Watanzania wengi maskini wanafia ndani kwa kukosa matibabu

Watanzania wengi maskini wanafia ndani kwa kukosa matibabu

Jana nilitoka nje ya wilaya niliyopo kwa ajili ya jambo flan flan, sasa wakati nikiwa huko ugenini mwenyeji wangu alichelewa kunifuata baada ya kumsubiri kwa muda alikuja.

Basi akasema amechelewa kuna jirani yake anaumwa sana yupo nyumbani basi wakati tunaongea kumbe alisahau simu huko alikotoka ikabidi nimsindikize na hichi ndicho kilichonitoa machozi.

Mgonjwa yupo katika hali mbaya, ni mama mtu mzima ambae anaugua sukari, mguu mmoja waliukata tayari sasa huu mguu mwingine hali ni mbaya jamani kidonda kikubwa kimetokea karibu na unyayo kinazidi kusambaa na kutoboa mguu, isitoshe hiyo sehemu ya kidonda panavuja/panachuruzika
maji.

Na pia mguu wote umekuwa mweusi, basi nikauliza kwanini hajapelekwa hospitapi hadi sasa wanadai hali ni ngumu nyumbani hapo na watoto hawana pesa kwani wanaishi kwa vibarua vibarua tu. Wazazi hao ni wazee na walikuwa wakulima wadogo tu.

Na kwa sasa hata mifugo ndani hawana kwani imetumika kwenye matibu tangu mguu wa kwanza na sasa hawana chochote.

Ukweli ni kwamba huyu mama anateketetea huku anajiona kutokana na umaskini uliopo. Hali ni mbaya na watoto wao pia hawana namna kutokana na uduni wa maisha.
Mkuu unajua leo hii hali, mbona sasa imezoeleka!!?,,nikujihangaikia si wenyewe kadri tuwezavyo na mungu muweza anatulinda.
 
Wee jamaa sijui una roho mbaya au vipi? Ulivyoona hivyo wewe ulitoa msaada gani? Kwa jinsi unavyojinasibu na kushangaa umasikini ningetegemea walau umpeleke hospitali na kugharamia japo huduma ya kwanza au toa basi 50k iwasaidie kumuuguza kuliko kuona ulichokiona na kubeza
Sasa kama amesaidia ndio ajitangaze hapa,wacha upuuzi wako wa kibongo kulaumu kila kitu.
 
Jana nilitoka nje ya wilaya niliyopo kwa ajili ya jambo flan flan, sasa wakati nikiwa huko ugenini mwenyeji wangu alichelewa kunifuata baada ya kumsubiri kwa muda alikuja.

Basi akasema amechelewa kuna jirani yake anaumwa sana yupo nyumbani basi wakati tunaongea kumbe alisahau simu huko alikotoka ikabidi nimsindikize na hichi ndicho kilichonitoa machozi.

Mgonjwa yupo katika hali mbaya, ni mama mtu mzima ambae anaugua sukari, mguu mmoja waliukata tayari sasa huu mguu mwingine hali ni mbaya jamani kidonda kikubwa kimetokea karibu na unyayo kinazidi kusambaa na kutoboa mguu, isitoshe hiyo sehemu ya kidonda panavuja/panachuruzika
maji.

Na pia mguu wote umekuwa mweusi, basi nikauliza kwanini hajapelekwa hospitapi hadi sasa wanadai hali ni ngumu nyumbani hapo na watoto hawana pesa kwani wanaishi kwa vibarua vibarua tu. Wazazi hao ni wazee na walikuwa wakulima wadogo tu.

Na kwa sasa hata mifugo ndani hawana kwani imetumika kwenye matibu tangu mguu wa kwanza na sasa hawana chochote.

Ukweli ni kwamba huyu mama anateketetea huku anajiona kutokana na umaskini uliopo. Hali ni mbaya na watoto wao pia hawana namna kutokana na uduni wa maisha.
Serikali ya ccm ndiyo umetufikisha hapa aisee! Kwa ufisadi wanaoufanya mungu awalaani aisee
 
Wee jamaa sijui una roho mbaya au vipi? Ulivyoona hivyo wewe ulitoa msaada gani? Kwa jinsi unavyojinasibu na kushangaa umasikini ningetegemea walau umpeleke hospitali na kugharamia japo huduma ya kwanza au toa basi 50k iwasaidie kumuuguza kuliko kuona ulichokiona na kubeza
Makasiriko ya nini mkuu, umejuaje kama yeye ana uwezo wa kiuchumj kusaidia?
 
