Watoto wa siku hizi wanadekezwa sana

Watoto wa siku hizi wanadekezwa sana

Umeambiwa beba sahani yako beba.
Kama ni mgeni wa kuja na kuondoka utaambiwa, wacha usihangaike, kama ni ngeni wa kufikia hapo ndiyo uuelewe utaratibu wa hapo.
kama huwezi unaacha unaondoka, wacha ujuwaji wa kutaka kuwapangia watu maisha yao.
When in Rome, do as the romans do.

Kwa hili uko sahihi
 
Kuna Nyumba zingine zina majiko ya wazi, yaani sinck la Vyombo linaoneka kutoka dining room!!
Acheni umbea kwenye nyumba za watu wewe mgeni sehemu zako ni 2 tu living room na dining room na kwa kuongezea public toilet

Vingine mwenye nyumba atake yeye kukuonyesha
 
Tatizo sio single mama, tatizo ni mwanaume aliyekataa mimba, ushoga unasababishwa na wanaume, either direct or indirect.

Msiwasingizie wanawakeee.
Na hakuna Mwanaume anae kataa Mimba bila sababu! Single Mama mjirekebishe ili wababa wa Watoto wenu wasiwakimbie!!
 
Acheni umbea kwenye nyumba za watu wewe mgeni sehemu zako ni 2 tu living room na dining room na kwa kuongezea public toilet

Vingine mwenye nyumba atake yeye kukuonyesha
Mkuu ugeni una madaraja,kuna wageni wengine mwisho wao ni siting room tu,na kuna wageni wengine hadi vyumbani wanafika!!
 
Mkuu ugeni una madaraja,kuna wageni wengine mwisho wao ni siting room tu,na kuna wageni wengine hadi vyumbani wanafika!!
Na kuna wageni wengine wao mwisho wao ni huko nje,hata siting room hawaingiii!!
 
Nenda kasome tafsiri ya neno "Udini" kwenye kamusi ya Kiswahili na utaeelewa namaanisha nini!!
Nasoma between the lines, na nnawafahamu sana kwa neno udini mnamaanisha nini.

Udini wangu mimi, wewe unakuwasha nini?
 
Kitendo cha kuhamia Dodoma kimetenganisha wazazi na kuchangia kushuka kwa maadili. Baba tuko Dom, mama anarudi usiku, housegirl ndo meneja wa familia. Watoto kama ni wa kiume utasikia mama na house girl wanapikezana "nitakuchapa", "nitamwambia babaako"
 
Dogo mmoja niko kwao nadiscuss kitu akaniambia shut up naangalia katuni.

Nikamwambia ntazima TV kama ndio inakupa jeuri akajibu "kwani siwezi kuwasha"

Nilichomoa adapter ya king'amuzi ukutani na hakuna aliyeniambia kitu
Hayo ndiyo mambo ya Kitanzania halafu tunajifanya tunajuwa.

Kwanza "sitting room" si pahala pa kuweka TV. Sitting room ni kwa ajili ya kukaa kuongea na wageni. Kuweka tv sitting room, watoto hapohapo, wageni hapohapo, ni kujikaribishia mmomonyoko wa maadili tu.

Ulivyoizima ulifanya la maana sana na ungewapa darsa, wasiweke tv chumba wanachokaribisha wageni.
 
Hayi bdiyi mambobya Kitanzania halafu tunajifanya tunajuwa.

Kwanza "sitting room" si oahala pa kuweka TV. Sitting room ni kwa ajili ya kukaa kuongea na wageni. Kuqeka tv sitting room, watoto hapohapo, wageni hapohapo, ni kujikaribishia mmomonyoko wa maadili tu.

Ulivyoizima ulifanya la maana sana na ungewapa darsa, wasiweke tv chumba wanachokaribisha wageni.
Sasa Kama Nyumba ni ndogo na Ina sitting room moja tu TV iwekwe wapi unapendekeza!!?
 
Sasa Kama Nyumba ni ndogo na Ina sitting room moja tu TV iwekwe wapi unapendekeza!!?
Isiwashwe kabisa wanapokuja wageni au muda mnapokaa kuongea kama familia. Ni kujipangia utaratibu tu.
 
Niliwahi kufika kwenye nyumba Fulani dogo alikuja na sindano anataka kunichoma mama yake akasema usikwepe atalia Sitasahau nilisepa hapohapo [emoji16]
Hahha Mimi ningechapa Kofi kama ingenichoma hiyo sindano hahah
 
Isiwashwe kabisa wanapokuja wageni au muda mnapokaa kuongea kama familia. Ni kujipangia utaratibu tu.
Kumbe wwe huwajui kina Junior,wao wanapoona wageni ndiyo huwa Sasa Wanaanza vituko vyao, Mara watake kuaangalia tv, yaani mradi fujo tu hapo Sebuleni!!
 
Wazazi tuache kuwadekeza watoto wetu ndo Mana matukio ya ubakaji na ulawiti yanaongezeka.

Leo nimeenda kumtembelea jirani yangu ni family friend nimemkuta yupo sebuleni na mtoto wake wa kiume wa darasa la sita afu mama amekaa kihasara tu mtoto anayaona mapaja ya mzazi wake baada ya kuingia Mimi ndo anajiweka vizuri ni malezi gani kwa mtoto wa kiume wazazi hasa wamama wajitafakari.

Single mother na nyie mna yenu sio kwamba tunawasema Sana mbadilike malezi yenu uzungu mwingi. Kuna jirani yangu ni single mother mtoto wake kila anachotaka yeye ni kumnunulia asililie kitu mtoto yuko nursery school wiki nzima mtoto hataki kwenda shule na mama yake anamchekelea tu sio malezi tunawapenda watoto wetu tuwalee na tuwape malezi kwa limit, samahani Kama nimekukwaza ukweli lazima tuambiane.

Na sisi wakina baba tunakosea tushirikiane na wake zetu kwenye malezi Mambo yasiofaa tuyakemee na tuache tabia ya kuvaa nusu uchi upo sebulani umekaa na watoto zako wa kike umevaa kibukta afu uko tumbo wazi haipendezi.

Wazazi, walezi, walimu,viongozi wa dini nk tushirikiane kwenye malezi ya hawa watoto wetu. Usipo muona mtoto kwa muda au hayupo mazingira ya nyumbani jiulize Yuko wapi uko aliko yupo salama na anafanya Nini.

TV, simu ni muhimu kwa watoto kama watajifunza ya maana tusiwaachie tu watoto waangalie wanachotaka
Nakumbuka home kipindi tuko wadogo ni kosa kubwa umekutwa unaangalia channel za tv zisizo na maadili Kama Trace nk au umeweka cd, vhs zenye age above 18+ inafanya watoto wadogo wafanye Yale wanayoyaona kweny tv, cm nk

Mtoto wa siku akiamka asubuhi hasa siku za wikiend Cha Kwanza kwenye tv kaweka channel anayotaka anaangalia bila wasiwasi enzi zetu muda kuangalia tv ulikuwa ni saa 4 asubuhi baada kumaliza kazi.

Malezi bora ni msingi mzuri wa watoto wetu kataa kudekeza. Tuwalinde watoto wetu.
Upo sahihi kabisa, vitoto vingi vya kizazi hiki havina adabu. Katoto hakakufahamu kanakurukiarukia kama ngedere, halafu unakuta kenyewe ni ka-kike. Malezi ya ki-zungu yanachangia kwa kasi sana kuporormosha misingi ya malezi mazuri. Huko mbeleni tutakosa taifa lenye maadili.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom