Pre GE2025 Waliomshauri Rais Samia kuwatengua Nape na Makamba, wamempotosha. 2025 Rais Samia atakwama!

Pre GE2025 Waliomshauri Rais Samia kuwatengua Nape na Makamba, wamempotosha. 2025 Rais Samia atakwama!

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)
Hawana ubavu wa kufanya chochote dhidi ya Ccm wala dhidi ya Mwenyekiti !
Mamba huwa ana nguvu akiwa majini lakini nje ya maji ni sawa na mjusi mkubwa. 😳🙌
CCM haitegemei kubebwa kwenye mbeleko. Ni ugonjwa mbaya hiyo ni short live strategy
 
Watangulizi wao wamefanya nn? Nchi hii mwenye maamuzi ya nini kifanyoke wapi ni mungu mtu (rais) tu. Mipango na bajeti ya wizara ni lazima ikubaliwe na mwenyekiti wa baraza la mawaziri (rais).

Kwahiyo tusiongopeane kwamba Kuna waziri anaweza kujifanyia mambo yake ktk wizara ili aache alama.

In Africa, the subordinate is not supposed to outshine their boss.
Jerry Slaa Ana kitu cha kusema kafanya nini na nini, lkn Nape hakuna zaidi ya vifurushi kupanda bei, kutaka mtandao wa Twitter usitumike Tz, January akiwa Wizara ya Nishati alizidisha mgao wa umeme na kuwa na majibu ya kitoto.
 
Kwa nchi zisizo na democracy ,rais akiwa anagombea muhula mwingine unafikiri kuna possibility ya kushindwa? Wahy unafikiri upinzani unapambana kupata katiba mpya na tume huru?
Siyo kwamba atakwamishwa na upinzani. Huyu wanaccm wenyewe wamepanga kumkwamisha.

Unafikiri ni kwann amewatengua mawaziri wengi? Kwann kawaondoa watu wengi waliokuwa wakifanya kazi ikulu? Kwanna kawabadilisha wakuu 4 wa idara ya usalama wa taifa.

Mama upepo unakata. Weka kumbukumbu ya comment yangu hii utakuja kunikumbuka
 
Siyo kwamba atakwamishwa na upinzani. Huyu wanaccm wenyewe wamepanga kumkwamisha.

Unafikiri ni kwann amewatengua mawaziri wengi? Kwann kawaondoa watu wengi waliokuwa wakifanya kazi ikulu? Kwanna kawabadilisha wakuu 4 wa idara ya usalama wa taifa.

Mama upepo unakata. Weka kumbukumbu ya comment yangu hii utakuja kunikumbuka

Issue ni kwamba Fomu inatoka moja tu na yeyote atakayenyanyua mdomo atapigwa kila kona na chawa wa mama ,utasemwa na msukuma ,utasemwa na kibajaji na hadi unaweze kutemwa chamani....Hakuna atakayempinga Mwenyekiti kiprotokali.
 
CCM haitegemei kubebwa kwenye mbeleko. Ni ugonjwa mbaya hiyo ni short live strategy
Ilikuwa inajulikana tangu zamani lakini Nape ndio amehitimisha kila kitu 👍

Amemwaga mchele kwenye kuku wengi,
Kila mwenye akili timamu amemuelewa 🙌👍
 
Jerry Slaa Ana kitu cha kusema kafanya nini na nini, lkn Nape hakuna zaidi ya vifurushi kupanda bei, kutaka mtandao wa Twitter usitumike Tz, January akiwa Wizara ya Nishati alizidisha mgao wa umeme na kuwa na majibu ya kitoto.
Nani alikua juu ya January wakatihuo
 
Makamba, Nape na Mwigulu wamekulia ndani ya CCM. Wanazijua siasa za bara na wanajua fitina na mbinu za ushindi.

Kwa Samia kuwavuruga Nape na Makamba wakati uchaguzi mkuu ukinukia ni mahesabu mabovu sana ya kisiasa ameyafanya Rais Samia.

Rais Samia hatoboi 2025.

Pia Soma
- Breaking News: - Uteuzi na Utenguzi: Nape, January na Byabato out! Jerry Silaa ahamishiwa Wizara ya Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari
Wewe hapa unataka huyo "Rais Samia ATOBOE 2025"?
Hata kwa msaada wa hao watu wako, huyo mtu wako HATOBOI 2025.
 
Nani amekwambia atagombea 2025? a deal is a deal …
Dah,
Mkuu 'Kijakazi', nawe leohapa unataka kutulisha upepo?
Huyo 'Chura Kiziwi' yupo tayari sana kuendelea kwenye nafasi hiyo kwa njia zozote zitakazo wezekana.
Deal gani ambayo unaizungumzia wewe?
 
Amefanya vizuri sana, haya si ndiyo mambo tunayoyapigia kelele kila siku? Mama ameonesha uthubutu, kwa kweli amenifurahisha sana.
Duh!

Haishangazi. Hata katika uvumulivu wa maumivu binaadam hutofautiana, sembuse katika maswala kama haya?

Kwa hiyo kwa upande wako, kisha maliza kazi katika maumivu yaliyo kuwa yakikusibu! Kuwatumbua Kipara na Neppy, anastahili mitano mingine!
 
Duh!

Haishangazi. Hata katika uvumulivu wa maumivu binaadam hutofautiana, sembuse katika maswala kama haya?

Kwa hiyo kwa upande wako, kisha maliza kazi katika maumivu yaliyo kuwa yakikusibu! Kuwatumbua Kipara na Neppy, anastahili mitano mingine!
Mkuu, mimi nina moyo wa shukrani na kuthamini kinachofanyika kwa nia njema hata kama ni kidogo.

Kweli, yapo mengi yanayohitajika kufanyiwa marekebisho au hata kufumuliwa upya lakini kuna ubaya gani kupongeza jitihada? Yani kwa sababu kaharibu mengi basi akifanya mema hata kwa uchache asipongezwe?

Hizi pongezi huenda zikamtia moyo wa kufanya makubwa zaidi. Kama tunavyomkosoa akiteleza tumpongeze akifanya vyema pia.

Naam, anastahili pongezi katika hili.
 
Back
Top Bottom