Watanzania tuelezwe ni wapi alipo Rais wetu Mpendwa John Magufuli, ni haki yetu kujua

Watanzania tuelezwe ni wapi alipo Rais wetu Mpendwa John Magufuli, ni haki yetu kujua

Status
Not open for further replies.
Kaka si wewe, nasikia machozi yananitoka kwa rais anayeipenda nchi yake halafu, wanatokea watu wa aina hii kuleta maneno ya uzushi na kejeli kubwa hivi. Hata kama kuna shida si wasubiri protocal zifanye kazi?!!!
Ni jambo jema wakatolea taarifa. Huu uvumi unanifanya nikose raha kabisa. Yaani hata sielewi kwa nini.
 
Jana watu wamekesha twitter 😂 nusu iliyopita kigogo kuvuruga tena watu. Watu wamevurugwa haswa, comments zinafutwa,nyuzi zinayeyuka.
 
Alafu baadae unawaona makanisani, misikitini!! Mkemea maovu hukemea kila uovu. Hao wanaharakati wanataka wao tu watendewe haki lakini haki za mahasimu wao wanataka hukumu hata za kufa kwa chuki tu!
Ni kweli MTAZAMO, kapotea siku mbili tuu maneno mengi ooh yuko wapi mtukufu, mara ooh tuambiwe ukweli.
Wakati Ben Saanane miaka mitatu sasa hajaonekana wala nguo zake hazijaokotwa. Azory miaka miwili katoweka kama ndege ya Malaysia.
Mie naamini sana katika maombi, najiuliza hivi yule Mkurugenzi wa Nachingwea kama hana kosa na hakusikilizwa bali alipokea matusi hadharani, jee akiwa mtu wa maombi na akawa kaomba kwa Mungu wake amlipie uonevu ule itakuwaje? Sio yeye tuu wako wengi kama yeye maombi yao hayawezi kutimia kwa sababu Mungu anaona kanunua Airbus? Au Bombardier?
Tafakari!
 
Huyu wetu haiwezekani akae miezi mitatu bila kuonekana. Hata wiki moja itazua taharuki kwasababu yeye mwenyewe si MTU wa kujifungia ndani kama mwali.
Kwani mpaka sasa hajaonekana hadharani kwa miezi mingapi

Akionekana kila siku shida asipoonekana shida.Mbona kule Nigeria buhari anaweza kukaa hata miezi 3 bila kujulikana aliko
 
Si mlikuwa mnamtukana kuwa kila siku anataka aonekane yeye tu kwenye tv? Juzi tu hapa alikuwa huko lindi kwenye ziara live tbc mkasema hamuangalii, leo mnamtaka mumuone?

Kwa taarifa yako hata mleta mada sio kammiss bali anachimba tu ili apate taarifa juu ya huu uvumi. Alikuwa anatukanwa na nani, acheni ujinga, watu walisema kweli iweje awe anaonyeshwa kila siku yeye, tena wakati wa kazi huku akiwa amepiga marufuku bunge live kuwa watu wafanye kazi? Hamna wa kummiss labda aliowapa maisha.
 
Heshima kwenu wakuu,

Kuna habari zinasambaa kwamba Rais wa Tanzania John Magufuli anaumwa wengine wanasema amekatiza Ziara huko Kusini ili kushughulikia Masuala mengine ya Kitaifa. Hili sina tatizo nalo.

Kinachoniumiza na kunitatiza ni kuona Taasisi ya Rais akiwemo Msemaji Mkuu wa Ikulu na Msemaji wa Serikali kutokanusha au kuweka sawa habari hizi zinazosambaa na kuacha watu waendelee kumsema vibaya Rais wetu. Ukiacha uongo ukaendelea kuongelewa unageuka kuwa kweli.

Rais sio mali ya Ikulu bali ni mali ya Watanzania wote wa vyama vyote, dini zote, rangi zote na Makabila yote.

Msemaji wa Ikulu, Gerson Msigwa huwa ni mwepesi kukanusha na kutupa update za Rais. Ajitafakari kwa hili kama vipi ajiuzulu tu. Kazi imemshinda ya kuwatumikia Watanzania.

Tunapata wakati mgumu kuelewa.

Kama anaumwa sio jambo la kushtua pia kwani maradhi kwa binadamu ni kawaida, kama anaumwa ni haki wananchi wake wakajulishwa na maendeleo yake yakaelezwa kwa uwazi.

Tumefanya hivyo kwa Baba wa Taifa Nyerere, Askofu Mkuu Mwandamizi Yuda Thadeus Ruwa'ichi, Benjamin Mkapa, Kikwete alipoumwa Tezi dume akiwa Rais na wengine wengi.




Kama yu mzima wa afya tujulishwe ili roho zetu zitulie.

Ni haki yetu kujua Rais alipo na maendeleo yake sababu anaishi kwa kodi zetu na tulimchagua wenyewe ndio maana Televisheni ya Yaifa inamuonesha popote aendapo bure ili wananchi wajue anachofanya Rais wao.

Hata kama kapumzika Ikulu, hakuna sababu ya kuzua taharuki.

Tunajua Rais wetu anapenda mpira hasa timu ya Taifa, Jana timu yetu imeshinda na kufuzu Michuano ya CHAN, hatujaona anapongeza na kushangilia kama kawaida yake.

Hata Msemaji wa Ikulu hajatuma picha akiangalia mpira wa watoto wake kama kawaida yao.

Tunamtaka Rais wetu.

Asanteni sana

TUJIKUMBUSHE;

"Taifa Stars wameipa heshima nchi yetu. Leo nimeona mpira, sio ule wa siku za nyuma."- Rais Dkt Magufuli akifurahia Tanzania kufuzu Fainali za Mataifa ya Afrika #AFCON2019
View attachment 1238150
Naunga mkono hoja, kunapotokea sintofahamu yoyote kuhusu hali ya rais wetu, wananchi tunapaswa kuelezwa.

Hata JK alipoanguka julwaani tulielezwa ni tatizo dogo tuu la fatigue amepumzika na yuko ok.

Hata baada ya tetemeko la Bukoba, kina sisi tulihoji ukimya wa rais. Rais sio mtu tuu huyu ni taasisi.
P
 
Lakini Mkuu kuna sintofahamu na taharuki kwa sasa,kwa nn tusijuzwe tuelewe yu wapi Rais wetu,Kuna maneno mengi sana ya mafumba ambayo yanaendelea kwenye mitandao ya kijamii tujuzwe tufahamu!
Hiyo taharuki iko wapi? mbona watu wanaendelea na shughuli zao kama kawaida
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom