Wafanyakazi 3 wa Uhamiaji wasimamishwa kazi kwa kosa la kutumia nguvu dhidi ya Alex Raphael

Wafanyakazi 3 wa Uhamiaji wasimamishwa kazi kwa kosa la kutumia nguvu dhidi ya Alex Raphael

WIZARA ya Mambo ya Ndani ya Nchi Idara ya Uhamiaji, imewasimamisha kazi wafanyakazi watatu kutokana na tukio la Askari wa Uhamiaji kutumia nguvu dhidi ya Alex Raphael Kyai kama video fupi iliyosambaa katika mitandao ya kijamii.

Akizungumza na wandishi wa habari leo Mei 30, 2021 Kamishina Jenerali wa Uhamiaji, Dk Anna Makakala, amesema mnamo Mei 27 mwaka 2021, Idara ya Uhamiaji ilimkamata mtuhumiwa wa utapeli anayefahamika kwa jina Alex Raphael Kyai katika Ofisi ya Uhamiaji Kurasini mkoani Dar es salaam ambaye aliongozana na mteja wa huduma za pasipoti, aliyemtambulisha kama mkewe.

Aidha Dk. Makakala amesema baada ya mahojiano, ilibainika kuwa mtuhumiwa huyo amekuwa na tabia ya kuwalaghai na kupokea fedha kutoka kwa wateja mbalimbali ili waweze kupata pasipoti kwa haraka, pia mtuhumiwa huyo amekuwa akijitambulisha kama Mtumishi wa Taasisi nyeti ikiwemo Taasisi ya Kuzuia na kupambana na Rushwa (TAKUKURU).

"Idara ya Uhamiaji inakiri kutokea kwa tukio hilo na pia inalaani kitendo kilichofanywa na askari wa Uhamiaji kwa kutumia nguvu kinyume cha sheria na maadili ya kazi zao, hata hivyo Idara ya Uhamiaji tayari imechukua hatua za kinidhamu dhidi ya askari hao" amesema Dk. Makakala.

Sambamba na hayo, Idara ya uhamiaji inatoa wito kwa Wananchi wote wanaohitaji huduma za kiuhamiaji kufika wenyewe katika ofisi za Uhamiaji, pia Uhamiaji wanawahakikishia kwamba idara itaendelea kutoa huduma zake kwa weledi, uwazi na bila kutumia mtu wa kati ( Vishoka).

Aidha Idara ya uhamiaji imetoa onyo kwa yeyote ambaye atajaribu kujifanya kuwa Afisa wa Uhamiaji au Afisa wa Serikali ili kumsaidia mtu mwingine kwa maslahi yake binafsi hatua kali dhidi yake zitachukuliwa kwa mujibu wa Sheria, Pia idara hiyo imewataka Watanzania wote kutoa ushirikiano katika kutoa taarifa za watu wanaofanya vitendo vya aina hiyo.

Pia soma; Maafisa uhamiaji Walivyomtesa mtuhumiwa, Je, Sheria inawaruhusu?

Kwenye maelezo ktk barua haikuonyesha popote kuwa maafisa wamesimamishwa kazi zaidi ya kuwa wamechukuliwa hatua za kinidhamu.
 
Mara nyingi Wanajeshi hutoa adhabu kali kwa mwarifu pasipo kumpiga
Unamaanisha nini sasa! What’s the difference? Kuna adhabu nyingine ni mbaya maradufu kuliko kupiga.
Mfano, hao askari wa uhamiaji kuna kuna kipindi walimlaza jamaa chali wakamwagia maji usoni. Hiyo inakuzuia kupumua..Mateso hayo yanaitwa Water boarding. Na yameharamishwa hata kimataifa.
 
Hizo adhabu wawe wanapeana jeshini, huyo jamaa wangeishia kumuua. Hakuna namna ya kumshtaki huyo mtu au kumwekea sanctions...
 
