Watanzania wengi maskini wanafia ndani kwa kukosa matibabu

Yes,
ilikua 50k last two yrs gentleman.

sibabaika kusema ukweli kwenye mabandiko yanakuja kutafuta attention na huruma.

hua naeleza ukweli.
kuna uzembe hata wa kifamilia dhidi ya huyo mgonjwa.

Sukari ni maradhi ambayo ni endelevu sana, ambayo mgonjwa anafaa kua standby mno kwa kuzingatia clinic, vigezo na masharti.

Walipaswa ilipogundulika ana tatizo hilo tu, wajichange na wamkatie bima ya afya, kwasabb mgonjwa huyo hastahili msamaha wa matibabu kwasabb ndugu zake wenye uwezo wapo. Hilo hawakulifanya na ni kosa la kifamilia.

Fuatilia hata huyo mgonjwa mwenyewe au hao ndugu zake wana Infinix new model za laki8 but wanatafuta huruma ati wao ni maskini.

That's very wrong.
Tuzipe afya zetu kipaumbele.

Gunia moja la Alizeti hivi sasa ni laki1.5 uzeni mkate bima za afya za mwaka mzima ndrugu zango wadau πŸ’
 
Kwamba hujui maisha harisi ya mtanzania?
umeelewa huo mpango ambao niko nao kama kiongozi kwaajili ya wanainchi?

Natoa wito hata kwako na wadau wengine wote humu JF huu mwaka kabla haujaisha, make sure una bima ya afya.

Hiyo iphone, Infinix, Samsung na Tecno kali sana unayotumia kutafuta tension na kutia huruma humu jukwaani haitakusaidia gharama za matibabu yako ukiugua.

Hakikisha unaipa kipaumbele Afya yako kwa kua na bima ya afya okay?πŸ’
 
Ukweli mchungu na pia machawa wengi hawawezi niunga mkono.
enzi za hayati maskini (99.99% ya watanzania) mana matajiri wako mbele huko. maskini walipata ahueni ya maisha pia hata kwenye swala la afya. mfano huyo mgonjwa angepelekwa hospital kwanza then naamini angepatiwa matibabu kutokana na ukali wa hayati mana ingekuwa ngumu kwa madaktari kumuacha then ingepatikana namna hata ya kuchangisha fedha na ikalipwa muda huo mgonjwa anaendelea vzuri. sasa hiyo familia inaogopa hata kufanya hivo mana mfumo wa kumuona daktari kwa laki moja umerudi, madaktari wamejivisha u mungu tena. wakati kipindi kile ukienda hospital hata na jero tu uko hoi utachangamkiwa utapewa matibabu mana wakizingua hayati anapitisha panga daaah maskini hatuna tena mtetezi .LETS PRAY EXTREMELY NO ONE CAN FIGHT FO US THAN GOD COZ OUR REAL FIGHTER ALREADY GONE. nanukuu hii kauli '' Nikifa mtanikumbuka kwa mazuri na si kwa mabaya'' hivo tuache maandiko yatimie.
R.I.P JOHN POMBE MAGUFULI..
WE MISSED YOU DADDY !!!
 
Ni sahihi elimu inahitajika, ila tukubali pia umasikini unachangia kwa kiasi kikubwa.
Unadhani watanzania wangapi hulo vijijini ama hapa mjini wana jeuri ya kuukwepa ugali na wali.

Mtu ana familia ya watu wa5, asubuhi kila mtu apate yai lake na mboga za majani, mchana familia ile kaugali kadogo na samaki mkubwa kila mtu, matunda ya kutosha, usiku sijui ale kitu gani.
Ni ngumu kwa uchumi wetu lakini pia maisha ya mtanzania kwenye kujitafutia kipato, mtu kazi zake ngumu ale robo kuku alale ama anywe kahawa na kipande cha yai kisha aende akabebe mizigo yake..

Elimu itolewe na serikali iboreshe standard ya maisha ya mbongo
 
Wewe nawe kwa kutetea uozo. Sasa hapo unaona kuna familia yenye iPhone hapo? Hapa wanazungumziwa watu ambao hata hela ya kula ni shida.
 
Sijui una umri gani, ama nawe ni wale machawa!!
Unaandika vitu vya hovyo kuliko maelezo umekazania tu iphone mara infinix, una uhakika wanazo?

Hiyo bima ya elfu 70k hebu iweke hapa nasi tuione.

Bima ni muhimu mie sipingi ila maisha ya mbongo ni changamoto, ni wachache sana wenye kumudu kuipata laki 2 ya pamoja,
Tembeeni muone, mjifunze.
 
