Waterbender
JF-Expert Member
- Oct 2, 2018
- 7,573
- 10,063
huo mkataba umesainiwa lini?Sijazihesabu, wewe zihesabu utuletee jibu.
Wakati unazihesabu, Sasa rudi kwenye mada. Achana na ajuza.
Akili kubwa inajadili maendeleo.
Akili ya kawaida inajadili matukio.
Akili ndogo (mbovu) inajadili watu.
DP World ni taasisi inayomilikiwa na Falme ya Dubai, kama vile TPA inavyomilikiwa na Serikali ya Tanzania, na zote zzimetajwa kwenye makubaliano. Kama hukuiona, hii hapa nimeitoa kwenye tafsiri yamakubaliano:Kama ni IGA, hiyo DP World inatokea wapi? Makubaliano ya nchi na nchi yanawezaje ku-single out kampuni moja kiuwekezaji?
IGA ni makubaliano ya nchi na nchi yakiainisha maeneo yenye mutual interest za kushirikiana. Dp World wanafanya nini kwenye makubaliano ya nchi na nchi? Kwani dp World ni nchi?
Wewe ni mtu mwelewa, lakini kwenye hili umepiga chini kwa kujifanya kutoelewa ndiyo maana unatumia nguvu nyingi sana kukwepa mjadala halisi ili kutimiza interests zako.
Nilijua unazo akili kumbe nawewe chenga.Chuki ni kama hiyo uliyoiwasilisha hapa,personal attack,kwanini usijikite kwenye mada na ukajadili mada badala ya kumjadili mleta mada?
Kwani mwisho thd ngapi ambazo mtu anaruhusiwa kufungua kuhusu bandari?
Wewe ulitaka mleta mada apitwe na nani kwa kufungua thd za bandari ili wewe uone ndio sawa?
Kwa hiyo ukifungua thd za bandari ndio unatumika? Vipi na wale wanaofungua thd za kupinga nao una amini kua wanatumika? Au unaamini wa upande mmoja tu kua ndio wanatumika?
Kwanza nakusikitikia kwa kutokuelewa. Pili nashukuru kuwa hjapinga kuwa makubaliano yamehadiliwa bungeni.Mkuu ndio maana nilimuuliza kama 'agreement' inaridhiwa na Bunge. Alikimbia na mwisho akasema hajui.
Ukweli ni kwamba katiba ya JMT (1977) Sura ya Tatu sehemu ya kwanza Bunge (63)-1(e) inasema bila utata '' Kujadili na kuridhia mikataba yoteinayohusu Jamhuri ya Muungano na ambayo kwa masharti yake inahitaji kuridhiwa''
Kwa mantiki hiyo kilichoridhiwa Bungeni ni Mkataba ingawa Spika ambaye ni Mwanasheria na Prof wa chuo kikuu anakwepa ukweli huu bila kuonyesha maridhiano yameanishwa wapi. At least FaizaFoxy amekwepa kujibu.
Hii ina maana nyingine, kwamba, Jamhuri ya muungano ni pamoja na Zanzibar. Sasa kuna sheria gani nyingine ambayo ipo juu ya katiba ya JMT? Hapa ndipo wanaosema kuna hoja za Uzanzibar wanapata nguvu sana.
Kwamba Wabunge wa Zanzibar ndani ya Bunge la JMT walikwenda Dubai kwa gharama za Tanganyika kama Watalii kwasababu hili jambo haliwahusu. Lakini je, haliwahusu? Katiba inatamka ni la muungano.
Ikiwa si jambo la muungano vipi waziri na mwenzake ambao ni Wazanzibar wasimamie jambo lisilo wahusu wakimshauri Rais Mzanzibar kwa masilahi ya Tanganyika ambayo wao kama Wazanzibar wameyakwepa ?
Wenye hoja ya Uzanzibar wana neno!
Ni kwa mantiki hiyo Zanzibar imepewa nguvu sana hata kusigina katiba. Hii si mara ya kwanza, tunakumbuka katiba ya Zbar 1984 toleo la 2010 imekiuka ile ya JMT, hakuna anayehoji kwasababu wanaofanya hivyo ni Wazanzibar.
Mbowe alipotoa tahadhari kama kiongozi mwenye wafuasi hilo likawa balaa. Kwamba Mtanganyika hawezi kusimamia masilahi ya nchi yake kwasababu haki hiyo kapewa mzanzibar peke yake.
Kwa tukio la Bandari kuna kufungua ''pandora box' au can of worms. Ni jambo baya lakini pia ni zuri kwasababu limeonyesha matundu yaliyopo na limesaidia sana kuwaamsha waliobeba Muungano kutaka haki ya kuwa na maamuzi ya nchi yao. Hoja ya Tanganyika haitaondoka na katiba mpya haikwepeki.
Mwisho, ikiwa tunakubaliana Bunge liliridhia Mkataba, mkataba ni jambo binding, kwasasa hatuwezi kuchomoa hata kwa bahati mbaya. Hapa ndipo tunajibu swali la Faiza kwamba, DP Haiendeshi bandari yoyote lakini tayari sisi umefanya commitment. Tukiondoka tu lazima kuna kitu watalamba.
Nimeshangaa huyu mjinga anakwambia ww una uwezo mdogo aisee.Idiot.
