita kati ya majangili na askari wa hifadhi za wanyama pori

Vita kati ya majangili na askari wa hifadhi za wanyama pori

Yani natamanigi Sana mazali kama haya yakukutana na majangili porini huko tena usiku. Huo mkono nitakaoutembeza maamaeee nitaacha historia na alama ya kudumu. Asante mleta mada Lazima sasa hivi nizame chaka niitendee haki black belt yangu.
Ebooooooooh [emoji849][emoji849][emoji849]
 
Tatizo ma game wengi mnajifanya mna huruma sana kwa wanyama, mkiwa bush mnajiona wenyewe ndo mshakua matarzan na kuusahau ubinadamu.

Hao wanyama mmewafata porini na kujimilikisha kama wenu, na roho mbaya ndio imewatawala sijui nani kawalisha sumu hiyo.

Naongea haya kwakua kuna dogo aliahawah pigwa nusu kufa kwasababu alikutwa na manati akiwa ameshika ndege mmoja aliyemuwinda
[emoji24][emoji24][emoji24][emoji24][emoji24]
 
Nyati msikie tu, bora ukitane na pride ya simba ila sio nyati nakumbuka miaka hiyo nilipokuwa nafanya tafiti katika mbuga ya Serengeti ile wakati wa kufanya darting kuna mzungu mmoja alikoswa koswa kupigwa pembe..
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
 
Hawa watu wa game kukukuta umebanika nyama porini na wao kukubanika Kama ulivyokuwa umebanika nyama hawaoni taabu kabisa!
Duuuuuuuh [emoji24][emoji24][emoji24][emoji24][emoji24]
 
Hakuna mwenye roho mbaya au ukatili … its just usipoua unauliwa !! Watu wana historia mbaya sna na majangili maaskari wanauliwa kila siku wanaacha familia zao yatima na kwenye hali ngumu ! Unapewa tuu pole na paredi la kuagwa bhasii ..
kuna mapori magumu mno kama moyowosi ,lukwati lumesule kule mnakutana na majangili ambao daah !!
Vijana wengi sana wamepoteza maisha hamjui tuu especial hawa ajira mpya …
Mtu unaamka nae mnaingia doria anarudi maiti life la porini weeeee

Selou imetulia sana mbona skuiz watu walikuwa wanangusha tembo like nothing happened !
[emoji24][emoji24][emoji24][emoji24][emoji24]
 
hao asikari uchwara wa wanyama pori wana roho mbaya sana na wana hamu ya kuua binadamu wenzao nakumbuka kuna wengine tulikuwa tunaishi nao nyumba moja walikuwa wakitukata macho mabaya bila sababu ikabidi tuwahamishe
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
 
Bora Ukutane na Majambazi kuliko kukutana na Jangili huyu ameshazoea kuziona damu.

Ni sawa na Bora ukutane na Muuzaji Bucha ya nyama kuliko kukutana na Mtu wa machinjioni ya mifugo hawa nao wana roho ngumu kuna jamaa angu aliwahi kuchomwa kisu mguuni kikatokea chini kwenye sori ya kiatu
Duuuuuh.
 
Usiombee ukutane na mziki wa askari wa wanyama pori,polisi wa uraiani cha mtoto

Ova
 
Humu kuna watu wanasema tu hawajui maisha ya porini ni vita rasmi. tulikamata mzee ana miaka kama sikosei 75+ nikakaa nae chemba kumuuliza maswali akasema yeye maisha yake ni porini hajui lolote maishani mwake ni Jangili mbobezi. Nikatoa ushauri tumuachie tukansindikiza mpaka kijijini kwake.
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23] khaaaaah
 
Vita yao sio ndogo kabisa, ila kwa uchawi jamaa wapo vizuri, ogopa kuna mtembea na fimbo tu na akipotea ni kapotea kweli kweli
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
 
