Wale tuliokosea kuoa tukutane hapa

Usiombe uchokwe mamawe hakuna rangi utaacha ona yaani mtu uishi nae miaka12 na ushee akulishe samaki na magamba[emoji848]we unaona ni sawa hii??unless kuna sehemu amevurunda ma ke akaona isiwe tabu utakula hivyohivyo bora liende
πŸ˜…πŸ˜…πŸ˜…πŸ˜…πŸ˜…πŸ˜… mauaji
 
πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚
 
Kama utaweka msaidizi tu sawa haina tatizo
 
Jamaa yangu suala la kuwafundisha watoto wife akaingilia kuwatetea inabidi ulinyamazishe kwa nguvu zote (hata kwa ngumi na damu). Binafsi siwezi kulivumilia
Kumbe wanaume halisi bado wapo. Suala la kuwanyoosha watoto ni la baba. Sisi tukiwa wadogo mama alikuwa anatwambia kuwa mmekosea ngoja baba yenu aje nimwrleze. Manake suala la nidhamu na kunyoosha vijana ni la baba. Unaogopaje kuwanyoosha wanao kisa mkeo hataki? Ujinga gani huo? Jiulize wakati unamleta hapo nyumbani alikuja na watoto? Watoto ni wako wewe baba na hata huyo mama mkitofautiana ndo maana watoto huwa anawaacha hapo kwa baba. Wanaume amka nyoosha watoto wenu acha kueaogopa wake zenu.
 
Hakuna mwanamke asiyependa kumdekeza mumewe apatapo nafasi, ila inategemea kwa mama mfanyakazi kama atapata muda jioni ni vizuri kupika na kumtengea mume ila ikitokea amechelewa kurudi labda , mume amuelewe na asicomplicate maisha kama dada yupo basi atasaidia kupika, ila mimi sitopenda dada amsevia mume wangu chakula ntajitahidi nimsevie mwenyewe ama ajisevie mwenyewe.

Ila on weekends kupika ni lazima mama mjengo nioneshe maujuzi jikoni harufu nzuri nyumba nzima hadi baba mjengo aseme leo kaingia mama mwenyewe jikoni rahaa.πŸ˜€

Ila wanaume nyie mnadeka sana eti tuwatengee chakula, maji ya kuoga wakati mlivokua single mlikua mnasugua hadi sufuria na michanga na kubeba madumu ya maji, ila ghafla umeoa basi umegeuka mtotoo huwezi hata kusogeza maji ya kuoga bafuniπŸ€ͺ. Ila fresh tu tunawapenda hivo hivo watoto wetu.
 
Sasa kuna raha gani umeoa mke na bado still unaishi maisha ya kutesekaπŸ˜…???
Hujawahi sikia jamaa anabezwa na demu kwamba aoe atajipikia mpaka lini?

Wanawake baadhi mnajua majukumu yenu sema wachache wasiojielewa ndo wanafanya uhuni wa makusudi wa kutaka mashindano na wanaume. Na hawa ndo wale kabla ya kuolewa wanajifulishaga na kupiga deki magetoni ili wakuchote tu uingie kingi!
 
Mkuu unaishi ughaibuni?
Naishi hapa hapa Tz.

Ila nimeamua kuacha kuishi kimazoea na kipumbavu,haiwezekani mtu na mkewe wote wanaenda kazini alafu mtu anafosi mke akirudi aanze kupika,kufua,kushughulikia nyumba n.k sasa huyo mke au chuma ?

Ukitaka hayo mwambie asifanye kazi akae nyumbani,mtimizie kila unachoweza alafu hapo akiwa hafanyi hizo kazi ndo mtu aje aanze lawama humu
 
Mimi kupata unyumba hadi yeye atake , kuna kipindi alinipiga desh wiki 2 , bac siku aliyokuwa na hamu , alianza kujichekesha toka dinner, mapema akaenda kwa bed [emoji2922], nami nikasema ngoja nimuoneshe nami nikawahi kwa bed nikalala nikampa mgongo , akajiongelesha wee mi nikajifanya nakoroma , hadi asubuhi [emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23], dah hizi ndoa hizi
 
Haha.

Mkuu ni haki mke akirudi kazini aanze kazi za nyumba bila msaidizi yeyote wakati na yeye anachoka pia kutokana na kazi ?
 
Katikati ya mstari naona una tatizo kubwa sana la kisaikolojia linalohitaji msaada wa haraka sana.... samahani kama umekwazika
Hapana mkuu huyo dada yupo sahihi kabisa,hili jambo haliwezekani kwa wanawake wengi.

Kwa wanaoweza acha wafanye,kwa ambao wanashindwa wasibezwe kwa sababu ni kweli na wao wanachoka.

Imagine mke mwalimu anarudi labda saa tisa kazini,akifika nyumbani kachoka hapo aanze kufua,kupika,kuosha vyombo huku wewe baba kama baba au mume umetulia kwenye sofa unachati jamii forum ukiwa na soksi miguuni zenye vitobo vimetafunwa na panya unasubiri kula.

Hii haikubaliki,nenda kamsaidie mkeo kazi kwa sababu wote mumetoka kazini.

Wanaume wengi wakitz bado tuna umwinyi sana na upuuzi flani ambao hauna maana yeyote,kwanza hizo kazi sio lazima kwa mwanamke kufanya kijamii tu ndio kwa kuwa wanawake wengi ni watu wa nyumbani ndio imeonekana ni kazi zao.
 
Inawezekana ukawa sahihi kulingana na maoni yako.....
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…