Pre GE2025 Waliomshauri Rais Samia kuwatengua Nape na Makamba, wamempotosha. 2025 Rais Samia atakwama!

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)
Wewe ni kipapa tu😂 katika siku ambayo mama atafanya jambo la msingi basi ni siku atakayowafurumusha hao wanafiki
 
Point. Tumeona Kwa Sabaya na Makonda. Kushangilia Nape na January kutemwa ni kupoteza muda😔
 
Uteuzi kila siku sijui kazi inafanyika mara ngapi?
Ndani ya miaka mitano uteuzi kila siku sasa sijui efficiency na competence vinatoka wapi?

Ukiona kila siku unanimous na kuteua tambua nawewe ni failure tu na mfumo mzima umeoza.
 
Ccm kama iliweza kusimama bila ya nyerere na hata lowasa alivyotoka chama kilikuwa imara, hawa wengine wakawaida sana, ccm ni taasisi imara sana kuliko unavyodhani
 
Acha ujinga, acha KUMTISHA mama, hao wote ni useless, hawawezi kushindana na Mkuu wa nchi, unataka kuniambia Nini??

Nape na January wanamzidi Mzee Kinana? Mkuchika na kikwete??

Mama anastahili Hongera sana kutoa hizo takataka, ilabado Mwigulu Mchemba amalize kama kifungashio Cha Nape na January 🤣🤣🤸🤸🤸
 

Sijaelewa, ina maana kushinda kwa samia na urais wake anategemea hao jamaa. Ushauri wako siyo kabisa!!!! Mwacheni Rais apange safu yake na atashinda bila hao jamaa.
 
Dkt Samia kafanya vizuri sana kuwatengua, naona mzee wa mawe bado mawe yake yamemsaidia kuwezesha wanaomshauri rais asimtengue. Ila Mh. Rais Dkt Samia ajue kabisa mhusika namba mbili wa kumharibia image ni huyu fedha. Huyu fedha ndiyo alihakikisha akishirikiana na rope kupandisha maisha kuwa juu kiasi kwamba mpaka sasa rais anachukiwa na watu wakilalamika anasema wahamie Burundi. Tena nashauri hawa akina N na J na huyu mawe wafungwe na kesi za uhaini wafie gerezani. Haiwezekani wamhujumu rais na taasisi yake, Dkt Samia walimdanganya kusema eti Dkt Magufuli ni mtu mbaya blabla. Mungu amsimamie Dkt Samia. Yaani hapa wananchi watamuelewa akimtoa huyu bwana fedha mwigulu tena akimfungulia na kesi za ufisadi itakuwa nzuri. Amteue Dkt Ashatu waziri wa Fedha au aangalie mtu ambaye atashusha gharama za maisha. Wizara ambazo zinaweza kumpa Mama Kura ni Fedha na Nishati
 
Wewe ndo hujui. Kawatengua ila waweke attention yote kwenye goli la mkono 2025.
 
Hao jamaa walikua wanajifanya hii nchi ni ya mama zao.

Afadhali tupumue kidogo hata kama ni kwa muda mfupi.

Kuishi chini ya wingu la dharau ni kadhia ya hali ya juu.
 
Pia waziri wa kilimo bashe pia amuondoe ni mla rushwa na kasababisha mpaka yule mchaga kafa kisa urefu wa kamba aliiombwa na bashe mkubwa kuzidi uwezo na alikuwa keshaleta mzigo wa mbolea. Dkt Samia ondoka kabisa mapandikizi ya wala rushwa na yule fedha.
 
Mkuu Kama Unawaza Maisha ya Wajumbe Hao wa CCM Kwamba Ndio Yameishia Hapa Basi Tambua Kua Wewe ni Miongoni mwa Watu MlioFail..!! Hupaswi Hata Kubet Mike kama Yako Itapasuka Vibaya Mno...!! Elewa Kua Misingi ya Watu Hao Yamejengwa na Chama Ambacho ni CCM

Tegemea Lolote Kua Wana sehem Yao Watawekwa Ili Kuliengoza Gurudumu la Nchi Hii...!!
Mama Samia Anakwenda na BEAT Mnayopiga Watanzania Kua Flani Abadilishwe...!! Ndio Mama Anafanya Hivyo ili Kupunguza Taharuki za Watu Wasiokua na Elimu Kwenye Chemistry Kuna Kitu Tunaita Balance Equation 😀

Usinene Ukamala...!!
Niko Turkey na Mama Enu Nakunywa Kahawa Saivi Nikiwaangalia Watanzania Mnavyotamani Vita Kula Uhai wenu..!! Kisa CCM Haitaki Kuachia Nchi Komaeni Muharibu Kila Kitu Wengine Wafariki na Wenye Bahati Wabakie Ili Muishi Kwa Amani
 
Kwanza ulibisha kwa britanicca kamwe hawawezi kuondoka hadi ukaweka nadhiri kwamba ikitokea basi utaamini kila analosema .. sasa umekuja na thread ya kalaumu mamlaka ya teuzi kwanini wameondoka... Either utakuwa mmoja wa hao au chawa wa hao jamaa.
 
Mama angempiga chini na Mwigulu. Hao watatu ni wataka urais kwa njia yoyote inabidi watulizwe. Mwigulu labda alishasoma upepo akatulizana ila Nape na Makamba wana ujinga mwingi na elimu za kuunga unga.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…