Watanzania fuatilieni kinachoendelea DRC. Hali kwa majirani zetu ni mbaya, ya hatari sana

Watanzania fuatilieni kinachoendelea DRC. Hali kwa majirani zetu ni mbaya, ya hatari sana

Mafisadi wakiwa na neema hawawakumbuki Raia, ila wakishaanz akufumuana Risasi wanataka kufanya hiyo vita ni ya Nchi nzima wakati sio kweli.
Wajikalie pembeni Miamba ipambane
'Vita havina macho', hao wananchi wa kawaida ndio waathirika wakuu wa vita popote inapotokea duniani.
Hiyo pembe unayotaka wakae ni ya wapi?!
Vita ni hadithi tamu kwa asiyehusika ila ni MZIGO MZITO kwa wahusika.
 
Jeshi letu linawasaidia Wacongo lakini na wenyewe inatakiwa wajitambue. Haiingii akilini nchi yenye utajiri na diaspora wengi miji yake kutekwa na kikundi tu cha watu. Congo kama wako serious waingie mkataba na Tanzania na South Africa ili kwa malipo/makubaliano maalum tuwalinde walau kwa muda wa miaka 20 huku wakiendelea kujenga upya mifumo yao ya kiuulinzi. Vinginevyo Tanzania na South Africa nazo zitauchoka mgogoro huu na hapo ndipo Congo itakapo pata hasara kubwa zaidi.
 
Hata Donald Trump ni Dictator tyu. Na ameshasema, watashughulikia wachina kwanza, halafu waje kulokota "rare earth" minerals.

Hizi sio vita zamasikini.
Wenyewe banakunywa kofi
Trump ni mpuuzi.
 
DRC inaathiriwa na utitiri wa majambazi kutoka nchi mbalimbali.Ni nchi tajiri kuliko zote duniani kwa upande wa mali asili.Huu utajiri ndio unaoivuruga DRC maana inatolewa macho na kila nyang'au.
 
Kuingia Goma kutokea Bukavu ni kipengele sababu miji hii inatenganishwa na ziwa Kivu.

Hapa wanatakiwa kuingilia Nyiragongo. Uzuri hesabu za kuingilia wapi hazipo sababutayari wapo Gomba.

Kinachotakiwa ni kuwapelekea kipigo cha haja, lazima tu watarudi nyuma na mji pekee watakao retreat ni Gisenyi.

Wakikimbilia Gisenyi , maana yake tayari wapo Rwanda (na siku zote ndipo wanapotokea na kukimbilia). Hapa watatakiwa kuongeza nguvu na kasi ya mashambulizi na kutojali mpaka, maana yake na wenyewe watavuka, wakivuka Rwanda itapaniki na kujibu, kitedo cha kujibu inakuwa tayari wameshai drug rasmi Rwanda vitani.

Rwanda ikishakuwa rasmi war mode, na wenye wana activate vikosi vilivyopo kule Bukavu ili viingie Rwanda wakiuvuka mto Ruzizi. Hapo ngoma inakuwa inogile.

Ili Goma itulie inatakiwa watu anaoweza kujitoa ufahamu. Ukijifanya ni mtu wa kutaka ku make sense kamwe eneo lile halitatulia.

Siku zote M23 wakizidiwa, mji wanaokimbilia ni Gisenyi, wakikimbilia Gisenyi wanawaacha. Yaani majeshi ya waasi wakimbilie nchi nyingine na silaha zao halafu nchi hiyo inabaki kiwaaminisha kuwa haihusiki? Ujinga huu.

Ku deal na Kagame inahitaji watu wanaoweza kujifyatua akili kama JK na General Mwakibolwa, an Kagame akishajua anakabiliana watu wa aina ile huwa anakuwa muoga sana. Huufyata mapema.
Mnachezeshwa ngoma msiyoijua na msisahau mnauchaguzi October 😁😁
 
Tuna mchango wetu katika kujaribu kuleta amani ya Congo, ingawa ni changamoto

TOKA MAKTABA :

29 January 2024

VITA MASHARIKI YA CONGO: Kikosi Kipya cha battalian ya Kitanzania Kilichopo Kivu Kaskazini Kikiwa na Mamlaka ya Kulazimisha amani
View attachment 3214140

Kikosi kipya cha wanajeshi wa Tanzania kimetumwa katika jimbo la Kivu Kaskazini lililokumbwa na vita mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo kama kikosi cha pili cha ujumbe wa Jumuiya ya Maendeleo ya Kusini mwa Afrika (SADC).

Kikosi cha Tanzania kitachukua nafasi ya jeshi la kikanda la Jumuiya ya Afrika ya Mashariki EAC na kuchukua jukumu la kushambulia, kulingana na vyanzo vya kijeshi.

"Wanajeshi wa Tanzania wanawasili ili kuongeza nguvu ya askari wa SADC ambao wana mamlaka ya kulazimisha waasi wakubali amani ," alisema Luteni Kanali Guillaume Ndjike, msemaji wa gavana wa kijeshi wa Kivu Kaskazini.

“Uko pale kupigana na adui, waasi wa M23. Haupo kwa doria za jiji au kufahamiana na watu wa Kongo. Tuko hapa kushughulikia lengo letu,” alisema Meja Jenerali Monwabisi Dyakopu wa Afrika Kusini SADF mkuu wa kikosi cha nchi wanachama wa SADC, katika hotuba yake ya kuwaribisha.

Wanajeshi hawa wa SADC, wakiwa na mamlaka ya kushambulia, watachukua nafasi zilizoachwa na jeshi la kikanda la EAC (Burundi, Sudan Kusini, Kenya na Uganda) kama ilivyoamuliwa na serikali iliyotaja kutoridhika na kuendelea kuwepo uasi katika maeneo yaliyovamiwa M23 na kutokuwa na utulivu.

Wakati huo huo, kikosi cha Afrika Kusini cha SADC ambacho kilikuwa cha kwanza kuwasili Goma Desemba 2023, hivi karibuni kilishambuliwa na kundi la waasi la M23.

Kutumwa kwa wanajeshi wa SADC mashariki mwa DRC kuliidhinishwa wakati wa Mkutano wa 43 wa Kawaida wa Wakuu wa Nchi na Serikali huko Luanda, Angola.

Kikosi hicho kipya kitaundwa na wanajeshi kutoka Malawi, Afrika Kusini na Tanzania kufuatia kuondolewa kwa wanajeshi 89 wa mwisho wa Kenya wa Jeshi la Kanda ya EAC ambao waliacha ardhi ya Kongo Alhamisi Desemba 21 kupitia Goma
Kwa maana hio mpaka sasa wjeshi tishio la SADC ni SANDF ya south africa pamoja na JWTZ ya Tanzania.
 
Back
Top Bottom