Wanafunzi Jenipher na Caren wa Iringa girls wanahitaji ushauri wenu,enyi GREAT THINKERS

hizi ni akili za miaka 20 iliyopita, sahv kontena linazoa wote ata wenye degree tupo nao mtaan tuna dandia pikipiki za watu kupiga daywork😂😂😂😂😁😁
Sasa Serikali inawawahisha huko mavyuoni ili igundue nini.. Hii nchi kuna vitu vya hovyo sana.. yani watu wazima kabisa wanakaa kupanga makolokolo tuu... Na mishara wanalipwa
 
Huu uzi mbona kama wa kimchongo! Huyu baba komando, yule baba mlinzi crew ya Hangaya, so what!!??
 
Waache haraka kwenye maisha.
Kama ni kuyala madushe watakula hadi wayachoke.
Waambie waendelee kusoma hapo hapo walipo wakileta ubishi tutawakeketa bila ganzi.
 
Kwann wasifiti?
Unaenda kusoma certificate ya procurement and supply au laws..
Unarudi unakuta kuna kaka zako na dada zako maelfu wana degree hadi masters wako mtaani utaenda nai sawa kwenye soko la ajira.!? Na ulipata four ya kuungaunga..

Maana serikali saivi inaungaunga combinations tu kuwaswagger watoto vyuoni.
 
Watoto wapo vizuri sana, wanaupeo mkubwa na wanafikiria mbali sana
Mawazo yao ni sawa na mawazo ambayo ningewapa kama wangeniomba ushauri
Amina
Tushirikiane tutafute namna ya kuwaendeleza hao watoto wasome ndoto zao

Kwenda A level ni kuua ndoto alizonazo mtoto

Naomba nikuulize, wanataka kusoma nn huko chuo???
 
Nadhani usingesema kazi za wazazi wao, ungepata ushauri mzuri tu humu ndani, ila kwa nafasi walizopo, sioni kinachowashinda kusoma chuo.

Mimi sio great thinker, ila sio loser vile vile. 😊
 
Vibinti vya siku hizi ni wajinga Sana, tulipata binti wa kazi kaletwa ati na kaka yake, tulipomuuliza elimu akajibu darasa la Saba, tukamwambia haina shida baada ya miezi sita utaanza kujianda na masoma angalau uwe na cheti Cha kidato Cha nne tukupeleke chuo binti kimya ukimzungumzia kusoma hajibu. Kumbe yule si kaka ni bwana wake (muuza chips si zake) kamtoa kijijini aje wajiandae kuishi pamoja, binti kakataa shule alitakiwa ajiunge kidato Cha tano mwaka juzi, mzee wake alilia Sana maana anauwezo na hawana shida kabisa, tulivyopata hizi habari tukatimua maana si mkweli
 
Hao wadada waache upuuzi, yaan wanawaza bata na uhuru wa chuo, hawana lolote, wabaki hapo shule wapige kitabu. Huo wanaofanya ni ulimbukeni unawasumbua

Nwei kupanga ni kuchagua. Kazi kwao.
Inawezekana hawawazi Bata, advance imekuwa sio muhimu, pia unaweza kujikuta umepoteza miaka yako 2 Bure tu.
Ila katika Hali hii ya wazazi kushikilia makali basi Hawa wanafunzi hawana namna, wabaki shule tu wamalize then waende chuo. Mipango Yao wataikuta tu, wawe wavumilivu.

Madam Amina68 baadae alasiri tukutane Manyara (karibu na miyomboni pharmacy) tupange namna ya kuwashauri wadogo zetu!
 

Ushauri:Safari ya elimu ,inategemea mhusika unapenda njia ipi.Na njia zote ni nzuri tu na zinakubalika.Njia hizo Ni njia ya vyuo ,na pia njia ya form 5na 6.Kuna Ma Prof wengi tu duniani wamepita njia ya vyuo.Yaan certificate ,diploma na kwenda chuo kikuu.Kuna wengine wamepita form 5 na 6.Nikitoa mifano.Marehemu,Prof Basigwa Mweregu.Huyu alikuwa Mwalimu wa shule ya msingi.Akajiendeleza mpaka kuwa Prof.Ndugu mleta uzi.Naomba uwashauri wazazi wa hao watoto,wawasikilize watoto wao.Wazazi wamekuwa chanzo Cha kuharibu maisha ya vijana wao kwa sababu wengi wamekalili ,tu kuwa nilazima kusoma A level.Pia wanaosoma diploma za udaktari wanakuwa wazuri kuliko form six.Asante
 
Uyo kwa avatar ni ww?

Natanguliza samahani (kwako na kwa mleta uzi) kwa kutoka nje ya mada.
 
Kwa mwalimu wa chuo kikuu, ni rahisi sana kumfundisha mwanafunzi aliyepitia kidato cha sita, ukilinganisha na yule aliyetoka form four na kujiunga na kozi za Diploma.
Shule ya A level ni shule iliyochangamka kwelikweli, sijui kwa nini watu wanaichukulia poa. Kiukweli nikiona CV ya mtu ambaye hana A level, huwa naona huyu mtu anakosa kitu flan hivi.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…