Wabunge wa Viti Maalum (CHADEMA) na kisa cha asiyefanya kazi na asile

Wabunge wa Viti Maalum (CHADEMA) na kisa cha asiyefanya kazi na asile

Mmeanza kutetemeka kama kawaida yenu na maneno mengi, mkutano wa leo na waandishi wa habari ndio utatoa majibu ya maswali yote.
 
Mbowe is a political genius.. Chadema hakitakaa kije kufa kisiasa hasa hasa kama chama kikuu cha kuaminiwa cha upinzani..

Mbowe hatoongea, atasubiri upepo upite then anapiga spin moja tu ya uhakika na mioyo yote ya waliojifanya kutoka au kutokuwa na imani na CDM itarejea..

Mmeambiwa muandamane mmejificha mitandaoni hamuonekani barabarani, mliwapuuzia na sasa eti mnakasirika wameenda bungeni mnataka wasiwapuuzie kama ninyi mlivyowapuuzia??
 
Mkutano wa leo wa nini? Nielimishe zaidi!
Chadema wamesema watafanya press na wanahabari leo saa tano asubuhi.

Nachomaanisha zaidi, maamuzi yatakayotolewa kwenye press ya leo ndio yatakayotoa majibu ya kweli ya kinachoendelea, na sio hizi hisia zako ulizoandika hapa.
 
Mbowe is a political genius.. Chadema hakitakaa kije kufa kisiasa hasa hasa kama chama kikuu cha kuaminiwa cha upinzani..

Mbowe hatoongea, atasubiri upepo upite then anapiga spin moja tu ya uhakika na mioyo yote ya waliojifanya kutoka au kutokuwa na imani na CDM itarejea..

Mmeambiwa muandamane mmejificha mitandaoni hamuonekani barabarani, mliwapuuzia na sasa eti mnakasirika wameenda bungeni mnataka wasiwapuuzie kama ninyi mlivyowapuuzia??
Umeandika vitu vya kufikirisha.

Kama Chadema waliamua kufanya hivyo (kujiongeza baada ya maandamano kutofanyika) na kuwapeleka hao wanawake bungeni basi wangekuja na kauli moja, lakini sio Mnyika aseme lake, na wale wanawake nao waseme lao.

Mbowe kuzungumza au kutozungumza leo haitakuwa na maana yoyote provided Katibu Mkuu ataongea, na ambacho atakisema katibu Mkuu ndicho kitachukuliwa kama msimamo wa chama ambacho Mbowe ndie mwenyekiti, hapa sioni tatizo.
 

Maridhiano maana yake ni talks (mazungumzo) yanazozaa muafaka wenye manufaa kwa Taifa na wadau na society nzima, kuanzia civil organisations zao, vyaa vyama vya siasa, juuia za kidini n. k na miongoni mwa vitu vya kujadiliana katika hayo maridhiano ni kwa mfano

1. Uwepo wa tume huru ya uchaguzi
2. Katiba mpya
3. Kufungulia wafungwa wa kisiasa
4. Kuheshimu haki za vyama kufanya siasa kwa mujibu wa sheria

Haimaanishi kugawana vyeo au nyadhifa na kisha mambo yaendelee vilevile business as usual!

Muelewe Lissu, ile ni akili kubwa
Hakuna akili kubwa pale, yule ni msaliti tu! Kaisaliti taifa, sasa hivi amesaliti na chadema. Ndo maana baada ya uchaguzi amekimbilia nje, hebu jiulize kama ana dhamira ya dhati na anamaanisha anachoongea kwa nini asiwe na wenzake hapa hapa tz? Shujaa na Jasiri wa kweli mnakuwa pamoja wakati wote, iwe shida, iwe raha nk. Yaani yeye amekimbilia ulaya halafu anawapangia ufipa nini cha kufanya? Hivi mtaelimika lini?
 
Kama huzijui siasa za ndani ya CHADEMA unaweza kudhani kuna suala la kisiasa ambalo Halima Mdee anaweza kulifanya bila ridhaa ya Mwenyekiti wa CHADEMA Taifa, Freeman Mbowe! Haiwezekani.

