Wanaume badilikeni fanyeni maendeleo, umri haurudi nyuma!

Mtaji wapi huyu jamaa alinikoleza nikakolea nikiwa nasoma PCB mpaka nikapata division 0. Hapo four Nina two yangu nzuri ya 21. Akaja kunioa Kwa ahadi ya kunipeleka clinical officer. Sasa naona nimekua officer wa watoto hata hamu ya shule sina tena.
Yeah!

Lea watoto hao ndiyo jicho lako la kesho ila kikubwa hasa masikilizano ndani ya nyumba unapotaka kuzungumzia ishu ya maendeleo yenu yawepo.
 
Mtaji wapi huyu jamaa alinikoleza nikakolea nikiwa nasoma PCB mpaka nikapata division 0. Hapo four Nina two yangu nzuri ya 21. Akaja kunioa Kwa ahadi ya kunipeleka clinical officer. Sasa naona nimekua officer wa watoto hata hamu ya shule sina tena.
Hujakaa sawa unapigwa mimba nyingine.
 
Vizuri zaidi ungemwambia amwambie wapunguze quality ya nyumba waende sehemu za kawaida ili kodi itakayobaki wajenge kwao.

Huyu mama anacholalamika yeye siyo anakaa nyumba mbaya anachotaka yeye wawe na nyumba yao kwa ajili yao na watoto wao
Kujenga sio lazima sana ka hela ya kuunga unga
 
Mtaji wapi huyu jamaa alinikoleza nikakolea nikiwa nasoma PCB mpaka nikapata division 0. Hapo four Nina two yangu nzuri ya 21. Akaja kunioa Kwa ahadi ya kunipeleka clinical officer. Sasa naona nimekua officer wa watoto hata hamu ya shule sina tena.
Acha akunyooshe we si ulimvwaga mwanangu Amasha kisa tamaa aisee umechakaa sana form four 2014 sahv watt watatu.
 
Mke wangu anawaza kubadilisha sofa zimechoka, mapazia mapya, aweke chini zuria na simu mpya maana simu yake katoto kalimpasulia hapo nitoe Hela,
Mimi badala ya kufanya hayo anayotaka nikamnunulia kiswaswadu halafu nikaenda kumwaga mawe Trip za kutosha kwenye kiwanja nilinunuaga halafu Hela zimeisha, hapa namskilizia sijui reaction yake sijui itakuwaje maana alijua naenda benki naleta Hela inatosha kufanya yote hayo anayotaka.
 
Hahaha jiandae Kwa kesi sisi Kuna muda pia hatueleweki! Badala ya kukusifu ataleta kisirani. Kwangu Mimi hapo upo vizuri
 
Unamuombea kifo mmeo,atakufa tuu utabaki na wanao.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…