Kwani bima ya afya ni Bure? Si mpaka uchangie kila mwaka. Mtu anakosa hela ya kula na umuongezee mzigo/mchango wa bima ya afya!
maskini ana aga dunia kitandani kwa kukosa fedha ya matibabu akiwa na Samsung Galaxy ya laki 8 dah, na wengine iphone ya m4.

Inashangaza mno, kwamba kipaumbele ni vitu laxury au afya?

huruma haijawahi kumsitiri au kunusuru afya au uhai wa mtu kwa uhakika, labda awe mjanja kama kibaraka wa mabwenyenye ya magharibi.

Mgonjwa ana simu kali kuliko ya doctor, yet hawezi kumudu gharama za matibabu na wala hana bima 🐒
 
Ni muhimu sana kwa mwaka huu mpya kila moja wetu, kuhakikisha kuwa na Bima ya afya.

Inashangaza na kufedhehesha sana, mtu ana iphone ya 4m, na hana bima ya afya ya efu70.

Ni muhimu sana kuzipa umuhimu na kipaumbele cha kipekee sana afya zetu, vinginevyo uliyoyaeleza hayakwepeki 🐒
Unaongelea wenye iphone ya 4m, unadhani watanzania wangapi wanamilili simu ya milioni 4?
Humu jf kwenyewe wenye jeuri ya kumiliki simu ya milioni 4 ni wachache mnoo.

Na maelezo ya jamaa amegusia watu wa vipato vya chini, mtu ambe hata kula yake tabu, mtu anaefanya kazi vibarua, anaweza kupata kazi 3 ama 4 katika wiki, kwa malipo ya elfu 10-15 kwa siku, hiyo hiyo ale yeye na mkewe, atizame wazazi wake, matibabu, usafiri n.k, huyu mtu anawezaje kulipia bima.
Achana na vijijini hapa mjini daslam tu. Kuna watu vipato haviruhusu kulipa bima.
 
maskini ana aga dunia kitandani kwa kukosa fedha ya matibabu akiwa na Samsung Galaxy ya laki 8 dah, na wengine iphone ya m4.

Inashangaza mno, kwamba kipaumbele ni vitu laxury au afya?

huruma haijawahi kumsitiri au kunusuru afya au uhai wa mtu kwa uhakika, labda awe mjanja kama kibaraka wa mabwenyenye ya magharibi.

Mgonjwa ana simu kali kuliko ya doctor, yet hawezi kumudu gharama za matibabu na wala hana bima 🐒
Umeandika kama vile huishi Tanzania
 
Unaongelea wenye iphone ya 4m, unadhani watanzania wangapi wanamilili simu ya milioni 4?
Humu jf kwenyewe wenye jeuri ya kumiliki simu ya milioni 4 ni wachache mnoo.

Na maelezo ya jamaa amegusia watu wa vipato vya chini, mtu ambe hata kula yake tabu, mtu anaefanya kazi vibarua, anaweza kupata kazi 3 ama 4 katika wiki, kwa malipo ya elfu 10-15 kwa siku, hiyo hiyo ale yeye na mkewe, atizame wazazi wake, matibabu, usafiri n.k, huyu mtu anawezaje kulipia bima.
Achana na vijijini hapa mjini daslam tu. Kuna watu vipato haviruhusu kulipa bima.
achana na iphone,
nenda muhimbili au amana uone wagonjwa wa kawaida kabisa hawana bima wala hawana uwezo wa kagharamia matibabu yao but simu walizonazo iwe Tecno, Infinix au sumsang ni za gharama mno kuliko hata za madaktari wanao wahudumia halafu ati huyo mtu ni maskini?


nadhani makosa ni kutokujua kipaumbele katika maisha yetu ni nini.
Wengi tunakimbilia vitu luxury kuliko afya na uhai.

Huyo maskini yuko radhi ajikakamue kununua smartphone mbovu kwa elfu 90 , huku akipuuza bima ya afya ya elf70.

Akiugua,
anakuja kutia huruma na kimbwelambwela hapa 🐒
 
Umeandika kama vile huishi Tanzania
Naishi Tanzania,
na ni kiongozi wa wananchi ambae kwenye suala la Afya kipaumbele changu cha kwanza katika awamu ijayo ni kuhakikisha, iwe iwavyo kila familia jimboni inakua na bima ya afya,

wanafunzi wa chule kuanzia chekechea had secondary, kama kiongozi wao nitaona namna ambavyo wazazi, wadau wa afya jimboni na tasisi mbalimbali za kitaifa na kimataifa na serikali tunaweza kusaidia kila mtoto nae awe na bima ya afya.