Halima Mdee ni mmoja wa watu ndani ya CHADEMA ambao ni sehemu ya Freeman Mbowe. Mwingine ni Godbless Lema na genge lake!

Kwa maana nyingine, ukimgusa kisiasa Halima Mdee unakuwa umemgusa kisiasa Mbowe! Yote anayofanya kisiasa Halima Mdee yanakuwa ni mkono wa Mbowe!

Kitu ambacho nampa hongera Mbowe ni uwezo wake wa kutumia ''wakala'' katika kutimiza malengo yake ya kisiasa. kwa wasiojua wanaweza kudhani wanapambana na ''mtu fulani'' ndani ya CHADEMA bila kujua kama wanapambana na Freeman Mbowe kwa kupitia ''wakala''.

Mbowe ndani ya madaraka anatumia nadharia inayosema, '' Always say less than necessary'' kama inavyobainishwa katika sheria ya 4 ndani ya kitabu kinachoitwa The 48 Laws of Power kilichoandikwa na Mmarekani, Robert Greene.

Kuna msema pia usemao, ''Ukiona kifaranga kipo juu ya chungu ujue chini kuna mama yake''. Hii ina maana kuwa, ukimuona Halima Mdee anatamba juu kisiasa ujue Freeman Mbowe yuko chini yake!

Muda ni mwalimu mzuri anayetoa mafunzo ya ukweli kwa wale wazito kujua au kung'amua ukweli wa mambo!
Uko sahihi kabisa.
 
Wale watu wana baraka za chama. Fedha imeshinda kwa mara nyingine tena (mishahara then michango na ruzuku kwa chama)

Wekeni tu akiba ya maneno maana wakiongea wao mtakuja kupiga U turn
 
Kama huzijui siasa za ndani ya CHADEMA unaweza kudhani kuna suala la kisiasa ambalo Halima Mdee anaweza kulifanya bila ridhaa ya Mwenyekiti wa CHADEMA Taifa, Freeman Mbowe! Haiwezekani.

Halima Mdee ni mmoja wa watu ndani ya CHADEMA ambao ni sehemu ya Freeman Mbowe. Mwingine ni Godbless Lema na genge lake!

Kwa maana nyingine, ukimgusa kisiasa Halima Mdee unakuwa umemgusa kisiasa Mbowe! Yote anayofanya kisiasa Halima Mdee yanakuwa ni mkono wa Mbowe!

Kitu ambacho nampa hongera Mbowe ni uwezo wake wa kutumia ''wakala'' katika kutimiza malengo yake ya kisiasa. kwa wasiojua wanaweza kudhani wanapambana na ''mtu fulani'' ndani ya CHADEMA bila kujua kama wanapambana na Freeman Mbowe kwa kupitia ''wakala''.

Mbowe ndani ya madaraka anatumia nadharia inayosema, '' Always say less than necessary'' kama inavyobainishwa katika sheria ya 4 ndani ya kitabu kinachoitwa The 48 Laws of Power kilichoandikwa na Mmarekani, Robert Greene.

Kuna msema pia usemao, ''Ukiona kifaranga kipo juu ya chungu ujue chini kuna mama yake''. Hii ina maana kuwa, ukimuona Halima Mdee anatamba juu kisiasa ujue Freeman Mbowe yuko chini yake!

Muda ni mwalimu mzuri anayetoa mafunzo ya ukweli kwa wale wazito kujua au kung'amua ukweli wa mambo!
Nimepitia mabandiko yote kuhusu hili sakata lakini hili la Msemakweli lina ukweli.Hapa Mbowe kacheza mchezo wa kuwazunguka viongozi wote wa juu,na mimi naongezea ,kwa maslahi yake mwenyewe.Ameona asipoteze vyote.
 
Hakuna aliye juu ya Chama!

Hii ni kauli ambayo CHADEMA imekuwa ikiitoa mara nyingi sana pindi panapotokea mtanzuko ndani ya chama unaohusisha nidhamu, taratibu na maslahi ya chama.

CHADEMA ilitoa kauli hiyo alipofukuzwa Zitto, Kitila, Mwigamba akina Silinde na hata walipohama watu wazito waliofanya kazi kubwa ya kuijenga CHADEMA enzi za uchanga wake.