Siyo unaambiwa tu, ndivyo ilivyo imeainishwa hiyo hata kwenye makubaliano yaliyopitishwa bungeni, jsomee kifungu hicho kama ulikuwa hujayasoma makubaliano:Unaambiwa mwekezaji walimuona tu kwenye maonesho pale Dubai basi wakampenda na wakagawa aendeshe bandari za bahari ya hindi ukanda wa Tanga hadi mtwara, na bandari za ziwa nyasa, tanganyika na victoria, hawa watu ni wapuuzi wa kiwango cha mwisho
Tena kuna mengi sana kwenye makubaliano, si bandari pekee. Jisomee:We si ulisema mambo ya dp yanaendelea bandarini na inaanza kazi soon mjadala wa nini tena yani we bibi hujitambui
Kilichokubaliwa na Bunge ni mkataba wa awali, kinachofuata hapo ni mikataba ya utekelezaji ambayo kimsingi mikataba hiyo itafuata msingi mama wa mkataba wa awali, ambao ndio ushahidi wa uwekezaji, na. Ndio maana watu tunapiga kelele sana wajirekebishe hatukatai uwekezaji lakini janja janja ndio hatutaki
Kwani mkataba siyo makubaliano?Wenyewe wanasema sio Mkataba ni Makubaliano
Tuoneshe huo mkataba wenye "msingi wa kipuuzi sana". uusemao. Maana mkataba wa utendaji sijauona hata mmoja na tunaitegemea iwe mingi sana. Kama mwenzetu unao japo mmoja tuoneshe na sisi tufaidike na hu upuuzi.Msingi wa mkataba ni wakipuuzi sana
Serikali haina makubaliano na DP World. Serikali ina makubaliano na Serikali ya Dubai.Ndugu Faiza mimi naona serikali ikae chini tena na hao DP World na kukubaliana terms zenye manufaa pande zote. Kama kuna mambo hayako sawa hadi tulipofikia basi yarekebishwe. Hakuna mtanzania kutoka CCM au upinzani anayeweza kuendesha bandari kwa ufanisi. JPM alipambana sana kuwabana bandarini ila hakuweza. Hawa DP nadhani ndo komesha ya mchwa waliopo bandarini. Jiulize kama CHADEMA huwa wanavurugana kwenye ishu ya viti maalum bungeni vipi kwa mfano wakipewa bandari? Yule Mama Tibaijuka aliyesema milioni 10 ni hela ya mboga itakuwaje akipewa usimamizi wa bandari? ILI KUONDOA LAWAMA BANDARI AENDESHE DP. Sisi tuchukue tu mgawo wetu. Marehemu Steve Jobs pamoja na kuwa mwanzilishi wa Apple Company ila wadau walishawahi kumtimua.
Kwanza mkataba urekebishwe mengine yanazungumzika. Hilo tu basi.Leo tuwache jazba, kejeli, matusi na ujinga. Hii kwa pande zote mbili, zinzoona DP World haifai na zinazoona DP World inafaaa tujadiliane kiustaarabu tuone "options " zetu ni zipi, zile zenye faida tuishauri serikali izifate, zile zisizo na faida tuishauri serikali isizifate.
Kama una jibu au majibu sawa, kama hauna majibu bali una swali lako pia, uliza tulijadili. Maswali na majibu yawe mafupi ili mjadala unoge.
Wale wa zamani tujikumbushe mijadala ya Jambo Frums ilivyokuwa inanoga na wale wa sasa wapunguze jazba.
Uongozi wa JF, @moderators tunahitaji muulinde huu uzi kwa uwepo wenu wa karibu, ili mjadala uende vizuri. Au nipeni u moderator wa mjadala huu tu ili niuendeshe inavyopaswa, mkiona siuendeshi kwa haki, mauodoa u miderator wangu.
Tuwe great thinkers ambao hata mtu atakaesoma huu mjadala aseme aaah, hyu ana point, aah huyu hili tumeliona.
Tuwe na maswali mengi ya kujiuliza lakini tujikite kwenye mada. Nalianzisha:
1) Sasa hivi nielewavyo mimi DP World wala Dubai hawaendeshi bandari yetu yoyote, kweli siyo kweli?
Tatizo halipo kwenye makubaliano aua mkataba, hata uwe kwa mdomo tu ukiwa na masgahidi basi unaweza kutafsirika kama makubaliano au mkataba.
Bandari za zanzibar hazimo kwa sababu wanasema kila mmoja anasimamia bandari zake
Huo mkataba uusemao, mimi binafsi sijauona, kwa hiyo ukiuzungumzia ni kama unampigia mbuzi guitar. Labda uuwekke hapa tuuone.Kwanza mkataba urekebishwe mengine yanazungumzika. Hilo tu basi.
Sasa mtu kama huyu ambae anaonyesha wazi kabisa chuki yake dhidi ya race nyingine utamfahamishaje au utajadili nae nini?
Siyo mada iliypo hapa, lakini utumwa lini ulikwisha? Iliyobadilika lugha tu, utumwa uko palepale, tena wa sasa ndiyo mbaya zaidi.Bibi ameamua kuturudisha utumwani kwa masultan wa UAE.
Sasa hata hayo unayotaka tuyazungumzie hayana nafasi kwasasa maana hatuyajui mkataba unasemaje.Huo mkataba uusemao, mimi binafsi sijauona, kwa hiyo ukiuzungumzia ni kama unampigia mbuzi guitar. Labda uuwekke hapa tuuone.
Sasa tufuyte mkataba hewa? Chukulia umeshafutwa. Tungoje mpya sasa. Au unasemaje?
Hamuwataki hao waarabu wewe na nani?