Wazazi Mnaosomesha Watoto Shule za Private jifunzeni kufanya tathmini ya Pesa mnayowekeza katika Elimu hiyo na matokeo yake (Hawatazeekea Nyumbani)?

Nyerere alisema elimu hamfanyi mtu asiwe masikini bali elimu humfanya mtu kujua namna ya kupambana na huo umasikini.
Kwahiyo hao wanaopeleka watoto Saint Kayumba wanawapeleka kufanya nini? Kama kuelimika ni English Medium basi Kuna wazazi wanauza vishata na sambusa ili watoto wasome kumbe wanaingizwa chaka (sikujua hili!)
 

Tathmin ya gharama utakayolipa soba au gharama ya mtoto kupewa mimba, kuolewa pre matured na kuachika ni kubwa Mara elfu!

Shule inasaidia mambo mengi!
 
EM zina ziada:
- Mazingira mazuri ya kujifunzia
-walimu wanaowajibika
-Nidhamu ni kipaumbele Kwa shule karibu zote
-Wanafundisha elimu ya dini Kwa uhakika
-usafi wa vyoo uko vizuri
-lugha za ziada kama Kifaransa zinafundushwa
-Usalama wa mtoto angalau unazingatiwa

Sasa huwezi kupata hivi vyote bila kulipia
 
Akili yako inawaza kuajiriwa tu tena serikalini!

Umewahi kumuona mwarabu au mhindi ofisi za umma Tz? Unafikiri hawasomi? Wanasoma Kayumba?

1.2M kwa mwaka ni sawa na 100K kwa mwezi ambayo ni sawa na 25K kwa week.

Hiyo 25K/week ni sawa na local beer
10/week.

Mbona hamtuletei hizi analysis za fedha kwenye pombe na uzinzi au huko uwekezaji unalipa?
 
Kwani hao watoto ma genius waliosoma Manzese Primary na sasa ni Madaktari bingwa, engineers si walisoma shule zenye mazingira magumu lakini wamefika mbali bila hayo mazingira mazuri
 
Mleta mada anazungumzia watanzania wa kawaida wenye kipato cha kawaida wanao poteza pesa kwenye EM
 
Ingekuwa ni hivyo kina Mo Dewji na Mbowe wasingekuwa na haja ya kwenda kusoma vyuo vikuu vya nje ili hali ukwasi wanao wa kutosha.
Hao sio wenzako mkuu, Mo dewji tangu lini asomeshe mtoto afu ategemee mwanae awe kijakazi kwenye kampuni Fulani mjini hapa? Hao watu wanasomesha watoto ili waje kuendeleza Biashara za familia; unamwaga milioni 20 kwenye elimu ya mwanao wakati hata kiwanja cha kumrithisha huna , ili iwaje?
Cha ajabu anamaliza chuo na anakua na qualifications sawa na saint kayumba ambaye naye kafika chuo hivyo hivyo (kwenye vyeti hawajali kama mwanao kasoma Saint Theresia secondary bali wanajali GPA, hata mtoto wa Maimuna muuza vitumbua aliyesoma Msengelo sekondari hana tofauti na mwanao kwenye macho ya muajiri)
 
Mbona hamtuletei hizi analysis za fedha kwenye pombe na uzinzi au huko uwekezaji unalipa?
Vipaumbele mkuu, jifunze kutofautisha uwekezaji na starehe; starehe sio lazima iwe na mantiki ila uwekezaji wa elimu lazima uwe na mantiki
Hela inayochomwa kwenye uzinzi na pombe nitaipangiliaje katika maendeleo?
 
Waliosomesha kanumba ndo wana viwanja vingi compared na hawa waliosomesha private? Uhalisia hao hao wanaosomesha hizo shule za gharama pia ndo wana maeneo prime, kazi nzuri na biashara kubwa kubwa
Ndugu yangu, kwa akili za Sasa za mtanzania anayesomesha saint kayumba hana hela hata za kufanya uwekezaji wa aina hiyo
Nachoongelea hapa ni hawa ndugu zangu ambao wanajikamua ipasavyo mtoto asome EM mpaka mara nyingine wanapiga pasi ndefu maofisini ilimradi ada zilipwe...... Siongelei hao wenye pumzi za kusomesha watoto EM na kufanya uwekezaji at the same time
 
Hizo ni failure zako binafsi kama mzazi na sio mfumo wa elimu , yaani jukumu la mwanao asipate mimba au asitumie unga unaliachia shule? Kweli?

Una umri gani? Mimi nimesoma, na nisingesoma probably ningeoa nikiwa na miaka 20 hiyo, ila Sababu ya shule nimeoa nikiwa na miaka 31, very matured, ni shule pekee ndo imenihifadhi mpaka na miaka 31, ningeacha mapema ningeanza kuface challenges mapema sana na pengine nisingeziweza Kama ambavyo nimezianza na 30
 
Umri wangu unafanana na wako, kwahiyo ungesoma saint kayumba ungekua umeoa ukiwa na miaka 20? Sijaelewa
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…