Miongoni mwa vitu vilivyowavutia wananchi kuhusu CHADEMA ni uwezo wa kusimamia nidhamu za wanachama wake hata viongozi, kuibua na kukemea ufisadi kwa hoja nzito n. k

Ndugu Mbowe, majuzi uongozi wa CHADEMA ulitoa kauli kwenye press conference kuhusu kinachoitwa "uchaguzi" uliofanyika majuzi. Uongozi ulikataa katakata kutambua matokeo ya uchafuzi huo, kwa sababu kwa vigezo vyote ule siyo uchaguzi, ni uchafuzi wa kutisha, ni udhalimu usio na haya, kiufupi ni matusi ya nguoni kwa wananchi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania!. Ni aibu!
Kwenye press hiyo, Mwenyekiti ulitamka wazi kuwa hamuutambui uchafuzi huo na Mkaenda mbele zaidi na kuonyesha baadhi ya karatasi za kura feki mlizofanikiwa kuzipata.

Sasa ndugu Mwenyekiti wananchi tunangoja Chama kichukue hatua, na hii hatua siyo ya kumuangalia nyani usoni lazima watu wawajibishwe!

Haiwezekani kuna watu wamesacrifice kwa ajili ya nchi halafu baadhi yao wananyatia kama fisi ili kudaka mfupa wa juhudi za watu waliogenuine kwa sababu ya ubinafsi uliokithiri!
Mwenyekiti Chama kichague moja, kiwe na double standard kwenye kushughulikia nidhamu za wanachama waliokiuka miongozo ya chama ili kiendelee kuheshimika na kuaminiwa na umma au kizuge, kitupige changanya la macho kwa kuendelea kuwakumbatia hawa wasaliti wakubwa wa wananchi!

Ndugu Mwenyekiti, CHADEMA itaaminika vipi kama hadharani wanatoa kauli X kumbe ikiwa sirini huenda ina misimamo Y?

Ndugu Mwenyekiti nakuomba sana, fukuza huyo Mwenyekiti wa baraza la Wanawake nchini Halima Mdee, mtu aliyepewa dhamana kubwa na wanawake lakini ameshindwa kulinda imani hii ya mamilioni ya wanawake Tanzania nzima!. Ameshindwa kuweka mbele maslahi ya vizazi na vizazi vyao kwa kukataa kutoungana na madhalimu na badala yake ameamua kuwapa legitimacy ya kisiasa kwa kuungana nao katika vikao vya dhulma dhidi ya demokrasia pana tunayoitafuta

Ndugu Mbowe, hii tuliyokuwa nayo ni turning moment kwenye historia ya chama , Mna option ya kuungwa mkono mara dufu kwa kuonyesha zero tolerance dhidi ya usaliti na kutoheshimu vikao vya chama, au muanze safari ya kuserereka kuelekea kupoteza imani kabisa kwa wananchi.

Na Magufuli anajua, njia pekee ya kuiangusha CHADEMA ni divide and rule kwamba walambishe pipi hawa kisha kaa pembeni uwasikilizie na wale waliobaki wanasemaje!

Pia Magufuli anatafuta legitimacy ndani ya nchi na nje ya nchi kwa udi na uvumba, The only way ya kujitoa kikaangoni ni kudiscredit madai yetu ya uchaguzi feki na ukiukwaji mkubwa wa haki za binadamu. Na njia mojawapo ya kufanikisha hilo mosi ni kupunguza sauti za kuzidai kupitia njia hiyo ya "kurusha fupa", wale watakaokamatia fupa watang'ang'ana na fupa huku wakimuacha aende zake. Pili anawademoralize wale ambao hawatakubaliana na mambo yake kuendelea kudai uchaguzi ulikuwa feki. Tatu anatuma message kwa wahisani na wanaoinyooshea kidole Tanzania kuhusu haki za binadamu kuwa tazama, mbona kwetu mambo shwari, mnaowatetea mbona wamekubali, nyie mna tatizo gani?

