Katika soma yangu nimekutana na hii aya. Naona inapishana na baiolojia niliyosoma miaka ile ya sekondari.
Quran 23:14
Kisha tukaiumba tone kuwa damu iliyoganda, na tukaiumba damu kuwa pande la nyama, kisha tukaliumba pande la nyama kuwa mifupa, na mifupa tukaivika nyama. Kisha tukamfanya kiumbe mwengine. Basi ametukuka Mwenyezi Mungu mbora wa waumbaji
English translation:
Then We made the sperm drop into a clinging clot, and We made the clot into a lump [of flesh], and We made [from] the lump, bones, and We covered the bones with flesh; then We developed him into another creation. So blessed is Allah, the best of creators.
Kwa usahihi ilipaswa kuanziwa aya ya nyuma yake isemayo;
28:12
“And indeed, We created humankind from an extract of clay,”
“Na hakika tumewaumba watu kutokana na udongo.”
28:13
“then placed each ˹human˺ as a sperm-drop in a secure place,”
“kisha tukamweka kila mtu kama tone la manii mahali pa usalama.”
28:14
“then We developed the drop into a clinging clot ˹of blood˺, then developed the clot into a lump ˹of flesh˺, then developed the lump into bones, then clothed the bones with flesh, then We brought it into being as a new creation. So Blessed is Allah, the Best of Creators.”
“Kisha tukalifanya tone kuwa pande la damu linaloshikana, kisha tukalitengeneza pande la damu kuwa bonge la nyama, kisha tukaliumba bonge hilo kuwa mifupa, kisha mifupa tukaivika nyama, kisha tukaifanya kuwa kiumbe kipya. Basi ametukuka Mwenyezi Mungu, Mbora wa Waumbaji.”
28:15
“After that you will surely die,”
“Baada ya hayo hakika mtakufa,”
Ukisoma tafsiri ya kiingereza na kiswahili unaelewa kwamba sperm inaingia kwenye damu iliyoganda. Nikatafuta wataalamu wa tafsiri kuhusu hiyo clot.
Hapana, na hapa ndipo ulipokosea mtirirko mzima, kuanzia pale aya inapoeleza kuhusu ‘Blood Clot’ inaongelewa hatua ndani ya tumbo la mama na si manii kama manii.
Prof Haanein Muhammad Makhloof, on page 508 of his Dictionary of the meanings of words of the Quran says that the Arabic word alaq translated into English as "clot" means frozen blood.
Maana ya neno za kiarabu “Alaq”
Kwa mujibu wa Dr. Zakir Naik ameeleza kuna maana tatu za neno “Alaq”
1. Kitu kama Ruba (leech-like substance) kiumbile na kitabia
Katika hatua za mwanzo za “embryo” huonekana kama ruba, mbali na muonekano huo pia hua na tabia kama ya ruba kwa maana hupata nutrisheni (nutrition) zake toka kwa mama kupitia placenta.
2. Kitu kinachoshika/ganda (Clinging substance)
Hapa kwa maana ya kuwa “Embryo” huganda kwenye ukuta wa uterus kwa miezi yote 9.
3. Kama Damu (Clot/ Conjured out of blood)
Katika hatua za mwanzo damu huwa haitembei na huonekana kukusanyika sehemu moja.
Maswali yangu
1. Sperm inaingia kwenye damu iliyoganda?
Hapana, manii huingia kwenye yai kulirutubisha, baada ya kueleza makao ya manii aya ilienda moja kwa moja kueleza yanayotokea tumboni kwa mama.
2. Damu iliyoganda inaishi ndani ya tumbo la mwanamke?
Inategemea wakati gani, wakati wa hatua za mwanzo huwa na kitu kama damu iliyoganda.
3. Quran haifahamu kuhusu yai la mwanamke?
Hapana, inafahamu, na katika Quran 28:14 katika lugha ya kiarabu limetumika neno ‘nutfah’ ambalo wafasiri wamelifasiri kuwa ni yai lililorutubishwa.
4. Sperm peke yake inaweza kuumbwa ikawa mtu?
Hapana, hatua zilizoeleZwa zilielezwa zinazokuwa zinatokea tumboni kwa mama.
5. Kauli kwamba tukamfanya kiumbe mwingine inamaanisha nini?
Kauli ile imetokana na ukweli kuwa hatua za mwanzo za ukuaji wa mwanaadamu tumboni hazitofautiani na za Samaki, Mjusi, Panya, Sungura na wengine mpaka pale mikono na miguu inapoanza kujijenga.