Wasukuma punguzeni huu ulaji wa chakula kingi namna hii

Wasukuma punguzeni huu ulaji wa chakula kingi namna hii

Sio Wasukuma pekee ndiyo Walaji wa chakula kingi. Nafikiri ni mikoa yote ya Kanda ya Ziwa ni Walaji wazuri wa chakula kingi.

Ulaji wa chakula kingi unategemea na shughuli mtu azifanyazo, kama utakuwa unafanya kazi nyingi za nguvu huna budi kula chakula kingi ili kupata energy ya kutosha kwenye shughuli zako.

Mimi pia nilikuwa Mlaji sana wa chakula nikiwa kule, baada ya kuja DSM nikapunguza kabisa.

Juzi nilipoenda Musoma kusalimia, nikakutana na msosi wa kula watu sita wa DSM lakini tukatakiwa kula watu watatu.

Kwanza walipakua wali Samaki tukala.

Baada ya dakika 15 wakaleta mezani ugali Samaki, eti walisema ule wali ilikuwa ni wa kuonja tu 🙌

Kwa kweli tunaoishi mijini ni kama hatuli kabisa, haiwezekani ule Chipsi sahani Moja eti ushibe, hizo nguvu za kuzalisha watoto 12 kama Wazee wetu zinatoka wapi 🙌
Babu walizalisha watoto 12 lakino waliachia wake zao wawalee kwa kukatia kila mmoja shamba na kuwapa ng'ombe. Wengine wakarogana, watoto wengine wakakosa privilege ya kusomeshwa kisa wa kike, sasa saivi tunataka kuwaiga huku 20X20 unanunua milioni 10 na Dar sijui bei gani.
 
Babu walizalisha watoto 12 lakino waliachia wake zao wawalee kwa kukatia kila mmoja shamba na kuwapa ng'ombe. Wengine wakarogana, watoto wengine wakakosa privilege ya kusomeshwa kisa wa kike, sasa saivi tunataka kuwaiga huku 20X20 unanunua milioni 10 na Dar sijui bei gani.
Binafsi isingekuwa haya maisha ya Kisasa na kufata mambo ya Dini ya Mke mmoja, ningeshakuwa na Watoto 20 saivi

Ukienda Vijijini unauziwa ekari 50 Kwa shilingi milioni 2.5 tu, wastani wa ekari Moja shilingi 50,000

Hapo ukijenga yale maboma kila Mke na boma lake, Kila boma umefunga Umeme wa Solar kwaajili ya mwanga

Wakati huo umenunua majembe ya kuvutwa na ng'ombe, ni mwendo wa kulima tu

Chakula hakikauki ndani, magunia na magunia

Siku hizi Elimu ni bure, watasoma kuanzia Shule ya msingi hadi wanafika Chuo Kikuu ambapo wanakutana na boom la Serikali
 
Habari za jumapili wakubwa.
Juzi kati nikamtembelea jamaa yangu flani hivi ni msukuma anaishi nje kidogo ya mji.
Ebana sijawahi kuona watu wanakula kama hawa watu.
Imeletwa nguna ya watu watatu tu mezani lkn hiyo nguna kwa wanaume wazembe kama wa dar wangeweza kula mwezi mzima.
Tumepiga nguna weeeee me nikasarenda nikawaacha wenyeji wakaisukuma mpaka ikaisha nikabaki mdomo wazi tu.
Ndugu zangu punguzeni huu ulaji wa hovyo namna hii.
We inakuathirije katika shughuli zako Kila siku za kutafuta mkate???
 
Wanaona sifa kula chakula kingi, wanasema kwao hakuna njaa wanalima sana. Mtoto mdogo anaanza kulishwa chakula kingi ili tumbo lipanuke awe anapakia chakula kingi hatimaye akiwa mkubwa awe na umbo kubwa. Mshangao ni pale wakienda chooni mtu anashusha kimba la kilo mbili! Kwa ulaji huo choo kitaachaje kujaa haraka?
Aisee hadi mimi nilishangaa kuona binti mdogo tu ameshusha mzigo mithiri ya gogo asee😂😂
 
Back
Top Bottom