Wakili Kibatala anajua sana alifanyalo. Ni lazima akuchanganye tu

Wakili Kibatala anajua sana alifanyalo. Ni lazima akuchanganye tu

Mbaya zaidi huyu ndiye aliyefungua jalada la kesi. Huyu anatakiwa ahojiwe hadi kieleweke. Jamhuri hapa wana hali ngumu sana na hii kesi. Naona hata Jaji kishaona muelekeo wa maji.

Ni aibu sana hii kesi, sijui kwa nini DPP hadi sasa yuko kimya, labda wanaogopa aibu ya "Kutokua na nia ya kuendelea na kesi" ukichukulia maelezo ya IGP Siro kwamba wana ushahidi mzito, ambaye nadhani ndiye alimuaminisha Chief kwamba kuna kesi ya ugaidi.

Tusubiri kesho tuone kama Inspector Swila atapanda kizimbani.
Natabiri kesho Inspekta Swila hatatokea mahakamani kwa maelezo kuwa hali yake sio nzuri hawezi kusimama au kukaa kuendelea kutoa ushahidi ili wapate nafasi ya kujaribu kujipanga na kutafuta shahidi mwingine. Kwa hali ilivyo Insp. Swila ameelemewa!
 
Kwa hiyo ulivyo mwehu unashauri tukamtoe Mbowe kinguvu huko jela?
Nashauri mngeacha huku kufurahia maswali ya Kitabala na kufikiria hali ya mwenzenu kule hamjaona alivyokonda? Mngefikiria jinsi ya kupata suluhisho la haya matatizo kabisa ila nyie mnaishia kupiga domo humu ila manyanyaso yanaendelea siku zote.
 
Huyu bwana stahili yake ni kukuhoji kwa muda mrefu sana. Yaani kielelezo kimoja kinaweza kwake kikawa na maswali Zaidi ya 25. Ana utaratibu wa kuhoji mpaka kufikia muda wa kuhairisha ili siku inayofuata aje na nguvu mpya na mawazo mapya. Amekuwa sana na utaratibu huo ambao kwa kweli umekuwa ukiwachanganya sana mashahidi.

Shahidi wa leo Swila ambaye leo ilikuwa siku yake ya tatu kuhojiwa tayari ameshachoka sana kwani hakumbuki tena aliyoyaongea juzi wakati akihojiwa na mawakili wengine, leo amekuja tayari kishasahau kila kitu utafikiri hakufanya rehearsal, hii ni ajabu sana.

Baada ya kuona leo anazidi kulemewa ilibidi Wakili wa Serikali anayeongoza jopo lao amsogelee na kumwelekeza amwombe Jaji kuhairisha kwa ajili ya tatizo la kiafya - Shahidi mwenyewe inaonesha alikuwa ana uwezo wa kuendela lakini wakili wake kaamua kuingilia kati ili wakampe nafasi ya kujipanga upya kutokana na namna ambavyo ameshavurunga!

Kibata Mwenyezi Mungu azidi kukubariki sana. Hukumu ya Mahakama ikitofautiana na umma tunavyoona basi Jaji huyu atakuwa na roho ngumu sana.

Anyway Acha Ibaki Hivyo!
mtoa mada nafikiri hujui kitu kuhusu sheria kibatala ni kama mwanamke wa kizaramo huwezi kumshinda kwa kushindana naye kuongea lakini kinachotakiwa pale ni point za shahidi kueleweka tu hayo maswali ya kumchanganya hayana point yoyote chamuhimu kimeshapatikana maelezo ya shaghidi yaliyobaki ni kama yale tunaitaga mazungumzo baada ya habari yaani anapoteza muda tu mbowe tayari yuko kitanzini hata kibatala anajuwa lakini anajifanya kupoteza muda wa watu tu hana kitu kibatala kama mwanamke wa kizaramo tantalila nyingiiiii lakini hakuna point za maana
 
87,000 x 3 mtu kakimbia,nyie hesabu ni ngumu sana kuliko hata hisabati. Hisabati mfano matrix unatiririka tu na my (...) (....) hadi jibu ni 600,000
 
Mwenzenu anasota kule nyie mnafurahia maswali ya Kibatala, wabongo ni shida sana Tundu Lissu nusu afe ila wabongo waliishia kuongea tu kama hivi na story imeishia hapo hivyo hata ikitokea Mbowe akafungwa hakuna wabongo watakachofanya na hizi sifa za maswali ya Kibatala yataishia hapo hapo.
Kwa hiyo ulitaka wafanyeje labda.
Waweke matanga na bendela za chama zipepee nusu mringoti?
 
Hivi suppose ni kweli awe anaumwa halafu mara kesho tunasikia ameenda zake hapo itakuwaje?
Nadhani utachukuliwa ushahidi kwa hatua aliyofikia, ingawa unakua haujakamilika kwa sababu Cross Examination inaibua uongo wa shahidi, sasa isipofika mwisho pale mawakili wa utetezi wanapotaka, haitawatendea haki watuhumiwa.
 
