Watu hawataki kutembeleana siku hizi, kila mmoja yuko bize kusaka shilingi

Watu hawataki kutembeleana siku hizi, kila mmoja yuko bize kusaka shilingi

Ubize wa maisha utatufanya watoto wetu waoane wenyewe kwa wenyewe utakuta mtoto wa bamkubwa anaanzisha mahusiano na mtoto wa bamdgo hii yote kutokutembeleana so kadhara yapo pia
 
Ubize wa maisha utatufanya watoto wetu waoane wenyewe kwa wenyewe utakuta mtoto wa bamkubwa anaanzisha mahusiano na mtoto wa bamdgo hii yote kutokutembeleana so kadhara yapo pia
Na hii kuwa bize sana kwenye kutafuta hela, inapelekea kuongezeka kwa mmomonyoko wa maadili
 
Kuna mzee mmoja nilikutana naye eneo moja la kazi miaka 12 iliyopita, na katika mazingira ya kazi tulikuwa tukiheshimiana sana, na tulikuwa tukiishi kama familia; leo tukale wapi au kunywa wapi, mara moja moja ilikuwa ni kitu cha kawaida.

Baada ya muda kupita aliamua kung’atuka na kwenda kujikita kwenye biashara zake katika mkoa mwingine.

Miezi miwili iliyopita, nilipata kasafari katika mkoa aliopo; nikaamua kumtafuta huyo mzee kwa njia ya simu, ili angalau niweze kuonana naye na tuweze kuzungumza mawili matatu; kama binadamu wanavyotakiwa kuishi.

Bahati nzuri, ilikuwa ni siku ya jumapili.

Mzee alifurahi sana, kupokea simu yangu na tukakumbushana mengi, na pia nikamwambia nipo hapa mkoani, naomba kama inawezekana angalau nije nikujulie hali.

Mzee akanijibu, samahani sana mambo yameingiliana, ndio najiandaa hapa kuelekea kwenye biashara yangu, kukagua mapato.

Alivyoniambia hivyo nikajiongeza na kumuambia, ‘’basi siku nyingine kama nafasi itapatikana, tutaonana tuombe uzima’’

Baada ya hapo nikasoma kitabu cha maandiko kama aya mbili hivi, ndipo nikahitimisha kwa kusema, maisha ya sasa hayahitaji kutembeleana kwa ajili ya kupiga stori; bali ni kutembeleana kwa malengo ya kwenda kupeana fursa za ‘win/win situation’

We una mtazamo gani?​
Dunia imeharibika
 
teknolojia imerahisisha maisha.
kama tumeshaongea kwa njia ya simu unataka tuonane ili iwe je? tupige selfie au?

kama shida ni pesa kuna mobile transactions za kutosha.
kama ni parcel kuna currier companies kila kona - kwa njia zote: nchi kavu, maji, anga. unachagua tu.

sasa hivi mtu unaonana na familia yako tu - mkeo/mumeo na watoto wenu.
 
Huu utamaduni tumeutoa wapi?
people don't have the best interest in you. unafiki ni mwingi sana. naongea kwa experience.
watu wanakutafuta ili wapate chochote kutoka kwako.
mtu unamkopesha pesa ikifika muda wa kumdai ugomvi. sasa yanini kujuana?

kama shida ni bia nnachukua kibunda changu naenda baa nakaa kaunta nanyonya vyombo vyangu nikimaliza nalipa bili yangu nakula kona kivyanguvyangu. maisha mazuri kabisa yasiyokuwa na stress.
 
Ratiba tu zimebadilika,hizi sio enzi za kutoka shamba saa7 mchana na kurudi kukaa kivulini kuvuta kiko, mtu utamkuta nyumbani saa ngapi? Ni kawaida tu hata wewe kuna muda huwezi onana na mtu
 
Sio watu hawataki mkuu.

Minaona kama maisha yamebadilika sana, pesa imekua mbele kwenye kila kitu.

Dunia imekua uwanja wa fujo na hata hata wazazi wamekua bize na kufanya kazi kuliko kufanya malezi.

Teknolojia nayo imerahisisha salam ambayo zamani tuliita ni nusu ya kuonana.
Hapo kwenye Technology Hapo
Umemaliza kazi Uncle.
 
Kuna mzee mmoja nilikutana naye eneo moja la kazi miaka 12 iliyopita, na katika mazingira ya kazi tulikuwa tukiheshimiana sana, na tulikuwa tukiishi kama familia; leo tukale wapi au kunywa wapi, mara moja moja ilikuwa ni kitu cha kawaida.

Baada ya muda kupita aliamua kung’atuka na kwenda kujikita kwenye biashara zake katika mkoa mwingine.

Miezi miwili iliyopita, nilipata kasafari katika mkoa aliopo; nikaamua kumtafuta huyo mzee kwa njia ya simu, ili angalau niweze kuonana naye na tuweze kuzungumza mawili matatu; kama binadamu wanavyotakiwa kuishi.

Bahati nzuri, ilikuwa ni siku ya jumapili.

Mzee alifurahi sana, kupokea simu yangu na tukakumbushana mengi, na pia nikamwambia nipo hapa mkoani, naomba kama inawezekana angalau nije nikujulie hali.

Mzee akanijibu, samahani sana mambo yameingiliana, ndio najiandaa hapa kuelekea kwenye biashara yangu, kukagua mapato.

Alivyoniambia hivyo nikajiongeza na kumuambia, ‘’basi siku nyingine kama nafasi itapatikana, tutaonana tuombe uzima’’

Baada ya hapo nikasoma kitabu cha maandiko kama aya mbili hivi, ndipo nikahitimisha kwa kusema, maisha ya sasa hayahitaji kutembeleana kwa ajili ya kupiga stori; bali ni kutembeleana kwa malengo ya kwenda kupeana fursa za ‘win/win situation’

We una mtazamo gani?​
We mara ya mwisho kumtembelea mshikaji wako nilikuwa lini?
 
Back
Top Bottom