Waishio milimani Jijini Mwanza watakiwa kuondoka kupisha mwekezaji

Waishio milimani Jijini Mwanza watakiwa kuondoka kupisha mwekezaji

Ulivyo Soma ni sahihi kabisa wala hujakosea. Ndohabari ya mjini, zile nyumba zote zilizopo kwenye mountain inabidi zitoke jamaa wa Brazil aje ajenge na Familia yake...
Uwekezaji ni muhimu, Mwanza umejengwa ovyo ovyo sana. Mji upangwe na barabara zipanuliwe na hizo apartments zitasaidia kupunguza tatizo la makazi.

Watu waondoke milimani na hivyo shacks za milimani zivunjwe haraka sana, tunaingia uchumi wa kati huku tuna makazi duni. Zijengwe apartments za bei rahisi na wananchi wetu wajifunze kulipia. Hakuna njia ya mkato kwenye maendeleo.
 
Shamte analipa alichomfanyia baba yake.Baba yake alikuwa waziri mkuu Zanzibar akapinduliwa na kutiwa kizuizini halafu yeye Baraka akajiunga na ASP Kisha CCM.
 
Mradi unaonekana utaupendezesha jiji la Mwanza, wasiwasi wangu tu wananchi wanyonge walipwe stahiki zao kabla ya kuhamishwa na haki itendeke ktk tathmini ya mali za watu, maana jiji lisije onea watu ktk kutoa fedha zao kulingana na thamani halisi ya mali zao.
 
Sasa hizo ni nyumba au takataka? Walitakiwa waondolewe kitambo tuu maana wanachafua Mji..

Hao watu wa milimani Nina uhakika watakuwa wa kwanza kuitikia mwito maana watapewa maeneo mazuri yaliyopimwa na Fidia juu..

Nyanzaga Kule Sengerema wamehama kupisha Mwekezaji wa mgodi mkubwa dhahabu sembuse hao maskini wa huko milimani?
Ya ngorongoro yanakuja mwanza. Mioyo ijiandae tu kuyapokea
 
Kwanini hao wawekezaji hawaendi kujenga kule Chato kwa lihayati ma(ya)janga
 
Ulivyo Soma ni sahihi kabisa wala hujakosea. Ndo habari ya mjini, zile nyumba zote zilizopo kwenye mountain inabidi zitoke jamaa wa Brazil aje ajenge na Familia yake.

--------

Wawekezaji hao wanatarajia kuwekeza kwenye sekta ya miundombinu, viwanda na utalii katika maeneo ya Igogo, Isamilo na Kegeto.

Akizungumza na Nipashe ofisini kwake hivi karibuni, Meya wa Jiji la Mwanza, Sima Constantine, alisema mpango huo unalenga kuboresha miundombinu pamoja na kukuza sekta ya utalii utakaogharimu Sh. bilioni 150.

Alisema makubaliano hayo yanahusisha wawekezaji kutoka nchini Brazil katika Jiji la Rio de Janeiro, ambao walifika jijini humo, kuangalia fursa za uwekezaji katika miundombinu, viwanda na utalii.

Costantine alisema maeneo mengine ambayo wawekezaji hao wanayalenga ni pamoja na ujenzi wa kiwanda cha pembejeo za kilimo kwa ajili ya kuwahudumia wananchi wa Kanda ya Ziwa.

“Sehemu zingine ni ujenzi wa barabara pamoja na nyumba za ghorofa katika milima mbalimbali ambayo inaangalia ufukwe wa Ziwa Victoria,” alisema.

Alitaja sehemu zingine watakazozigusa kuwa ni pamoja na kutengeneza eneo la ufukwe wa Ziwa Victoria sehemu ya kliniki, Nera jirani na kituo cha polisi wa majini ambalo litatengenezwa na kuwa sehemu za uwekezaji na utalii.

Constantine alisema mpango huo utasaidia ukuaji wa uchumi wa Jiji la Mwanza na mtu mmoja mmoja.

Alisema wawekezaji hao wana umoja wao nchini Brazil unaojulikana kama ‘Africa Unity’ na mpaka sasa wamewekeza nchini Dubai na Ethiopia.

Aliongeza kuwa katika makubaliano ya mpango huo, Jiji la Mwanza litatoa ardhi na wawekezaji watatoa mtaji, teknolojia na mradi huo utakapokamilika utanufaisha pande zote mbili.

ULIPAJI FIDIA
Akizungumzia uwekezaji wa maeneo ya milimani, Constantine alisema, jiji limepewa jukumu la kulipa fidia katika maeneo ya Igogo, Isamilo na Kegoto ambayo yapo mlimani ili kupisha uwekezaji huo.

Constantine alisema wawekezaji hao wamekubaliana na jiji litafute ardhi na kukamilisha mipango yote ndani ya miezi mitatu kuanzia mwanzoni mwa mwezi huu kabla ya kazi hiyo kuanza.

Aliongeza kuwa wawekezaji hao wanaendelea kutafuta maeneo mengine ya kuwekeza ikiwamo mikoa ya Dodoma na Arusha.

Chanzo: Nipashe
Wakigoma itumike loliondo style
 
Mbona hii kitu ilikuwepo toka awamu ya nne jameni? Kigoto kuliwekwa beacon, Kiseke mlima wa Hali ya hewa, Igogo na Isamilo.Mwenda zake alijua huu mchongo na ndio uliompa kura Kanda ya Ziwa 2015 kwa kuchukua tatizo Hilo kuwa fursa kwake nakumbuka tukiwa CCM Kirumba ktk kampeni Wananchi wa maeneo husika walizirai na kulia akasema hakuna mtu kuguswa, so it's just a matter of time waje na Buzuruga
 
Utu gani? Hizo ni nyumba auntakataka? Kuwaacha kwenye Hali hiyo ya umaskini ndio utu? Acha upumbavu..

Kule magomeni wanapisha viwanja Serikali inajenga wanapewa floor za Juu harafu floor za Chini na vyumba vya Kati inakuwa mali ya Serikali inaingiza pesa..

Hata hao watoke kwenye huo umaskini wakapewa viwanja vizuri nje ya Mji na Fidia harafu hayo maeneo yako potential yaendelezwe serikali ipige pesa.
Mbona zanzibar hawauzi ila wanakodisha maeneo kwa wageni?
 
Mods badilisheni title ya mtoa mada imekaa kichochezi….Hata uwanja wa ndege wa kimataifa terminal two watu walihamishwa Sasa hivi kuna airport ya kisasa so sio ajabu
 
Kama ni kwaajili wa kuboresha madhari ya jiji naunga mkono hoja..tunaomba tu hiyo master plan yao tuione.

Mwanza ni jiji liendane na hadhi hiyo...pia wabakize baadhi ya vilima vipandwe miti ili kuleta hali nzuri ya hewa katikati ya mji.

#MaendeleoHayanaChama
 
Mbona hii kitu ilikuwepo toka awamu ya nne jameni? Kigoto kuliwekwa beacon, Kiseke mlima wa Hali ya hewa, Igogo na Isamilo.Mwenda zake alijua huu mchongo na ndio uliompa kura Kanda ya Ziwa 2015 kwa kuchukua tatizo Hilo kuwa fursa kwake nakumbuka tukiwa CCM Kirumba ktk kampeni Wananchi wa maeneo husika walizirai na kulia akasema hakuna mtu kuguswa, so it's just a matter of time waje na Buzuruga
Buzuruga mlima upi?
 
Back
Top Bottom