Mbona wanajeshi nao wanawasulubu watu but viongozi wao huwezi ona wako kinyume nao.Rejea chadema kupigwa segerea,kichapo wakatizao bahati mbaya maeneo ya jeshi, vijana wavaao nguo za jeshi la nje mfano kofia,nk
 
Idara ya uhamiaji imewasimamisha kazi Askari wake watatu kwa tuhuma za kutumia nguvu kinyume cha sheria na maadili ya kazi zao dhidi ya Mtuhumiwa wa utapeli Alex Raphael Kyai kama ilivyoonekana katika video fupi iliyosambaa.

Mtuhumiwa huyo anadaiwa kulaghai na kupokea fedha kutoka kwa Wateja mbalimbali ili waweze kupata pasipoti kwa haraka pia amekuwa akijitambulisha kama Mtumishi wa Taasisi nyeti ikiwemo TAKUKURU.

"Hatua ambazo Idara imechukua dhidi ya Askari, tumewasimamisha kazi kupisha uchunguzi wa tukio lenyewe lakini pia Mtuhumiwa tumemfikisha kwenye mamlaka husika ili aweze kuendelea na utaratibu mwingine kisheria" ——— Dr. Anna Peter Makakala, Kamishina Jenerali wa Uhamiaji
Wataje majina ili na wao watu wao wa karibu wajue
 
Sawa,ila hao vishoka wamezidi
Acha wapate fundisho

Ova
Kweli kabisa . Hatahivyo, ni vyema wakapata fundisho kali kwa utaratibu sahihi. Askari wakiachwa wakaamini wanawajibu wa kutoa mafundisho kitu ambacho si kazi yao, siku watakupa tuhuma ya uongo na mafundisho juu..
 
Kila nikifikiri naona hii serikali na sheria zetu nizakiboya sana..
Inawezekana vipi mtu tapeli yaani mnyanganyi wa kiakili au mnyonyaji wa riziki za watu kuhenyeswa kidogo tena sana na hata damu hazijatoka afisa aliyehenyea ajira asimamiswe kazi kiyaiyai kama hivyo...is not fair!!!!

Sent from my SM-A205F using JamiiForums mobile app
 
Sema hao Uhamiaji wameshindwa kutumia fursa pesa imejileta yenyewe hioveti unaipiga tifu upate sifa badala ya kuikamata na kuipa kesi bila milioni 3 Hakuna kufuta kesi.Sema hapo hakuwepo mchaga tu asingeachia hio takukuru feki bila pesa.Wenzetu police wanajua kuzitumia fursa hizi kachezee police watakupa chumba bure kutoka ni lzm ulipie.
 
Mtuhumiwa bonge ,mle hakosi pressure angewafia je...

Sent from my Infinix X657 using JamiiForums mobile app
Yale yale ya yule Dereva aliyevutwa kwenye Gari akaaga dunia wakaishi kumsukumia lawama Marehemu.

Hivi hata kuheshimiana utu tunahitaji Mwalimu atoke taifa jingine aje kutufundisha?.

Ni aibu kubwa maana hili sasa litaonekana popote Duniani na tutaonekana taifa lenye Watu wasiohesimiana.
 
Lengo lilikuwa jema lakini wakatumia approach ovyo kabisa. Hauwezi tumia adhabu za kijeshi kwa raia. Raia wana sheria zimetungwa kwa ajili yao na si vinginevyo. Sasa yamewageuka.....wamelikoroga lazima walinywe.
 
WIZARA ya Mambo ya Ndani ya Nchi Idara ya Uhamiaji, imewasimamisha kazi wafanyakazi watatu kutokana na tukio la Askari wa Uhamiaji kutumia nguvu dhidi ya Alex Raphael Kyai kama video fupi iliyosambaa katika mitandao ya kijamii.

Akizungumza na wandishi wa habari leo Mei 30, 2021 Kamishina Jenerali wa Uhamiaji, Dk Anna Makakala, amesema mnamo Mei 27 mwaka 2021, Idara ya Uhamiaji ilimkamata mtuhumiwa wa utapeli anayefahamika kwa jina Alex Raphael Kyai katika Ofisi ya Uhamiaji Kurasini mkoani Dar es salaam ambaye aliongozana na mteja wa huduma za pasipoti, aliyemtambulisha kama mkewe.

