Wakati magari mengine yakitupwa na kutelekezwa, Tamisemi waomba magari ya Bil 16, kununua magari 81

Wakati magari mengine yakitupwa na kutelekezwa, Tamisemi waomba magari ya Bil 16, kununua magari 81

Magari mazima kabisa yameegeshwa ili wauziane land cruiser bei ya bajaji. Nchi hii bila CCM kutoka madarakani tutaendelea kuumizwa sana.
Itoke ccm alafu waingie hawa?
20230404_100946.jpg
 
Niliwahi kutaka kununua Nissan patrol mayai kwa milion 7 nikazidiwa ujanja wa watoto wa mjini
Ile gari ilikuwa na shida kwenye mfumo wa mafuta na ilipopelekwa D.T. Dobie makisio yakawa over 20 million kuitengeneza
Kwa kawaida serikali ikishapokea makisio ya namna hiyo huwa hawahangaiki tena kutengeneza kwakuwa ikishaandikwa over 20 maana yake inaweza kufika hata 50M

Basi bwana fundi wa karakana akanimegea siri kwamba ile gari ni nzima kabisa isipokuwa mpira wa mafuta toka kwenye tank kwenda kwenye engine ulikuwa umefinywa kwenye body na chasis, kuna siku walinyanyua body wakati wa kurudisha wakafanya uzembe pipe ikafinywa kidogo
Kwahiyo mfumo wa mafuta ukawa haufanyi kazi vizuri.. Akaniambia matengenezo yake hayazidi elfu 20.. Sikuamini.. Na yeye alikuwa anataka 1m tuu
Chelewachelewa utamkuta mtoto si wako, kusita na kujivutavuta kwangu, nafika eneo la tukio nakuta gari inavutwa, biashara ilishawahiwa . Yule fundi alinichukua mpaka garage moja pale Ilala kushuhudia alichosema...
Huwezi kuamini ndani ya lisaa gari ilikuwa sawa tunapiga nalo misele

Asilimia 90 ya magari ya serikali yanayoitwa mabovu matengenezo yake hayazidi milion 5
Connection ya kuyanunua sasa ndo shuhuli
 
Huu udokta wa mchongo ni balaa, kwanini asiige kwa HICHILEMA?, "Unataka V8 kanunue na hela yako full stop, Hela ni kwa ajili ya miradi ya maendeleo kwa wananchi"
 
Kwa akili hizi bora kutawaliwa na wazungu!!inawezekana kabisa wazungu wanapo tutukana wapo sahihi.
Magari 81 kwa billion 16 na ushee hii ni dharau kwetu watanzania!!hivi hawa Ma RC, Ma DC, Ma RAS nk wanatumia Nini Kwa sasa!?Ina maana hawawezi kuendelea kutumia magari hayo mpaka maskani?

Kiukweli muafrica Hana vision Wala mission!! Ni mbinafsi,mchoyo,mlafi,nk inshort ni primitive!

20230414_143928.jpg
 
Wewe mleta mada ni Gaidi. Wazungu ni Magaidi ambao hawawezi kupewa nafasi tena kuja kututawala. Wasithubutu hata kufikiria kuwa kuna kauwezekano wakuja kufanya hivyo.

Ulegee
 
wanafikiri kwa kutumia yale maeneo ya kukalia kwenye viti yaani matacle
 
Magari mazima kabisa yameegeshwa ili wauziane land cruiser bei ya bajaji. Nchi hii bila CCM kutoka madarakani tutaendelea kuumizwa sana.
nchi inahitaji chama kipya kabisa kianzishwe sambamba na katiba mpya maana hata vyama vya upinzani vya sasa ni CCM B
 
nchi inahitaji chama kipya kabisa kianzishwe sambamba na katiba mpya maana hata vyama vya upinzani vya sasa ni CCM B
Tatizo hao wenye kutoa usajili ndiyo hao mafisadi wenyewe chama chenye mwelekeo wa kuwatoa madarakani hakiwezi kupata usajili.
 
Back
Top Bottom