Waliofukuzwa CHADEMA waanza kupewa vyeo Bungeni, Grace Tendega awa Mwenyekiti wa LAAC

Waliofukuzwa CHADEMA waanza kupewa vyeo Bungeni, Grace Tendega awa Mwenyekiti wa LAAC

Tafuta akili maana huna, nani kakwambia wabunge wa viti maalum wanasababisha chama kipate ruzuku?
Matokeo ya Uchaguzi wa Oktoba 2020 unasababisha Ruzuku hiyo, Hoja kwa nini Ruzuku ni halali harafu matokeo na kazi za Uchaguzi wa Oktoba 2020 ni Haramu?! Ninaomba ufafanuzi.
 
Ni swali zuri sana.

Pili, wanaenda Bungeni kwa kutumia chama gani? Kama wanatumia CDM, kuna kila sababu ya kufungua kesi ya kupinga matumizi ya jina lao. Wanaweza kuitwa Wabunge wa Spika , pindi wakiitwa Chadema kuna tatizo

Tatu, hivi hapa hakuna ukikwaji wa katiba? Wako wapi wanasheria au taasisi zinazosimamia mambo haya?
Hivi haiwezekani kufungua kesi

JokaKuu tindo
Spika amekwishasema wasiwe na hofu 'atawalinda' hivyo hizo kesi watakazofungua Chadema haziwezi kubadili lolote.
 
Yaani ukiangalia namna Magufuli na genge lake wanavyopeleka mambo ni kama wana trigger kwa nguvu zote kuleta machafuko nchi hii.

Basi tu ni kama wabongo hawajawa tayari.
Rejea Mkasa wa mwarabu na ngamia wake. Tanzania Rais ana "absolute power". Anaweza hata kuamrisha mpita njia yoyote apigwe risasi hadharani na asiwepo wa kumchukulia hatua.

Nakumbuka Trump alipojigamba kuwa amekuwa maarufu kiasi kwamba angeweza kumpiga risasi mtu katikati ya 5th Avenue bila kuathirika: "man, I'm so popular; I could stand in the middle of Fifth Avenue and and shoot somebody and I wouldn't lose voters!". Bahati mbaya yake US si banana republic. Leo hii anatafuta pa kuficha uso kwa aibu.

MaRais tuliokuwa nao huko nyuma walikuwa na haya (soni) kutumia kikamilifu mamlaka makubwa ya Rais wa Tz. Walikuwa na kauoga fulani kula nguruwe mzima. Huyu wa sasa hana kabisa chembe ya soni wala hofu; anagonga hatua kwa hatua. Mkitikisika kidogo, "kamati ya amani" inaletwa kuwapoza moto. Na kwa vile waTz ni watu "wastaarabu sana" wanaojali amani, utulivu na matumaini (ya kufikirika) ya ulaji wao na familia zao kuliko kitu chochote, muda si mrefu atafanikisha kushindilia "full dose" ya dawa aliyoiandaa.
 
View attachment 1680489

Grace Tendega, mmoja wa Wasaliti waliojiteua na kuapishwa na Ndugai kuwa wabunge wa viti maalum kutoka Chadema, leo ametunukiwa kuwa Mwenyekiti wa Kamati ya Hesabu za serikali za mitaa ( LAAC )

Bado haijafahamika kama aliomba nafasi hiyo au amepewa bure.

Bali swali kubwa ni hili , ni yupi mwingine atayekikwaa cheo cha bure miongoni mwa wasaliti waliosalia ?
Mkuu, haujajifunza kutoka kwa Trump? Anabaki kulalama ila watu wanasonga mbele kwa speed ilele. We endelea kulalama, huyo ndo mwenyekiti tayari, au nasema uongo ndugu yangu? Mitano tena.
 
Kwakweli sina kabisa akili na wala hujakosea ndugu yangu katika hili.
Haya basi nielekeze wewe mfumo mzima wa Ruzuku ukoje na sheria husika.
Ukinielekeza mfumo mizma ukoje na sheria zinazosimamia hili suala utakuwa umenisaidia mno.
hebu angalia vyama vyote vinavyopewa ruzuku , je vina wabunge ?
 
Kwakweli sina kabisa akili na wala hujakosea ndugu yangu katika hili.
Haya basi nielekeze wewe mfumo mzima wa Ruzuku ukoje na sheria husika.
Ukinielekeza mfumo mizma ukoje na sheria zinazosimamia hili suala utakuwa umenisaidia mno.
Acha na ruzuku, wewe kwa akili yako hao unaowaita wabunge wapo kihalali?
Tuanzie hapa
 
Lakini ipo siku tutakuja kusema kumbe kwenye gulio la washenzi ndipo wenye mizaha utumia fursa hiyo kuonesha uwezo na vipaji vyao kuijenga nchi.
Ingawa mizaha kuna wakati inaweza kuondoa malengo na matarajio ya wengi kama kweli gulio litajwalo lina washenzi wenye uchu/matamanio yenye mlengo wa kuwajali wachache na kujinufaisha wenyewe.
Hii ni fursa kwa chama husika kujifunza namna ya kuendana na mabadiliko yenye sura ya Utaifa,ni wajibu wao pia kutafuta maridhiano ndani ya chama kama yapo na kuadhimia namna bora ya kutatua kasoro zilizopo.
Wamefukuzwa hakuna mjadala mwingine
 
Ndivyo Jiwe alivyotaka Bunge hili liwe hivyo.

La kijani kitupu na anachotaka yeye asihojiwe chochote kwa madudu anayofanya, ndiyo maana hivi sasa amekigeuza kijiji chake cha Chato kama Ikulu ndogo!

Hakuna mtu anayehoji maamuzi ya "kipuuzi" ya dizaini hiyo na ukihoji unatumbuliwa!
Watanzania lazima tujishangae, inakuwaje tunaruhusu mshamba mmoja atuendeshe anavyotaka na si tunavyotaka? Kenya huwezi kufanya upuuzi kama huu
 
Acha utapeliii, mungewafukuza halafu leo hiii mkakubali kula ruzuku iinayotokana na uwepo wao bungeniii??? Tulizeni mizuka wabunge hao wakachape kaziii
Nani kakudanganya kwamba ruzuku imetokana na hawa wasaliti ?
 
Tafuta akili maana huna, nani kakwambia wabunge wa viti maalum wanasababisha chama kipate ruzuku?
Wabunge wenyewe ni ruzuku, ndiyo maana WANAUME wa Chadema walitaka kuwachagulia washikaji.
 

Grace Tendega, mmoja wa Wasaliti waliojiteua na kuapishwa na Ndugai kuwa wabunge wa viti maalum kutoka Chadema, leo ametunukiwa kuwa Mwenyekiti wa Kamati ya Hesabu za serikali za mitaa ( LAAC )

Bado haijafahamika kama aliomba nafasi hiyo au amepewa bure.

Bali swali kubwa ni hili , ni yupi mwingine atayekikwaa cheo cha bure miongoni mwa wasaliti waliosalia ?
Kwenye siasa hakuna rafiki au adui wa kudumu,pambana na hali yako,si umemuona Maalimu halafu huo usaliti mbona haupo kwenye ruzuku anayochukua Mbowe?basi kataeni na ruzuku ndio tuwaone wa maana.
 
Back
Top Bottom