In English Science is the study of nature, kwa lugha ya kiswahili, Sayansi ni somo linalochunguza kuhusu asili.
Sayansi haigundui kitu kipya, bali chunguzi na majaribio zinairuhusu kupata uelewa juu ya ambavyo tayari vipo japo binadamu hawana ufahamu navyo.
Kwa mfano, sio kweli kwamba dawa ya kudumu ya UKIMWI, Kansa, Homa ya ini, Kisukari na magonjwa mengine sugu hazipo, zipo ila Sayansi haijamudu kuzijua.
Ninachojaribu kusema ni tusiitumie Sayansi kama kipimo cha usahihi kwa asilimia mia, ndio maana kuna baadhi ya zilizoitwa gunduzi za kisayansi ila baadae zikaja kupingwa na gunduzi zilizofuata kwa kuonekana hazikuwa sahihi.
Nikirudi kwenye swali lako, siko kiimani sana ila hayo maandiko kwa hicho kipande ulichoweka yako sahihi sana. Nadhani kikubwa ni tutofautishe kati ya tafsiri na maana, tujikite kuelewa yalichokusudia.