Watoto wa siku hizi wanadekezwa sana

Watoto wa siku hizi wanadekezwa sana

Malezi yote hutokana na mazingira kla mtu analea mtoto wake kutokana ma mazingira yanayomzunguka

Afu tujifunze kitu jaman kla mtu analea vle anataka lea mwanae sasa mambo ya kuingilia malezi ya mtu mwingne kwa mwanae uyo ni udikiteta na ukuda

Malezi ya leo sio malezi tulokulia tulio weng
Unatembea barabaran unakutana na binti kaongozana na familia yake ila kavaa kimini kifupi au surual iliyobana sasa ww km mpita njia unataka ufanye nn wakat wazazi wake wamemruhusu
Jaman kla mtu atabeba mzgo wake
We ukilea mwanao kwa maadili unayoona ww ni sahihi bas usihoji wenzio kwa malezi yao ambayo wanaona wao ni sahihi

Kwa kifupi kla mtu ashinde mechi zake
Watu hawapangii wengine namna ya kulea ila hawataki kusumbuliwa na matokeo ya malezi ya mtu mwingine, mfano umepata wageni wenye watoto halafu mara watoto waanze kupanda juu ya friji, tv , meza nk, au waanze kimbizana mpaka rooms nk.
 
Kumbe wwe huwajui kina Junior,wao wanapoona wageni ndiyo huwa Sasa Wanaanza vituko vyao, Mara watake kuaangalia tv, yaani mradi fujo tu hapo Sebuleni!!
Kama ni ngeni si unawaambia wazazi wake mfanye uliloendea. Au ndiyo mgeni wa Kitanzania kuhamia kwa shemeji?
 
Motto akiwa na tabia njema ni wa baba akiwa na tabia Mbaya ni wa mama
 
Kuna mtoto alienda na mama yake ugenini,dogo akagoma kula wali na maharage akasema mimi nimezoea kwetu nakula wali na mayai..
Kama alivyosema mleta uzi,yaani dogo wa darasa la 6 anadeka wakati nikiwa na umri kama huo,nilikuwa nafua nguo mwenyewe,natwanga pumba kisha nachanganya na damu ya ng'ombe nampikia ugali mbwa wa pumba na damu ya ng'ombe(watu wa machinjioni kila silu walikuwa wanatuuzia damu ya ng'ombe),asubuhi sana lazima niamke kumfungia mbwa bandani na kumfungulia saa 4 usiku,nilikuwa naenda shamba kupanda au kwenye palizi,kila jumamosi nampeleka mbwa kumuogesha kwenye ofisi za idara ya mifugo.
Wageni wakija nyumbani,nawasalimia kisha natoka nje naenda kucheza mpira.
Leo unakuta dogo hata kufagia nje hataki,kuna jamaa mmoja ana mdogo wake ana miaka 17 nilishangaa eti dogo hajui kupika ugali yeye anachojua ni kuchemsha chai tu
 
Yani mimi sipendi ujinga ujinga aisee..mimi nilinyooshwa nikiwa mdogo sikuelelewa kimayai kabisa na nilikua mtoto wa mwisho..na wanangu wanafuata humo humo...ni aibu sana wtt kwenda ugenini kuvuruga vitu vya watu...lilia vitu visivyowahusu...kimbia kimbia hovyo...mimi wanangu wako very discplined yani wakienda mahali unaweza dhani hawapo..mpka warudi kwao...tumshirikishe Mungu kwny malezi...
 
Back
Top Bottom