Hakuna haja ya kutia huruma hapa wakati ukiuza gunia moja tu la alizeti unaweza kupata bima ya afya ya mwaka mzima 🐒
 
Ni muhimu sana kwa mwaka huu mpya kila moja wetu, kuhakikisha kuwa na Bima ya afya.

Inashangaza na kufedhehesha sana, mtu ana iphone ya 4m, na hana bima ya afya ya efu70.

Ni muhimu sana kuzipa umuhimu na kipaumbele cha kipekee sana afya zetu, vinginevyo uliyoyaeleza hayakwepeki 🐒
mkulima mdogo wa mazao ya chakula huko kijijini anatoa wapi iphone? achilia tu hata uwezo wa kulipia hiyo bima ya afya! unaujua umaskini wa watanzania waishio vijijini au unaongea porojo za kisiasa?
 
achana na iphone,
nenda muhimbili au amana uone wagonjwa wa kawaida kabisa hawana bima wala hawana uwezo wa kagharamia matibabu yao but simu walizonazo iwe Tecno, Infinix au sumsang ni za gharama mno kuliko hata za madaktari wanao wahudumia halafu ati huyo mtu ni maskini?


nadhani makosa ni kutokujua kipaumbele katika maisha yetu ni nini.
Wengi tunakimbilia vitu luxury kuliko afya na uhai.

Huyo maskini yuko radhi ajikakamue kununua smartphone mbovu kwa elfu 90 , huku akipuuza bima ya afya ya elf70.

Akiugua,
anakuja kutia huruma na kimbwelambwela hapa 🐒
Bima ya afya kwa 70k??

We umeamua kudivert ujumbe wa mleta mada kwa sababu unazozijua mwenyewe.

Mleta mada kazungumzia masikini ambao vipato vyao kwa siku havieleweki.
We unabadilisha mada unasema mara iphone ya milioni 4, mara sijui kimeenda kimerudi, infinix sijui nini.. Kwa dunia ya sasa simu sio luxury, simu ni hitaji la muhimu pia, zipo za luxury, lakini hizi za mawasiliano tu ni muhimu na kuna watanzania hata hizo infinix za 90 elfu hawana, wanatumia kiswaswadu cha tecno kina rubber band kila kona.

Sasa huyu umuambie mambo ya bima, anaipatia wapi laki 2 kasoro, tena ya pamoja, kulipa bima?

Mkuu au wewe ni chawa wa watawala nini??
 
Watanzania wengi wanakufa kwa kisukari, nahisi kisukari yaweza kua sababu #1 kwa vifo nchini. Na tatizo kubwa ni sababu watu wengi hawana elimu ya wale nini waache nini, bongo kila mtu ni "piga ugali 80% mbona 20%" wanapiga wanga asubuhi hadi usiku, nutrition ni kitu nadhani kingefundishwa shuleni kila mtu aelewe kua kula vibaya ni kitu kitakuua vibaya sana. Nimeona watu wengi wana kisukari wanabadilisha mlo kisukari kinapotea kabisa wanaishi vizuri tu.
 
Wee jamaa sijui una roho mbaya au vipi? Ulivyoona hivyo wewe ulitoa msaada gani? Kwa jinsi unavyojinasibu na kushangaa umasikini ningetegemea walau umpeleke hospitali na kugharamia japo huduma ya kwanza au toa basi 50k iwasaidie kumuuguza kuliko kuona ulichokiona na kubeza
Nami nilikuwa natiririka na habar yake nione alifanya Nini ila nasikitika nilichotegemea sikukiona.
 
Naishi Tanzania,
na ni kiongozi wa wananchi ambae kwenye suala la Afya kipaumbele changu cha kwanza katika awamu ijayo ni kuhakikisha, iwe iwavyo kila familia jimboni inakua na bima ya afya,

wanafunzi wa chule kuanzia chekechea had secondary, kama kiongozi wao nitaona namna ambavyo wazazi, wadau wa afya jimboni na tasisi mbalimbali za kitaifa na kimataifa na serikali tunaweza kusaidia kila mtoto nae awe na bima ya afya.

Hakuna haja ya kutia huruma hapa wakati ukiuza gunia moja tu la alizeti unaweza kupata bima ya afya ya mwaka mzima 🐒
Kwamba hujui maisha harisi ya mtanzania?
 
Back
Top Bottom