Aidha Dk. Makakala amesema baada ya mahojiano, ilibainika kuwa mtuhumiwa huyo amekuwa na tabia ya kuwalaghai na kupokea fedha kutoka kwa wateja mbalimbali ili waweze kupata pasipoti kwa haraka, pia mtuhumiwa huyo amekuwa akijitambulisha kama Mtumishi wa Taasisi nyeti ikiwemo Taasisi ya Kuzuia na kupambana na Rushwa (TAKUKURU).

"Idara ya Uhamiaji inakiri kutokea kwa tukio hilo na pia inalaani kitendo kilichofanywa na askari wa Uhamiaji kwa kutumia nguvu kinyume cha sheria na maadili ya kazi zao, hata hivyo Idara ya Uhamiaji tayari imechukua hatua za kinidhamu dhidi ya askari hao" amesema Dk. Makakala.

Sambamba na hayo, Idara ya uhamiaji inatoa wito kwa Wananchi wote wanaohitaji huduma za kiuhamiaji kufika wenyewe katika ofisi za Uhamiaji, pia Uhamiaji wanawahakikishia kwamba idara itaendelea kutoa huduma zake kwa weledi, uwazi na bila kutumia mtu wa kati ( Vishoka).

Aidha Idara ya uhamiaji imetoa onyo kwa yeyote ambaye atajaribu kujifanya kuwa Afisa wa Uhamiaji au Afisa wa Serikali ili kumsaidia mtu mwingine kwa maslahi yake binafsi hatua kali dhidi yake zitachukuliwa kwa mujibu wa Sheria, Pia idara hiyo imewataka Watanzania wote kutoa ushirikiano katika kutoa taarifa za watu wanaofanya vitendo vya aina hiyo.

Pia soma; Maafisa uhamiaji Walivyomtesa mtuhumiwa, Je, Sheria inawaruhusu?

Ni jambo jema sana maana kujichukulia sheria mkononi kuna madhara mengi kwa raia na ni precedent mbaya kwa watu kama watendaji wa serikali wanaopaswa kutenda jambo lolote 'with the authority of the law'. Kinyume na hapo ni kutenda 'arbitrarily' na watu hawatanyamaza kupaza sauti zao na mara nyingi kwa msaada wa mitandao ya kijamii mambo yaliyokuwa yakimalizwa kimyakimya leo hii ukiyafanya tu yanaonekana hadharani. Jidanganye kutumia ubabe kutumia madaraka au ofisi yako vibaya, utaonekana na utakuwa na kesi ya kujibu. Kuna njemba mmoja nilichangia jana kuhusu jambo hili, nikisema kujichukulia sheria mkononi siyo ustaarabu kabisa maana serikali imeweka utaratibu kwa mtu yeyote anayedhaniwa au anayeonekana kuwa mhalifu na inabidi ufuatwe, lakini huyo njemba akaniita 'idiot'. Sasa nadhani atajua nani kati yangu na yeye ni 'idiot in practice'.
 
WIZARA ya Mambo ya Ndani ya Nchi Idara ya Uhamiaji, imewasimamisha kazi wafanyakazi watatu kutokana na tukio la Askari wa Uhamiaji kutumia nguvu dhidi ya Alex Raphael Kyai kama video fupi iliyosambaa katika mitandao ya kijamii.

Akizungumza na wandishi wa habari leo Mei 30, 2021 Kamishina Jenerali wa Uhamiaji, Dk Anna Makakala, amesema mnamo Mei 27 mwaka 2021, Idara ya Uhamiaji ilimkamata mtuhumiwa wa utapeli anayefahamika kwa jina Alex Raphael Kyai katika Ofisi ya Uhamiaji Kurasini mkoani Dar es salaam ambaye aliongozana na mteja wa huduma za pasipoti, aliyemtambulisha kama mkewe.

Aidha Dk. Makakala amesema baada ya mahojiano, ilibainika kuwa mtuhumiwa huyo amekuwa na tabia ya kuwalaghai na kupokea fedha kutoka kwa wateja mbalimbali ili waweze kupata pasipoti kwa haraka, pia mtuhumiwa huyo amekuwa akijitambulisha kama Mtumishi wa Taasisi nyeti ikiwemo Taasisi ya Kuzuia na kupambana na Rushwa (TAKUKURU).

"Idara ya Uhamiaji inakiri kutokea kwa tukio hilo na pia inalaani kitendo kilichofanywa na askari wa Uhamiaji kwa kutumia nguvu kinyume cha sheria na maadili ya kazi zao, hata hivyo Idara ya Uhamiaji tayari imechukua hatua za kinidhamu dhidi ya askari hao" amesema Dk. Makakala.

Sambamba na hayo, Idara ya uhamiaji inatoa wito kwa Wananchi wote wanaohitaji huduma za kiuhamiaji kufika wenyewe katika ofisi za Uhamiaji, pia Uhamiaji wanawahakikishia kwamba idara itaendelea kutoa huduma zake kwa weledi, uwazi na bila kutumia mtu wa kati ( Vishoka).

Aidha Idara ya uhamiaji imetoa onyo kwa yeyote ambaye atajaribu kujifanya kuwa Afisa wa Uhamiaji au Afisa wa Serikali ili kumsaidia mtu mwingine kwa maslahi yake binafsi hatua kali dhidi yake zitachukuliwa kwa mujibu wa Sheria, Pia idara hiyo imewataka Watanzania wote kutoa ushirikiano katika kutoa taarifa za watu wanaofanya vitendo vya aina hiyo.

Pia soma; Maafisa uhamiaji Walivyomtesa mtuhumiwa, Je, Sheria inawaruhusu?

Hiyo taarifa ya uhamiaji haisemi kuwa wamewasimamisha au mimi sijui kusoma kiswahili?
 
Huyo Tapeli hajafanya Jambo jema Ila nao maofisa wetu wa vyombo vya dola wajifunze kutumia reasonable force ku handle mtuhumiwa.

Ukimkamata mtuhumiwa inakua vyema ukamfikisha kituo Cha polisi na sio kumdhalilisha kwa namna yeyote.

Jambo hili limejengeka Kwa muda mrefu sana katika jamii yetu kuwaadhibu watuhumiwa kabla ya kuwafikisha kwenye vyombo vya sheria.

Tatizo linaweza kuwa limetokana na mifumo labda kutotoa matokeo ambayo baadhi yetu tunadhani ndio sahihi,

Ila jamii inapaswa kuelemishwa kwamba ukiachana na matokeo ya huko ambako utampeleka mtuhumiwa unapaswa kumfikisha Kwanza polisi.
Aliyewarekodi wakiwa wanatoa Etra drill ndio amewaonza.
Jwtz ndio jeshi lenye nidhamu aende akatapeli huko. Hakuna clip itaruka lkn atasomba maji kujaza pipa kutumia ndevu[emoji23]
 
Lengo lilikuwa jema lakini wakatumia approach ovyo kabisa. Hauwezi tumia adhabu za kijeshi kwa raia. Raia wana sheria zimetungwa kwa ajili yao na si vinginevyo. Sasa yamewageuka.....wamelikoroga lazima walinywe.
Taarifa mbona haisemi wamesimamishwa?
 
Kila nikifikiri naona hii serikali na sheria zetu nizakiboya sana..
Inawezekana vipi mtu tapeli yaani mnyanganyi wa kiakili au mnyonyaji wa riziki za watu kuhenyeswa kidogo tena sana na hata damu hazijatoka afisa aliyehenyea ajira asimamiswe kazi kiyaiyai kama hivyo...is not fair!!!!

Sent from my SM-A205F using JamiiForums mobile app
Askari mnateteana kwa mambo ya kikatili...sasa mahakama zipo za kazi gani?.

Hata aliyeua huna haki ya kumuhukumu kabla ya kumfikisha Mahakamani.

Na kama hizo ndio adhabu mnazotamani kuwapa Wengine basi mfanye utaratibu ziwe sehemu ya sheria za nchi ili Mahakama ikishahukumu muanze kuwadhalilisha Watu.
 
Yale yalikuwa mazoezi Wala sio adhabu nadhani Kuna shida pahali.

Kuna zile njemba za .... KJ au hata Hawa wa PT kule mziki wake n mwingine aisee

Hao uhamiaji binafsi naona Yale n mazoezi tuu kwa mtu alieikosea adabu taasisi ya kijeshi
 
Back
Top Bottom