bitimkongwe
JF-Expert Member
- Oct 21, 2009
- 7,794
- 7,551
hiyo ni dhana yako, au mazingira unayoishi ndiyo yanakufanya uwaze hivyoHamna anayesomesha mtoto English Medium ana target za aina hiyo , tunadanganyana hapa
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
hiyo ni dhana yako, au mazingira unayoishi ndiyo yanakufanya uwaze hivyoHamna anayesomesha mtoto English Medium ana target za aina hiyo , tunadanganyana hapa
Kwahiyo hao wanaopeleka watoto Saint Kayumba wanawapeleka kufanya nini? Kama kuelimika ni English Medium basi Kuna wazazi wanauza vishata na sambusa ili watoto wasome kumbe wanaingizwa chaka (sikujua hili!)Nyerere alisema elimu hamfanyi mtu asiwe masikini bali elimu humfanya mtu kujua namna ya kupambana na huo umasikini.
Katika kila jamii, elimu hupewa nafasi ya kipekee kama nyenzo ya kufanikisha maendeleo ya mtu binafsi na taifa kwa ujumla. Wazazi huwekeza kwa gharama kubwa kuhakikisha watoto wao wanapata elimu bora, wakiamini kuwa elimu ni ufunguo wa maisha bora. Lakini swali la msingi linabaki: Je, uwekezaji huu unatoa faida inayolingana na gharama zinazotumika?
Katika makala hii, nitachambua gharama za kumsomesha mtoto hadi chuo kikuu, nikiilinganisha na hali halisi ya soko la ajira nchini Tanzania. Pia, nitatoa tafakari mbadala kuhusu thamani ya ardhi kama uwekezaji, pamoja na mbinu ambazo mzazi anaweza kutumia kupunguza gharama za elimu bila kuathiri ubora wa maarifa anayoyapata mtoto wake.
GHARAMA ZA KUMSOMESHA MTOTO: TAKWIMU ZINASEMAJE?
Wazazi wengi hujitoa kwa hali na mali kugharamia elimu ya watoto wao. Kwa mujibu wa makadirio yafuatayo, mzazi anayemsomesha mtoto mmoja kutoka darasa la kwanza hadi chuo kikuu anahitaji angalau:
1. Elimu ya Msingi (Darasa la 1 - 7):
Tsh 800,000 kwa mwaka x 7 miaka = Tsh 5,600,000
2. Elimu ya Sekondari (Kidato cha 1 - 4):
Tsh 1,200,000 kwa mwaka x 4 miaka = Tsh 4,800,000
3. Elimu ya Juu ya Sekondari (Kidato cha 5 - 6):
Tsh 1,200,000 kwa mwaka x 2 miaka = Tsh 2,400,000
4. Chuo Kikuu (Mwaka wa 1 - 3):
Tsh 2,500,000 kwa mwaka x 3 miaka = Tsh 7,500,000
Jumla ya gharama kwa mtoto mmoja inakuwa Tsh 20,300,000, na kwa watoto watatu inafikia Tsh 60,900,000.
Lakini je, mzazi anayefanya uwekezaji huu ana uhakika wa kupata faida kupitia ajira ya mtoto wake baada ya kuhitimu?
HALI YA SOKO LA AJIRA: UHALISIA ULIOPO
Kwa mujibu wa takwimu za Tume ya Vyuo Vikuu Tanzania (TCU), mwaka wa masomo wa 2023/2024 uliona ongezeko la udahili wa wanafunzi wa shahada ya kwanza kufikia 186,289 (Mwananchi).
Hata hivyo, soko la ajira haliwezi kuwahudumia wote. Takwimu za Ofisi ya Taifa ya Takwimu (NBS) zinaonyesha kuwa kila mwaka nafasi za kazi mpya serikalini na sekta binafsi hazizidi 50,000. Kwa hesabu rahisi:
Wahitimu wa vyuo kwa mwaka: 186,289
Nafasi za ajira zilizopo: 50,000
Wahitimu wasiopata ajira mara moja: ~136,289
Uwezekano wa kupata ajira mara moja: ~27%
Kwa maneno mengine, asilimia 73 ya wahitimu wa vyuo vikuu hawapati ajira mara moja.
