Nimeuliza wana uhakika gani hakupeleka kero yao bungeni au mahala panapohusika?
Kwani Tanzania kuna sehemu isiyo na kero ya wananchi? Masaki tu kule wanapokaa mabalozi na washua kuna kero hadi za takataka kutokusanywa kwa wakati!
Nchi hii wananchi kutokana na ujinga wenu mnapigana na msichokijua. Mbunge hakusanyi kodi, mbunge sio afisa masuhuli. Kwa katiba yetu hii mbunge ni boshen tu.
Siku mkipata akili vizuri mtajua shida ni Katiba yetu ndo mtafanya maamuzi sahihi. Ila kwa kuwa kwa sasa bado mna ujinga mwingi, endeleeni tu na ujinga wenu. Na mkiweza mtafukuza wabunge wote kila siku.