Watu wa Pemba mnaweza vipi kuishi sehemu pagumu kama huku?

Wabara na Wahuni kuitwa Wanyamwezi ni sababu ya watu wawili,
Hiyo ya wahuni sijui, lakini wabara kuitwa Wanyamwezi siyo sababu ya Lipumba na Mapalala.

Katika miaka ya arubaini mpaka sitini (enzi ya Muingereza) ikifika wakati wa kuchuma karafuu Pemba kulikuwa na meli inakuja kuchukua vibarua kutoka Bara (enzi hizo Tanganyika). Waliokuwa wanakwenda Pemba kipindi hicho kwa asilimia kubwa walikuwa Wanyamwezi/Wasukuma na Wadigo kutoka Tanga. Aidha vijana wengi na wafanyabiashara kutoka Unguja walikuwa wanahamia Pemba kwa muda. Kwa kweli fedha ilikuwa nje nje katika kipindi cha karafuu. Hata wahindi walikuwepo kwa wingi sana na maduka yao yakiuza kila unachokitaka na hasa mapambo ya wanawake kutoka India.

Uchumaji wa karafuu unahitaji vibarua wengi ili karafuu zichumwe kwa muda mfupi bila kuharibika (zinachumwa katika stage maalumu ya ukuwaji) otherwise zinaharibika na kuwa 'matende' na zinakuwa hazina thamani kibiashara. Kwa hivyo nguvukazi ilikuwa inakuja wanapiga mzigo na baadae wanarudi nyumbani. Lakini kama kawaida kuna baadhi huwa wanabakia kule kule na kuendelea na maisha yao. Hawa waliobaki wengi walikuwa ni Wanyamwezi na ndiyo maana wabara wote tena wakaitwa hivyo.

Enzi hizo karafuu ilikuwa na bei kweli kweli kwa hivyo msimu wa kuchuma karafuu ilikuwa kama sherehe fulani hivi visiwani. Walikuwepo 'wauza urembo (mapambo ya kina mama)' walikuwa wanauza mpaka vijijini. Mfano mfanyabiashara akikutana na mtu akanunua kitu lakini akapungukiwa na fedha basi atamkopesha na yule aliyekopa atamlipa tu hata kama watakutana baada ya mwaka mmoja (walikuwa waaminifu sana).
 
Muongo Sana wewe,tangu zamani watu wanaoenda Sana visiwani ni wanyamwezi,hata vibarua mashambani ni wanyamwezi,Sasa wao kila atokae Bara humuita mnyamwezi,kabla ya mapalala na lipumba
 
Nimecheka hapo eti "Samaki Pemba ni bei ghali kuliko Singida"je umeweza kujua sababu ni nin?...
 
Uislam ni Mila/utamaduni unaojitegemea,unaposema wanafuata Kama Mila unadhihirisha uelewa wako mdogo wa Mila na dini,chuki kwa Wabara inakuja kwa kuwa muungano ni WA kulazimisha,wanaamini hivyo,wanaamini muungano umewarudisha nyuma na umeharibu utamaduni wao, unaposema mungu Hana dini unatia shadda kwenye umbumbumbu wako kuhusu mungu
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…