Hili linaibua swali muhimu: Je, mzazi aliyelipa ada kwa miaka 16-20 anaweza kupata mrejesho wa uwekezaji wake ndani ya muda mfupi?
UWEKEZAJI MBADALA: THAMANI YA ARDHI JIJINI DAR ES SALAAM
Hebu tuchukulie mfano wa mzazi aliyekuwa akitumia wastani wa Tsh 3,000,000 kwa mwaka kwa mtoto mmoja katika elimu tangu miaka ya 1990s. Kama angewekeza pesa hii kwenye kununua viwanja jijini Dar es Salaam, leo hii thamani yake ingekuwa ya mamilioni.
Kwa mfano, mnamo 1995, viwanja katika maeneo kama Tegeta vilikuwa vinauzwa kwa kati ya Tsh 500,000 – 2,000,000. Leo hii, kiwanja cha ukubwa wa 1,200m² katika Mbweni kinauzwa kwa Tsh 85,000,000 (Jiji.co.tz).
Kwa maneno mengine, mzazi aliyenunua kiwanja miaka ya 1990s kwa Tsh 2,000,000 leo anaweza kuwa na mali yenye thamani ya zaidi ya Tsh 200,000,000.
Hii inaonyesha kuwa kuna uwezekano mkubwa wa mzazi kupata faida kubwa zaidi kwa kuwekeza katika ardhi badala ya kutegemea ajira za watoto wao kama njia ya kupata mrejesho wa gharama za elimu.
NJIA YA KUOKOA GHARAMA ZA ELIMU PASIPO KUPOTEZA UBORA
Je, kuna namna mzazi anaweza kumpa mtoto elimu bora kwa gharama nafuu?
Jibu ni ndiyo!
Njia mojawapo ni kumpeleka mtoto shule za serikali na kisha kuongeza maarifa kwa njia ya tuition.
Mfumo huu umefanikiwa katika nchi kama Kanada, ambako homeschooling na masomo ya ziada (tutoring) vimeongezeka kwa 36% kila mwaka, huku gharama ya elimu kwa mtoto mmoja ikiwa chini kwa 90% ukilinganisha na shule binafsi (Moe.go.tz).
Kwa hesabu rahisi, mzazi anaweza kutumia Tsh 120,000 kwa mwaka kwa tuition bora badala ya Tsh 1,200,000 kwa shule binafsi, hivyo kuokoa hadi Tsh 1,080,000 kwa mwaka kwa mtoto mmoja.
HITIMISHO: NI WAKATI WA KUHOJI UWEKEZAJI WETU KATIKA ELIMU
Hakuna anayepinga thamani ya elimu, lakini ni muhimu wazazi kuhoji kama njia wanazotumia kugharamia elimu zina manufaa makubwa kwa watoto na familia kwa ujumla.
Kwa kutumia shule za serikali pamoja na masomo ya ziada, mzazi anaweza kuokoa hadi 90% ya gharama za shule binafsi na kutumia fedha hizo kwa uwekezaji wa muda mrefu kama ardhi, biashara au hisa.
Uamuzi wa leo utaathiri maisha ya kesho. Je, ni busara kuwekeza zaidi ya Tsh 60,900,000 kwa watoto watatu bila uhakika wa faida, au ni heri kutumia kiasi hicho kwa uwekezaji wenye uhakika wa marejesho?
Mtoto wako atajiajiri vipi wakati wewe umesomesha mtoto kwa kujibana na mikopo?Kwani lazima wote waajiriwe??
Wengne watajiajiri, kikubwa maisha yaende.....
Kisa ajira chache ndo wasisomeshe.
Kwani hao watoto ma genius waliosoma Manzese Primary na sasa ni Madaktari bingwa, engineers si walisoma shule zenye mazingira magumu lakini wamefika mbali bila hayo mazingira mazuriEM zina ziada:
- Mazingira mazuri ya kujifunzia
-walimu wanaowajibika
-Nidhamu ni kipaumbele Kwa shule karibu zote
-Wanafundisha elimu ya dini Kwa uhakika
-usafi wa vyoo uko vizuri
-lugha za ziada kama Kifaransa zinafundushwa
-Usalama wa mtoto angalau unazingatiwa
Sasa huwezi kupata hivi vyote bila kulipia
Mleta mada anazungumzia watanzania wa kawaida wenye kipato cha kawaida wanao poteza pesa kwenye EMAkili yako inawaza kuajiriwa tu tena serikalini!