Wewe nawe kwa kutetea uozo. Sasa hapo unaona kuna familia yenye iPhone hapo? Hapa wanazungumziwa watu ambao hata hela ya kula ni shida.
Kama afya ni uozo puuzia sasa, na vile vile huna haja kuja kufuta tension na huruma humu JF ikiwa suala la Afya yako mwenyewe ni uozo, itakukost gentleman.

Bima ya afya ni muhimu mno kwa kila moja wetu. Huyo mgonjwa hastahili msamaha wa matibabu kwa mujibu wa vigezo na masharti ya afya kwasabb ni wazi ana ndugu wenye uwezo, ambao wao wamejitutumua kulipa gharama za afya ambazo sasa zinawalemea badala ya kumkatia bima mgonjwa ili kupunguza gharama na usumbufu kwao.

My friends, ladies and gentlemen,
Mambo haya ni kujipanga vizuri inawezekana. Kateni bima za afya, vinginevyo anachopitia mgonjwa huyo hakiepukiki.

Bima ya Afya sio uozo, usipuuzie kua nayo πŸ’
 
Acha uchawa
 
Unatetea uozo. Hata sentensi rahisi huwezi kuelewa. Unatetea uozo wa serikali kwenye afya. Kwani hujui wananchi wengi wanaishi chini ya $1 kwa siku? Hio bima wanaipataje?
 
Eti huyo nae anapewa jimbo halafu tunashangaa hapa tulipofika!
 
Jambo la msingi zaidi gentleman,
zingatia mawaidha na nasaha zangu muhimu, na za maana sana kuhusu umuhimu wa kila moja wetu kua na Bima ya Afya,

Vinginevyo kinacho mkuta mgonjwa anaeelezewa hapo na mdau hakiepukiki.

una simu kubwa ya gharama, lakini hata Panadol huwezi kununua, vocha yenyewe ya jero hujaweka kwenye simu yako wiki ya pili sasa.

Kipi bora sasa kati ya simu ya gharama au bima ya afya isiyo ya gharama?

Tujali afya zetu zaidi ya kutafuta tension na huruma za wadau kwa mambo ambayo unaweza kujipanga nayo tu gentleman,

relax, usipanic πŸ’
 
Kaka weee kama unandugu wenye uwezo ni wewe Kuna familia hazina hata hao watu nyie ndo wale hamjatembea kuona watu wanavoishi acha dhihaka uwezo wako usifananishe na wengine
 
Acha uchawa
hakikisha una Bima ya afya mwaka huu, vinginevyo utakumbuka ukweli huu ukiwa umelala nyumbani unaumwa na huna hata mia mbovu mfukoni kwaajili ya Panadol.

Bima ya afya itakusaiadia, kua nayo tafadhali gentleman πŸ’
 
Eti huyo nae anapewa jimbo halafu tunashangaa hapa tulipofika!
Na inawezekana kabisa kwa akili ndogo za viongozi wetu wanavyopenda sifa, nyimbo za mapambio, anaweza pewa uteuzi na yeye kwa kulijua hilo ndio maana anafanya huu uchawa, huku kujitoa akili si bure kuna jambo analilenga.

Tumefika hapa sababu ya kupata viongozi viazi viazi kama huyu bwana.
Akishakuwa mkuu wa wilaya huyu unategemea nini.
 
Kaka weee kama unandugu wenye uwezo ni wewe Kuna familia hazina hata hao watu nyie ndo wale hamjatembea kuona watu wanavoishi acha dhihaka uwezo wako usifananishe na wengine
Bima ya afya ni nafuu zaidi kuliko kulipa gharama za matibabu moja kwa moja, my lady kama ulikua hufahamu ama hujui umuhimu wa bima.

Bima ya afya ni elfu 70 kwa mwaka.
Gonjeka halafu uende ukatibiwe hospitali yoyote ile leo January, utaacha pale hosiptali sio chini ya elfu40-50.

Nenda tena ukatibiwe mwezi May, utalipia kiwango cha pesa sawa na hicho cha January, vip ukiugua tena Oct na December kwa gharama ile ile?

Ni muhimu kua na bima ya afya bila ubishi my lady πŸ’
 
Ndio maana mashujaa wanaonaga heri wakafe mstari wa mbele atleast wakipigania kitu fulani! Kuliko jinsi tunavyokufa tukijiona bila sababu 😒
Bima ya afya inakupatia angalau uhakika wa matibabu ya afya yako kwa kiasi fulani unapogonjeka,

hakuna bingwa wa maisha humu duniani ndrugo zango. Hakunaga haja kukata tamaa na kuangamia kwa kukosa maarifa πŸ’
 
Bima ya afya inakupatia angalau uhakika wa matibabu ya afya yako kwa kiasi fulani unapogonjeka,

hakuna bingwa wa maisha humu duniani ndrugo zango. Hakunaga haja kukata tamaa na kuangamia kwa kukosa maarifa πŸ’
Bima huwa ni bure mkuu?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…