Natabiri kesho Inspekta Swila hatatokea mahakamani kwa maelezo kuwa hali yake sio nzuri hawezi kusimama au kukaa kuendelea kutoa ushahidi ili wapate nafasi ya kujaribu kujipanga na kutafuta shahidi mwingine. Kwa hali ilivyo Insp. Swila ameelemewa!
Hii picha inaonekana ilishapangwa tangu jana au asubuhi, kwa sababu alianza na hoja ya kutojisikia vizuri, akasema ataendelea "hivyo hivyo"
 
Nashauri mngeacha huku kufurahia maswali ya Kitabala na kufikiria hali ya mwenzenu kule hamjaona alivyokonda? Mngefikiria jinsi ya kupata suluhisho la haya matatizo kabisa ila nyie mnaishia kupiga domo humu ila manyanyaso yanaendelea siku zote.
The lights are on but nobody's home!!

U resemble this.
 
Kwa hiyo ulitaka wafanyeje labda.
Waweke matanga na bendela za chama zipepee nusu mringoti?
Mimi nilitaka wamfikirie mwenzao kule anakonda na wafikirie ni jinsi gani ya kupata suluhisho la kuondokana na haya manyanyaso yote haya ila ajabu ndio kwanza wanafurahia maswali ya Kibatala.
Hata kama hawana la kufanya ila ndio wafurahie maswali ya Kibatala wakati mwenzao hadi sasa keshakonda na wakiamua wanaweza kumfunga na hayo maswali ya Kibatala ndio yatakuwa na msaada upi sasa?
 
Sipati picha Lissu angekuwepo kufanya collabo na kibatala daaah mashahidi wengi wangekimbia
Halafu hiyo ndio ingezuia Mbowe kufungwa endapo wangetaka kumfunga? Ila sie wabongo sijui tutazinduka lini
 
Mwenzenu anasota kule nyie mnafurahia maswali ya Kibatala, wabongo ni shida sana Tundu Lissu nusu afe ila wabongo waliishia kuongea tu kama hivi na story imeishia hapo hivyo hata ikitokea Mbowe akafungwa hakuna wabongo watakachofanya na hizi sifa za maswali ya Kibatala yataishia hapo hapo.
Ulitaka tufanyeje mkuu,tumtoe kinguvu au,tuliza mshono fuatia movie ukiwa na popcorn,kibatara amefanya niwadharau askari wetu
 
Huyu bwana stahili yake ni kukuhoji kwa muda mrefu sana. Yaani kielelezo kimoja kinaweza kwake kikawa na maswali Zaidi ya 25. Ana utaratibu wa kuhoji mpaka kufikia muda wa kuhairisha ili siku inayofuata aje na nguvu mpya na mawazo mapya. Amekuwa sana na utaratibu huo ambao kwa kweli umekuwa ukiwachanganya sana mashahidi.

Shahidi wa leo Swila ambaye leo ilikuwa siku yake ya tatu kuhojiwa tayari ameshachoka sana kwani hakumbuki tena aliyoyaongea juzi wakati akihojiwa na mawakili wengine, leo amekuja tayari kishasahau kila kitu utafikiri hakufanya rehearsal, hii ni ajabu sana.

Baada ya kuona leo anazidi kulemewa ilibidi Wakili wa Serikali anayeongoza jopo lao amsogelee na kumwelekeza amwombe Jaji kuhairisha kwa ajili ya tatizo la kiafya - Shahidi mwenyewe inaonesha alikuwa ana uwezo wa kuendela lakini wakili wake kaamua kuingilia kati ili wakampe nafasi ya kujipanga upya kutokana na namna ambavyo ameshavurunga!

Kibata Mwenyezi Mungu azidi kukubariki sana. Hukumu ya Mahakama ikitofautiana na umma tunavyoona basi Jaji huyu atakuwa na roho ngumu sana.

Anyway Acha Ibaki Hivyo!
Ukweli kibatala bongo bahati mbaya
 
Ushahidi wa kujifunza dawa yake ndiyo hiii...ni lazima ujichanganye tu na ndiyo maana mawakili wa Serikali wanakuwa na objection nyingi kujaribu kuokoa mtiririko wa ushahidi mzima wa kesi usiharibike.

Ila washashindwa..hamna kesi humo, TZ hatuko serious, wastage of our nation resources sababu tu za kukomoana kisiasa.
Tatizo la kuchanganyikiwa hawa mashahidi wa Jamhuri ni kujaribu kutetea uongo. Ngumu sana kutetea ukweli mbele ya mawakili, maana huwezi jua swali watakalouliza.

Ukweli humweka mtu huru!
 
Nashauri mngeacha huku kufurahia maswali ya Kitabala na kufikiria hali ya mwenzenu kule hamjaona alivyokonda? Mngefikiria jinsi ya kupata suluhisho la haya matatizo kabisa ila nyie mnaishia kupiga domo humu ila manyanyaso yanaendelea siku zote.
Kwahiyo unashauri watu wafanyaje ili mbowe atoke?
 
Ukiona shahidi anahojiwa hadi anapata homa mahakamani ujue hapo hamna kesi!
MaCCM hamuhitaji kesi kufunga wapinzani wenu. Mnawasweka tu ndani , kama mnavyomfanyia mzee Mbowe..
Chama dola bwashehe..
 
Back
Top Bottom