Sio kwa nyati mpweke binadamu anasubjri sana huyo kiumbe ni bora ukutane na kundi lao ila sio nyati mmoja
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23] na wao wanakua na stress? Nimecheka sana lol
 
Kuna mkasa ule wa Mkuu wa Polisi Loliondo marehemu Kong'oa. Alienda mbugani nadhani ilikuwa Ngorongoro wakafanikiwa kukamata Majangili kumbe kuna wengine wamejificha kuna mmoja alikohoa jangili akainama mzee alifumuliwa gobore la kifuani. Ikabidi JWTZ waingie msituni. Jangili yeye anachojua ni kuwa kaingia vitani maisha yake kayakabidhi Wanyama na askari pori.
Duuuuuh [emoji24][emoji24][emoji24][emoji24][emoji24]
 
Mkuu hapa napata shaka na hii hadithi yako....milima Udzungwa askari wanafanya doria ya miguu tu na jangili hawezi kuingia na pikipiki kule mlimani kutokana na landscape ya milima ile....hasa kijiji cha Mng'ula ulipotaja, maeneo haya mto ambao mtu anaweza zama na kufa maji unapita barabarani kabisa kwa maana hiyo kama kweli walifanyiwa hivi niwazi watu wangeona...kwa hivyo si kweli kabisa hii hadithi
Unazijua zile pikipiki Sanlog sijui hizi ambazo town zinatumika kubebea mkaa? Achana na TVS na Boxer. Hizo Sanlg ni gari inapanda popote ile pikipiki tumezikamata sana porini jangili anakimbia anakuachia haina hata side mirror.
 
Ukikutwa na nyama ya swala ni uhujumu uchumi jela miaka mingi kweli??. Yaani Afrika, Arusha nyama ya swala ni kosa. Ndio maana hayati John Pombe aliwaita mabeberu, yaani sheria zao ziwe mpaka huku.
Had Songea pia, nyama ya swala, mbalapi, ngiri, ngorombo, nguruwe pori, ukikutwa miaka 30 jela.
 
Wale wanadai walikuwa Wasomali jeshi liliingilia kati walitembezewa kibano sana. Majangili hatari usije kuombea kukutana nayo ni hawa Wasomali na Warundi na Wanyarwanda ndugu wale ni vita. Kuna pori la katavi na kuna sehemu ya pori la Inyonga kwenye Mpung'o jangili anakatiza. Wameteka sana mabasi. Kuna wakati serikali walikuwa wanalia na wizi wa nyaya za simu zote zilikuwa zinaishia porini mikononi mwa jangili. Niliamua kuachana na maisha ya msituni yana raha na kero ni kubwa. Kuna siku tulikuta tent la Watalii mzee Tembo kalichakaza vibaya kumbe ndani walibeba Maepo.
[emoji24][emoji24][emoji24][emoji24][emoji24][emoji24][emoji24]
 
Abeid Mziba hafai hafai kabisa. Sijui zile hasira na chuki zinatoka wapi? Simba mwenyewe hawezi kumfuta Mbogo akiwa pekee yake. Dude lina hasira hili. Hata wawe 1000 anaweza kuchomoka mmoja tu analianzisha zogo. Kuna simba alilitaka kuua Nyati akadandia mgongoni kilichompata. Nyati alipita kwenye chaka lenye mimba yule Simba alitoboka macho, tulimkuta yupo hoi bin taabani. Mbogo akiwa na hasira anatoa machozi na analia yule na mikamasi kama yote. Mungu kamnyima tu meno ya kuua na kucha. Hii dunia tungekoma. Siku nikitulia nitaleta mkasa wa shekhe mmoja alitaka kumchinja Nyati mara baada ya kupigwa risasi tukamwambia usiende kufa kwa hilo dude lazima atoe haja kubwa akasema oooh sisi waislamu hatuli kibudu[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23] mungu amlaze mahala pema. Nyati ipo na akili mingi tena ukimjeruhi ooooh utajuta.
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23] ila nyie watu jaman lol
 
Back
Top Bottom