Sasa ndugu Mbowe, nakuomba, kama uko real, na kama uongozi wa CHADEMA hauko nyuma ya huu ujinga, Fukuza uanachama wanawake wote hao 19 ili kutunza imani ya wananchi na wanachadema wote.

Najua, Umetoka mbali na akina Halima, mnaweza kuwa ni marafiki wakubwa, lakini maslahi mapana ya nchi na CHADEMA hayawezi kulindwa na kitendo walichokifanya.

Muweke pembeni kwa ajili ya kulinda principle na urafiki wenu uendelee nje ya shughuli za chama. Ukikosea principle this time, hiyo principle itakuja kwa namna nyingine ikuvunje!

Kama wameenda kwa baraka za uongozi wa CHADEMA tunaomba uongozi mzina na uliojihusisha na ujinga huo ujiuzulu mara moja.

Ila kama wamekiuka masharti ya vikao vya chama kwa kula njama kuhujumu maamuzi ya chama kwa ajili ya maslahi yao binafsi, basi fukuza uanachama wote hao, chama kitaendelea kusonga mbele na wao wataendelea kubaki na ubunge wao wanaoupenda sana kuliko future ya nchi, na maisha yataendelea!

Ndugu Mwenyekiti, usaliti lazima uendane na gharama kubwa, mkiuacha usaliti huu basi hiyo ni precedence itakayokuwa ikitekelezwa na wajao ambao katika juncture muhimu ya struggle za chama watanunuliwa na kufanya usaliti wao wakijua hakuna consequence yoyote ya usaliti.

Mwenyekiti, Katibu na kamati kuu ya CHADEMA, the ball is in your court, mkifunika kombe, basi mtageuka nyie wanaharamu. Washughulikieni hawa wasaliti ili chama kizidi kupata heshima na kiwe imara zaidi!
Lissu anasemaje?
 
Mbowe is a political genius.. Chadema hakitakaa kije kufa kisiasa hasa hasa kama chama kikuu cha kuaminiwa cha upinzani..

Mbowe hatoongea, atasubiri upepo upite then anapiga spin moja tu ya uhakika na mioyo yote ya waliojifanya kutoka au kutokuwa na imani na CDM itarejea..

Mmeambiwa muandamane mmejificha mitandaoni hamuonekani barabarani, mliwapuuzia na sasa eti mnakasirika wameenda bungeni mnataka wasiwapuuzie kama ninyi mlivyowapuuzia??
Mbowe anawajua vizuri hawa wanaopiga kelele kwenye mitandao ya kijamii kama ni ''debe tupu...''

Nakwambia hawa hawa baada ya kauli ya Mbowe utawasikia wakisema, ''tumeamua kwenda bungeni kwa sababu hatuwezi kumwachia fisi bucha''.

Hawa ''makamanda'' hawana msimamo bali wana makelele tu mengi yasiyoeleweka!
 
Chadema wamesema watafanya press na wanahabari leo saa tano asubuhi.

Nachomaanisha zaidi, maamuzi yatakayotolewa kwenye press ya leo ndio yatakayotoa majibu ya kweli ya kinachoendelea, na sio hizi hisia zako ulizoandika hapa.
Nimekuelewa! Asante.
 
Mbowe anawajua vizuri hawa wanaopiga kelele kwenye mitandao ya kijamii kama ni ''debe tupu...''

Nakwambia hawa hawa baada ya kauli ya Mbowe utawasikia wakisema, ''tumeamua kwenda bungeni kwa sababu hatuwezi kumwambia fisi bucha''.

Hawa ''makamanda'' hawana msimamo bali wana makelele tu mengi yasiyoeleweka!
Bado unaendeleza hisia.

Kama ni kumuachia "fisi butcher" lazima ufuate maamuzi ya chama chako, sio kupingana na maamuzi ya viongozi wako halafu useme hutaki kumuachia "fisi butcher"

Hiyo defence kwangu haina maana, kuna viashiria vingi vinavyoonesha hao wanawake wamelaghaiwa na CCM, hasa nikikumbuka yule alietolewa jela juzi Singida, DPP akamuachia kwa nolle, then akapandishwa gari haraka kuwahi Dodoma akaapishwe.
 
Back
Top Bottom