Wanaopinga ndoa wana matatizo au wamekulia kwenye familia zenye mgogoro

Wengi wanaokataa kuoa ukiwauliza watakwambia wanawake hawajatulia, kwa jibu hilo inasadiki kwamba wengi wameshuhudia au kusimuliwa matitizo ya ndoa fulani ndiyo maana wakawa na msimamo huo.

#YNWA
mtu yoyote anae ***** hawezi kuoa mfano huyo hapo chini kazeeka bila mke na kundi lake
 
Wametendwa hao, hivyo wanatafuta pa kuponea, wanaangalia mifano michache ya wenyewe hela wakichapiwa, wakiomba talaka, wakilalamika maswaibu yao, na wao wanaconclude kuwa wasioe. Ndoa inahitaj mwanaume na mwanamke waliopevuka vizuri kiakili na Wana Nia ya dhati kuishi pamoja. Ndoa sio tendo la ndoa, ukiendana akili hii utakwama maana si kila wakat utalipata Hilo tendon kwa viwango unavyotaka, ukienda kwenye ndoa ukawa unawaza pesa lazima utundike daruga mapema tuu. Waache waendelee kujipa moyo lakini ndoa ni tamu
 
Kwa kweli ndoa ni tamu sana asikwambie mtu tuachane na maneno ya mtaani. Ingia ujionee mwenyewe
 
Wewe ndiye mwenye matatizo ya akili kabisa. Kama unajivunia ndoa ni huna akili.
KATAA NDOA KWA AFYA YAKO KIAKILI, KIMWILI NA KIROHO.
 
Wewe ndiye mwenye matatizo ya akili kabisa. Kama unajivunia ndoa ni huna akili.
KATAA NDOA KWA AFYA YAKO KIAKILI, KIMWILI NA KIROHO.
Kama nawe ni mmoja wa wanaopinga kuoa basi jitambue tu kuwa unahitaji msaada wa kisaikolojia. Ukikaa sawa utakubali tu na utaenjoi ndoa yako
 
°Wengi wao ni kutoka kwenye family zenye migogoro mingi sana ndio maana wameathirika kisaikolojia
 
Sio broken family tu

Wengi wao hasa wakiume, ni wasio na uwezo wa kusimamisha
Wasio weza kuzalisha.
Wagonjwa wa ukimwi

Wanatumia hiyo mbinu kujiweka kando ili wasiaibike
 
Ni mwendo wa kula tunda kimasihara hakuna kuoa
 
Sio broken family tu

Wengi wao hasa wakiume, ni wasio na uwezo wa kusimamisha
Wasio weza kuzalisha.
Wagonjwa wa ukimwi

Wanatumia hiyo mbinu kujiweka kando ili wasiaibike
Mkioa nyinyi inatosha mkuu[emoji23]
 
Your browser is not able to display this video.
 
Hakuna sehemu kwenye biblia au msaafu ulioandika ni lazima mtu kuoa au kuolewa ni uamuzi wa mtu husika,ndo maana Paulo alisema hakulazimishi kufuata mawazo yake bali ni vyema kuishi mwenyewe ili kuepuka changamoto za ndoa
 
Subiri tuzeekezeeke kwanza labda tunaweza kufikiria upya kuhusu ndoa, lkn kwa sasa ni HAKUNA KUOA
 
Pambana na hali yako kwa uburu. Most married men don't cares about your status, wanawaza ada, chakula bima za afya n.k.
 
Wengine wamepigwa matukio dabodabo na maslei queen wao kwahiyo hawana hamu kabisa na mahusiano,lazima wakatae ndoa hao!
Vijana tafuteni real wives muone kama hamjaenjoy maisha,tena wamejaa tele shida moja ni kuwa hawapo kidimbwi wala elements na huko instagram wengi wao hawapost hata picha moja kama waleeeee!
 
Watu badala ya kupeana mbinu za kutoboa haya maisha wanashauri watu waoe utalawalisha hao watoto nn? Utawasomesha na nn? Lazima ufikirie haya kama kipato chako ni Cha kusuasua, usichukulie advantage ya mababu zetu walikua wakilima hata robo Heka gunia 20 Leo hii mvua hakuna, shamba bila mbolea havioti, pembejeo ghali, ukisoma ajira hakuna.

Labda mtuandikie mnayaendeshaje haya maisha? Mnafanya kazi gan?
Wale wanao enjoy national cake [emoji512][emoji512] labda wasiache kuoa.

Usiige kwa kua Fulani kafanya hivi na ww ufanye kama hujui njia anazopita, don't apply the same way even if you know where s/he passes through....

Oa kwa ajili ya kujenga kizazi Bora sio uzalishe watoto wa mitaani au umtese mtoto wa mtu ( mke). Usioe kwa ajili ya ngono tu. Ndoa ni taasisi kubwa Sana kwa ambao hawajui Siri.

Usipoa sio dhambi Bali ni pale utakapoa na kushindwa kutekeleza majukumu ya taasisi hio. Kamwe usitengeze laana na vizazi vya ajabu.

Kama unawezo wa kutunza familia oa mapema kwa sababu utatengeza kizazi Bora, mtoto apate elimu nzuri, matibabu, afya njema kwa ajili ya kizazi cha baadae. Create the best generation, the grateful children who will not blame their parents that they make them in bad situation.

The children who will not cry because of poverty. Create the way for them to enjoy the life of this world [emoji288][emoji288].

Alisikika mzazi mmoja akisema "acha tu wakikua watajitafutia" wamekua kuku wa kienyeji?

Hao wanaosema Wanaokataa ndoa ni mashoga wao ndio wanazalisha mashoga kwa sababu ya kutowaandalia watoto maisha Bora japokua ushoga wakati mwingine unasababishwa na upungufu au ongezeko la hormone whether male-female or female-male hormones.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…