Umewahi kumuona mwarabu au mhindi ofisi za umma Tz? Unafikiri hawasomi? Wanasoma Kayumba?
1.2M kwa mwaka ni sawa na 100K kwa mwezi ambayo ni sawa na 25K kwa week.
Hiyo 25K/week ni sawa na local beer
10/week.
Mbona hamtuletei hizi analysis za fedha kwenye pombe na uzinzi au huko uwekezaji unalipa?
Hao sio wenzako mkuu, Mo dewji tangu lini asomeshe mtoto afu ategemee mwanae awe kijakazi kwenye kampuni Fulani mjini hapa? Hao watu wanasomesha watoto ili waje kuendeleza Biashara za familia; unamwaga milioni 20 kwenye elimu ya mwanao wakati hata kiwanja cha kumrithisha huna , ili iwaje?Ingekuwa ni hivyo kina Mo Dewji na Mbowe wasingekuwa na haja ya kwenda kusoma vyuo vikuu vya nje ili hali ukwasi wanao wa kutosha.
Hadhi ya mtoto huku anazidiwa IQ na mtoto aliyesoma Kayumba?Kuna issue ya hadhi, ambayo haihusiani na elimu atakayopata mtoto bali pia heshima atakayopata mzazi.
Think think.
Hizo ni failure zako binafsi kama mzazi na sio mfumo wa elimu , yaani jukumu la mwanao asipate mimba au asitumie unga unaliachia shule? Kweli?Tathmin ya utakayolipa soba au gharama ya mtoto kupewa mimba ni kubwa Mara elfu!
Shule inasaidia mambo mengi!
Nikuulize ,Una mtoto na unaishi naye?Kwani hao watoto ma genius waliosoma Manzese Primary na sasa ni Madaktari bingwa, engineers si walisoma shule zenye mazingira magumu lakini wamefika mbali bila hayo mazingira mazuri
Kuna wanafunzi wengi tu wamesoma Kayumba na Maisha yanawaendea safi and vice versa acha kukariri.ukiona unataka kupunguza gharama wapeleke wako uko kayumba, kila mtu ana njia zake na maamuzi yake namna alee kizazi chake.
Vipaumbele mkuu, jifunze kutofautisha uwekezaji na starehe; starehe sio lazima iwe na mantiki ila uwekezaji wa elimu lazima uwe na mantikiMbona hamtuletei hizi analysis za fedha kwenye pombe na uzinzi au huko uwekezaji unalipa?
Ndugu yangu, kwa akili za Sasa za mtanzania anayesomesha saint kayumba hana hela hata za kufanya uwekezaji wa aina hiyoWaliosomesha kanumba ndo wana viwanja vingi compared na hawa waliosomesha private? Uhalisia hao hao wanaosomesha hizo shule za gharama pia ndo wana maeneo prime, kazi nzuri na biashara kubwa kubwa
Hizo ni failure zako binafsi kama mzazi na sio mfumo wa elimu , yaani jukumu la mwanao asipate mimba au asitumie unga unaliachia shule? Kweli?
Kuna watanzania wasio wa kawaida?Mleta mada anazungumzia watanzania wa kawaida wenye kipato cha kawaida wanao poteza pesa kwenye EM
Umri wangu unafanana na wako, kwahiyo ungesoma saint kayumba ungekua umeoa ukiwa na miaka 20? SijaelewaUna umri gani? Mimi nimesoma, na nisingesoma probably ningeoa nikiwa na miaka 20 hiyo, ila Sababu ya shule nimeoa nikiwa na miaka 31, very matured, ni shule pekee ndo imenihifadhi mpaka na miaka 31, ningeacha mapema ningeanza kuface challenges mapema sana na pengine nisingeziweza Kama ambavyo nimezianza na 30
Kuna watanzania wasio wa kawaida?
Kila mtu ana vipaumbele vyake,kama mtu kaamua kupoteza pesa yake kwa namna hiyo HAKUNA SHIDA.