Mtoto wa Baba
JF-Expert Member
- Sep 1, 2018
- 3,123
- 4,023
[emoji1][emoji1]Kwanza mim mwanang lazima avae suruwal yenye pindo kwa chin na lazm achomekee.avae na saa na lazima shat iwe panga la pasi.na lazima atumie deodorant za kwapa.marufuk kunyoa kiduku
Muda wa wazazi kutoka nyumbani asubuhi unapishanaIla kweli aisee..Mimi huku nawaona hawafanani na mwanafunzi..Mimi sijasoma zaman sana lakini angalau tulikuwa tunavaa decently, sketi ndefu, shati unachomekea unavaa na Tai. Kiatu cheusi na socks. We used to look smart!
Lakini siku hizi hata socks hawavai, hasa watoto wa kiume, sijui kimetokea nini.
Ila tusiwalaumu wao tuanze na wazazi maana wakati mtoto anatoka kwao wazazi wanatakiwa wahakikishe yuko sawa na shule pia walimu wanatakiwa waangalie uvaaji wa mwanafunzi wao maana huwezi kuwa mwalimu wa shule ambayo mwanafunzi wamevaa kihuni kihuni na ukawa comfortable. Wazazi na walimu wawe wa kwanza kulaumiwa.
Ndiyo maana....Mwenyewe kuchomekea nilikua sipendi miaka ya 2,000's
KuwaNdiyo maana....
Sidhani kama kuto kuchomekea ni utovu wa nidhamu .. sijui ni nani alileta scam hii na nidhamu ya woga nchi kama MarekaniMwenyewe kuchomekea nilikua sipendi miaka ya 2,000's
Hili bomu la utovu wa nidham nani analilea?
Unaweza kufikiri wizara ya elimu imebadili utamaduni wa uvaaji!
Siku hizi watoto wa shule za sekondari hususani hizi za kutwa hawapendi kabisa kuchomekea sare za shule, katika 100 utakuta watano tu ndiyo wanaochomekea!
Hata ukitazama hizo suruali wanazovaa nyingi ni njiwa (yaani hazifuniki kiwiko) Mashati yao ya shule mengi ni madogo hayafiki kiunoni (Vitopu) Wengine hawana hata vibebeo (mabegi) wanabeba daftali kitozi mkononi Haya yote yanatia sana mashaka tunaandaa wasomi gani
Je, hii style ya uvaaji tunaandaa watumishi wenye sifa gani huko baadae?
Je, nani anastahili hizo lawama? Wizara, wazazi au walimu?
Au tusubiri watumishi wasio na nidhamu baadae ndipo tuwakanye!?
Huku kwetu visheria kibaoSidhani kama kuto kuchomekea ni utovu wa nidhamu .. sijui ni nani alileta scam hii na nidhamu ya woga nchi kama Marekani
Watu wanapiga free style tena nguo za nyumbani na shule inaenda
Kwa style ya kukosa nidham madansa na bodaboda ndo wengiKwa hiyo shule zote zinaandaa watumishi?
Kwa style ya kukosa nidham madansa na bodaboda ndo wengi
Kuchomekea ndo kipimo cha nidhamu?Lakini hata mtaani kunahitaji nidham, hawa hawa ndo wakwe wenu baadae watawaolea watoto wenu
Umeshasema enzi zenu sasa hizi ni enzi zingine mzee.halafu wanava viatu bila soksi enzi zetu huwezi vaa bila kuchomekea na soksi safi tatizo ni nini!
Kukosa nidhamu ni kitendo binafsi cha kutozingatia utaratibu uliowekwa!Unatfsirije kukosa nidhamu? Kuchomekea ni nidhamu?
Nani kakudanganya nidhamu ndo itakufanya uwe bora kielimu?Nashangaa sana.kama mdau wa elimu nasikitika.Tena nawaona hawa wa hizi shule za kata.sijajua hivi huwa walimu wa nidham siku hiz hakuna au? Kwanza wanashona vinjiwa na vichupa anavaa vimoka hana soks.yaan elimu na nidhamu ni mate na ulimi.usipokuw na nidham jua tu utaishia kusindikiza wenzio.
Wanafunzi wengine yote hayo hawafanyi ila ndio wanaoongoza mitihani na masomo darasani.Kwanza mim mwanang lazima avae suruwal yenye pindo kwa chin na lazm achomekee.avae na saa na lazima shat iwe panga la pasi.na lazima atumie deodorant za kwapa.marufuk kunyoa kiduku
Taasisi yoyote duniani ina Uniformity!Kuchomekea ndo kipimo cha nidhamu?
Haya mawazo ndo yanachelewesha maendeleo kwa taifa.
Nenda hata mtandaoni tu tafuta picha za wanafunzi wa dunia ya kwanza then angalia kama wanahangaika kuchomekea unakoona wewe ndiyo nidhamu.
Na kutokuchomekea kwao bado ndo innovators wa technolojia mbalimbali unazotumia wewe mchomekea shati.
Swali ni kwamba kuvaa sare ndo nidhamu?Taasisi yoyote duniani ina Uniformity!
Jeshini hata kama ni mtaalam wa Kara k, lazima uvae kadri ya vazi lilivyoelekezwa!
Shule ni miongoni mwa taasisi! Lazima Uvae kama mwanaTaasisi husika!
Kushindwa kufanya hivyo ni utovu wa nidham!
Sare ziko pote kwenye taasisi hata makanisani kuna sare, hata misikitini kuna sare, hata kwa waganga kuna sare!
Hadi wachawi wana sare! Ambapo hutambuana na ndo nidhamu yao katika taasisi!
Nimekupa tafsiri ya nidham post namba #176Swali ni kwamba kuvaa sare ndo nidhamu?
Mbona askari wanafukuzwa kazini kila siku na wanavaa hizo sare unazokazania ndiyo nidhamu?
Hao walimu wenyewe wanafukuzwa kazi kila uchwao kwa kutokuwa na nidhamu sasa maana ya nidhamu ni sare / kuchomekea ama ni matendo ya mtu anavyoishi na jamii husika?
Wizara ikitoa tamko dogo tuu la maadili inatosha mkuu. Ni swala la kuongea hadharani kwenye vyombo vya habari "mwangwi" wake unapiga kigoma hadi mtwaraKwa ujumla nidham ya wanafunz wengi imeshuka especially shule za kata, siasa zimetawala sana unakuta mtoto anafanya makosa wakuu wa shule wanogopa kutoa adhabu kwa sababu za kisiasa kuwa wataonekani hawajali, coz suala hilo ataingiloa diwan, M/Kiti wa chama, mtendaji wa kata/mtaa/kijiji, so siasa zimezidi sana,
Lakin pia mzazi haoni umuhimu wa kumfatilia mwanane coz elimu ni bure lakini kungekuepo na ada angefatilia koz anasikia uchungu kwa ada yake, sasa halip ada anafatilia nini, mwisho wa siku nidhamu inaporomoka na ufaulu unashuka